Vita ya kugombea mali za aliyekuwa Mchungaji, Marehemu Getrude Rwakatare sasa imeshika kasi

Vita ya kugombea mali za aliyekuwa Mchungaji, Marehemu Getrude Rwakatare sasa imeshika kasi

Utajiri wa familia za kiafrika haudumu kwa generation zaidi ya 1

Na hapa ndipo wazungu, wahindi na Waarabu wanaptupiga gepu

Kila mara utasikia migogoro ya kugombea mali za tajiri mweusi mara Mengi, mara bilionea Msuya, Lwakatare, kuna yule Mrema wa Ngurdoto n.k

Ila ni mara chache sana kusikia tifu kama hizi kwa matajiri wa ki Asia au kizungu
Tuna kitu cha kujifunza.
Kwa mtizamo wangu;
1. Kw sababu pamoja na kusoma, inawezekana lengo moja wapo ni kusaka utajiri basi muda wote wa kusoma sharti watoto wajifunze kile baba/mzazi anachofanya
2. Kuna muda watoto kutokana na kuwa isolated na shughuli za mzazi, inawezekana wakawa hawana shughuli za kufanya wakitegemea wazazi wakienda mbele ya haki waanze kuvurugana. Ni vizuri mzazi kuhakikisha watoto wote wana kazi zao either ajira binafsi au kuajiriwa ila atleast wawili au mmoja wakawa/akawa included kwenye system ya biashara za familia kwa sababu haiwezekani watoto wote wakawa wafanyikazi au CEOs
3. Kugawa shares kwa kila mtoto (equally), kwa wale waliopo kwenye system wapewe mshahara wawe kwenye ajira kama wafanyikazi wengine kwenye biashara
4. Biashara za familia zirasimishwe kikatiba kifamilia ili kujua nini muundo wa biashara na namna familia inavyofungamana nayo na namna kizazi cha kwanza mpaka cha nne na kuendelea kimeainishwa kinavyonufaika (equally).
5. Familia ijikite zaidi katika mashauriano ya kifamilia katika jambo lolote linalotokea badala ya kujikita zaidi kwenye sheria katika kutafuta haki. Familia ikubaliane hasa kwenye utamaduni wa kutumia wazee maalumu wa kuwashauri katika mashauriano yoyote pale mgogoro unapotokea badala ya kukimbilia mahakamani, twaweza kujifunza kutoka uhindini na umasaini au ukuryani

NB: kwa uzoefu wangu, mtoto toka mdogo akiwa karibu na mzazi mzazi akimpa mwongozo wa kile anachofanya mtoto si rahisi kukengeuka japo inawezekana kwa kuzingatia mfano wa mwanamfalme wa uingereza.
 
VITA ya kugombea mali za aliyekuwa Mchungaji wa Kanisa la Assemblies of God - Mlima wa Moto, Marehemu Mchungaji Getrude Rwakatare sasa imeshika kasi huku ikizidi kuwagawa watoto wake.

Taarifa za kuwepo kwa vita hii zimekuja ikiwa ni miezi kadhaa baada ya mtoto mkubwa wa kiume wa Marehemu Rwakatare, anayefahamika kwa jina la Tibe Kenneth Rwakatare kumuandikia barua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, akimueleza jinsi ndugu zake wanavyokiuka sheria kwa kutenda makosa ya jinai, akiwatuhumu kughushi nyaraka za mauzo ya baadhi ya mali za marehemu mama yake, Mchungaji Rwakatare.

Tibe Kenneth Rwakatare aliandika barua hiyo Disemba 31, 2021 ikiwa na kichwa cha maneno kinachosomeka ‘mauzo batili plot no 259 Udindifu Bagamayo.’

Katika barua hiyo, Tibe aliandika kumweleza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa uuzwaji wa kiwanja hicho umehusisha nyaraka za kughushi pamoja na kutolipwa kwa kodi stahiki za Serikali.

Akithibitisha kuandika barua hiyo, Tibe aliiambia Tanzania PANORAMA Blog kuwa amedhulumiwa haki yake na ndugu zake hivyo hakuwa na jingine zaidi ya kuandika barua hiyo.

Wakili kiongozi wa Kampuni ya Uwakili ya Haki Kwanza Advocates, Alloyce Komba ambaye ametoa ufafanuzi kuhusu tuhuma zilizotolewa na Tibe dhidi ya ndugu zake, amesema adhabu itakayowakabili watuhumiwa wakibainika mahakamani kutenda jinai hiyo ni kifungo.

“Kosa la kughushi, adhabu yake iwapo mahakama ikimtia hatiani mtu kwa ushahidi usio na shaka yoyote ni kufungwa kwa mujibu wa kifungu cha 337 cha sheria ya kanuni za adhabu, sura ya 16 ya sheria za Tanzania, toleo la 2019.

“Mtu anapaswa kuripoti polisi kosa lolote la jinai linalofanywa na mtu yoyote ili mradi awe na ushahidi wa kutosha.

“Ni kosa pia kunyamazia kosa la jinai. Ndiyo maana mtu hukosa kwa kutenda (commission) au kutotenda (omission), mfano kutomzuia mtoto kutumbukia kisimani wakati unaona anacheza karibu na kisima,” alisema Wakili Komba.

Mwanasheria mwingine aliyezungumza na PANORAMA kwa sharti la jina lake kuhifadhiwa alisema tuhuma zilizotolewa na Tibe dhidi ya ndugu zake ni nzito na iwapo zitathibitika mahakamani hawatakwepa mkono wa sheria.

“Sheria zipo lakini inashangaza watu wanatenda makosa ya makusudi kama haya ambayo adhabu yake ni kali.

“Huyu anayewatuhumu wenzake naye hayuko salama kwa sababu ni wazi anajua vema jinsi ndugu zake walivyotenda hiyo jinai, walivyoghushi kwa sababu ni ndugu zake hivyo alipaswa kutoa taarifa polisi.

“Sasa inashangaza kijana msomi kukaa kimya huku akijua kuna jinai inafanyika. Kwa vile kalipeleka kwa waziri tumpe nafasi ya kulifanyia kazi,” alisema.

Kwa mujibu wa kifungu cha 338 cha sheria ya kanuni ya adhabu, sura ya 16 ya sheria za Tanzania, toleo la 2019 ambayo Tanzania PANORAMA Blog imeiperuzi inaeleza kuwa mtu akibainika mahakamani kwa kughushi wosia, hati za umiliki ardhi, hundi n.k adhabu yake ni kifungo cha maisha jela.

Hilo likiwa halijapoa, mtoto mwingine wa kiume wa Marehemu Mchungaji Rwakatare anayefahamika kwa jina la Muta Robert Rwakatare ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kawe kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) alizungumza na mwandishi wa Tanzania PANORAMA Blog na kumshutumu ndugu yake Tibe Kenneth Rwakatare kwa kutwaa kimabavu Shule ya Sekondari ya St. Mary’s International School, Dodoma Campus ambayo ni mali waliyoachiwa na marehemu mama yao.

Muta alieleza kuwa shule hiyo ni miongoni mwa shule zilizokuwa zikimilikiwa na Marehemu Mchungaji Rwakatare enzi za uhai wake lakini hivi sasa Tibe imeibadilisha jina na kutwaa umiliki wake.

Alisema ikiwa chini ya umiliki wa mama yao, ilikuwa ikijulikana kwa jina la St. Mary’s International School, Dodoma Campus, lakini sasa baada ya kubadilishwa jina inafahamika kwa jina la St. Mary’s Dodoma.

Muta alisema Tibe sasa anachukua mapato yote ya shule hiyo na eneo ilipojengwa nalo amelibadilisha jina na kuweka la kwake.

Watu walio karibu na familia hiyo wameeleza kuwa chanzo cha mzozo wa umiliki wa shule hiyo baada ya Marehemu Mchungaji Rwakatare kufariki ni mmoja wa watoto wake kuwazunguka wenzake na kuhamisha fedha zote zilizokuwa kwenye akaunti ya shule kwenda akaunti yake binafsi na pia akaanza kuchukua mapato yote ya shule hiyo.

Kwamba baada ya hilo kubainika, Tibe aliamua kuitwaa shule hiyo, akaibadilisha jina na majina ya akaunti za benki, hatua ambayo sasa inalalamikiwa na ndugu zake.

“Huyu ndugu yetu anashangaza sana kuanza kuandika barua kwa viongozi wa Serikali akitutuhumu kwa kukiuka sheria za nchi, eti tunaghushi nyaraka wakati yeye ndiyo bingwa wa kughushi nyaraka kuanzia Brela mpaka ardhi na anayemtumia kufanya hizo kazi za kughushi anafahamika, ni kijana aliyesoma kwenye moja ya shule zetu. Anachotaka amiliki yeye mali zote za mama.

“Ana madudu mengi mno lakini sie hatujishughulishi naye matokeo yake akiona tunamzuia kuchukua kila kitu anatafuta huruma nje ya familia kwa kutuchongea serikalini.

“Amejimilikisha shule ya Dodoma na kuibadili jina na akaunti za benki wakati shule hiyo ina mkopo wa benki moja kubwa nchini. Wewe unaweza kubadili umiliki wa mali ambayo ina mkopo wa benki kweli? Muulizeni na yeye hilo kalifanikishaje?

“Anamiliki mali nyingi sana za mama ambazo mapato yake yote yanaingia mfukoni mwake na hakuna anayemsumbua lakini yeye jambo dogo tu analalamika na kuandika barua huku na kule.

“Tulipouza hizo ardhi nyingine na kugawana mbona hakusema lolote? Kamuulizeni anataka nini hasa maana shule aliyotupora baada ya kuibadilisha jina imeondolewa kwenye orodha ya mali za marehemu mama. Hivi sasa anaimiliki yeye bila ridhaa ya sisi ndugu wengine.

“Nyumba za kupangisha za marehemu mama, zile ‘Appartments’ za Tabata zaidi ya 25, vyumba vya biashara 20, kote anachukua kodi yeye na pia mgodi wa dhahabu Chunya nao kachukua lakini bado anatupiga vita,” alisema Muta.

Alipoulizwa Tibe kuhusiana na madai hayo alisema hana muda wa kuyazungumzia.

Tanzania PANORAMA inaendelea kumtafuta Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ili kulizungumzia hilo.


Source: Tanzania-Panorama
Huyo Tibe ni mbinafsi SANA eti kiss mtoto wa kwanza ndo alizimishe Mali zote ziwe zake
 
hii dunia ukitafuta mali sana ni kama unaanzisha vita ya watoto baadae....cha muhimu ni kuandika urithi mapema
Mirathi inakuwa challenged mahakamani

Kuomba Mungu tu

Afrika kuna kitu kimejificha unakuta wazazi wengi wenye akili sana ziwe za darasani ,kutafuta mali nk huzaa mitoto haina akili.Mfano ni huyo marehemu Mama Rwakatare
 
Mama alikuwa na watoto wangapi? Je watoto wote hao ni kwa mwanaume mmoja ? kama ni mwanaume mmoja kwa nini wafikie hatua hii?

ni maswali tu ndugu zangu tukipata majibu yake pasi tunaweza kupata pa kuanzia.
 
Watoto ni Wanne na Wote Baba mmoja.
Mama alikuwa na watoto wangapi? Je watoto wote hao ni kwa mwanaume mmoja ? kama ni mwanaume mmoja kwa nini wafikie hatua hii?

ni maswali tu ndugu zangu tukipata majibu yake pasi tunaweza kupata pa kuanzia.
 
Hivi kweli mali zote hizo za mama bado unagombea udiwani kuna shida sio bure.

Udiwani una faida kubwa sana. Maana mkurugenzi wa manispaa uliyopo anakuwa rafiki yako. Uwekezaji wako unakuwa hausumbuliwi sumbuliwi na watu wa serikalini. Na pia kwenye ma viwanja yakigaiwa wewe unapewa tu kwa urahisi
 
Wenyewe waarabu wanamkabidhi m1 ndio kiongozi wao.

Huwa wanaanza mapema sana kuwafundisha watoto wao biashara. Unakuta mtoto mdogo yupo dukani na wazazi wake. Alishafika miaka 20 anajua karibu kila kitu jinsi ya kuendesha biashara.

Ukweli wanaamiana sana, hawadhulumiani kama sisi. Hata wasomali na Igbo wako hivyo.
 
VITA ya kugombea mali za aliyekuwa Mchungaji wa Kanisa la Assemblies of God - Mlima wa Moto, Marehemu Mchungaji Getrude Rwakatare sasa imeshika kasi huku ikizidi kuwagawa watoto wake.

Taarifa za kuwepo kwa vita hii zimekuja ikiwa ni miezi kadhaa baada ya mtoto mkubwa wa kiume wa Marehemu Rwakatare, anayefahamika kwa jina la Tibe Kenneth Rwakatare kumuandikia barua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, akimueleza jinsi ndugu zake wanavyokiuka sheria kwa kutenda makosa ya jinai, akiwatuhumu kughushi nyaraka za mauzo ya baadhi ya mali za marehemu mama yake, Mchungaji Rwakatare.

Tibe Kenneth Rwakatare aliandika barua hiyo Disemba 31, 2021 ikiwa na kichwa cha maneno kinachosomeka ‘mauzo batili plot no 259 Udindifu Bagamayo.’

Katika barua hiyo, Tibe aliandika kumweleza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa uuzwaji wa kiwanja hicho umehusisha nyaraka za kughushi pamoja na kutolipwa kwa kodi stahiki za Serikali.

Akithibitisha kuandika barua hiyo, Tibe aliiambia Tanzania PANORAMA Blog kuwa amedhulumiwa haki yake na ndugu zake hivyo hakuwa na jingine zaidi ya kuandika barua hiyo.

Wakili kiongozi wa Kampuni ya Uwakili ya Haki Kwanza Advocates, Alloyce Komba ambaye ametoa ufafanuzi kuhusu tuhuma zilizotolewa na Tibe dhidi ya ndugu zake, amesema adhabu itakayowakabili watuhumiwa wakibainika mahakamani kutenda jinai hiyo ni kifungo.

“Kosa la kughushi, adhabu yake iwapo mahakama ikimtia hatiani mtu kwa ushahidi usio na shaka yoyote ni kufungwa kwa mujibu wa kifungu cha 337 cha sheria ya kanuni za adhabu, sura ya 16 ya sheria za Tanzania, toleo la 2019.

“Mtu anapaswa kuripoti polisi kosa lolote la jinai linalofanywa na mtu yoyote ili mradi awe na ushahidi wa kutosha.

“Ni kosa pia kunyamazia kosa la jinai. Ndiyo maana mtu hukosa kwa kutenda (commission) au kutotenda (omission), mfano kutomzuia mtoto kutumbukia kisimani wakati unaona anacheza karibu na kisima,” alisema Wakili Komba.

Mwanasheria mwingine aliyezungumza na PANORAMA kwa sharti la jina lake kuhifadhiwa alisema tuhuma zilizotolewa na Tibe dhidi ya ndugu zake ni nzito na iwapo zitathibitika mahakamani hawatakwepa mkono wa sheria.

“Sheria zipo lakini inashangaza watu wanatenda makosa ya makusudi kama haya ambayo adhabu yake ni kali.

“Huyu anayewatuhumu wenzake naye hayuko salama kwa sababu ni wazi anajua vema jinsi ndugu zake walivyotenda hiyo jinai, walivyoghushi kwa sababu ni ndugu zake hivyo alipaswa kutoa taarifa polisi.

“Sasa inashangaza kijana msomi kukaa kimya huku akijua kuna jinai inafanyika. Kwa vile kalipeleka kwa waziri tumpe nafasi ya kulifanyia kazi,” alisema.

Kwa mujibu wa kifungu cha 338 cha sheria ya kanuni ya adhabu, sura ya 16 ya sheria za Tanzania, toleo la 2019 ambayo Tanzania PANORAMA Blog imeiperuzi inaeleza kuwa mtu akibainika mahakamani kwa kughushi wosia, hati za umiliki ardhi, hundi n.k adhabu yake ni kifungo cha maisha jela.

Hilo likiwa halijapoa, mtoto mwingine wa kiume wa Marehemu Mchungaji Rwakatare anayefahamika kwa jina la Muta Robert Rwakatare ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kawe kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) alizungumza na mwandishi wa Tanzania PANORAMA Blog na kumshutumu ndugu yake Tibe Kenneth Rwakatare kwa kutwaa kimabavu Shule ya Sekondari ya St. Mary’s International School, Dodoma Campus ambayo ni mali waliyoachiwa na marehemu mama yao.

Muta alieleza kuwa shule hiyo ni miongoni mwa shule zilizokuwa zikimilikiwa na Marehemu Mchungaji Rwakatare enzi za uhai wake lakini hivi sasa Tibe imeibadilisha jina na kutwaa umiliki wake.

Alisema ikiwa chini ya umiliki wa mama yao, ilikuwa ikijulikana kwa jina la St. Mary’s International School, Dodoma Campus, lakini sasa baada ya kubadilishwa jina inafahamika kwa jina la St. Mary’s Dodoma.

Muta alisema Tibe sasa anachukua mapato yote ya shule hiyo na eneo ilipojengwa nalo amelibadilisha jina na kuweka la kwake.

Watu walio karibu na familia hiyo wameeleza kuwa chanzo cha mzozo wa umiliki wa shule hiyo baada ya Marehemu Mchungaji Rwakatare kufariki ni mmoja wa watoto wake kuwazunguka wenzake na kuhamisha fedha zote zilizokuwa kwenye akaunti ya shule kwenda akaunti yake binafsi na pia akaanza kuchukua mapato yote ya shule hiyo.

Kwamba baada ya hilo kubainika, Tibe aliamua kuitwaa shule hiyo, akaibadilisha jina na majina ya akaunti za benki, hatua ambayo sasa inalalamikiwa na ndugu zake.

“Huyu ndugu yetu anashangaza sana kuanza kuandika barua kwa viongozi wa Serikali akitutuhumu kwa kukiuka sheria za nchi, eti tunaghushi nyaraka wakati yeye ndiyo bingwa wa kughushi nyaraka kuanzia Brela mpaka ardhi na anayemtumia kufanya hizo kazi za kughushi anafahamika, ni kijana aliyesoma kwenye moja ya shule zetu. Anachotaka amiliki yeye mali zote za mama.

“Ana madudu mengi mno lakini sie hatujishughulishi naye matokeo yake akiona tunamzuia kuchukua kila kitu anatafuta huruma nje ya familia kwa kutuchongea serikalini.

“Amejimilikisha shule ya Dodoma na kuibadili jina na akaunti za benki wakati shule hiyo ina mkopo wa benki moja kubwa nchini. Wewe unaweza kubadili umiliki wa mali ambayo ina mkopo wa benki kweli? Muulizeni na yeye hilo kalifanikishaje?

“Anamiliki mali nyingi sana za mama ambazo mapato yake yote yanaingia mfukoni mwake na hakuna anayemsumbua lakini yeye jambo dogo tu analalamika na kuandika barua huku na kule.

“Tulipouza hizo ardhi nyingine na kugawana mbona hakusema lolote? Kamuulizeni anataka nini hasa maana shule aliyotupora baada ya kuibadilisha jina imeondolewa kwenye orodha ya mali za marehemu mama. Hivi sasa anaimiliki yeye bila ridhaa ya sisi ndugu wengine.

“Nyumba za kupangisha za marehemu mama, zile ‘Appartments’ za Tabata zaidi ya 25, vyumba vya biashara 20, kote anachukua kodi yeye na pia mgodi wa dhahabu Chunya nao kachukua lakini bado anatupiga vita,” alisema Muta.

Alipoulizwa Tibe kuhusiana na madai hayo alisema hana muda wa kuyazungumzia.

Tanzania PANORAMA inaendelea kumtafuta Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ili kulizungumzia hilo.


Source: Tanzania-Panorama
Hizi mali za kupata kwa janja janja huwa hazina mrithi. Angalia jinsi familia nzima ilivyoacha kupambana kwa kusubiri mali za mzazi. Wataziuza zote
 
Back
Top Bottom