Vivutio vya utalii Tanzania na faida za utalii wa ndani

Soma Media, Nenda Google search Kigwangala..

Kama wewe ni kilaza, mwombe hata Mke wako, au hata mchepuko akusomee
Umeanza vizuri. Ghafla umeondoka relini. Fuata njia usitawaliwe na hasira unaposema ukweli. Endelea kujenga hoja utaeleweka. Be patient wala usichukulie kill comment ni provocation. Huenda mjibu mada ana nia njema kuku challenge ueleweshe umma zaidi. Take it positively na uchukue kama nafasi ya kuelimisha.
 
Nimekaa nchi fulani ya bara la Asia mwaka mzima utalii wa ndani umekua kwa kasi yaani wewe unaetoka nje unaweza kwenda kutembelea sehemu ukakosa nafasi wamejaa wenyewe tuu! Nilichosikitika zaidi vivutio vyao vingi ni vya kutengeneza sio vya asili kama vyetu lakini wana uzalendo wa kupenda vyao.Ushauri wangu kwa serikali iandae watoto na vijana wa sasa kuwa wazalendo na kuipenda nchi yao ili wawe wajumbe wazuri hapo baadae halafu utalii ni kujitangaza lazima tuwe na mbinu za kujitangaza namaanisha tujitangaze mpaka kuwavutia walio nje na ndani.
 
Umejitahidi kuchambua lakini umesahau hoja moja ya msingi ambayo haisemwi lakini ni ya muhimu sana nayo ni USALAMA. Hata kama yakawepo hayo yote kama hakuna usalama ni kazi bure. Matukio ya kutekwa mauaji au kunyang´anywa mali za watu hususani inapotokea kwa wataliii wenyewe linapoteza watalii wengi sana. Matukio hayo ya utekaji na mauaji yanasambaa na kusababisha hofu kwa watalii. Hakuna ambaye atahatarisha maisha yake, USALAMA ni kitu mihimu sana.
 
Wewe ndo afisa mawasiliano wa tourism industry?
Kama ndiyo, basi Idaara ya maliasili ina budget ya kugharamia kupata taarifa na kero na maoni za wateja, itumie kulipia hii thread then JF mod wapin juu.
Na kama hawataki kugaramia mawazo? Lakini hawajakataza watu kujitolea mawazo.
 
Tozo/kodi nyingi sana.

Elimu yetu hasa watoa huduma bado sana, kitu inaitwa customer care kwa taifa letu hakijapewa kipaumbele kihivyo.
 
Changamoto kubwa inayoikabili sekta hii ambayo hata Mtoa mada imekukamata ni kuthani kuwa utalii Wanyapori na Mlima Kilimanjaro pekee. Hakuna torism product diversification. Katika ngazi ya Kitaifa, maeneo ya yanatumika kama Kumbukumbu za Taifa, Vituo vya Elimu na Mafunzo; na Vivutio vya Utalii. Aidha, katika ngazi ya Kimataifa maeneo ya kihistoria ya Tanzania yamekuwa na umuhimu wa kipekee kutokana na mchango wake katika sekta za kisayansi, kielimu, kiutamaduni na kiuchumi. Umuhimu huu ni pamoja na: kuonesha ushahidi wa Chimbuko na maendeleo ya binadamu (Zinj - Olduvai Gorge); Viumbe na wanyama wengine (Dinosaurs); Vita ya kwanza na Pili ya Dunia; Biashara ya Utumwa na vipusa na kupingwa kwake; Tawala za Kikoloni na kupingwa kwake; matumizi ya zana za mawe; na njia za awali za kuhifadhi Kumbukumbu za matukio kabla ya ugunduzi wa maandish (Nichoro ya Miambani - Kondoa).

Tanzania inasifika Kimataifa kufuatia uvumbuzi wa fuvu la ZAMADAMU aliyeishi miaka milioni 1.75 iliyopita katika Bonde la Olduvai; Nyayo za zamadamu aliyeishi miaka millioni 3.6 iliyopita huko Laetoli; uwepo wa Michoro ya Miambani Kolo -Kondoa; na miji ya kihistoria kama vile Kilwa na Bagamoyo. Aidha, Tanzania imefahamika kupitia ugunduzi wa Mijusi wakubwa (Dinasoria) katika Mkoani ya Lindi (Teandaguru) na Songwe. JE, NI WATALII WANGAPI WANATEMBLEA HAYA MAENEO ? YANA HUDUMA ZA UTALII ? KUMBUKA KUWA SIO LAZIMA SERIKALI ISIMAMIE HAYO MAENEO, SERA NA SHERIA ZINARUHUSU WATU BINAFSI KUPIGA PESA KUPITIA MAENEO HAYO.
 
Asalaam aleikum uliyo yazungumza yote ni sawa kabisa. Nimeona tatizo lingine kubwa na linalo kera kwa watalii waingiapo Julius Kambarage Nyerere Airport. Watalii huwachukua muda wa 3 hours au zaidi ili kupata visa na kulipia yaani unapanga que muda wote 3 hours to 3 hours and a half bila kujali wazee watoto na less able people ambao wa nakuja kutalii na bado wanatozwa 50 dollars each. Na hali hii nimeishudia kwa miaka mingi. Watalii wanashangaa na kuuliza je hii ndio kawaida kutumia zaidi ya masaa matatu na zaidi. Nimeongea na moja wa watalii anasema ametumia 24 hours from Australia via Qatar na hakufurahiswa na ile hali pale. There is no air conditioning no sofas or chairs he said he will think twice kuja tena Tanzania ni jambo linalo udhi na kusikitisha na uonevu kwa wageni hawa. Serikali iliangalie hili kwa jicho la tatu.
 
Natamani hii comment kuihamisha nimplelekee mhusika uso kwa uso atwambie nini kinaendelea. Kuhusu suala la wahindi na wazungu kujazana kwenye sector ya utalii ni dhahiri kwamba sisi wabongo tumeshindwa au hautuwezi. tujitadhimini wapi tunashindwa ili na sisi tuingie kwenye hiki kinyang'anganyiro tuache kutumika kama maboya.
 
Serikali ione umuhimu wa kuanzisha tv channel pekee ya kuonesha vivutio vya utalii vya ndani kama ilivo channel ya Geo wild Animals katika ving'amuzi vya DSTV,AZAM,ZUKU n.k tofauti na kutegemea TBC tu jambo ambalo linaweza kuongeza kiasi cha watalii wanao ingia nchini.
 
Sio wazo baya ila inatakiwa na sisi tuifanye kama kazi kwa kwenda kurekodi wanyama wetu
Kama una hobby hiyo na una camera zako nzuri huwezi kujua unaweza kukutana na maajabu mengi ambapo ni nadra na bahati kuona kinatokea
Wazungu wameuza sana hizi documentary na kuwa na hela ndefu sana.

Let's do it

Sent from my SM using Tapatalk
 
safi sana.
 

Nimemfiikishia mlengwa wa TTB na Imigration pale Airport waifanyie kazi. Kupanga foleni hsta mimi niliona, niliwahi kukaa siku nzima na raia wa Sierra Leon jasho lilinitoka.
 
Nimemfiikishia mlengwa wa TTB na Imigration pale Airport waifanyie kazi. Kupanga foleni hsta mimi niliona, niliwahi kukaa siku nzima na raia wa Sierra Leon jasho lilinitoka.
Na ajabu kubwa ni kwamba watu na viongozi wa naona kama vile wao hawahusiki. Hii hujuma ni kubwa. Nawakumbusha tu viongozi husika ya kwamba airports ndio kioo cha Tanzania. Mtalii (tourist) asipopata mapokezi mazuri hata Holiday yake itakua ruined na ndio ikawa mwisho wa Mtalii kuja kwetu na kutangaza kuwa Tanzania hajapapenda kwa rafiki zake au kwenye mitandao ya kijamii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Adui mkubwa wa hii sector ni ponint number mbili hapo juu. Halafu kibaya zaidi makampuni mengi yakitali hasa pale Arusha inasemekana ni ya majirani zetu.

Sasa nini kifanyike? Mimi nashauri serikali iweke mfumo mzuri na madhubuti wa ukusanyaji wa kodi kwenye hii sector maana dalili zinaonesha kutakuwa na ukwepaji mkubwa wa kodi miongni mwa wafanyabiashara ya utali.

Pili, Wizara ihakikishe ina utangaza utali wa ndani kwanza na kuweka miundombini rafiki ikiwemo kuwa na mabasi maalum kwenye vituo vikubwa
vya mabasi vitakavyokuwa vinasfirisha watu kwa bei nafuu siku za weekend kutembelea hifadhi zetu. Watanzani tunapenda kutembelea hifadhi zetu tatizo ni mlolongo mrefu na wengi hatujui wapi pakuanzi.

Wizara ihakikishe inautangaza vivutio vyetu nje, kwa kutumia michezo, balozi zetu, diaspora, nk.
 
Uko sawa kabisa mkuu. Pia utalii wa ndani muhimu hivyo uhamasishaji ufanyike na gharama zipungue za kuingia katika vivutio mbalimbali hasa vya wanyama na hifadhi za misitu ya asili nchini.
 
Tuendelee kushare information kama hizi, ili wajue na kurekebisha. Mid September nina session na watu wa uhamiaji airport kujua procedures na process za kupata visa.. ili kurahishisha kazi yangu ninayotaka kuianza. Vinginevyo ni janga unaleta wagenni unaishia kuwa stranded. Kupunguza urasimu usiokuwa na tija.
 
Ni vema watanzania tuwe na utaratibu wa kuitangaza nchi yetu kwenye mataifa mbalimbali kwa vile nchi yetu ina vivutio vingi vya kitalii vitakavyo wapendeza watalii watakaotembelea nchini.

#NajivuniaKuwaMtanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…