Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Vita vya Kagera 1979: Kwanini Jeshi letu lilipitia mipaka ya Sudan badala ya kukatiza hapo kati kufika Kampala?

Kiongozi kuna sehem umeongelea "Bato ya Lukaya"

Kuna sehem inaitwa "umulwekubyo" (Kona)

Hii "bato" wanasema ndo ilimaliza vita...

1. Mapambano ya Lukaya yaliendeleaa kwa muda gani....?

2. Inasemekan hapa Amin alipoteza Askari wengi hadi kufika 300 au 400 wakiwemo walibya zaidi ya 100 na wengne kutekwa
Katika mazingira ya vita nyie mnajickiaje kuona askari zaidi ya 300 wamelala..?

3. Kama ulishiriki hii "bato" unaweza tueleza nn ilkuwa "failure" ya waganda hapa kiasi cha kupotea wengi kiasi ikii....?

4. Vita uwa ina mengi je ni kweli uko frontline kuna makafara na matambiko yalikuwepo msitunii....??

5. Kuna mahali nilisoma kuwa Kamanda Nshimanyi alkula "ambush" ambayo ilimcost askari 25~35, nn ilkuwa tatzo...??

6. Ulikuwa chini ya Kamanda yupi na katika platoon ako au battalion ako...? Unakumbk "great loss" kwen ilkuwa kupoteza askari wangap katika pambano moja

Asantee

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi sikwenda frontline; nilikuwa Communications Makao Makuu ya Brigade ya Magharibi (wakati huo) kama sehemu ya askari wa akiba tuliokuwa mobilized kwa ajili ya vita; ina fact mobilization ilianza kabla hata Nyerere hajatoa ile hotuba yake ya "uwezo tunao"

Baada ya vikosi vyetu kufika pale na kuteka ile kambi ya Mbarara, mapigano direct ya Lukaya yaliendelea usiku na mchana kwa kama siku tatu hivi; ila hiyo ndiyo yaliyoua watu wengi sana huenda kuliko mapigano mengine yoyote katika vita ile. Tatizo kubwa la mapigano ya Lukaya ilikuwa ni kwa vile walipigania kwenye matope 24 hours.

Failure ya waganda ni kuwa jeshi letu liliwaelemea kwa kila kitu; watu wanaweza kuja na sababu mbalimbali lakini jeshi letu lilikuwa imara sana kuliko wao. Tuliwabana mbavu sana

Askari kupigwa ambush na kuuwawa vitani ni jambo la kawaida kabisa; ningeomba lisitiliwe mkazo sana kama failure ya huyo Kanali Nshimanyi ingawa sina kumbukumbu zake.
 
Kiongozi kuna sehem umeongelea "Bato ya Lukaya"

Kuna sehem inaitwa "umulwekubyo" (Kona)

Hii "bato" wanasema ndo ilimaliza vita...

1. Mapambano ya Lukaya yaliendeleaa kwa muda gani....?

2. Inasemekan hapa Amin alipoteza Askari wengi hadi kufika 300 au 400 wakiwemo walibya zaidi ya 100 na wengne kutekwa
Katika mazingira ya vita nyie mnajickiaje kuona askari zaidi ya 300 wamelala..?

3. Kama ulishiriki hii "bato" unaweza tueleza nn ilkuwa "failure" ya waganda hapa kiasi cha kupotea wengi kiasi ikii....?

4. Vita uwa ina mengi je ni kweli uko frontline kuna makafara na matambiko yalikuwepo msitunii....??

5. Kuna mahali nilisoma kuwa Kamanda Nshimanyi alkula "ambush" ambayo ilimcost askari 25~35, nn ilkuwa tatzo...??

6. Ulikuwa chini ya Kamanda yupi na katika platoon ako au battalion ako...? Unakumbk "great loss" kwen ilkuwa kupoteza askari wangap katika pambano moja

Asantee

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijajua maswali haya unamuuliza nani nikijua itapendeza zaidi!!!
 
Mimi sikwenda frontline; nilikuwa Communications Makao Makuu ya Brigade ya Magharibi (wakati huo) kama sehemu ya askari wa akiba tuliokuwa mobilized kwa ajili ya vita; ina fact mobilization ilianza kabla hata Nyerere hajatoa ile hotuba yake ya "uwezo tunao"

Baada ya vikosi vyetu kufika pale ma kuteka ile kambi ya Mbarara, mapigano direct ya Lukaya yaliendelea usuku na mchana kwa kama siku tatu hivi; ila hiyo ndiyo iliyoua watu wengi sana huenda kuliko mapigano mengine yoyote katika vita ile. Tatizo kubwa la mapigano ya Lukaya ilikuwa ni kwa vile wanapigania kwenye matope 24 hours.
Kuna sehemu humu JF Historia yangu ya vita vya Kagera nilielezea kwa kirefu kuhusu KIPIGO CHA LUKAYA ikumbukwa pale Lukaya ilikuwa ni AMBUSH kwa maana pale tuliweka mtego wa kuvizia na kwa bahati nzuri waliingia mkenge na kupata kipigo cha mbwa koko!!Na si kweli kuwa mapigano ya hapo Lukaya yaliendelea usiku na mchana kwa siku tatu hiyo ilikuwa AMBUSH tu kwa lugha rahisi yalikuwa mapigano ya kushitukiza!!!.
 


Yaani jirani yako akija nyumbani kwako na kumbaka mke wako mbele yako utasema hakuna haja ya kumpigania mke wako? Nachukulia kama wewe ni mtoto wa kiume. Iwapo vita ile haikuwa na ulazima, basi hatuna haja ya kuwa na JWTZ tena
 
Mkuu pia niliwahi kusikia kwamba Ghadaffi alipeleka wanajeshi wake na vifaa vya kivita Uganda zikiwemo ndege za kivita baada ya Amin kuelemewa na kumuomba msaada. Hao pia walipata kipigo kitakatifu na wengi kutekwa lakini Mwalimu akawaachia huru na kuwarudisha kwao baada ya vita kuisha.

Hii ni mentality ya kutokujiamini tu, kudhani kuwa sisi ni inferior kwa kila kitu. Vile vile ni kutokuelewa historia halisi

Elewa kuwa jeshi la Uganda wakati huo lilikuwa chini ya Amini, siyo kuwa Jeshi lilikuwa limegawanyika. Chanzo kikubwa cha kuelekea Amin kumpindua Obote ni kwa vile alikuwa anasuka jeshi kuwa lake na kuwa ana-sideline wasiokuwa wafuasi wake kwa kutumia hela za serikali, na Obote alipomtaka aeleze matumizi ya hela za jeshi ndipo akaamua kumpindua. Ni kikundi kidogo kilichokuwa kimebaki upande wa Obote ambacho ndicho kilikimbilia Tanzania kikiongozwa na akina Oyite Ojok na Tito Okello ambacho kiliitegemea sana Tanzania kwa miaka yote minane ya utawala wa Amini; kilikuwa hakifiki hata batallion moja. Baada ya kuangushwa kwa Amini na jeshi lote la Uganda kuvunjwa na TPDF, ndipo UPDF ilipoanzishwa na kufundishwa na TPDF, unaweza kuona hata jina lenyewe. Mvutano wa madaraka uliotokea ndani ya Uganda baada ya Amini kuwa amsheaangushwa na jeshi letu kuwa limesharudi nyumbani ndio uliosababisha Museveni aanzishe jeshi lake la msituni NRA ikiwa ni mwaka 1983. Museveni mwenyewe alipandikizwa kutokea Tanzania; wengine ni kama Dani Wadada Nabudere ambaye alikuwa anafundisha UDSM kabla ya vita.

Hata kama unaidharau Tanzania, kubali kuwa TPDF ilikuwa jeshi imara sana wakati huo. Kumbuka lilikuwa limeshapitia mapigano mabalimbali kusini mwa Afrika kwa hivyo lilikuwa na experience kubwa sana kuliko jeshi lolote Afrika ya Mashariki.
 
Mkuu pia niliwahi kusikia kwamba Ghadaffi alipeleka wanajeshi wake na vifaa vya kivita Uganda zikiwemo ndege za kivita baada ya Amin kuelemewa na kumuomba msaada. Hao pia walipata kipigo kitakatifu na wengi kutekwa lakini Mwalimu akawaachia huru na kuwarudisha kwao baada ya vita kuisha.
In fact walibya wengi sana waliuwawa na wengine walitekwa; Nyerere akaamuru wale mateka warudishwe kwao libya salama. Ghadaffi akatoa saluti kwa Nyerere.
 
Kichuguu Unaweza kuwa unakumbuka kosa jingine la kutaka kupeleka battalion msitari wa mbele bila tahadhari. Aliyetaka kufanya hivyo ni commander mmoja aliyeitwa Mlay. Nyerere alikuja kumkemea sana na kumwambia Mlay unataka kuua watu?
 
Yaliyodnikwa kwenye article uliyokwoti hapa yana sehemu kubwa kupikwa tu, kwa mfano ni kuwa kati ya jambo ambalo Nyerere aliilaumu sana OAU ni kule kushindwa kumkemea Amin; Nyerere alilalamaika sana kwa nini OAU wasimkemee tu. Halafu hilo la msumbiji kama nilivyosema hapo juu sina uhakika nalo, kwani halikuwa kwenye circles za mimi kujua labda kama Echolima aliyekuwa frontline analijua, mimi sikuwa frontline. Ila vile vile inawezekana ni vivyo hivyo taarifa za kupikwa tu. Baada ya mobilization ya Mgambo, Polisi, Magereza na JKT; jeshi letu lilikuwa kubwa sana karibu mara mbili ya jeshi Uganda ndiyo maana nina wasiwasi sana kuhusu kupata msaada wa Askari kutoka Musumbiji. Labda wanazungumza askari wa Tanzania waliokuwa Musumbiji wakati huo walirudishwa nyumbani; lakini bado niko open. Kuna general mmoja wa Amini wakati huo baada ya vita aliwahi kuhojiwa na kunyesha jinsi Jeshi la Tanzania lilivyopanuka kwa muda mfupi sana kulingana na Intelligene walizokuwa wanapata. Siku nikiipata tena article ya interview hiyo nitaileta hapa

2429329_Screenshot_2020-06-15-22-04-28-1.png
Si kweli kuwa Tanzania was caught unprepared for war nchi yetu ilikuwa imejiandaa vya kutosha ndiyo maana kuanzia 1977 na 1978 vijana wengi sana walichukuliwa na kuajiriwa kwenye kambi mbalimbali za Jeshi waliokuwepo enzi hizo wanaweza kukiri hilo.Kuhusiana na Msumbiji kutuma vikosi vyake kuja kusaidia katika vita vya kagera hiyo si kweli lakini kwa Mwandishi wa habari hiyo alikuwa yuko sahihi kwa juujuu tu.Ukweli ni kuwa sisi kama Tanzania tulikuwa na wanajeshi wetu huko Msumbiji walikuwepo huko kusaidia Ukombozi wa msumbiji na baada ya kupata uhuru waliendelea kubaki huko kusaidia Jeshi la FLELIMO kujenga nchi yao baada ya kutokea vita vya kagera ilibidi wanajeshi wetu warudi kusaidiana na wenzao ambao tuliokuwa nyumbani na ni kweli tulikuwa tunawahitaji sana hasa kuutumia uzoefu wao katika medani ya vita.Na mimi binafsi katika kikosi changu nilikuwa nao wanajeshi waliotoka msumbiji tulipigana nao bega kwa bega mpaka mwisho.Kwa hiyo kwa mtu wa nje anaweza kusema tulipata msaada kutoka msumbiji lakini kiukweli wale walikuwa wanajeshi wetu ambao walienda kusaidia mapambano ya Ukombozi wa msumbiji.Na huo ndiyo ukweli!!!
 
Kichuguu Unaweza kuwa unakumbuka kosa jingine la kutaka kupeleka battalion msitari wa mbele bila tahadhari. Aliyetaka kufanya hivyo ni commander mmoja aliyeitwa Mlay. Nyerere alikuja kumkemea sana na kumwambia Mlay unataka kuua watu?
Kabla vita haijaaza baada kuvamiwa, amri zilitoka kwa Yusuf Himid aliyekuwa brigade commander wetu (Magharibi); kwa hiyo inawezekan yule kanali alikuwa anatekeleza amri halali ya brigedia simkumbuki tena. Kumbukumbu zangu za makanali wengi ni ndogo sana sasa hivi labda kwa sababu walikuwa wengi, ninajua zaidi matendo ya Mabrigadier na mameja General na makanali wachache waliongara tu, kama Ben Msuya kwani ndiye aliyeiteka Kampala na akang'ara sana; Lupogo na Kitete- yes huyu ndiye aliyekuwa chief tactician kabla hajapanda kuwa brigadier na kuongoza brigade mojawapo kwenye frontline; huko nyuma niliandika Lupogo lakini tactician alikuwa Kitete.
 
Kwa taarifa yako majeshi ya Uganda yalikuwa vizuri sana kabla ya uasi.

Vita ilipoanza tulipoteza wanajeshi wengi mno japo taarifa zilifichwa, binamu yangu amepigana na amesimulia mengi mno ambayo serikali haikuweka na haitaweka wazi.

Hivyo unaposema kwani tulizunguka, unafikiri hao jamaa walikuwa dhaifu kiasi hicho?

Vita ina mbinu nyingi, moja wapo ni kumzunguka adui wakati yeye anapambana na wale waliom face... ghafla snashangaa anashambuliwa eneo ambalo asikutegemea.


Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa kama binam yako alipigana mbona yeye hakufa kama hao wengine,tatizo alikufunga kamba umuone na yeye mwamba kumbe alikuwa anashinda camp akipanga panga silaha hakuna hata siku moja ameenda kwenye uwanja wa vita kujua kinachoendelea.

Unasemaje wamekufa watu wengi serikali ikaficha hali ya kuwa wote tunajua vita haina macho yeyote na idadi yoyote wanaweza kufa kwanini ifichwe?
 
Kabla vita haijaaza baada kuvamiwa, amri zilitoka kwa Yusuf Himid aliyekuwa brigade commander wetu (Magharibi); kwa hiyo inawezekan yule kanali alikuwa anatekeleza amri halali ya brigedia simkumbuki tena. Kumbukumbu zangu za makanali wengi ni ndogo sana sasa hivi labda kwa sababu walikuwa wengi, ninajua zaidi matendo ya Mabrigadier na mameja General na makanali wachache waliongara tu, kama Ben Msuya kwani ndiye aliyeiteka Kampala na akang'ara sana; Lupogo na Kitete- yes huyu ndiye aliyekuwa chief tactician kabla hajapanda kuwa brigadier na kuongoza brigade mojawapo kwenye frontline; huko nyuma niliandika Lupogo lakini tactician alikuwa Kitete.
Mkuu unaamini wakati wa vita ya Kagera tulikuwa na viongozi wachawi? Makanali, brigadiers, major generals, etc.,?
 
Sasa kama binam yako alipigana mbona yeye hakufa kama hao wengine,tatizo alikufunga kamba umuone na yeye mwamba kumbe alikuwa anashinda camp akipanga panga silaha hakuna hata siku moja ameenda kwenye uwanja wa vita kujua kinachoendelea.

Unasemaje wamekufa watu wengi serikali ikaficha hali ya kuwa wote tunajua vita haina macho yeyote na idadi yoyote wanaweza kufa kwanini ifichwe?
Unaweza kuta alikuwa mfagizi hata zilipokuwa silaha haruhusiwi hata kusogelea.
 
Mkuu unaamini wakati wa vita ya Kagera tulikuwa na viongozi wachawi? Makanali, brigadiers, major generals, etc.,?
hapana; kuna stori nyingi za kupikwa mitaani. Kuna watu waliwahi kusema Brigadier Mayunga alikuwa ana uchawi fulani kwamba alikuwa anaweza kuingia kwenye vikosi vya maadui bila kuonekana, lakini hizo zote ni conspiracy theories tu. Siyo kweli
 
hapana; kuna stori nyingi za kupikwa mitaani. Kuna watu waliwahi kusema Brigadier Mayunga alikuwa ana uchawi fulani kwamba alikuwa anaweza kuingia kwenye vikosi vya maadui bila kuonekana, lakini hizo zote ni conspiracy theories tu. Siyo kweli
Lakini Mayunga hakuwa na mambo yanayotia shaka wakati wa vita? Yaani yasiyokuwa ya kawaida?
 
Mkuu Kichuguu shukrani kwa kumbukumbu nzuri post #12 na #14,watoto wadogo wanajazwa ujinga na story za kuunga unga kutoka kwa watu ambao hata hawajui bunduki inashikwaje.

Mimi ni kizazi baada ya hii vita early 80s but siwezi kukaa kubishana eti “walikufa watu wengi sana” nani asiyejuwa vita ni kifo?huyo mzazi mwenyewe anamruhusu mwanae kwenda jeshini kichwani akijua muda wowote ataletewa badge yake kwamba mwanao kumbukumbu yake hii hapa kuwaje tukatae watu kufa,je hao Uganda ndo walipoteza watu wachache sana?vita tulishinda hatukushinda hiyo ndo habari ila kwamba watu walikufa wangapi siyo habari waliifia nchi na wanaenziwa.
 
Back
Top Bottom