Vita ya kugombea mali za aliyekuwa Mchungaji, Marehemu Getrude Rwakatare sasa imeshika kasi

Vita ya kugombea mali za aliyekuwa Mchungaji, Marehemu Getrude Rwakatare sasa imeshika kasi

Watagombea hata hicho kidogo ulichokuwa nacho....

Mali zisizohamishika ni tatizo kubwa. Ni bora ziuzwe zooooote, watu wagawane kila mtu asepe.

Mimi mwenye ile shule ya St Marys Sinza lazima ningeitolea macho tu 😃😃😃😃
Kuna nyingine mwanza imeuzwa kimya kimya ikageuzwa chuo najua hapo wamepiga si chini ya 1.5 billion ...! Nouma sana
 
Kuna nyingine mwanza imeuzwa kimya kimya ikageuzwa chuo najua hapo wamepiga si chini ya 1.5 billion ...! Nouma sana
Am telling you.... ni bora kila kitu kiandikwe, kiuzwe.

Kuna familia naijua, mzee wao alifariki miaka ya mapema 2000; na wosia aliandika vizuri. Kila mtu akachukua chake, leo wameanza kutoleana macho, mmoja wao biashara aliyoachiwa ameendeleza vizuri, wenzie walivuruga zao. Wanakuja kusema wanaomba mgao wa mali za baba!
 
Mitoto haina akili. Inauza Mali badala ya kuendeleza? Badala wakae kikao na uthamini wa kila Mali ufanyike ili wajue jinsi ya kugawana na kulipa madeni bank wanaanza kuuza na kujimilikisha kinyemela. Muda mfupi Sana kila kitu kitapotea. Tupeni muda tu.
Hapo ndipo Wahindi na Waarabu wametuzidi.
 
Mmmm na Mimi nikadai sadaka yangu na zaka.......sipendi na Mimi dhuluma
 
Utajiri wa familia za kiafrika haudumu kwa generation zaidi ya 1

Na hapa ndipo wazungu, wahindi na Waarabu wanaptupiga gepu

Kila mara utasikia migogoro ya kugombea mali za tajiri mweusi mara Mengi, mara bilionea Msuya, Lwakatare, kuna yule Mrema wa Ngurdoto n.k

Ila ni mara chache sana kusikia tifu kama hizi kwa matajiri wa ki Asia au kizungu
Umeenda au kuishi Asia??
 
Waarabu wanawezaje? Sijawai sikia mgogoro wa waarab
Wanajipanga.Mzazi wala haandiki hata hisia

Ingekuwa waarabu watoto wote wangekaa kikao pamoja kujipanga namna ya kuendesha hizo mali.Wangechaguana mmoja awe mkurugenzi mtendaji ,mwingine wa utawala,mwingine wa fedha nk na kuziendesha hizo mali pamoja wakawa wanalipana mishahara kila mwezi na wanagawana faida mwisho wa mwaka

Lakini mitoto ya kiswahili pasua kichwa yaani mali zote zile zinasambaratika kwa muda mfupi .Muda si mrefu hao watoto wa Lwakatare watakuwa maskini wa kutupwa
 
Wazaz wanakomaa watoto waende shule tu huku shuleni wanafundishwa ubinafsi na uzungu. Wanasahau kuwafundisha utafutaji na misingi ya familia. Na kuwajengea upendo.
Kabisa
 
Mitoto haina akili. Inauza Mali badala ya kuendeleza? Badala wakae kikao na uthamini wa kila Mali ufanyike ili wajue jinsi ya kugawana na kulipa madeni bank wanaanza kuuza na kujimilikisha kinyemela. Muda mfupi Sana kila kitu kitapotea. Tupeni muda tu.
Hapo ndipo Wahindi na Waarabu wametuzidi.
Hakukuhitajika kugawana walitakiwa tu wajipange kwa pamoja jinsi ya kuzisimamia hizo biashara kwa pamoja,Madeni ni ya biashara hizo biashara zenyewe zingeyalipa vila shida kama wangesimamia na kuziendeleza vizuri kwa pamoja

Hata kama wao uwezo wa kuzisimamia hawana wangeajiri mkurugenzi mtendaji wa kuzisimamia wao wabaki kama wakurugenzi wa Board na wanasiasa

Kitendo cha kugawana hizo biashara na kugawana madeni ni kujitafutia umaskini tu.
 
Back
Top Bottom