Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nilikupa ushauri tu dadaMie haziwezi kupitiliza kama zinazopitiliza zako na za mkeo mana wote mnapitiamo umo umo so mme na mke haijulikani ni yupi
Sio kweli huo ni mtazamo wako usio na ushahidiUnafahamu kuwa bila lockdown Ulaya na Marekani vifo vingekuwa mara 2 ya idadi ya sasa?
UK coronavirus LIVE: Covid-19 death toll could be 40% higher than reported as experts warn rush to ease lockdown 'could cause resurgence'Sio kweli huo ni mtazamo wako usio na ushahidi
Yaah hapa ni muhimu kila mtu kujikinga bila kusubili kuambiwa unakuta mtu anapiga kelele ya kua iwekwe lockdown lakin mda huo yupo mtaani hasa nae anasubili serikali iseme tutailamu serikal bure
Si kweli kwamba hakuna kinachofanyika labda wewe huoni wala husiki kwa hiyo huna habari na kinachofanyika kuhusu CoronaHapa naandika kwa majonzi kwa kusikia jinsi Watanzania wenzetu wanavyougua Corona na wengine kupoteza maisha.Poleni nyote.
Kinachoumiza zaidi ni namna baadhi yetu tunavyoteteana hata kunapokuwa na uzembe kwenye hatua zinazochukuliwa kutulinda na Corona.
Kuna wanaosema Nahodha wetu ni shujaa,mwenye uthubutu na tupo salama ilhali abiria tunaona hatari iliyopo mbele yetu.
Nahodha wetu tunaambiwa yupo mapumzikoni,je tukisema kajitosa baharini na kutuachia chombo kielee kwenda kuzama tunakosea?
Corona bila lockdown itatumaliza, ilikuwa Arusha, Dar na Zanzibar hatukuona haja ya lockdown eti tutakufa njaa. Sasa tuna wagonjwa mikoani na hakuna kinachoonekana kufanyika, hatujaamua bado kulock maeneo yenye wagonjwa.
Tunafahamu kuwa hakuna dawa, chanjo, vifaa tiba, maabara za uchunguzi na vifaa vya kujikinga hasa kwa watoa huduma za afya.
Tuamini kuwa tupo salama?Tuamini kuwa Nahodha hajajitosa na kuacha chombo katikati ya mawimbi makali?
Wanam miss kwa sababu amewavushwa kwenye janga la korona, vifo hakuna na kesi hakuna, kweli wamem miss.
Makosa yalitokea pindi tulipoufuta unyapara... lakini ifike wakati tukemeane vilivyo na elimu itolewe ipasavyo maana hata suala la kunawa ni kama bado halijaeleweka vemaLeo nilibahatika kupanda daladala jirani yangu alikuwa anakula, nikamwambia kwa ugonjwa huu wa corona siyo vizuri kula kwenye daladala 'tulikuwa kwenye kiti cha nyuma cha coaster' akasema sawa lakini bado aliendelea kula bagia zake hapa tunajifunza kwamba watu wengi hawana elimu ama nikuishi kwa mazoea