Vituko vya watoto na ripoti za matokeo

Vituko vya watoto na ripoti za matokeo

Hao ndiyo unakuta darasa zima wamepata Div one. Wanakuwa wanazidiana point tu. Kwa wastani huo hata angekuwa wa 80 ni poa tu kwangu.
Yaani nilishangaa sana niliposoma notice board wa mwisho yaani 95 ana average ya 64
 
Kuna dogo ye kafungua report yake, kabadili namba halafu uso mkavu hashtuki Wala Nini, [emoji28]na hajafanywa kitu

Sie enzi hizo ufungue report kabla ya mzazi, adhabu yake Ni kuchapwa mbele ya shule nzima
[emoji23][emoji23][emoji23]hapo unakuta namba zimechengana balaa, haziendi hata kwa MAGAZIJUTO
 
Yaani nilishangaa sana niliposoma notice board wa mwisho yaani 95 ana average ya 64

Sasa huo wastani wa 64 shule nyingine unakuta ndiyo kati ya tano bora darasani
 
Dogo kaniambia tu amekuwa wa nne au wa 16 so nichague mimi amekuwa wangapi. Alafu kasepa zake masjid! Ni mdogo chekechea ya pili na maongezi yalikuwa ni katika simu.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Huyu wakwangu juzi aliniomba buku ya kitabu cha matokeo mwl wao aliwaagiza, nikampa. leo naulizia matokeo yako wapi anasema ile hela kapoteza baada ya kumbana sana anasema alinunua big boom za hela yote.
dah[emoji23]
 
Huyu wakwangu juzi aliniomba buku ya kitabu cha matokeo mwl wao aliwaagiza, nikampa. leo naulizia matokeo yako wapi anasema ile hela kapoteza baada ya kumbana sana anasema alinunua big boom za hela yote.
😹😹😹
 
Yani unajisikia vibaya mno,bahati nzuri nilimdanganya kuwa siku hiyo nilikuwa nimekunywa “ chungu” (Red wine) huwa anaiita hivyo. So sikuwa vizuri,but next time sitokunywa kwanza chungu mpaka tumalize H/Work,akajibu “Ok Mama next time be careful” lkn moyoni nilijisemea leo nimepuyanga mwanangu[emoji3][emoji3].

[emoji1787][emoji1787]
Mengine hata google hayapo
 
Mimi pacha wangu tuliahidiana atakaeingia top 10 anapata baiskeli kali zile za kisasa.

Wamepambana kweli kujisomea watimize ile ahadi. Bahati mbaya mmoja kawa wa 42 mwingine wa 38.kati ya 126
Shule yao matokeo ya mitihani kitaifa huwa wanapata grade A wanafunzi 80% ,B 20% hawanaga grade C.

Nimenuniwa siku ya pili sasa, tukishasalimiana tu hawataki stori na mimi. Sasa sijui kosa langu liko wapi?

Wanataka " niwakope" baskeli halafu mwezi wa 12 ndio wapambane kuingia top 10.nimewaambia HAKUNA!
 
Watoto ndo wanarudi likizo

Swalehe hapa karudi kawa wa 34 namwuliza imekuwaje umeporomoka toka namba moja ananambia

Baba kwani elfu moja na elfu kumi ipi kubwa nkamjibu elfu kumi

Akanambia Basi sawa mzee , Mimi ndo namba kubwa hapo kuliko wote 😁 na kuliko pacha wake Micaela (yeye kawa wa tano )nmeshindwa kumjibu chochote maana Kuna homework alileta akakosa zote nlifanya nae kwenda shuleni wakamwambia wewe na baba yako wote wajinga 😥😂

Nmewaacha na ugomvi hapa yeye na dada ake waamue nani ana namba kubwa 🤦🏾‍♂️

Wewe umekutana na kituko gani ?
Achatu yaani walimu wanaleta homework utadhani wanaugomvi na sisi wazazi khaaa
 
True story.

Kuna dogo alikuwa anafanya vibaya shuleni.

Akapeleka ripoti kwa baba yake. Ripoti mbaya.

Baba akamuuliza, imekuwaje umefanya vibaya hivi?

Mtoto akajibu, mimi sina akili, sina kumbukumbu. Nikisoma nasahau.

Baba akawa kama kakubali jibu. Hakuhoji zaidi.

Siku mbili zikapita, yule mtoto akaona mtu anasoma gazeti. Akaomba yule mtu akimaliza kusoma ampasie gazeti.

Dogo akawa anafunguka, anasema anataka kuangalia msimamo wa ligi, kwani Simba ina pointi hizi, Yanga ina pointi hizi, magoli ya kufunga mangapi, michezo iliyobakia mingapi, akawa anatiririka data nyingi za soccer pale.

Sasa yule baba yake pale pale akamuuliza. Wewe si umesema huna akili, shuleni ukisoma unasahau? Sasa haya mambo ya msimamo wa ligi mbona unayakumbuka vizuri sana?

Baba akasema, wewe tatizo lako si akili, akili unazo nzuri tu, tatizo lako huna interest na shule.
Hawa huwa wana makusudi sana

Lakini all in all tuwajenge watoto wakue katika kile kitu wanapenda mfano huyo dogo anaweza kuwa football analyst mzuri sana
 
Back
Top Bottom