Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

.....
......mifuko ya jamii kama NSSF wangewekeza huko kwaajili ya wazawa haswa mahoteli ....ili wabongo angalau waonye matunda
Hili linawezekana ila hii kazi risk yake ni kubwa sana sidhani kama mifuko hii itakubali..
Na lingine vionhoinwetu hawatakubali .. Wanapenda wageni ili wawe wanaenda kuchukua %
 
Unachosema ni kweli kabisa.
kwa hali ya sasa ukimwambia mtu wa kwamba anaweza enda talii ngorongoro au Serengeti anaona kama ni jambo la watu matajiri tu na si la watu wa kada ya kawaida.

Hakujawa na hali rafiki.

Pia kuna siku nilikuwa katika hifadhi mojawapo hapa nchini, likaja kundi la watu wakiwa wamekodi gari kufika pale ofisi ya TANAPA wakawa wanataka kufanya malipo ya kuzuru ile mbuga na kulipia gari lililowaleta. Sasa shida ikawa wao wana pesa taslim mkononi lakini maafisa wa TANAPA wanawaambia wanatakiwa wawe na kadi ya CRDB kufanya malipo. Wale jamaa walijikuta safari yao imevurugika wa kukosa mtu mwenye account CRDB. Yote hii ni kutokana na kutokutoa taarifa pale wanapofanya mabadiliko au maboresho kwa huduma zao (TANAPA/Wizara).
....
.....Well Noted Mkuu

hilo la KADI linakimbiza kabisa utalii wa ndani target yao ilikuwa wazungu tu ...TANAPA pitieni huu uzi ...THEY should have the "ocean brain" Watanzania kwanza wengine baadaee...

Asante Mkuu kwa mchango wako ....
 
Hili linawezekana ila hii kazi risk yake ni kubwa sana sidhani kama mifuko hii itakubali..
Na lingine vionhoinwetu hawatakubali .. Wanapenda wageni ili wawe wanaenda kuchukua %
....
.......Mkuu wanajenga hoteli za kawaida tu kama za huku mtaani self safii tu na kozikodisha kwa wazawa kuziendesha Mangi watu watakwenda
 
Mkuu


Mkuu nashukuru kwa heshima uliyonipa kuhusu kesi kwa sasa niko kwenye mchakato wa kutoa kitabu, nitawajulisha kikitoka.
Kuhusu mada husika natarajia pia mchango wako hapa.
Watanzania wengi pamoja serikali yetu tunaamini kuwa kwa sababu tuna Simba, Faru,Twiga, Tembo, Mbwa mwitu na Fisi Chui Simba pamoja Nyumbu basi wanadhani watakii dunia nzima watahangaika ili waje Tanzania watazame sura za wanyama wakila majani.

Watalii hawana haja na sura ya Nyumbu wa Simba wala Tembo wai wanataka kuona mazingira ya kuvutia yaliyo tofauti na mahali pengine na kuwe hamna usumbufu.

Mkuu nadhani mchango wangu kiduchu huu.
 
....
.....nilijifunza kitu Sustainable Tourism kule Namibia wenzetu wako mbali sana haswa utalii wa ndani

mfano tu Serengeti au Ngorongoro kwa mbongo ni vigumu sana kufika huko zaidi ya kulala kwenye mabweni.....

nahakika Tanapa or NCCA wakitengeneza mazingira mazuri mfano zijengwe Lodge za Watanzania ndani ya hifadhi kwa 30,000 mpaka 40000 tsh per day bia bei ya kitaa na chakula ....usafiri wa basi mayai special kwa wabongo ...ndani ya hifadhi kuwe na malori maalum ya kuvinjari....na hakika watu watamiminika kama mvua...

cha msingi kuweka mazingira yanayofanana na utamaduni wetu .....watu tutakwenda
Ngorongoro zipo nyumba za kulala wageni kwa bei reasonable kabisa. Sijui Serengeti sijafika mda sasa. Changamoto ya utalii wa ndani ni bei kali sana kurent gari zuri kukupeleka mbugani, hapa watanzania wengi hawamudu. Kingine tozo kwa waTz.....mimi sikubaliani kulipa zaidi ya 11,000 kwa kichwa kwa mTz. Hii ni tozo Ngorongoro, Manyara nako tozo kwa kichwa ni juu. Nasema hivi kwasababu miaka michache imepita ilikuwa 1,500 tozo kwa mTz ikapanda 5,000 sasa hivi ndiyo wameamua iwe 11,500 Huwasielewi wanatumia vigezo gani? High season? Ku-discourage mass tourism au ni nini? Utalii wa ndani utakuwa unafanywa na elites tu.....vinginevyo unatakiwa ujipange kwelikweli kuona wanyama na madhari nzuri ya nchi yako ambayo unaamini hakuna mwenye hati miliki nayo.
 
View attachment 421962

View attachment 421964

View attachment 421965

Kwa miaka mingi sasa sekta ya utalii nchini imeshindwa kuchangia pato la taifa kama inavyostahili. Kuna changamoto nyingi sana ambazo zimesababisha jambo hilo lakini naomba nitaje chache kisha na wenzangu mnaweza kuchangia na kuishauri serikali hatua za kuchukua ili kuimarisha sekta hii muhimu kwa ustawi wa uchumi wetu.

1. Sekta hii haijatangazwa ipasavyo ndani na nje ya nchi na serikali

2. Sekta hii imekumbatiwa na watu wachache na kupitia umoja wao wameifanya sekta hii kuwa kama mali yao binafsi na ni wao wanaoishauri serikali kuweka masharti magumu ili kuendelea kunufaika wao peke yao.

3. Kuna masharti magumu yanayokwaza wafanyabiashara wadogo kuingia kwenye sekta hii na hivyo kunufaisha wadau wachache

4. Miundo mbinu katika hifadhi zetu ni kikwazo katika kukuza biashara hii ya utalii

5. Vyuo vyetu vya utalii ni vichache vinatoa mafunzo duni yasiyoendana na ukuaji wa sekta hii na wahitimu wengi wanaomaliza kusoma wanakuwa na uwezo wa kufanya kazi za chini na zile nafasi kubwa kushikwa na wageni

6. Kutokuwepo kwa vivutio na mahoteli makubwa katika miji mikuu yenye hadhi ambayo ipo jirani na mbuga zetu za wanyama

7. Kutokuwepo au kutoboreshwa kwa maeneo yenye historia ya miji mbalimbali hapa nchini

8. Maonyesho ya utalii kutopewa kipaumbele na kufanywa katika mikoa miwili tu Kilimanjaro na Arusha

9. Kutokuwepo kwa taarifa za mara kwa mara kuhusu takwimu za watalii wanaoingia nchini na nchi wanazotoka zaidi ya kupatikana kwenye hotuba za waziri bungeni.

10. Ushiriki mdogo wa maonyesho ya utalii nje ambapo serikali haisaidii kuwawezesha wafanyabishara wadogo wa utalii kushiriki maonyesho haya

Nini kifanyike:

1. Serikali ijikite kwa nguvu zote kutangaza utalii katika mataifa mbalimbali ili kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea nchi zetu. Juhudi hizi ziende sambamba na kutoa mialiko maalum kwa watu maarufu duniani kutembelea vivutio vyetu na serikali kuchangia baadhi ya gharama na ziara hizo ziwekwe mwenye vyombo vya habari vya hapa nchini na nje.

2. Kuna fukuto la mgawanyiko katika umoja wa wafanyabiashara ya utalii kati ya wale wafanyabiashara wakubwa na wale wadogo. Na mgawanyiko huu unatokana na wafanyabishara wakubwa kutetea maslahi yao zaidi na kuwaacha wafanya bishara wadogo wakikosa pumzi. Serikali inatakiwa kutengeneza mazingira yatakayowawezesha wafanyabishara wa utalii kuwa na mazingira mazuri ya kufanya bishara zao bila kujali uwezo wao wa kimtaji, lakini pia kuwe na utaratibu wa kuwatambua wafanyabishara wanaouza safari kupitia mitandao ya kijamii na utaratibu huo iwe ni pamoja na kuwapatia leseni na utaratibu wa kulipa kodi, hii itasaidia serikali kuongeza mapato kwa ukusanyaji kodi kwani kwa miaka mingi sekta hii imekuwa ni kichaka cha wafanyabiashara wasio waaminifu kukwepa kodi kwa mbinu mbalimbali, Tunaweza kufanya utafiti kwa nchi kama Afrika Kusini na visiwa vya Mauritius na Shelisheli au Botswana ili kujua wenzetu wamewezaje kuboresha sekta ya utalii katika nchi zao na serikali inanufaikaje na mapato ya utalii katika nchi zao

3. Serikali ilegeze masharti ya kupata leseni za kuanzisha kampuni za utalii kwani siku hizi kuna aina nyingi za kuuza safari ambapo huduma nyingine zinaweza kufanywa na mtu mwingine kama huduma za ndege, huduma za magari kuna makampuni mengi ya kukodisha magari nk. Iwapo serikali itabadilisha masharti ya usajili wa makampuni ya utalii itaongeza wafanyabishara wengi katika sekta hiyo na hivyo kujiongezea kipato cha uhakika.

4. Tuna miundo mbinu mibovu sana katika vivutio vyetu vya utalii na mfano halisi ni ilipo mbuga ya Selous. Hii ni mbuga ambayo ingetumiwa na wageni wanaokuja jijini Dar kutembelea na kuona wanyama mbalimbali ukiwemo mto Rufiji. Hii ni mbuga ambayo ingeweza kutuingizia kipato kama kungetengenezwa mazingira ya kuwepo kwa Treni itakayokuwa inafanya safari zake hadi Kisaki na kurudi kila siku na pale kukawa na Hoteli kubwa na wawekezaji wa utalii wakapewa maeneo ya kujenga ofisi zao na kuboreshwa kwa barabara inayoingia Selous ingerahisisha watalii kutumia treni hadi Kisaki na pale wanapokelewa na kupelekwa mbugani na magari kwa kupitia barabara zilizoboreshwa. Naamini wageni wengi wanaoishi jijini Dar wangetumia fursa hii kutembelea Selous kila mwishoni mwa wiki. Kwa sasa njia ya usafiri wa gari unachukua saa kumi kupitia Matombo na saa 7 kupitia Rufiji ili kuingia mbugani huku ndege ndogo zikitumia dakika 45 lakini ni ghali sana watu wenye kipato cha kawaida kumudu. Serikali inaweza kuwashirikisha wadau wa utalii ili kupata mawazo yao namna nzuri ya kuboresha miundo mbinu yetu katika hifadhi zetu

5. Serikali iongeze vyuo vya utalii ikiwa ni pamoja na kuboresha mitaala ili kuinua elimu inayotolewa na vyuo hivyo. Kwa sasa vyuo vyetu vya utalii ni vichache na elimu inayotolewa humo ni ya kuwaandaa vijana wetu kuja kuwa vibarua na siyo kuwa viongozi katika sekta hiyo. Kwa sasa sekta ya utalii ndiyo inayoajiri wageni wengi kuliko sekta nyingine hapa nchini huku wengine wakiingia na kufanya kazi kiujanja. Tunahitaji mkakati makini ambao utaboresha elimu ya utalii kwa vijana wetu ili kupunguza ukosefu wa ajira. Zipo baadhi ya nafasi katika mahoteli yetu na makampuni ya utalii ili kuzishika labda ukapate elimu hiyo nje ya nchi au upate mafunzo kazini. Hii ni aibu kwa nchi yetu yenye vivutio vingi vya utalii kutegemea nguvu kazi kutoka nje huku vijana wetu wakiendelea kuwa vibarua

6. Tunahitaji katika mikoa ambayo iko karibu na vivutio waalikwe wawekezaji wa kuwekeza katika mahoteli na pia katika mikoa hiyo yatengwe maeneo ya historia ya makabila ya mkoa huo na maeneo mbalimbali yatengwe kwa ajili ya utalii na yaboreshwe ili watalii wanapokuja kabla ya kutembelea vivutio vyetu huko mbugani wapate fursa ya kujifunza utamaduni wa eneo husika na kujua asili ya eneo hilo na watu wake.

7. Serikali kwa kushirikiana na wadau wa utalii iboreshe maeneo yenye historia ya miji mbalimbali hapa nchini na kuitangaza ikiwemo ujenzi wa masanamu ya watu walioacha historia katika miji hiyo kama kule Tabora kina Mtemi Milambo au kina Kishosha Ng’wanamalundi

8. Kuwe na mkakati wa kutoa kipaumbele kwenye maonyesho ya utalii na yawe yanafanywa katika mikoa yote yenye vivutio ili kuimarisha utalii wa ndani hii iwe ni tofauti na ile ya kimataifa inayofanyika Arusha na Moshi, lakini hata hiyo ya Arusha na Moshi inapaswa kuboreshwa kwa kuiga wanavyofanya katika nchi za wenzetu

9. Taarifa za mara kwa mara kuhusu takwimu za watalii wanaoingia nchini na nchi wanazotoka ni muhimu ili kuwarahisishia wafanyabishara wa utalii kujua soko liko wapi, uwepo wa kitengo kitakachokuwa kinakusanya taarifa hizo na kuziweka mtandaoni kutasaidia kujua ni wapi tumejitangaza na wapi hatujajitangaza ili kuelekeza nguvu zetu huko.

10. Kuwe na mkakati wa kuhakikisha wafanyabishara wa utalii wanashiriki kwa wingi kwenye maonyesho ya utalii katika nchi mbalimbali ili kupata fursa ya kutangaza vivutio vyetu.

Naomba nipishe michango mingine kutoka kwa wadau mbalimbali ili tuweze kuishauri serikali namna nzuri ya kuboresha sekta hii ya utalii.
NASHAURI WAZIRI WA MALI ASILI NA UTALII NA WAKURUGENZI WAKE WAWE WANACHAGULIWA KWA KUFANYIWA INTERVIEW NA MCHUJO KUTOKANA NA TAALUMA ZAO KAMA ZINAKIDHI HADHI YA UHIFADHI,WAAJIRIWE KWA MIKATABA MAALUMU.

NASHAURI PIA WADAU WA SEKTA HII WAHESHIMIWE HUSUSANI WAZAWA KWANI NDIO WANAOITANGAZA NCHI VYEMA,HAKI ZAO ZILINDWE NA ZIBORESHWE,HIZI KAMPUNI NDOGO NDOGO ZINAPENDWA SANA NA WAGENI NA NDIO WAFANYA MARKETING WAZURI SANA NA KUITANGAZA TANZANIA,MSIWADHARAU SIO JAMBO DOGO HILI,IKIBIDI UUNDWE UMOJA WAO NA MAMLAKA YA MAPATO IHUSUSHWE ILI KUWALINDA KATIKA COMFLICT OF INTEREST

NASHAURI SERIKALI IPIGE MARUFUKU BAADHI YA MAKAMPUNI MAKUBWA MALIPO YA WAGENI KUFANYIKA NJE YA NCHI,KWANI KINACHOTUMWA HUKU NI HELA YA DIESEL NA PARK FEES TU,MALAZI NAKADHALIKA NYINGI HUBAKIA KULEEEE NA MKIONA LODGES NA MAKEMPU YAMEJAA MJUE 1.5 HELA IPO LONDON AU BOMBAY NYINGINE NI HIZI KAMPUNI NDOGONDOGO WAMELIPIA LIVE AMBAZO TOKEA ANAPOKEA MGENI KIA MPAKA ANA MRUDISHA KIA BAADA YA SAFARI AMESHA KOMBWA KAFAIDA CHAKE HUKO NJIANI EITHER NA TRAFIKI AU WENGINEO! NASISITIZA UUNDWE UMOJA WAO
 
....

NASHAURI SERIKALI IPIGE MARUFUKU BAADHI YA MAKAMPUNI MAKUBWA MALIPO YA WAGENI KUFANYIKA NJE YA NCHI,KWANI KINACHOTUMWA HUKU NI HELA YA DIESEL NA PARK FEES TU,MALAZI NAKADHALIKA NYINGI HUBAKIA KULEEEE NA MKIONA LODGES NA MAKEMPU YAMEJAA MJUE 1.5 HELA IPO LONDON AU BOMBAY NYINGINE NI HIZI KAMPUNI NDOGONDOGO WAMELIPIA LIVE AMBAZO TOKEA ANAPOKEA MGENI KIA MPAKA ANA MRUDISHA KIA BAADA YA SAFARI AMESHA KOMBWA KAFAIDA CHAKE HUKO NJIANI EITHER NA TRAFIKI AU WENGINEO! NASISITIZA UUNDWE UMOJA WAO

Dublin
 
Hongera Sana wenye kuelewa wataelewa hasa viongozi WA maliasili
Tuna Kila sababu ya kuwa matajir tatizo viongozi wabovu hii sekta unaweza tamani kujifukia ukiwaza yule wazir jina kapuni anamchukua bongo movie aunt kutangaza utalii....tembo wameuwawa had inatia Huruma..twiga hadi airport wanasafirishwa...mlima Kilimanjaro watalii wanapitia Kenya....Tanzanite ndo usiseme

Tumekalia kiti cha gold ila tunaomba kila uchao hii sekta ingekuwa Na wazalendo tungekuwa Na pato kubwa Sana la pesa tunaingiza
 
Hiii sector ya utaliii inahitaji apace overhauling kuanzia kwenye management mpaka infrastructures, ni swala la aibu sana nchi kama Tanzania kuzidiwa na majirani kwa gap kubwa sana kimapato hiliali hao majirani wanatumia hizo hizo rasilimali zilizopo Tanzania.
 
Wakati fulani nilikuwa naongea na mmiliki wa kampuni ya utalii kutoka nchini Kenya, akaniambia kwamba kule kwao baada ya kuandamwa na Alshabaab walianzisha kampeni maalum waliyoiita TEMBEA KENYA, Hii kampeni ilianzishwa na serikali yao ili kulinda ajira za wafanyakazi katika sekta ya utalii ambayo iliyumba kiasi cha kutishia ajira za wafanyakazi wengi nchini humo katika sekta hiyo.

Makampuni mengi ya utalii zikiwemo hoteli zilipunguza gharama za safari za utalii na mahoteli pamoja na camps zilipunguza pia gharama za malazi na chakula kwa wazawa na wananchi walihamasishwa kufanya utalii wa ndani ambapo kulikuwa na muitikio mkubwa na serikali katika kuunga mkono kampeni hiyo ilichangia wafanyakazi katika sekta mbalimbali kufanya utalii wa ndani na mikutano na makongamano yalihamishiwa huko ili ku generate revenue katika makampuni ya utalii na mahoteli.

Kampeni hiyo ilipelekea kuzaliwa kwa Kampuni ya Bonfire homepage ambayo ilianzishwa na wajasiriamali wadogo mtu na mkewe bila mtaji mkubwa ambao walianza kwa kuuza safari za utalii kupitia mtandao wa facebook.

Wajasiriamali hawa walianza kwa kupatana na Mahoteli yaliyoko kwenye mbuga za wanyama na camps na ku book vyumba vingi kwa mpigo kisha kuviuza kwa mtindo wa groups kwa gharama nafuu na kuhamasisha wazawa kulipa kidogo kidogo kabla ya safari na hapo mtu anajihakikishia safari yake ya kutalii kwa gharama nafuu zilizopunguzwa kutokana na kuuzwa kwa vyumba vingi kwa mpigo.

Hivi sasa kampuni hiyo ni kubwa na ni miongoni mwa walipa kodi wakubwa nchini humo na sasa imevuka mipaka ambapo sasa inauza safari za nje kama Dubai na nchi za ulaya na Marekani jambo ambalo imejijengea sifa na kutwaa tuzo mbalimbali ikiwemo ile ya Qatar Aiways kutokana na manunuzi ya tickets kwa shirika hilo.

Hii ni changamoto kwa nchi yetu kuruhusu wajasiriamali wadogo kujiingiza kwenye biashara hii kwa kuuza safari za utalii kwa njia ya mitandao ya kijamii ili kujiongezea kipato na kujiimarisha kiuchumi. Tunaweza kuiga wenzetu waliafanya nini kwa mfano tunaweza kujifunza kupitia Kenya na Afrika Kusini.

Iwapo kutawekwa utaratibu mzuri wa kupanua wigo wa wafanyabiashara wa utalii hakika serikali itakusanya fedha nyingi sana za kodi na hivyo uchumi wetu kukua kwa kiwango cha ajabu.

Ombi langu kwa wizara ya Utalii.

Naomba wapitie uzi huu na kuchukua mawazo mazuri ya wadau na kuyafanyia kazi ili nchi yetu isonge mbele. Hii ni nchi yetu sote na tuna wajibu kama wananchi kuishauri serikali ili kujenga uchumi imara utakaonufaisha serikali na wananchi wake na vizazi vijavyo.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika.
 
Jambo lingine ni elimu kwa umma, Wa TZ wengi hawajui umuhimu wa kutembelea mbuga zetu za wanyama na gharama za utalii kwa wazawa zipunguzwe ili kuwavutia Watanzania wengi kutembelea vivutio hivi.

Kuna wakati nilisikia Benki moja nchini ikitangaza kwamba imeandaa safari za wafanyabiashara kwenda nchini china kibiashara na gharama zilikuwa resonable kabisa kwa safari na malazi. Hili lingeweza kufanyika pia kwa safari za Utalii. Mabenki yangekuja na wazo hilo kwa kuwahamasisha wateja wao kulipa kidogo kidogo kwa safari za utalii wa ndani kipindi cha Low Season ambapo gharama za safari na hoteli hupungua sana. Hii itawawezesha kutengeneza faida na pia kuongeza wateja.
 
Maoni yangu vyuo vinavyojiita vya utalii vilivyoko vichochoroni vihakikiwe kwani hivi ndivyo vinavyozalisha vibarua badala ya kutoa taaluma stahiki inayoendana na ukuaji wa sekta ya utalii.

Hivi sasa kuna utititri wa vyuo ambavyo hata mitaala yao ni ya hovyo na vifaa vya kufundishia hawana zaidi ya kutoa mafunzo ya nadharia kwa miezi mitatu na kuwasukumia wanafunzi kwenye mahoteli ili kupata uzoefu wakati hata taaluma yenyewe ni ya mashaka matupu.

Hivi vyuo navyo ni Jipu inabidi vitumbuliwe.
 
Kuweka kumbukumbu sawa:

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI KATIKA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII, MHESHIMIWA ESTHER NICHOLAS MATIKO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI KUHUSU MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA BAJETI WA MWAKA 2015/16 NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KATIKA WIZARA HIYO KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017

SEKTA YA UTALII

HOTELI ZA KITALII NDANI YA HIFADHI


Mheshimiwa Spika, takribani 80% ya watalii wanaoingia nchini hulala katika hoteli mbalimbali zikiwemo za ndani ya hifadhi. Licha ya hoteli za ndani ya hifadhi kuchangia kiasi kikubwa cha mapato ya Wizara hii, hoteli hizo zimekuwa na changamoto nyingi jambo linaloathiri ufanisi wake na mapato yatokanayo na hoteli hzio.

Mheshimiwa Spika, ndani ya hifadhi kuna hoteli za wawekezaji wazawa na zile za raia wa kigeni. Lakini hoteli za wazawa zimekuwa zikikumbwa na changamoto kubwa sana. Mathalani wakati wa msimu wenye wateja wachache (low season) hoteli za wawekezaji wa kigeni hutenga vyumba yaani hufanya “block booking” kwa wageni wao katika hoteli hizo za wazawa kwa kipindi cha muda mrefu na kwa gharama ndogo (low price), hivyo basi inapofika kipindi cha msimu wenye wateja wengi (high season) tayari unakuta hoteli hizi za wazawa zinakuwa haziwezi tena kuuza vyumba hivyo na hawawezi tena kufaidika na bei za high season kwa kuwa vyumba hivyo vinakuwa vimeshachukuliwa (blocked). Aidha; changamoto nyingine ni kwamba; fedha hii inayokuwa imelipwa kwa vyumba hivi vya hoteli za wazawa ni ndogo na inakatwa kodi kubwa , lakini Hoteli zile za wawekezaji wageni hupokea wageni wengi kwa kipindi hicho cha high season kwa bei kubwa na huwa haikatwi tena kodi.

Mheshimiwa Spika , pamoja na hayo, imekuwa ni vigumu sana makampuni madogo ya utalii kuweza kumudu soko la ushindani kwa kuwa vipaumbele vya kupata vyumba vya hoteli kwa ajili ya kulaza wageni kutolewa kwa makampuni makubwa pekee na zaidi yale ya kigeni. Hii inasababisha makampuni madogo ya ndani kushindwa kuhimili soko la ushindani na mengi hufilisika kabisa. Suala hili sio tu linaua hoteli za wazawa hapa nchini bali pia linaisababishia serikali hasara kubwa ya kupoteza mapato.

Mheshimiwa Spika, Nchi hii ina Tume ya Haki ya Ushindani (Fair Competition Commision) ambayo imebainisha wazi katika tovuti yake kwamba: “FCC has a mandate to regulate the competitive market. “FCC deals with all issues of anti- competitive conduct, abuse of dominance and has provision for curtailing merges and acquisitions if outcomes are likely to create dominance in the market or lead to uncompetitive behavior”

Mheshimiwa Spika, kwa tafsiri rahisi kabisa ni kwamba tume hiyo ina mamlaka ya kuhakikisha kunakuwepo na kiwango cha uadilifu miongoni mwa washindani katika masoko. Hivyo basi Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kuhakikisha jambo hili linatafutiwa ufumbuzi kwa kuwa ni wajibu wa serikali kunusuru makampuni haya ya wazawa ili kuweza kumudu soko la ushindani wa kibiashara. Aidha, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kutumbua pia majipu katika eneo hili ambapo wawekezaji katika hoteli za hifadhini wamekuwa wakiwanyonya wawekezaji wazawa na hivyo kudumaza juhudi za Serikali na wananchi za kukuza uwekezaji wa ndani katika sekta ya utalii.

LESENI YA KUENDESHA BIASHARA YA UTALII (TALA LICENCE)

Mheshimiwa Spika, Licha ya hotuba ya Rais John Pombe Magufuli wakati akilizindua Bunge la kumi na moja mwezi Novemba , 2015 kueleza nia ya kuwasaidia Watanzania wanaotaka kuwekeza hapa nchini; hakuna dalili za utekelezaji wa azma hiyo ya Serikali jambo linatoa taswira kuwa kauli ile ilikuwa ni ya kisiasa tu.

Mheshimiwa Spika, nasema hivi kwa sababu kumekuwa na urasimu na tozo nyingi za kuendesha biashara hii ya Utalii jambo ambalo limekuwa ni kikwazo kikubwa kwa wawekezaji wa ndani na hivyo kushindwa kumudu ushindani katika sekta hiyo. Mzigo mkubwa umewaelemea wafanyabiashara wadogo na wengi wao wako katika hatari ya kufunga biashara hizo kwa kushindwa kupambana kwenye soko la ushindani. Kwa mfano katika malipo ya leseni , makampuni ya nje yanalipa dola elfu tano ($5000) na makampuni ya kitanzania ni dola elfu mbili ($2000).

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani ina mtazamo kwamba hiki kiwango cha (flat rate) ya dola 200 kitazamwe upya kwa kuwa kwa kuwa kinawaumiza wawekezaji wadogo/wachanga katika sekta hiyo. Mathalani, unakuta kampuni yenye magari 5 inalipa tozo sawa na kampuni yenye magari 300. Huu ni uonevu wa hali juu kwa wafanya biashara hawa wadogo na ni kinyume na kauli ya Rais katika kuwasadia wafanyabiashara wadogo. Kwa sababu hiyo, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekeza tozo ya dola 1000 kwa wawekezaji wadogo . Aidha, tunapendekeza pia orodha ya tozo ipuguzwe ili kubaki na tozo chache ambazo ni nafuu ili wawekezaji wadogo waweze kumudu.

Mheshimwa Spika, Pamoja na tatizo hilo la tozo serikali inawataka wafanya biashara hawa wadogo katika sekta hii ya utalii kuwa na uwezo wa kumiliki idadi ya magari yasiyopungua matano (5) ili waweze kupata leseni. Hii inaonyesha dhahiri kuwa Serikali hii ya CCM inataka biashara ya utalii iendele kuhodhiwa na watu wachache wenye fedha nyingi jambo ambalo linaondoa dhana nzima ya uchumi shirikishi ambapo kila mtanzania anatakiwa kuwa na fursa sawa katika kujenga uchumi wa nchi.

Mheshimiwa Spika, nasema hivi kwa sababu gharama ya kumiliki gari kwa ajili ya safari za utalii mbugani ni shilingi za kitanzania milioni 120 mpaka 200. Bei ya chini kabisa ya gari ambalo limeshatumika ,kwa umbali wa kilomita 400,000 na kuendelea ni milioni 25 na kuendelea. Kwa hali hiyo, ni vigumu sana kwa mtanzania wa kawaida kuweza kumudu gharama hizo na kuweza kumiliki magari matano ili apatiwe leseni ya kufanya biasahara ya usafirishaji wa watalii.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kubadili utaratibu wa sasa wa utoaji wa lesni kwa wafanyabiashara wanaosafirisha watalii kwa kuondoa sharti la umiliki wa magari matano ndipo wapewe leseni ya kufanya biashara hiyo. Tunapendekeza kiwango cha umiliki wa magari kama kigezo cha kupata leseni kipunguzwe hadi kufikia magari mawili.

UWEKEZAJI KATIKA IDARA YA UTANGAZAJI WA VIVUTIO VYA UTALII

Mheshimiwa Spika, Biashara ya Utalii ni matangazo. Pamoja na vivutio vingi vya utalii tulivyo navyo, kama vivutio hivyo havitatangazwa ipasavyo, tusitegemee kupata watalii wa kutosha na kwa sababu hiyo tusitegemee pia kukusanya mapato ya kutosha katika sekta hiyo. Ili tuweze kunufaika katika sekta hii kwa kiwango kinachokusudiwa ni lazima kuwe na mpango madhubuti na bajeti ya kutosha kufanya matangazo ya vivutio vyetu vya utalii nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kulieleza Bunge hili, imeandaa mpango gani wa utangazaji wa vivutio vya utalii na imetenga fedha kiasi gani kwa ajili ya kugharamia matangazo hayo kwa mwaka mpya wa fedha 2016/17. Lengo la kuitaka Serikali kufanya hivyo, ni kuisaidia kuwekeza katika utangazaji wenye tija, isije ikawa inatumia fedha nyingi kwenye utangazaji halafu faida inayopatikana ni ndogo kuliko fedha iliyotumika kufanya utangazaji. Hoja ya Kambi Rasmi ya Upinzani hapa ni kuwa na uwiano kati ya fedha tunazotumia kwenye utangazaji na tija inayopatikana (proportional result between input and output).

MIUNDOMBINU KATIKA SEKTA YA UTALII

Mheshimiwa Spika, Utalii wa nchi yetu unategemea sana huduma bora katika viwanja vya ndege. Hali ya viwanja vya ndege nchini bado hairidhishi. Hali hii inaathiri mapato yatokanayo na utalii kwa kuwa ubovu wa miundo mbinu na huduma katika viwanja hivi vinasababisha vishindwe kutumika kabisa au kutumiwa na wageni wachache kutokana na hadhi zake.

Mheshimiwa Spika, Mathalani uwanja wa Kilimanjaro International Airport (KIA) hakuna taa za kutosha za kutoa ishara nyakati za usiku na ni hatari sana kwa waongoza ndege na abiria, mashine za kupokea mizigo ziko chache sana na wageni husubiri muda mrefu sana ili kupokea mizigo na hakuna maeneo maalum lililojengwa kwa ajili ya kupokea wageni. Jambo hili linaleta usumbufu mkubwa kwa wageni na hata wale wanaowapokea wageni hao.

Mfano mwingine ni kiwanja cha ndege cha Musoma kilichojengwa kwa kiwango cha changarawe na hivyo ndege nyingi haziwezi kutua. Uwanja wa Musoma ni muhimu hasa kwa wageni wanaotembelea Mkoa wa Mara kwa shughuli za utalii wa wanyama.Ni dhahiri uwanja huo ungeboreshwa ungechangamsha zaidi shughuli za kitalii kwa kuwa ni karibu na nchi jirani ya Kenya,na pia ungehamasisha wageni kutembelea kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mheshimiwa Spika, Changamoto za miundo mbinu na huduma ziko takribani kwenye viwanja vyote nchini ikiwa ni pamoja na Songwe,JKNA, Dodoma, Kigoma n.k . Athari za Changamoto hizi zilijionyesha dhahiri wakati wa mgogoro kati ya Tanzania na Kenya ambapo Idadi kubwa ya wageni waliokuwa wanakuja Tanzania walionyesha kuwa hushukia uwanja wa Jomo Kenyatta.

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka serikali kuboresha viwanja hivi vya ndege ili kuvutia wageni wengi zaidi na hata wawekezaji wanaotamani kuleta ndege zao hapa nchini waweze kuwa na uhakika wa usalama wa ndege zao na abiria pia. Vilevile, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kuhakikisha watendaji wote ndani ya viwanja hivi wanapata elimu ya namna ya kuwahudumia wateja kwa ukarimu zaidi (customer care and hospitality).

NJIA YA MALIPO KATIKA VIWANJA VYA NDEGE NA HUDUMA MBALIMBALI ZA HOTELI KWA WATALII (MODE OF SERVICE PAYMENT)

Mheshimiwa Spika, katika viwanja vyetu vya ndege na hata mahoteli ya kitalii nchini bado malipo mbalimbali yanafanyika kwa pesa taslimu (cash payment). Takribani 9.3% ya wageni wanaoingia nchini hulipa kwa kutumia credit card na 89.8% wanafanya malipo kwa njia ya fedha taslimu kwa mujibu wa ripoti ya International Visitor’s Exit Survey Report ya mwaka 2013/2014.

Mheshimiwa Spika, nchi nyingi duniani zinatumia mfumo wa kieletroniki wa kufanya malipo mbalimbali kwa njia ya kadi yaani (credit card) . Nchi nyingi zilizoendelea hutumia mfumo huu ili kupunguza hatari za kubeba fedha nyingi ikiwa ni pamoja na kuibiwa, kupoteza n.k

Mheshimiwa Spika, wageni wanapokuja nchini hukutana na changamoto za kulazimika kufanya malipo kwa njia ya fedha taslimu ilhali wengi wao hawasafiri na fedha.Wageni hawa wanakumbana na usumbufu mkubwa wa kuchukua fedha katika mashine (ATM) ili waweze kufanya malipo. Hali hii imewafanya wageni wengi wanaoingia nchini kupata usumbufu mkubwa na kuona nchi yetu ni nchi iliyojaa urasimu.

Mheshimiwa Spika, Serikali kuendelea kuruhusu tabia ya kutumia mfumo wa kizamani wa kupokea fedha taslimu ilhali njia ya kadi ni salama zaidi kwa wageni wetu na hupunguza mianya ya wizi, ubadhirifu na hata rushwa basi huko ni kuendelea kuturudisha nyuma kusikoendana na matumizi sahihi ya mabadiliko ya kiteknolojia. Mfumo huu ukitumiwa vizuri utarasihisha kuongeza zaidi manunuzi (purchasing power) ya bidhaa zetu za kitanzania zinazouzwa katika mahoteli na maeneo mengine ya nchi.

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka serikali kuanza kuwaelimisha wadau wa sekta ya utalii kujua manufaa ya matumizi ya kadi (credit card),pia kuwahamasisha kuanza kutumia mfumo huu ili kuendana na soko la utalii la kimataifa,na kuendelea na mabadiliko ya kiteknolojia duniani.

Vilevile Kambi Rasmi inaitaka serikali kuhakikisha kuwa pale mgeni anapolipia fedha za visa anapewa risiti ya kielectroniki kama ilivyo katika mfumo wa serikali unaowataka wafanya biashara wote nchini kuzitumia.
 
Hii sekta nina hasira nayo sana...

Kiufupi Ujinga wa kwanza ambayo ni mistake kubwa sana ... Hii sekta imeshikiliwa na wahindi .. Na wageni ndio wenye mahoteli ndio wengi wao wana makampuni ya kiutalii..
Unategemea nini?

Huku ukija serikalini viongozi wetu ni wachumia matumbo wala rushwa wakubwa.

POINT HII---

Mfano..Leopard Tour ni Kampuni kubwa ya Mhindi, pia anapewa bei rahisi zaidi na Hotel & Lodges (Mhindi) anaendesha.

Sopa Lodges nazo za wahindi

Leopard owner ni Makamu mwenyekiti TATO
 
serikali yetu haina mazingira rafiki kwa sisi wazawa tunaotaka kuendesha biashara hii hapa nchin zaidi ya kuendelea kuwapigia magoti hawa wakubwa.
 
serikali yetu haina mazingira rafiki kwa sisi wazawa tunaotaka kuendesha biashara hii hapa nchin zaidi ya kuendelea kuwapigia magoti hawa wakubwa.
Ndiyo tuseme sasa hapa kwamba nini kifanyike?
 
Back
Top Bottom