Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

Mtambuzi utalii ni muhimu lkn zile kesi za kina mkwizu nazo muhim sana ebu fanya kuzileta maana tumezimis sana
 
Big up mtambuzi.. Thread positive kama hizi ndo nazipendaa...Sio mtu anatukana kwa kisingizio cha kushaurii. Nani atasikiliza mawazo ya mtu anayetoa mapopu
 

Nakubaliana na hoja zako isipokuwa namba 1 na 5.

Kuhusu hoja #1: Mpaka sasa sijaona assessment yoyote ikionesha impact ya uwekezaji ambao tumeshaufanya katika matangazo ya vivutio vya utalii nchini. Bila kuona hiyo assessment, siwezi ku-support uwekezaji zaidi kwenye matangazo. Huo ni uchochoro wa kuiba hela. Ni nini impact ya kuweka matangazo kwenye viwanja vya EPL? Je watalii wanaokuja nchini wanafanya hivyo kwa kushawishiwa na matangazo? Wanapata wapi habari kuhusu vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania? Unaweza kukuta matangazo tunayolipia mamilioni hayana impact yoyote. Tunafanya mambo kwa mazoea kwa kuwa lengo ni kuiba. Na nahisi kwenye eneo hili tumeibiwa sana. Safari za nje kuhudhuria maonesho ya utalii zimefanyika kiholela sana. Kusema tu serikali ijikite kwa nguvu zote kutangaza utalii ni kutengeneza mazingira ya fedha za umma kuibiwa. Ni lazima kuwa specific na kufanya mambo kwa tija.

Kuhusu hoja #5: Wingi wa vyuo hautatatua tatizo. Actually, utaongeza tatizo kwa kuzalisha utitiri wa watu wasio na sifa. Kinachokosekana ni apprenticeship programs pamoja na certification program. Ili kuwa guide, ni lazima uwe certified kama ambavyo NBAA ina certify wahasibu. Huo utaratibu haupo. Matokeo yake, watu wakifeli shule wanakimbilia kuwa tour guide. Huo ni mfano tu but the same applies to hoteliers, travel agents etc. Biashara ya utalii ni delicate sana. Mgeni akipata experience mbaya, athari ni kubwa. Mtu alipe maelfu ya dola halafu anapata guide mediocre, wanakuwa disappointed sana. Na magaidi wengi ni ujanja ujanja tu. Very few are qualified.
 
Kuna changamoto nyingine imeanza hivi karibuni ile ya wafugaji kuvamia na kuingiza mifugo yao katika hifadhi bila ya kufuata utaratibu. Suala hili lisiporatibiwa linaongeza ushindani wa malisho na uwezekano wa maambukizo ya magonjwa kwa wanyama pori. Inabidi serikali na wadau wakae na kutatua changamoto hii. Ikiwezekana watumie utaratibu unaotumika Ngorongoro (NCA).
 
hii ndo post ya maana kuliko zote ambazo nimewahi kuzikuta hapa jamii forums, sababu imejitosheleza vya kutosha.
Ngoja nichafue hali ya hewa.. Members wenye zaidi ya 5 years humu ni ngumu kukuta wameandika pumba. Lakini mtu kajiunga June 2016 ana posti 5000 inamaanza kwa mwezi anatuma post zaidi ya book na per day anatuma post zaidi ya 30 ujue huyo ni kimeo. Kuandika content inahitaji tafakuri na lazima uwe ni msomaji mzuri wa vitu vyenye content ili uwe muandishi mzuri...😀😀😀😀
 
Utalii wa Ndani nilishatembelea Ngorongoro, Pazuri sana Manyara kama tulibaniwa hatukuweza fika ziwani ila tulilala hostel na Tarangire tulitalii ila tulibaniwa pia hatukuweza fika chemchem ya maji ya moto hivyo kiufupi sikupapenda ilikuwa Mwaka elfu moja mia tisa na tisini na tano.

Ngorongoro tulitelemka na gari moja matata four wheel drive umbo lake kama la lile bus lililotumika kwenye movie ya War bus langi ya green. tulizungunga na tuliweza teremka tukaona viboko,Simba,Tembo,Nyati Swala na wanyama wengi Kifaru hatukumuona kudadeki bila kusahahu Masai..

Safarini niliweza kuona Mazao ya Sunflower maeneo ya Karatu niliweza kuwa level moja na Mawingu yana kiubaridi ila yapo kama Moshi(Ukungu) kihewa kizito kizito hivi

tulifika Snake park tukaona Nyoka wa aina mbali mbali Na Ngamia pia

Pale Momera Kwa Dr. Nagi Tanzanite kuna wanyama ila pamechoka.

Sina Deni kubwa kwa Serikali kuhusu Utalii wa Ndani Bado Mikumi japo nilishawahi pita kwa Treni na wanyama niliwaona... Kusini pia bado kwa kina Livingstone nakobado sijafika... Kilipoanguka Kimondo napo sijawahi fika japo Mbeya nilishawahi fika lol
 
Hongera mkuu na ninaamini ipo siku utatembelea vivutio vingine, tutumie jukwaa hili kuishauri serikali namna ya kuboresha sekta hii ili wazawa nao wapate fursa ya kutembelea na kufaidi mema ya nchi
 

Mkuu nakubaliana na wewe kwa asilimia 100. naamini hayo uliyopendekeza yakifanyiwa kazi tutafika mbali sana kiuchumi
 

Ushauri mzuri sana huu.
Naamini wahusika wakiusoma watachukua hatua stahiki na kuufanyia kazi
 
Ha

Hao wakubwa walipe usd 3000 na wadogo usd 1000.
 

Hunting safaris zipigwe marufuku. Tuwe na photographic safaris tu ambazo pia zina pesa nyingi na ujangiri utakwisha kabisa. Kwanza kuua wanyama bila utaratibu ni sadistic na kuna watu wanaiita sporting! Hii ndiyo imemaliza wanyama huko ulaya na marekani. Africa kusini sasa eti kuna ranchi za wanyamapori!!!!!! wanyampori wanatakiwa wawe huru katika makazi yao ya asili ambayo makubwa yamebaki Tanzania tu. TAWA waweke utaratibu wa kupunguza wanyama wanaozidi malisho na wananchi wapate kitoweo cha nyama ya wanyamapori kama enzi za TAWICO.
 
Ushauri mzuri mkuu.
Ahsante sana kwa kushiriki mjadala.
 
Tumtumie Daimond. Mi ndio ushauri wangu japo aseme I am from the country of Serengeti and Kilimanjaro ans Zanzibar
 
Wadau nina M. A ya utalii hapa nakomaa natafuta fursa sijui nitoke vipi ?
Nafikiria nitafute college hizi nikafundishe.
Ngoja nisugue kichwa I am sure nitapata solution.
Ila mtaani kugumu sana aisee dah!! Sijui kwa nini nilichagua kusoma hii course.
 
Tumtumie Daimond. Mi ndio ushauri wangu japo aseme I am from the country of Serengeti and Kilimanjaro ans Zanzibar
Ila mdau kuna fungu lipo la kutangaza utalii wetu.
Unakumbuka ile kula uliwe ya JK? Alikuwa anaongelea kuspend kwenye matangazo ya kiutalii.
 
Tumtumie Daimond. Mi ndio ushauri wangu japo aseme I am from the country of Serengeti and Kilimanjaro ans Zanzibar
Tunahitaji mkakati mahsusi utakaoweza kufanikisha jambo hilo lisije likafanyika kienyeji au kisiasa. Tushirikishe wataalamu katika kutengeneza mapping plan
 
Mkuu kwa kuanza naomba tuwasiliane tutengeneze fursa, haya yanayozungumzwa hapa bila kuthubutu kwa ku approach idara za serikali husika hakuna litakalofanyika.

Tuanze kuonyesha njia, kwamba jambo fulani linawezekana serikali itatukuta tumeashaandaa mazingira wao itakuwa ni jukumu lao kuandaa regulations.
 
Poa Nitakutafuta kiongozi.
Kwanza hii thread ngoja niipitie mwanzo mwisho.
Sikupata muda wa kutulia kuisoma.
Najua kuna mawazo mengi sana ya wadau hapa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…