Viongozi wa G7 wailaumu China kwenye mkutano wao unaofanyika Italy

Viongozi wa G7 wailaumu China kwenye mkutano wao unaofanyika Italy

Xi Jinping

JF-Expert Member
Joined
Jun 14, 2023
Posts
3,651
Reaction score
11,548
Leo ni siku ya tatu na ya mwisho ya mkutano wa mataifa yanayounda G7; ambao umewakilishwa na maraisi wa USA, U.K, France, Germany, Italy, Japan na Canada na mawaziri wa fedha kutoka nchi hizo.

Ajenda kuu ilikuwa China.

Maeneo ambayo yamejadiliwa kuhusu China:

1. CHINA INAHATARISHA VIWANDA NA MAKAMPUNI YA NCHI ZAO
Mataifa hayo yameilalamikia China kuwa imekuwa ikifanya industrial overcapacity, hivyo soko la dunia limefurika bidhaa za China hasa kwenye sekta ya green technology kama magari ya umeme, green tech kama solar panels na wind turbines na uzalishaji wa chuma.

Bidhaa hizo zimekuwa zikiuzwa kwa bei nafuu sana kuliko bidhaa za aina hiyohiyo za nchi za Magharibi hivyo inahatarisha viwanda vyao kwani vinashindwa kushindana na bidhaa za China kwenye soko la mataifa yao na la dunia.

Nchi hizo zimesema kuwa hawataacha kushirikiana kibiashara na China wakitambua kuwa ni nchi muhimu duniani kwenye global supply chain.

Ila wataendelea kuchukua hatua ili kulinda biashara, wafanyakazi na viwanda vyao dhidi ya bidhaa za China zenye ubora ambazo zinauzwa kwa bei rahisi.

2. KITENDO CHA CHINA KUDHIBITI MADINI MUHIMU
China imekuwa ikidhibiti uuzaji nje (exportation) madini ya gallium, germnium na graphite ambayo ni muhimu sana kwenye viwanda vinavyotengeneza vifaa vya umeme na mawasiliano kama smartphone (LED), chips, electronic circuits, transistors, solar cells na kwenye magari ya umeme.

Nchi hizo zimeishutumu China kwa kufanya hivyo kwani inasababisha uhaba wa madini hayo kwa mataifa mengine yanayotengeneza bidhaa zinazoyatumia madini hayo kama malighafi.

3. KUISAIDIA RUSSIA KATIKA VITA VYA UKRAINE
Nchi za G7 zinaituhumu Beijing kuwa imekuwa ikiisaidia jeshi la Urusi.

Washington imeishutumu Beijing kwa kusaidia Urusi kupitia uzalishaji wa pamoja wa drones na usafirishaji wa zana za mashine zinazohitajika kwenye utengenezaji wa makombora ya ballastic missiles na silaha zingine.

4. UBABE WA CHINA KATIKA SOUTH CHINA SEA NA ASIA-PACIFIC
Nchi za G7 zimesema vitendo vya China kama kuizunguka Taiwan na kufanya mazoezi ya kijeshi vinaweza kupelekea vita na mgogoro mkubwa sana.

Pia vitendo vya China kujenga visiwa bandia katika bahari ya Kusini ya China, militarization, migogoro ya kimipaka na kujitanua katika eneo la Asia-Pacific na vitisho dhidi ya Ufilipino.

Nchi zote (G7) zimekubaliana kwamba zitafikisha ujumbe huo kwa uwazi katika ngazi ya juu kabisa kwa taifa la China.


Je, ni nani anayeipa G7 mamlaka ya kuamuru lililo sawa au lisilo sahihi?
 
Wao walivyotawala kipindi Cha ukoloni mbona China ilikaa kimya.
Huu mwaka ni kuwafosi. Kule Hamas,Hezbola, Houthis Iran Vs Us &Israel huku China &Singapore war hapo hapo Eastern Europe moto unawaka na Caribbean kumeanza kuchangamka dunianimrkuwa ya moto kidogo hakika 2024 ni remarkable year
 
Waache kulialia. Wao walivyoivamia China miaka 150 iliyopita na kuwafanyia unyama wachina walitegemea Wachina wa leo watakubali udhaifu wa kale?

China ina idadi ya watu inayozidi nchi zote hizo combined, wanataka China ifanye nini kuwezesha watu wake waishi maisha mazuri?

China iendelee hivyohivyo kama inavyofanya sasa hivi, isikubali kurudishwa nyuma.

Ila kwenye nukta ya South China sea. China nayo iache ubabe, nchi moja huwezi kujipa miliki ya bahari eti yote yako kisa eti wafalme wako miaka 1000 iliyopita walipeleka ngalawa huko!
 
Leo ni siku ya tatu na ya mwisho ya mkutano wa mataifa yanayounda G7; ambao umewakilishwa na maraisi wa USA, U.K, France, Germany, Italy, Japan na Italy na mawaziri wa fedha kutoka nchi hizo.

Ajenda kuu ilikuwa China.

Maeneo ambayo yamejadiliwa kuhusu China:
1. CHINA INAHATARISHA VIWANDA NA MAKAMPUNI YA NCHI ZAO
Mataifa hayo yameilalamikia China kuwa imekuwa ikifanya industrial overcapacity, hivyo soko la dunia limefurika bidhaa za China hasa kwenye sekta ya green technology kama magari ya umeme, green tech kama solar panels na wind turbines na uzalishaji wa chuma.

Bidhaa hizo zimekuwa zikiuzwa kwa bei nafuu sana kuliko bidhaa za aina hiyohiyo za nchi za Magharibi hivyo inahatarisha viwanda vyao kwani vinashindwa kushindana na bidhaa za China kwenye soko la mataifa yao na la dunia.

Nchi hizo zimesema kuwa hawataacha kushirikiana kibiashara na China wakitambua kuwa ni nchi muhimu duniani kwenye global supply chain.

Ila watsendelea kuchukua hatua ili kulinda biashara, wafanyakazi na viwanda vyao dhidi ya bidhaa za China zenye ubora ambazo zinauzwa kwa bei rahisi.

2. KITENDO CHA CHINA KUDHIBITI MADINI MUHIMU
China imekuwa ikidhibiti uuzaji nje (exportation) wa madini ya gallium, germnium na graphite ambayo ni muhimu sana kwenye viwanda vinavyotengeneza vifaa vya umeme na mawasiliano kama smartphone (LED), chips, electronic circuits, transistors, solar cells na kwenye magari ya umeme.

Nchi hizo zimeishutumu China kwa kufanya hivyo kwani inasababisha uhaba wa madini hayo kwa mataifa mengine yanayotengeneza bidhaa zinazoyatumia kama malighafi.

3. KUISAIDIA RUSSIA KATIKA VITA VYA UKRAINE
Nchi za G7 zinaituhumu Beijing kuwa imekuwa ikiisaidia jeshi la Urusi.

Washington imeishutumu Beijing kwa kusaidia Urusi kupitia uzalishaji wa pamoja wa drones na usafirishaji wa zana za mashine zinazohitajika kwenye utengenezaji wa makombora ya ballastic missiles na silaha zingine.

4. UBABE WA CHINA KATIKA SOUTH CHINA SEA NA ASIA-PACIFIC
Nchi za G7 zimesema vitendo vya China kama kuizunguka Taiwan na kufanya mazoezi ya kijeshi vinaweza kupelekea vita na mgogoro mkubwa sana.

Pia vitendo vya China kujenga visiwa bandia katika bahari ya Kusini ya China, militarization, migogoro ya kimipaka na kujitanua katika eneo la Asia-Pacific na vitisho dhidi ya Ufilipino.

Nchi zote (G7) zimekubaliana kwamba zitafikisha ujumbe huo kwa uwazi katika ngazi ya juu kabisa kwa taifa la China.

Je, ni nani anayeipa G7 mamlaka ya kuamuru lililo sawa au lisilo sahihi?
Wanatapatapa tu hao
 
Waache kulialia. Wao walivyoivamia China miaka 150 iliyopita na kuwafanyia unyama wachina walitegemea Wachina wa leo watakubali udhaifu wa kale?

China ina idadi ya watu inayozidi nchi zote hizo combined, wanataka China ifanye nini kuwezesha watu wake waishi maisha mazuri?

China iendelee hivyohivyo kama inavyofanya sasa hivi, isikubali kurudishwa nyuma.

Ila kwenye nukta ya South China sea. China nayo iache ubabe, nchi moja huwezi kujipa miliki ya bahari eti yote yako kisa eti wafalme wako miaka 1000 iliyopita walipeleka ngalawa huko!
Mwenye nguvu mpishe
 
Leo ni siku ya tatu na ya mwisho ya mkutano wa mataifa yanayounda G7; ambao umewakilishwa na maraisi wa USA, U.K, France, Germany, Italy, Japan na Italy na mawaziri wa fedha kutoka nchi hizo.

Ajenda kuu ilikuwa China.

Maeneo ambayo yamejadiliwa kuhusu China:
1. CHINA INAHATARISHA VIWANDA NA MAKAMPUNI YA NCHI ZAO
Mataifa hayo yameilalamikia China kuwa imekuwa ikifanya industrial overcapacity, hivyo soko la dunia limefurika bidhaa za China hasa kwenye sekta ya green technology kama magari ya umeme, green tech kama solar panels na wind turbines na uzalishaji wa chuma.

Bidhaa hizo zimekuwa zikiuzwa kwa bei nafuu sana kuliko bidhaa za aina hiyohiyo za nchi za Magharibi hivyo inahatarisha viwanda vyao kwani vinashindwa kushindana na bidhaa za China kwenye soko la mataifa yao na la dunia.

Nchi hizo zimesema kuwa hawataacha kushirikiana kibiashara na China wakitambua kuwa ni nchi muhimu duniani kwenye global supply chain.

Ila watsendelea kuchukua hatua ili kulinda biashara, wafanyakazi na viwanda vyao dhidi ya bidhaa za China zenye ubora ambazo zinauzwa kwa bei rahisi.

2. KITENDO CHA CHINA KUDHIBITI MADINI MUHIMU
China imekuwa ikidhibiti uuzaji nje (exportation) wa madini ya gallium, germnium na graphite ambayo ni muhimu sana kwenye viwanda vinavyotengeneza vifaa vya umeme na mawasiliano kama smartphone (LED), chips, electronic circuits, transistors, solar cells na kwenye magari ya umeme.

Nchi hizo zimeishutumu China kwa kufanya hivyo kwani inasababisha uhaba wa madini hayo kwa mataifa mengine yanayotengeneza bidhaa zinazoyatumia kama malighafi.

3. KUISAIDIA RUSSIA KATIKA VITA VYA UKRAINE
Nchi za G7 zinaituhumu Beijing kuwa imekuwa ikiisaidia jeshi la Urusi.

Washington imeishutumu Beijing kwa kusaidia Urusi kupitia uzalishaji wa pamoja wa drones na usafirishaji wa zana za mashine zinazohitajika kwenye utengenezaji wa makombora ya ballastic missiles na silaha zingine.

4. UBABE WA CHINA KATIKA SOUTH CHINA SEA NA ASIA-PACIFIC
Nchi za G7 zimesema vitendo vya China kama kuizunguka Taiwan na kufanya mazoezi ya kijeshi vinaweza kupelekea vita na mgogoro mkubwa sana.

Pia vitendo vya China kujenga visiwa bandia katika bahari ya Kusini ya China, militarization, migogoro ya kimipaka na kujitanua katika eneo la Asia-Pacific na vitisho dhidi ya Ufilipino.

Nchi zote (G7) zimekubaliana kwamba zitafikisha ujumbe huo kwa uwazi katika ngazi ya juu kabisa kwa taifa la China.

Je, ni nani anayeipa G7 mamlaka ya kuamuru lililo sawa au lisilo sahihi?
Katika bandiko lako, sijaona popote ambapo G7 "imeamuru".
 
China ata ufyata tu ni swala la muda tu.
China ataufyata kwa Kosa lao ni lipi?

Wamesahau kwamba wao ndio walipigia chapuo soko huria?

Walijua watatawala milele?

Hawataki kukubali mabadiliko?
Haya wanayofanyiwa na china Sasa hivi,ndiyo walitufanyia sisi third world na hao wachina,tulilalamika sana wakatudharu sana,Sasa kibao kimegeuka wanaanza kulialia.

Wao ndio waasisi wa free market wache nguvu ya soko ndio iamue bei,wao wabaki na mavitu Yao ya Bei kubwa.

Hawa viumbe walidhani Dunia hii ni Mali Yao.
Wakati wachina walipokua wakomunist waliwapiga vita Kali,Leo wamekua sio wakomunist pia wanawapiga vita.
Sasa wachina wafanyeje?

Wana wivu sana Hawa wazungu,muda wao wa kutesa umekwisha wakubali TU mabadiliko,Dunia ndivyo ilivyo.
 
Wao walivyotawala kipindi Cha ukoloni mbona China ilikaa kimya.
Huu mwaka ni kuwafosi. Kule Hamas,Hezbola, Houthis Iran Vs Us &Israel huku China &Singapore war hapo hapo Eastern Europe moto unawaka na Caribbean kumeanza kuchangamka dunianimrkuwa ya moto kidogo hakika 2024 ni remarkable year
Je, sasa ni wakati wa new world order free from western domination?
 
China iendelee hivyohivyo kama inavyofanya sasa hivi, isikubali kurudishwa nyuma
Dawa ya nchi za Magharibi hasa Marekani ni kwenda nao kibabe usikae kinyonge

Ukiwa mnyonge Marekani itakufanyia kama walivyoifanya Japan miaka ya 1980 kwenye Plaza Accord Agreement wakati Japan ilipokuwa mshindani mkuu wa Marekani ilipotawala kwenye soko la dunia na kutishia US tech hegemony

 
Ila kwenye nukta ya South China sea. China nayo iache ubabe, nchi moja huwezi kujipa miliki ya bahari eti yote yako kisa eti wafalme wako miaka 1000 iliyopita walipeleka ngalawa huko!
Je, madai yao ni ya kweli au ni uchokozi? Mbona Marekani ana kambi za kijeshi nyingi sana hapo Filipino

Kati ya Marekani na China ni nani hasa anafanya expansionism kwenye Asia-Pacific

Marekani imekuwa ikifinya joint drills na baadhi ya mataifa ya Asia-Pacific na kuleta meli vita na manowari mpaka kwenye mpaka wa kimataifa wa China wa baharini

Je, ni nani mchokozi?
 
Back
Top Bottom