Vita ya marafiki ni kali sana kwenye mafanikio kuliko mtu baki

Ilinikutaga hii ,mtu akipata Hela yake,anakula kimya kimya ,ikiisha akijua umelipwa utadikia niazime laki hivi
 
Ni kweli mkuu...Mbona mm nawasave sana mkuu!...
Kweli mkuu na maisha yanata reciprocity ya hivyo lakin mkuu cha kujifunza sio kila mtu anajua hivyo, watu wengi ni wabinafsi na hata wao huwa hawajui kama wabinafsi, nna rafik siku nyingi aliwah kunipa laki sita kwa maagizo kwamba niirudishe after a week kabla haijafika week akaanza kuitaka hela na anasema mwanamke wake anaitaka aisee alinisumbua nikatafuta nkampa lakini nikikumbuka wakati anajitafuta namwacha kwangu kalala namwachia na pocket money nachoka, so nikaja kuamua kumchinja kwenye maswala ya hela na vitu vingine. Mkuu watu wengine ndio walivyoumbwa ndio mana me huwa nasema watu wengine hawanaga roho mbaya ila walimwengu ndio wanawafunza roho mbaya…
 
Sijasema mwandiko kuhusu usahihi namaanisha style.

Hao unaofahamu ulitakiwa utarajie matokeo uliyopata kutokana na wao kusumbua kurejesha hela yako.
Mtu anayesumbua kurejesha hela, huwa hakusaidii endapo utataka. Na mara nyingi atakusema vibaya au kuleta kinyongo ukitumia nguvu kiasi kupata hela yako. Ni sawa na wateja njaa kali, huomba discount kubwa na hununua vitu cheap, hulalamika zaidi na huwa hawarudi.

Kuna classmate wangu anasona MD yeye ni rafiki kwenye kula bata, kukulazimisha mtoke out ukatumie 150k yake ni kawaida kwake ila kukusaidia 100k kwenye mambo yako umrejeshee baadae ni vigumu. Huyu anakupa 150k yake utumie akitarajia baadae atakwama umpe 150k atumie kula bata.
Nina mzee ndugu yetu kwenye ukoo ni billionaire, kwenye list ya watu wa kuaminika kwake nipo ila hawezi nikopesha hata 1M ila ukimpa proposal ambayo atapata share anakupa hela. Anataka ombi liwe na details zinazogusa hivi "nipe 20M kuna deal 1,2,3 tutapata ROI in 4 months na baadae tutaanza gawana faida utapata 50%".

Leoleo kuna mtu nimepewa deal ila sijui napataje kulifanikisha nikampigia jamaa yangu mmoja huwa ananisaidia akanipa details nikamaliza na kupata faida sio mbaya, nikamtoa ya soda. Juzi niliingiza hela kiasi na kuna jamaa nilimuelekeza kazi siku za nyuma Jmosi akapata hela akataka kunitumia kidogo kama shukrani nikakataa, najua nitamtumia nikiwa na shida aniboost.

Kufupisha story nasemaje: Kila mtu ana code ya kutoa hela yake, haitoshi tu kusema ni mtoaji. Na vilevile kila mtu ana tamaa na hela yake, kitendo cha kukupa hela ni risk hivyo kuna watu hawataki kuingia risk isiyo na return. Kikwete anasema kihuni kwamba ukila sharti na wewe ukubali kuliwa.
 
Msaada siyo haki yako,hivyo usipopewa usi lalamike
 
Pia chukua hii, usipende kutegemea msaada wowote ule kutoka kwa mtu yeyote yule. Pokea msaada unaokuja wenyewe bila wewe kuutafuta. Ukiishi hivyo hakuna kenge itakusumbua hapa mjini.
Rahisi Sana kuandika hivi ukiwa uko kwenye amani au mda ambao changamoto ya kuhitaji msaada wa watu ijakufiks
 
Pia chukua hii, usipende kutegemea msaada wowote ule kutoka kwa mtu yeyote yule. Pokea msaada unaokuja wenyewe bila wewe kuutafuta. Ukiishi hivyo hakuna kenge itakusumbua hapa mjini.
Nadhani ni busara kumwambia pia kuwa akisaidia mtu asitegemee kurudishiwa wema!! Hii itamisaidia kujua kuwa kwemue mapambano ya utafutaji yupo alone na kama misaada si ya kutegemea hata kama uliowasaidia wanakuona ukitaabika.
 
Afadhali umewagundua mapema hao wanafiki.
 
Mbeba boksi wa Copenhagen unaleta mbwembwe kwa WALA VUMBI
 
Ok mkuu sa hv vp wakikuomba msaada wa fedha au shida inakuaje..umesamehe ukamove on au umekausha tu!
 
Umefanya kazi, mshahara wako mpaka utafute hela ndiyo uupate. Hii kweli code.

Mkuu fight kimpango wako, habari za kutegemea watu utashangaa umri unakimbia bila kufanya la maana. Kutegemea watu ni sawa na kusubiri ufanikiwe kwa miujiza.
Nimeiweka hii mkuu nashkuru sana..hiyo code ni simple tu ukijiongeza utaijua tu...!
 
Hakukumbuka fadhila kwa ajili ya dem...halafu...kweli watu wanakufundisha kuwa na roho mbaya...wakati we huna
 
Nimekupata mkuu....Risk sasa itakua applied in both ways.

Lerson learnt..
In a hard way
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…