Uchaguzi 2020 Viongozi wa CHADEMA hatua mlizochukua zitawatia aibu kubwa

Uchaguzi 2020 Viongozi wa CHADEMA hatua mlizochukua zitawatia aibu kubwa

Ignorance is an ultimate choice in the age of Information
 
Kama wanataka kumuua angefika hata huko Namanga? Acheni uongo wenu.
Lissu alipigwa risasi 16+ , ikiwa ni baada ya kutishiwa kama sasahivi wanavyodai kutishwa. Mbaya zaidi wapiga risasi,watekaji, wapotezaji, .......... hawajulikani!
 
Hii ni dalili kuwa hamlitakii mema taifa letu na ipo siku mtaliletea janga kubwa. Ndio maana aliyekuwa mbunge wa Temeke kupitia CCM aliwahi kutoa ombi kuwa Chadema ni chama cha wapenda vurugu hivyo kinastahili kufutwa.

Baada ya kushindwa uchaguzi kwenye box la kura na wananchi kuichagua Ccm sasa mnataka kuiaminisha jumuia ya kimataifa kuwa hapa Tanzania kuna ukiukwaji wa haki za binadamu. Je mbona mlipokuwa wabunge hizi propaganda zenu hatukuzisikia?

Sasa hivi mmezua mchezo mchafu eti mnatafuta hifadhi kama wakimbizi wa kisiasa kuwa kuna tishio la kuuliwa na vyombo vya dola. Mnachotaka tu ni kuchafua taswira ya nchi yetu kuwa hakuna amani na kuna ukiukwaji wa haki za binadamu. Je kama kuna ukiukwaji wa haki za binadamu mbona UN wapo kimya na wana ofisi hapa Tanzania.

Kama vyombo vya dola vilitaka kumuua G Lema wangemuacha yupo salama wiki zote hizi mbili tangu uchaguzi uishe? L Nyalandu anatafuta kick kuwa anakimbia kuuliwa hivi mwanasiasa ambae unataka kuuliwa watu watakuacha hizi siku zote upo salama?

Godbless Lema alipokuwa mbunge alikumbana na kesi nyingi sana,na mpaka alikaa mahabusu miezi minne mbona alipotoka mahabusu hakukimbilia Kenya kwenda kuomba hifadhi kama mkimbizi wa kisiasa?

Kwa ujumla ni kutokubali matokeo ndio sababu ya kutaka kuchafua taswira ya nchi yetu. Na kukosa ubunge ambao kwenu mlidhania nia ajira za kudumu ndio sababu mnataka kwenda kujifanya wakimbizi.

Na hii propaganda mlioamua kuitumia itabuma na mtaaibika zaidi na huu ndio unaenda kuwa mwisho wenu mbaya kisiasa. Maana watanzania wana akili na hawadanganywi kitoto.

Nota bene : Kila propaganda mlizoanzisha zote zilibuma,kumbukeni wakati wa Covid-19 mlipata aibu kubwa,amabayo imewanyima kura.
Fungua akili yako kidogo tu, na usiwe shabiki maandazi.
Kwanini uwe na chuki kwa bindamu wenzio.
Kwani siasa ni ugomvi
Unataka watu wakitendewa ndivyo sivyo ,wapongeze tu. Ulisikia wapi
Hata kunapokuwa na mechi ya simba na yanga, kunakuwa na malalamiko juu ya goli au magoli yaliyofungwa na upande mwingine. wewe unataka refa akikosea asiambiwe
 
Kwani ni uongo. Mbona lisu alitoa alert kuwa anafuatiliwa polisi wakapuuzia halafu ikawa kweli. Sasa Bora kujihami ukifuatiliwa kuliko kupuuzia na kupigwa marisasi Kama lisu. Mi nawapongeza viongozi wa chadema wanaosalimisha maisha yao kabla ya kupigwa marisasi Kama lisu. Jpm anawatafuta kwa udi na uvumba
 
Kwa hiyo ulitaka G. Lema na nyalandu wauawe kwanza halafu wafufuke ndo wake kusema kuwa wanafatiliwa?
 
Fungua akili yako kidogo tu, na usiwe shabiki maandazi.
Kwanini uwe na chuki kwa bindamu wenzio.
Kwani siasa ni ugomvi
Unataka watu wakitendewa ndivyo sivyo ,wapongeze tu. Ulisikia wapi
Hata kunapokuwa na mechi ya simba na yanga, kunakuwa na malalamiko juu ya goli au magoli yaliyofungwa na upande mwingine. wewe unataka refa akikosea asiambiwe
Umeandika nini?
 
Akishawamaliza hawa, ni zamu yako kugeukiwa, ni suala la mda tu, mark my words.
 
Kwa hiyo ulitaka g. Lema na nyalandu wauawe kwanza halafu wafufuke ndo wake kusema kuwa wanafatiliwa?
Unadhani kama watu wanataka kukuua ukiwa Kenya hawawezi kukufuata? Huyu anaeneza sumu mbaya kuchafua nchi yetu. Kama walitaka kumuua wangemuua mapema tu.
 
Wanajiondolea tu credibility za trustworthiness mbele ya watanzania na dunia.

Ukisikiliza mahojiano aliyofanya BBC unapata picha Lema ndani ya mwezi atakuwa Arusha mtu ambae maisha yake yapo hatarini anarudi kufanya nini kwenye mazingira hatari.

Plan zao uwa short sighted someone needs to tell Lema mtu anaetaka kukudhuru hana deadline date, maana anadai atarudi hali ikitulia.
 
Kura ziliibiwa wapi? Mnatengeza clip za uongo kuaminisha watu upuuzi! Kama waliiba si mfungue kesi na sio kwenda nje kuwa wakimbizi.
Sijui kwa sehemu nyingine. Ila kwa TUNDUMA walikomba sio kuiba kule. Hata mbele ya Mungu akiniuliza kuhusu TUNDUMA ntajibu.
 
Unadhani kama watu wanataka kukuua ukiwa Kenya hawawezi kukufuata? Huyu anaeneza sumu mbaya kuchafua nchi yetu. Kama walitaka kumuua wangemuua mapema tu.
akina nani hao wauaji. inaonekana unawajua.
ipo siku nawe yatakukuta, we endelea kushabikia ujinga
 
Hivi wewe ulikuwa wapi wakati viongozi wa CHADEMA walipokamatwa na kuambiwa watafunguliwa mashitaka ya ugaidi hivi kweli hao wabunge wastaafu ni magaidi.

Wewe unaona sawa wananchi wa tanzania kunyimwa haki yao ya huduma ya internet. Wewe unaona sawa watu walivouwawa huko pemba ili kupitisha wabunge wa chama tawala.

Huo uchaguzi unaousema wewe ni huu huu ulikuwa na mabegi ya kurazilizopigwa mtaani tena wakionesgwa polisi wameyashikilia. Hivi umeshamsikia nani kafikishwa mahakamani kwa hivyo vitendo vya jinai
 
akina nani hao wauaji. inaonekana unawajua.
ipo siku nawe yatakukuta, we endelea kushabikia ujinga
Mimi siwajui ,ila hata kama una jirani ana uhasama na wewe akitaka kukuua hawezi kusema anakuua kimya kimya. Hii ya kutishiwa wiki mbili ni uongo tu.
 
Hivi wewe ulikuwa wapi wakati viongozi wa CHADEMA walipokamatwa na kuambiwa watafunguliwa mashitaka ya ugaidi hivi kweli hao wabunge wastaafu ni magaidi. Wewe unaona sawa wananchi wa tanzania kunyimwa haki yao ya huduma ya internet. Wewe unaona sawa watu walivouwawa huko pemba ili kupitisha wabunge wa chama tawala. Huo uchaguzi unaousema wewe ni huu huu ulikuwa na mabegi ya kurazilizopigwa mtaani tena wakionesgwa polisi wameyashikilia. Hivi umeshamsikia enani kafikishwa mahakamani kwa hivyo vitendo vya jinai
Non sense na nje ya mada.
 
Hii hadithi unaweza kuwasimulia watoto wa Dada yako hapo sebleni kwa shemeji yako wakakuelewa.
Watu wa aina ya mleta mada ndio wanao haribu hata nyumba za Dada zao kwa kutembea na shemeji wakati Dada hayupo
 
Hii ni dalili kuwa hamlitakii mema taifa letu na ipo siku mtaliletea janga kubwa. Ndio maana aliyekuwa mbunge wa Temeke kupitia CCM aliwahi kutoa ombi kuwa Chadema ni chama cha wapenda vurugu hivyo kinastahili kufutwa.

Baada ya kushindwa uchaguzi kwenye box la kura na wananchi kuichagua Ccm sasa mnataka kuiaminisha jumuia ya kimataifa kuwa hapa Tanzania kuna ukiukwaji wa haki za binadamu. Je mbona mlipokuwa wabunge hizi propaganda zenu hatukuzisikia?

Sasa hivi mmezua mchezo mchafu eti mnatafuta hifadhi kama wakimbizi wa kisiasa kuwa kuna tishio la kuuliwa na vyombo vya dola. Mnachotaka tu ni kuchafua taswira ya nchi yetu kuwa hakuna amani na kuna ukiukwaji wa haki za binadamu. Je kama kuna ukiukwaji wa haki za binadamu mbona UN wapo kimya na wana ofisi hapa Tanzania.

Kama vyombo vya dola vilitaka kumuua G Lema wangemuacha yupo salama wiki zote hizi mbili tangu uchaguzi uishe? L Nyalandu anatafuta kick kuwa anakimbia kuuliwa hivi mwanasiasa ambae unataka kuuliwa watu watakuacha hizi siku zote upo salama?

Godbless Lema alipokuwa mbunge alikumbana na kesi nyingi sana,na mpaka alikaa mahabusu miezi minne mbona alipotoka mahabusu hakukimbilia Kenya kwenda kuomba hifadhi kama mkimbizi wa kisiasa?

Kwa ujumla ni kutokubali matokeo ndio sababu ya kutaka kuchafua taswira ya nchi yetu. Na kukosa ubunge ambao kwenu mlidhania nia ajira za kudumu ndio sababu mnataka kwenda kujifanya wakimbizi.

Na hii propaganda mlioamua kuitumia itabuma na mtaaibika zaidi na huu ndio unaenda kuwa mwisho wenu mbaya kisiasa. Maana watanzania wana akili na hawadanganywi kitoto.

Nota bene : Kila propaganda mlizoanzisha zote zilibuma,kumbukeni wakati wa Covid-19 mlipata aibu kubwa,amabayo imewanyima kura.
ila jumuia za kimataifa zinafahamu kuwa lisu alipigwa risasi kibao,na hakuna aliyekamtwa,twasira yetu imeharibiwa na ccm academia,ccm asili isingetufikisha hapa
 
Back
Top Bottom