Vita ya Corona: Nahodha wetu katelekeza chombo Baharini, tutaponaje?

Vita ya Corona: Nahodha wetu katelekeza chombo Baharini, tutaponaje?

Wetu Mimi na nani?Hivi mkiulizwa mnaongoza nchi huku mmefumba macho utasemaje?
Kwa taarifa yako Mimi ni abiria wa chombo kinachoenda mrama kwa sababu Nahodha kajitosa,hayo ya Mh.Lissu ni hoja nyingine.
Acha ramli,tusaidiane kumrejesha Nahodha wetu.Kama hataki kazi tuliyompatia atujulishe rasmi tumtafute Nahodha wa ukweli.
Ni bora hats asingekiondoa chombo Bandarini 2015 kama alikuwa anajifahamu yeye mawimbi hayamudu.
Sina uhakika kama safari ya nchi ya ahadi tutafika maana duuu
 
Kweli wewe Ni mzushi unafikiri raisi ni kama vyicheo vyenu vya pale ufipa kutengua na kuteua Ni uamuzi wake atakapo ona msaidizi yupi atenguliwe yupi ateuliwe kumbe kwako ni big ishu ungedili Kwanza na matatizo ya Sacco's yenu ingekuwa Bora zaidi SUMU HAIONJWI KWA MDOMO
Watanzania wanaangamia kwa Corona wewe unahamasisha habari za CDM?Msiwatoe watu kwenye reli,tuambie tuanze lini Partial/Total Lockdown kama nchi?
Mliidharau Corona na kuifananisha na Malaria,ajali,Ebola na mapambio kuwa ni ka.Corona sasa mnajificha?Mnasisitiza maombi,nani kawaambia Virusi vinadhibitiwa kwa ibada?Hizi ibada tungeendelea kuzifanyia majumbani maana haikosi kina walioambukizwa katika siku tatu za maombi.
Mikusanyiko ingekuwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya tu.Wengine wote wangeenda majumbani kipindi tunafunga shule na vyuo,Bunge lisingekutana na hats mahabusu wanaodhaminika wangeachiliwa.
Ila kwa sababu za kizembe,Watanzania bado wanatengenezewa mazingira ya mikusanyiko kwa visingizio hafifu kama uchumi kuyumba,mtakufa njaa nk.
Corona inavyosambaa kwa kasi hii,tutajengaje huo uchumi?Twendeni lockdown, tupime Corona kwa watu wote,tuongeze motisha na risk allowances na special insurance policy kwa watakaopata corona kazini kwa watumishi wa afya,askari magereza,uhamiaji na polisi nk.
Corona siyo kacorana tujipange kikamilifu,tushikamane Watanzania wote na Nahodha wetu arudi kuongoza mapambano.
 
Yupo lockdown watanzania chapeni kazi chukueni tahadhali mzingatie maelekezo ya wataalam wa afya! Nadhan kauli Kama hii ukiidadavua kwaa umakini huna haja ya kulialia mzee yupo wapi yeye kashachukua tahadhali wewe je! Kazi ni kwako

Sent using Jamii Forums mobile app

"The Epitime Of Cowardliness' kumbe Ansbert anamjuwa hasa .....mtu hata mijadala ya wazi ,mihadhara , na maandamano anaogopa .....itakuwa VITA ???
 
Mbona kabla ya korona kila siku alionekana kwenye tv akizindua miradi je sasa hiv anaogopa haka kamafua😆😆😆😆
 
Umesema Viongozi Wakuu kwani Waziri Mkuu Majaliwa siyo Kiongozi Mkuu?
Kuna mkuu zaidi yake. Na huyo ndiye haswa ana wajibu huu. Tumeona dunia nzima hao wakuu wakifanya kwa vitendo kuonyesha wanajali maisha ya 'waajiri' wao.
 
Leo nimependa kuuliza hili swali kwasababu ya haya yanayoendelea. Nchi ipo kwenye tension kubwa lakini hatuoni hatua madhubuti (tangible) zikichuliwa na Rais kama kiongozi mkuu na Amiri jeshi mkuu.

Naona Marais wa nchi nyingine wakitoa taarifa kwa umma kuhusu mikakati inayochukuliwa kuepuka au kudhibiti janga hili la corona na jinsi hali halisi ilivyo.

Ikumbukwe pia kuwa Rais ni Comforter in Chief. Sasa kama hatimizi haya na mengine kuna uhalali gani wa kuendelea nae?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Leo nimependa kuuliza hili swali kwasababu ya haya yanayoendelea. Nchi ipo kwenye tension kubwa lakini hatuoni hatua madhubuti (tangible) zikichuliwa na Rais kama kiongozi mkuu na Amiri jeshi mkuu.

Naona Marais wa nchi nyingine wakitoa taarifa kwa umma kuhusu mikakati inayochukuliwa kuepuka au kudhibiti janga hili la corona na jinsi hali halisi ilivyo.

Ikumbukwe pia kuwa Rais ni Comforter in Chief. Sasa kama hatimizi haya na mengine kuna uhalali gani wa kuendelea nae?

Sent using Jamii Forums mobile app

Nikielimishwa zaidi kuhusu neno Kujificha na maana yake nitarudi Kuchangia ila ninachokijua Rais Dkt. Magufuli hajajificha.
 
Kajamaa ni kapuuzi sana,kwenda kujificha huko ndichi.
 
Tanzania imekua na viongozi kadhaa,

Lakini viongozi hawa wakati wa majanga/vita siku zote walikua na watu wao wakiwapa moyo na kuwajulisha nini kinaendelea au nini mpango wetu tuliyo nao kama taifa!!

Nyerere alikua mstari wa mbele kuongoza majeshi yetu kumtoa iddi amini kagera na hakujificha mafichoni!!

Lakini kwa sasa tuna janga, tuko vitani lakini kiongozi wetu hatumuoni! Mbaya zaidi ameondoka kabisa "kagera" ya korona yaani kawaacha watu wake wapambane yeye hatujui alipo!!

Marais wa mataifa wengine kila siku wanatoa updates na kuwapa moyo wananchi wao sisi huku naona mambo ni tofauti!!

Nauliza je KIONGOZI wetu yuko wapi? kwanini katuacha wakati tuko vitani?
 
Yupo Mkuu ,ila ni kama ametufikishia kale ka 'Ujumbe wa kila mmoja na aubebe Mzigo wake mwenyewe.
 
Back
Top Bottom