Vyama vinavyong'ang'ania madaraka kama CCM ndiyo huleta machafuko na mapinduzi Afrika

Vyama vinavyong'ang'ania madaraka kama CCM ndiyo huleta machafuko na mapinduzi Afrika

Its a zero sum game.

Dola sio peremende unamega halafu unampatia mwenzio amalizie, hilo hakuna.
================

CHADEMA uzeni sera na sio vitisho.
Wizi wa kura unaofanywa na CCM wakisaidiana na vyombo vya usalama ndio sababu hatuna uchaguzi huru,JPM aliiba kura za wabunge nchi nzima, wapinzani wanashinda sana na sio siri
 
Mnasema hivi lakini kwa katiba hii ya kipuuzi mtakuja kuichoma hii nchi halafu katiba lenu la kipuuzi linazuia kupeleka mahakamani matokeo ya urais yaliyoibiwa ccm ndio italeta machafuko kwenye hii nchi kizazi cha wajinga wa vijijini kinaondoka wanabaki vijana wasiopenda upuuzi wenu wa kusifiana kijinga.
Naona umepaniki,utasubiri sana,ila kama unadhani kutatokea vurugu sababu ya CCM kushinda uchaguzi hapo umepotosha,chini ya ccm ,nchi iko salama hata kwa miaka 1000,usijitie hofu bure kijana
 
Aisee!!!

Yaani CCM huwa sijui mkoje... Mbowe anaongoza nchi gani!!??
Mkuu hapo ndipo hawa jamaa wanaonekana hamnazo, watu tunajadili mambo ya vyama yeye anamtuhu mtu, ukiambiwa watu wana mashaka na elimu yako, una anza kunaleta matusi.
 
Leo nimeunganisha matukio ya vyama vikongwe vya siasa Afrika ambavyo vimeonesha weledi wake na kufanya nchi zao ziwe za kupigiwa mfano Afrika.

Chama cha kwanza ni chama cha United National Independency Party (UNIP) Cha Zambia ambacho kilitawala Zambia tangu mwaka 1964 hadi mwaka 1991.

Mwaka 1991 UNIP walishindwa uchaguzi dhidi ya chama cha Movement for Multparty Democracy (MMD) kilichokuwa kinaongozwa na Fredrick Chiluba.
Mpaka Leo Zambia kumetulia na UNIP wamekubaliana na matokeo.

Chama cha pili ni Kenya Africans National Union (KANU). Mwaka 2002 Muungano wa vyama vya siasa uliojulikana kwa jina la National Rainbow Coalition (NARC) ulishinda uchaguzi.

KANU wala hawakushughulika kupindua matokeo kama tabia ya CCM ilivyo wanaposhindwa uchaguzi. Maisha ya KANU huko Kenya yanaendelea na siasa zinasonga mbele.

Chama cha mwisho ni African National Congress (ANC) cha Afrika ya kusini.

Kwenye uchaguzi wa mwaka huu ANC imekataliwa na waafrika ya kusini. ANC wamepata asilimia arobaini (40%) wakati vyama vingine vimepata Asilimia sitini (60%).

ANC wala hawajifaragui kukubali matokeo badala yake wanatafuta kuunda Serikali na vyama vya siasa vingine walivyoshindana navyo kwenye uchaguzi.

Afrika nzima kwenye purukushani za mapinduzi na machafuko ni kule ambako vyama vilivyoko madarakani hukataa matokeo au mabadiliko.

CCM tabia yake ya kupora matokeo imewanogea hadi kwa Sasa hawaoni tena aibu kupora uchaguzi.

Walianza mwaka 1995 kule Zanzibar na baadae mwaka 2019/2020 wakaiba uchaguzi mzima.

Iko siku tabia hii ya kukataa kushindwa ya CCM italiletea Taifa letu madhara.
ccm hawezekani kimkakati, haiwezekani kisiasa na haiwezekani kiuchumi iko kisasa mno, imeshindikana....

na kwakweli haina sabababu hata moja ya kumuibia mtu au chama ambacho hakina hata hicho kinacholalamikiwa ati kimeibiwa:pedroP:

kwa kuhitimisha,
unapotosha umma kwa uongo dhaifu sana, ambao unapaswa kupuuzwa na wana ccm wote nchini, lakini pia na waTanzania wote kwa ujumla wao :pulpTRAVOLTA:
 
Mmmh,mkuu mimi mwalimu,nipo huku liwale-lindi,ukitaka kunipata mimi njoo moja kwa moja hadi shule ya msingi mpigamiti,utanipata,sina cheo Ccm tofauti na kuwa na kadi ya chama.
Mwalimu na mwana CCM....😛😛😛😛

Waalimu hawana shida tayari CCM imezitatua kupitia "waalimu wazalendo".
 
Democratic Alliance pamoja na ku merge na vyama vingine kama Inkatha bado ni chama kile kile cha kulinda privileges za wazungu.Same old wine in a new bottle.
Hujagundua hivyo wewe ni naive na wishful thinker.
Bora wazungu kuliko wale blacks
 
Ccm haiwezi kushindwa,maana vyama ponzani havina muekekeo wa kunitetea mimi mtanzania wa chini tofauti na inavyofanya ccm
Vyama vya upinzani vikutetetee dhidi ya nani!??

Kimantiki ni kama unasema kuwa CCM (Chama kilichoko madarakani) inaonea watanzania kiasi cha kuhitaji chama cha kuwatetea.

Lakini wewe unayehitaji kutetewa ndiye huyo huyo unayetetea chama kinachosababisha uhitaji utetezi.
 
CCM hayana akili, nakumbuka years ago yalikuja na kigezo cha mgombea uraisi lazima awe na degree ili kuzuia Mbowe, katiba haisemi hivyo lakini na iko clear Kwa sifa za mgombea, I hope hii issue ingeenda mahakama Kuu tuone kama na wao Wana akili au ni chawa tuu wa executive branch
 
Ccm haiwezi kushindwa,maana vyama ponzani havina muekekeo wa kunitetea mimi mtanzania wa chini tofauti na inavyofanya ccm
Wakifanya kweli mnawateka na kuwapiga risasi kama beni na lisu wakipoa kama mbowe mnawazodoa sasa mnalolitaka litafika tuuuu
 
Wakifanya kweli mnawateka na kuwapiga risasi kama beni na lisu wakipoa kama mbowe mnawazodoa sasa mnalolitaka litafika tuuuu
Kabisa... Hawa jamaa ni zaidi ya uongo, maana wanadanganya kwenye kila jambo hadi uongo wenyewe unaonekana kuwa ni ukweli.
 
Wakifanya kweli mnawateka na kuwapiga risasi kama beni na lisu wakipoa kama mbowe mnawazodoa sasa mnalolitaka litafika tuuuu
Haliwezi fika,kizazi chako hadi cha nne kitapita bila kushuhudia haya unayoyatamani,
 
Hapa kwetu Tz hakuna hayo Mungu alishatubariki Kwa sana!

Tuna mfumo wetu wa check and balance tu bila madhara Kwa wengi pale mambo yakiwa mabaya!!

Wanaiita "safe process "wataalam wa mambo hayo!
 
Back
Top Bottom