Vita vya Syria vina mchanganyiko sana, ila dikteta Assad ni uovu wenye afadhali (lesser evil) kuliko waasi Wanajihadi

Cha kushangaza zaidi nchi zetu zina amani ila hatuzipi maendeleo hizo nchi za kiarabu zenye vita kila siku
 
Ndio swali langu lilipo hapo mkuu.
Hao Mabikra 70 na ushee sijui wataanza kutoa penzi kwa Sunni au kwa Shia au watawagawana?! Kwakweli maswali ni mengi sana kuliko hata majibu.

Kwasababu Magaidi yanavyouwana huko Syria na mengine yanazidi kuongezeka kutokea Lebanon Iraq na Iran mpaka sasa vifo ni 1000+
 
Waasi wameshindwa kuuteka Mji wa Hama wamekumbana na upinzani mkali kutoka kwa Majeshi la Syria Arab Republic +Russia+Hezbola+ Shia Millitias.

Je hii offensive ya Waasi ndio imefikia mwisho?! Je wataanza kurudishwa nyuma?! Yetu macho na Popcorns 🍿 na Bia bariidi.
 
Ina maana Hezbollah na wanamgambo kutoka Iran ndio wanaopigana badala ya jeshi la Syria ?.

...Sasa wafadhili wake wote wana hali ngumu, Assad atakiona cha moto.
 
Sunni hakuna mgawanyiko! Sunni inaundwa na ncha 4.

Hizi ncha zinaitwa madheheb, ndipo kuna Hanafi, Hanbali, Maliki na Shafii.

Hakuna mahali popote ukasikia hayo madheheb yamegombana, hakuna!
Tanzania na ukanda wa Afrika mashariki kwa ukubwa ni madheheb ya Shafii. Madheheb yaliyobakia ni yana wafuasi wachache kama shia, ibadhi n.k na hatujawahi kusikia hata siku moja wakigombana.

Sufi siyo dheheb, sufi ni mojawapo katika matawi ya elimu mtu anaamua kushughulika nayo! Wanasema sheria ni timilifu la kiwiliwili, Sufi ni timilifu la kiroho. Kwenye usufi wapo madheheb ya Shafii, Hanbali, Hanafi na Maliki. Wote utawakuta humo. Hilo ni tawi la elimu la tazkiya (elimu ya kuitakasa nafsi).

Kwenye usufi kuna madheheb napo!
Kuna Shisti, Naqshibandi, Sahrawardii, Qadir, Shadhalii n.k

Mtu anaweza akawa sunni na asiwe kwenye usufi n.k

Wahabi ndiyo Salafi na ndiyo Answar Sunna. Hayo majina yote yanawakilisha dhehebu moja Siyo dhehebu tofauti.

Hili dheheb lipo tofauti na madheheb yote ya juu niliyoyaorodhesha. Hili dheheb linapingana na madheheb yote ya hapo juu kwa namna yake. Na madheheb ya hapo juu yanapingana na Salafi au wahab kwa namna yao pia.

Kupingana kwao ni kielimu si kimapigano ya kimwili.

Na salafi au wahab wamegawanyika! Wapo ambao wenye msimamo mkali sana na wapo ambao wapo safi hawana matatizo yoyote kwenye jamii.

Tanzania na ukanda wa Afrika mashariki wengi wao ni Sunni madheheb ya Shafii, ambapo humo kwenye Usunni wapo ambao wanaofuata sufi.

Madheheb mengine ni Shia, Ibadh Wahab/Salaf n.k
 
Hicho kinchofanywa na makundi kama HTS huko Syria kinafaa kuitwa Jihad?

Au ni vita vya wenyewe kwa wenyewe kutokana na mgogoro wa kisiasa uliovalishwa vazi la kidini Ili kuvutia waumini kushika silaha ?
 
Waasi wa Kisunni wamelivamia Gereza kuu la Aleppo na kuwafungulia Wanamgambo wa ISIS waliokuwa wamefungwa hapo.

Vita inazidi kuchukua mkondo wa Kigaidi.
 
Hicho kinchofanywa na makundi kama HTS huko Syria kinafaa kuitwa Jihad?

Au ni vita vya wenyewe kwa wenyewe kutokana na mgogoro wa kisiasa uliovalishwa vazi la kidini Ili kuvutia waumini kushika silaha ?
Sio jihadi na ndio point yangu hii, HTS walikua wanaitwa Al Nusra Aka Al Qaeda, sijawahi maisha yangu kusikia Ulamaa yoyote wa Kiisilamu akitoa Fatwa kwamba Al Qaeda Wanapigana Jihadi. Na hata ukiangalia matendo yao hayaendani na Uisilamu bali ni Exactly matendo Yaliyofanywa na wakoloni ambayo kila siku tunaimbishwa kwenye Somo la Historia, Divide and Conquer.
 
Huwezi kusikia Ulamaa yeyote akisema hadharani kwamba Al Nusra au Al-Shabaab wanapigana jihadi ya haki kwa sababu atawekwa kwenye us terror watch list na maisha yake yatakuwa magumu sana.
 
Huwezi kusikia Ulamaa yeyote akisema hadharani kwamba Al Nusra au Al-Shabaab wanapigana jihadi ya haki kwa sababu atawekwa kwenye us terror watch list na maisha yake yatakuwa magumu sana.
UNAFKIRI Maulamaa they even care about USA? Pengine hata hujui Ulamaa ni nini, mtu akishafikia hio level maisha ya Dunia hana tena.

Hapo Saudi kuna Scholars wapo Against government hadi wanauliwa they even don't care na bado wanasema ukweli, hayo mambo ya kuwa dubbed terrorist na government ni ya kwenu, kwa Mtu level ya Scholar haya wezi mtingisha imani

Kwenye uisilamu hakuna Kumung'unya maneno kama ni kweli ni kweli kama so kweli bali si kweli.

Na kuna sehemu kibao dunia ya sasa Mathalan kama Palestina scholars kadhaa wanakubali ile ni Jihadi, so sio suala la kuogopa ama kutoogopa bali ni suala la ukweli na haki na uovu.
 
Hayawi hayawi sasa yamekuwa Jamii ya Wakristo imeanza kuchinjwa huko Idlib hawa Waasi wa Kisunni ni Magaidi wa ISIS walichobadilisha ni jina tu.
 
Hayawi hayawi sasa yamekuwa Jamii ya Wakristo imeanza kuchinjwa huko Idlib hawa Waasi wa Kisunni ni Magaidi wa ISIS walichobadilisha ni jina tu.
Mbona hueleweki? Au umeamua kujifyatua. Mara unamnanga Asad na kuwasifia Waasi na Israel. Mbona kama lishoga jipya mtaani.
 
Mbona hueleweki? Au umeamua kujifyatua. Mara unamnanga Asad na kuwasifia Waasi na Israel. Mbona kama lishoga jipya mtaani.
Mimi naongelea mgogoro wa Syria kama ulivyo, lakini inavyoonekana hao Waasi wa Kisunni hawajaacha mbinu zao za kigaidi ambazo mwanzo walisema wameachana nazo na kuzihakikishia Jamii za Minorities Wakristo Druze nk. Kuwa hawatazivamia na kuwachinja.

Lakini sio kweli kuna taarifa kuwa huko Idlib Jamii za Kikristo zimeanza kuuwawa na Waasi.
 
Ndege za Kivita za Marekani A10 'Warthog' zimeanza kuwasaidia Waasi karibia na Mji wa Deir Ez Zor.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…