Vyama vinavyong'ang'ania madaraka kama CCM ndiyo huleta machafuko na mapinduzi Afrika

Vyama vinavyong'ang'ania madaraka kama CCM ndiyo huleta machafuko na mapinduzi Afrika

Napenda kukuhakikishia ya kuwa CCM itaendelea kusalia madarakani na kuongoza Taifa letu kwa kadri ya uhai wa Taifa hili. Hii ni kutokana na ubora wa sera zake zinazogusa maisha ya watu na kuwa na ajenda zinazoendana na mahitaji ya kila kundi pamoja na wakati.
 
Napenda kukuhakikishia ya kuwa CCM itaendelea kusalia madarakani na kuongoza Taifa letu kwa kadri ya uhai wa Taifa hili. Hii ni kutokana na ubora wa sera zake zinazogusa maisha ya watu na kuwa na ajenda zinazoendana na mahitaji ya kila kundi pamoja na wakati.
Yaani kwa sera CCM ni bora kuliko ANC!?

hebu weka hapa sera hata moja ya CCM ambayo wewe unaona Bora!!
 
Yaani kwa sera CCM ni bora kuliko ANC!?

hebu weka hapa sera ya CCM ambayo wewe unaona Bora!!
CCM ndio chama kiongozi Barani Afrika.ndio chama kilichobeba matumaini ya watanzania na waafrika.ndio maana watu wengi sana huja kujifunza masuala mbalimbali hapa Nchini juu yakuendesha chama katika mfumo wa kitaasisi.angalia vyama dhaifu kama CHADEMA ambavyo uchaguzi tu wa ndani unawagawa na kuwasambaratisha.ona namna Msingwa alivyokuja hadharani kuongea mambo yaliyopaswa kuzungumzwa katika vikao.
 
Napenda kukuhakikishia ya kuwa CCM itaendelea kusalia madarakani na kuongoza Taifa letu kwa kadri ya uhai wa Taifa hili. Hii ni kutokana na ubora wa sera zake zinazogusa maisha ya watu na kuwa na ajenda zinazoendana na mahitaji ya kila kundi pamoja na wakati.
🤣 🤣 🤣
 
CCM ndio chama kiongozi Barani Afrika.ndio chama kilichobeba matumaini ya watanzania na waafrika.ndio maana watu wengi sana huja kujifunza masuala mbalimbali hapa Nchini juu yakuendesha chama katika mfumo wa kitaasisi.angalia vyama dhaifu kama CHADEMA ambavyo uchaguzi tu wa ndani unawagawa na kuwasambaratisha.ona namna Msingwa alivyokuja hadharani kuongea mambo yaliyopaswa kuzungumzwa katika vikao.
🤣 🤣 🤣
 
Mjibu swali lake na siyo kuruka ruka hapa.Kwanini Mbowe yupo madarakani Muda wote? Huko CHADEMA hakuna watu wengine wenye uwezo wa kuongoza?
Hii siyo mada ya bandiko hili na wala haishabihiani na hoja yangu Kwa CCM.

Mifano nimetoa ya vyama vya siasa ila jamaa yako analeta mambo ya mtu binafsi

Kama ningekuwa nimetolea mfano wa Stephen Wasira badala ya CCM hapo ndipo ingekuwa sawa kuleta hoja ya Mbowe.
 
Hii siyo mada ya bandiko hili na wala haishabihiani na hoja yangu Kwa CCM.

Mifano nimetoa ya vyama vya siasa ila jamaa yako analeta mambo ya mtu binafsi

Kama ningekuwa nimetolea mfano wa Stephen Wasira badala ya CCM hapo ndipo ingekuwa sawa kuleta hoja ya Mbowe.
Jibu swali kwanini Mbowe amekaa muda mrefu kwenye uwenyekiti wake? Kwanini hamjambadilisha kwa kuchagua mwingine?
 
Leo nimeunganisha matukio ya vyama vikongwe vya siasa Afrika ambavyo vimeonesha weledi wake na kufanya nchi zao ziwe za kupigiwa mfano Afrika.

Chama cha kwanza ni chama cha United National Independency Party (UNIP) Cha Zambia ambacho kilitawala Zambia tangu mwaka 1964 hadi mwaka 1991.

Mwaka 1991 UNIP walishindwa uchaguzi dhidi ya chama cha Movement for Multparty Democracy (MMD) kilichokuwa kinaongozwa na Fredrick Chiluba.
Mpaka Leo Zambia kumetulia na UNIP wamekubaliana na matokeo.

Chama cha pili ni Kenya Africans National Union (KANU). Mwaka 2002 Muungano wa vyama vya siasa uliojulikana kwa jina la National Rainbow Coalition (NARC) ulishinda uchaguzi.

KANU wala hawakushughulika kupindua matokeo kama tabia ya CCM ilivyo wanaposhindwa uchaguzi. Maisha ya KANU huko Kenya yanaendelea na siasa zinasonga mbele.

Chama cha mwisho ni African National Congress (ANC) cha Afrika ya kusini.

Kwenye uchaguzi wa mwaka huu ANC imekataliwa na waafrika ya kusini. ANC wamepata asilimia arobaini (40%) wakati vyama vingine vimepata Asilimia sitini (60%).

ANC wala hawajifaragui kukubali matokeo badala yake wanatafuta kuunda Serikali na vyama vya siasa vingine walivyoshindana navyo kwenye uchaguzi.

Afrika nzima kwenye purukushani za mapinduzi na machafuko ni kule ambako vyama vilivyoko madarakani hukataa matokeo au mabadiliko.

CCM tabia yake ya kupora matokeo imewanogea hadi kwa Sasa hawaoni tena aibu kupora uchaguzi.

Walianza mwaka 1995 kule Zanzibar na baadae mwaka 2019/2020 wakaiba uchaguzi mzima.

Iko siku tabia hii ya kukataa kushindwa ya CCM italiletea Taifa letu madhara.
Mwaka 2025 CCM itashinda kwa kishindo Uchaguzi Mkuu. Hakuna chama cha kuiondoa CCM madarakani na Wajinga eti wataleta machafuko nchi hii watashughulikiwa ipasavyo!
 
Jibu swali kwanini Mbowe amekaa muda mrefu kwenye uwenyekiti wake? Kwanini hamjambadilisha kwa kuchagua mwingine?
Uelewa wako umeuweka ki-CCM Sana.

Ni sawa mtu aseme Yanga kwenye ligi ya mwaka 2023/2024 iliifunga Simba 5-1, halafu wewe useme "mbona Saido Ntibanzokiza amewahi kufunga goli 5 kwenye mechi moja!!??".

Sasa Yanga kuifunga Simba 5-1 kuna husiana vipi na Saido kufunga goli 5 kwenye mechi moja!!!

Au mnataka kumaanisha kuwa Mbowe ni sawa na CCM yote!!?
 
Uelewa wako umeuweka ki-CCM Sana.

Ni sawa mtu aseme Yanga kwenye ligi ya mwaka 2023/2024 iliifunga Simba 5-1, halafu wewe useme "mbona Saido Ntibanzokiza amewahi kufunga goli 5 kwenye mechi moja!!??".

Sasa Yanga kuifunga Simba 5-1 kuna husiana vipi na Saido kufunga goli 5 kwenye mechi moja!!!

Au mnataka kumaanisha kuwa Mbowe ni sawa na CCM yote!!?
Acha kimalezi isiyo na sababu .wewe jibu swali kwanini Mbowe amekaa muda mrefu sana kwenye Uwenyekiti? Hakuna watu wengine wenye uwezo wa kuongoza huko CHADEMA?
 
Acha kimalezi isiyo na sababu .wewe jibu swali kwanini Mbowe amekaa muda mrefu sana kwenye Uwenyekiti? Hakuna watu wengine wenye uwezo wa kuongoza huko CHADEMA?
Nawezaje kujibu swali lisilo na mahusiano na bandiko hili!??

Kujibu ni kujiabisha kuonesha sijui nilichoandika.

Mabandiko kuhusu Mbowe humu Jf yapo mengi ya kutosha nendeni huko mkajadili.
 
Leo nimeunganisha matukio ya vyama vikongwe vya siasa Afrika ambavyo vimeonesha weledi wake na kufanya nchi zao ziwe za kupigiwa mfano Afrika.

Chama cha kwanza ni chama cha United National Independency Party (UNIP) Cha Zambia ambacho kilitawala Zambia tangu mwaka 1964 hadi mwaka 1991.

Mwaka 1991 UNIP walishindwa uchaguzi dhidi ya chama cha Movement for Multparty Democracy (MMD) kilichokuwa kinaongozwa na Fredrick Chiluba.
Mpaka Leo Zambia kumetulia na UNIP wamekubaliana na matokeo.

Chama cha pili ni Kenya Africans National Union (KANU). Mwaka 2002 Muungano wa vyama vya siasa uliojulikana kwa jina la National Rainbow Coalition (NARC) ulishinda uchaguzi.

KANU wala hawakushughulika kupindua matokeo kama tabia ya CCM ilivyo wanaposhindwa uchaguzi. Maisha ya KANU huko Kenya yanaendelea na siasa zinasonga mbele.

Chama cha mwisho ni African National Congress (ANC) cha Afrika ya kusini.

Kwenye uchaguzi wa mwaka huu ANC imekataliwa na waafrika ya kusini. ANC wamepata asilimia arobaini (40%) wakati vyama vingine vimepata Asilimia sitini (60%).

ANC wala hawajifaragui kukubali matokeo badala yake wanatafuta kuunda Serikali na vyama vya siasa vingine walivyoshindana navyo kwenye uchaguzi.

Afrika nzima kwenye purukushani za mapinduzi na machafuko ni kule ambako vyama vilivyoko madarakani hukataa matokeo au mabadiliko.

CCM tabia yake ya kupora matokeo imewanogea hadi kwa Sasa hawaoni tena aibu kupora uchaguzi.

Walianza mwaka 1995 kule Zanzibar na baadae mwaka 2019/2020 wakaiba uchaguzi mzima.

Iko siku tabia hii ya kukataa kushindwa ya CCM italiletea Taifa letu madhara.
Hizo nchi ulizozitaja zina vijana wanaojielewa si kama Tz ya akina mwashambwa ambao wanaongea kiurahisi tu.kenya huwezi kumrubuni mtu,wala Zambia au Malawi.Tz watu wanagongwa hadi bia moja
 
Back
Top Bottom