Uchaguzi 2020 Vyama vya upinzani msipogomea uchaguzi 2020 bila tume huru tutawashinikiza sisi wanachama

Uchaguzi 2020 Vyama vya upinzani msipogomea uchaguzi 2020 bila tume huru tutawashinikiza sisi wanachama

Vyama vya upinzani chondechonde msije mkakubali kuingia kwenye uchaguzi 2020 bila tume huru.

Hulka na tabia ya jiwe na serikali yake mmeshaiona hawana aibu heshima staha Wala huruma kwenu Wala hawaifwati katiba.

Kama jiwe ameweza kuchezea uchaguzi wa serikali za mitaa bila kufanywa lolote Wala kutokea chochote msitegemee atakuwa mstaarabu octoba 2020.

Mkae mkijua kabisa Kama wakati wa JK kwa demokrasia ile tulishinda na bado tukahujumiwa vipi Sasa wakati wa dikteta jiwe?

Anzeni Sasa nawashauri mwezi huu wa kwanza usiishe kabla hamjaiambia dunia kuhusu ulazima wa kuwepo tume huru ya uchaguzi.

Bahati nzuri dunia nzima inamchukia jiwe na inamfahamu hulka yake sapoti itakuwa kubwa Sana na mwangwi wake utasikika Sana kuliko wakati wowote katika historia ya taifa letu.

Upinzani kumbukeni mnashindana na mtu asie na chembechembe ya ustaarabu hata kidogo Hilo mlijue.
JK alikuwa muungwana huyu ni kinyume chake ni mtu asie wa kawaida hivyo haitaji treatment ya kawaida.

Mkiingia kwenye UCHAGUZI bila kushinikiza tume huru mjue mmebariki suicide (mauwaji) maana ni sawa na kwenda kupigana na Askari mwenye smg wewe ukiwa na njiti ya chelewa Kama fimbo Kama silaha yako ya utetezi dhidi ya smg.

Upinzani kumbukeni watu wamechoka haya maisha wanasubiri mtu wa kumfunga paka kengele watoto wa mjini wanasema mtu wa kulianzisha au kukinukisha (kwa kufuata Sheria za nchi) mtapata sapoti kubwa mno.

Mpinzani wenu ambae ni CCM hakubaliki popote na jamii yoyote ya watanzania ila anatumia dola na propaganda kuwadanganya watu anakubalika kumbe sivyo.

Upinzani narudia Tena na Tena na Tena msije mkaingia kwenye ballot box mkitegemea favor itakuwa imekula kwenu.

Bashiru mmemsikia amesema wazi msitegemee tume huru Maana tume haipigi kura huu ni ujumbe tosha kwenu.

Polepole kawaambia wanaandaa mpango wa kutawala miaka 70 ijayo huo ni ujumbe kwenu upinzani akili kumkichwa.

Jiulizeni kwanini wanaanza kuweka mzinga/kuchonga mzinga wa mwewe (tiss) Zanzibar? Hio inapaswa kuwa alarm kwenu upinzani.

Kuna yanayofanyika gizani na hadharani kuandaa hujuma dhidi ya mazingira yoyote yatakayojiinua kuwabeba msije sema hatukuwaambia.

Kusoma hamuwezi hata picha hamuioni?

Narudia Tena upinzani mwezi huu wa January usiishe bila kutoa tamko Kali la kudai kisheria na kikatiba mabadiliko ya katiba.

Madai yenu mya file UNO/EUROPEAN UNION/ BALOZI ZOTE NK kwajili ya rejea na ufwatiliaji.

Narudia Tena mnapambana na mtu asie muungwana mkiwa soft atawaumiza mkiwa stiff atawaumiza.

Usiku mwema!!!!!

Muhimu ni hiyo katiba mpya ya warioba
 
Vyama vya upinzani chondechonde msije mkakubali kuingia kwenye uchaguzi 2020 bila tume huru.

Hulka na tabia ya jiwe na serikali yake mmeshaiona hawana aibu heshima staha Wala huruma kwenu Wala hawaifwati katiba.

Kama jiwe ameweza kuchezea uchaguzi wa serikali za mitaa bila kufanywa lolote Wala kutokea chochote msitegemee atakuwa mstaarabu octoba 2020.

Mkae mkijua kabisa Kama wakati wa JK kwa demokrasia ile tulishinda na bado tukahujumiwa vipi Sasa wakati wa dikteta jiwe?

Anzeni Sasa nawashauri mwezi huu wa kwanza usiishe kabla hamjaiambia dunia kuhusu ulazima wa kuwepo tume huru ya uchaguzi.

Bahati nzuri dunia nzima inamchukia jiwe na inamfahamu hulka yake sapoti itakuwa kubwa Sana na mwangwi wake utasikika Sana kuliko wakati wowote katika historia ya taifa letu.

Upinzani kumbukeni mnashindana na mtu asie na chembechembe ya ustaarabu hata kidogo Hilo mlijue.
JK alikuwa muungwana huyu ni kinyume chake ni mtu asie wa kawaida hivyo haitaji treatment ya kawaida.

Mkiingia kwenye UCHAGUZI bila kushinikiza tume huru mjue mmebariki suicide (mauwaji) maana ni sawa na kwenda kupigana na Askari mwenye smg wewe ukiwa na njiti ya chelewa Kama fimbo Kama silaha yako ya utetezi dhidi ya smg.

Upinzani kumbukeni watu wamechoka haya maisha wanasubiri mtu wa kumfunga paka kengele watoto wa mjini wanasema mtu wa kulianzisha au kukinukisha (kwa kufuata Sheria za nchi) mtapata sapoti kubwa mno.

Mpinzani wenu ambae ni CCM hakubaliki popote na jamii yoyote ya watanzania ila anatumia dola na propaganda kuwadanganya watu anakubalika kumbe sivyo.

Upinzani narudia Tena na Tena na Tena msije mkaingia kwenye ballot box mkitegemea favor itakuwa imekula kwenu.

Bashiru mmemsikia amesema wazi msitegemee tume huru Maana tume haipigi kura huu ni ujumbe tosha kwenu.

Polepole kawaambia wanaandaa mpango wa kutawala miaka 70 ijayo huo ni ujumbe kwenu upinzani akili kumkichwa.

Jiulizeni kwanini wanaanza kuweka mzinga/kuchonga mzinga wa mwewe (tiss) Zanzibar? Hio inapaswa kuwa alarm kwenu upinzani.

Kuna yanayofanyika gizani na hadharani kuandaa hujuma dhidi ya mazingira yoyote yatakayojiinua kuwabeba msije sema hatukuwaambia.

Kusoma hamuwezi hata picha hamuioni?

Narudia Tena upinzani mwezi huu wa January usiishe bila kutoa tamko Kali la kudai kisheria na kikatiba mabadiliko ya katiba.

Madai yenu mya file UNO/EUROPEAN UNION/ BALOZI ZOTE NK kwajili ya rejea na ufwatiliaji.

Narudia Tena mnapambana na mtu asie muungwana mkiwa soft atawaumiza mkiwa stiff atawaumiza.

Usiku mwema!!!!!
Kweli kabisa
 
Hakuna bora hapo kuchakachua ni kuchakachua tu.Wakijitokeza wengi itatengenezwa propaganda kwamba si unaona wananchi wanaunga mkono juhudi,ndo maana wamejitokeza kwa wingi kupiga kura.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana, hujanielewa nimeandika nini. Na kwa kuwa wewe ni "TruthLover" ni matumaini yangu utatulia na unisome kwa makini.

Wanaojitokeza kwa wingi kupiga kura ni kwamba wamehamasishwa na wanatambua maana ya kura zao.

Hawa hawakubali kuporwa haki yao ya kuwachagua viongozi wao. Watasimama kidete kutetea haki hiyo.

Hili halitokei/halijatokea kwa sababu watu hawajahamasishwa kukataa kunyang'anywa haki hiyo. Na wakiwa wengi hakuna mwenye uthubutu wa kuwazuia wasiidai haki hiyo.

Tume haiwezi kuwa na uthubutu wa kuchezea kura za watu (wengi) wenye hamasa ya kuilinda haki yao.

Sasa kama bado hunielewi, sina njia ya kukuelewesha.

Labda uje na swali jingine, ambalo ni hao watu hamasa hiyo wataitoa wapi? Jibu pia nimekwishaligusia kwenye yale niliyoandika mwanzo.
 
Kudai tume huru ya uchaguzi sio kosa kudai mabadiliko ya katiba sio kosa baada ya maumivu ya jiwe na CCM yake kwa miaka 5/10 hatuko tayari kabisa kumpata jiwe mwingine kwa miaka kumi ijayo !! Never shall that be allowed to happen!!! It is an oath!!!

Naunga mkono hoja post yako namba moja. Upinzani kushiriki uchaguzi huu wenye mazingira ya kishenzi ni kupoteza muda. Mimi nilipendekeza waanze hilo mwezi machi, ila hata wakianza sasa hawana la kupoteza. Na hata wakisema watashiriki, sisi wapiga kura wao hatutajuandikisha kupiga kura. Sasa ni wakati sahihi, hatuko tayari tena kwa chaguzi za kishenzi.
 
Mkuu 'Superbug', soma #3 ya Mkuu 'UmkhontoweSizwe' hapo chini.

Achana na mambo ya kudai Katiba Mpya, huu sio wakati wake, itakuwa ni kupoteza nguvu bila manufaa juu yake.

Kudai Tume Huru ndio kazi yenyewe,; lakini nayo kwa hakika sasa hivi haiwezi ikapatikana. Tume Huru haina manufaa yoyote kwa Magufuli, kwa hiyo hana sababu ya kushughulika nayo.

Njia pekee inayoweza kuileta hiyo tume ni 'shurti' isiyo ya kawaida. Sasa anza kufikiria 'shurti' isiyo ya kawaida itatoka wapi. Hapa ndipo panapohitaji kutumia vichwa ili kutafuta njia za 'shurti' asizoweza kuzikataa Magufuli.

Wewe unalo pendekezo lolote juu ya hili?

Mimi nina pendekezo kwa Vyama vya Upinzani vyote nchini.

Tokea sasa, wajitahidi kadri iwezekanavyo kuwaanda na kuwahimiza wananchi wengi kwenda kupiga kura bila ya kukosa.

Pawe na wingi wa wapiga kura ambao nchi yetu haijapata kuuona tokea tuwe na siasa za vyama vingi

Kutokuwepo kwa 'Tume Huru" isiwe sababu ya wananchi kutokwenda kupiga kura, na badala yake ndicho kiwe kichocheo cha wapiga kura wengi kujitokeza kwenda kupiga kura.

Bila shaka, vyama vya upinzani watataka watu hawa waliowahimiza kupiga kura wawape kura zao.

Hili ndio tegemeo, lakini hata kama haitakuwa hivyo lakini zile kura zikaheshimiwa na Tume Huru kumpata mshindi bila ya mizengwe, hata kama ni Magufuli atakuwa amepewa kura hizo za haki haitakuwa nongwa, na nina hakika hata wapinzani watalikubali hilo.

Maana ya watu wengi kujitokeza kupiga kura ni kuwanyima 'Tume ya Uchaguzi' kuharibu kura chache za wananchi.

Natumaini hapa utanielewa ninachokisema hapa.

Lakini najua wapo watakaoendelea kung'ang'ana kuwa haijalishi ni watu kiasi gani wamepiga kura, bado Tume itachakachua!

Ni kipi bora, wachakachue za wachache wakijua hata wakileta purukushani itakuwa rahisi kuwadhibiti, au kura za wengi, ambao kwa wingi wao wakiongozwa na hao waliowapa kura zao kudai haki yao? Jaribu kunijibu swali hilo.

Kutoshiriki katika uchaguzi kwa vyama, na kwa wananchi kutokwenda kupiga kura huo ni ushindi mnono kwa CCM. Sote tumekwishalishuhudia hili.

Ya nini kurudia makosa yaleyale ya siku zote?

Ni hivi kalamu 1, kwenda kushiriki chaguzi ambazo hujuma ziko wazi ni kupoteza muda. Tudai tume huru kwa nguvu zote, na tuonyeshe taifa na dunia hakuna uchaguzi bali ubatili. Ni bora kutokushiriki uchaguzi kuliko kushiriki uchaguzi ambao watu wataishia kupata vilema.
 
Ni hivi kalamu 1, kwenda kushiriki chaguzi ambazo hujuma ziko wazi ni kupoteza muda. Tudai tume huru kwa nguvu zote, na tuonyeshe taifa na dunia hakuna uchaguzi bali ubatili. Ni bora kutokushiriki uchaguzi kuliko kushiriki uchaguzi ambao watu wataishia kupata vilema.
Hili ni swala tofauti, kama nakuelewa.

Na kama ni hivyo ninavyokuelewa ulichoandika, sina shaka ya kuunga mkono hoja yako. Nitakubaliana nawe kama hivyo unavyopendekeza ndivyo itakavyokuwa.

Mimi ninavyokuelewa ni hivi. Nisahihishe kama nakosea.

Hakuna uchaguzi wa aina yoyote utakaofanyika bila ya kuwepo "Tume Huru."

Je, hiyo ndiyo maana yake?
Utekelezaji/uzuiaji wa uchaguzi wa aina yoyote ya uchaguzi usifanyike unawezekana?


Nitashukuru sana ukiyajibu haya.

Niseme wazi, yote mawili, yaani:
1) kuhimiza wananchi wakapige kura kwa wingi; na
2) hili la "kuzuia uchaguzi usifanyike bila ya kuwepo Tume Huru,)
Yote ni kazi ngumu sana inayowakabila vyama vya upinzani na asasi zote zinazopigania haki kuyatimiza. Ni kazi ngumu ambayo nimekuwa nikiihimiza CHADEMA waifanye kwa bidii huko mitaani, mtu kwa mtu, na mlango kwa mlango.

Hii sio kazi rahisi tu ya kukurupukia siku/miezi kadhaa kabla ya kufanyika uchaguzi.

Ni kazi ngumu, lakini ni kazi inayofanyika kwa viongozi walio na 'determination' ya kuifanya kwa ufanisi.
 
Ni hivi kalamu 1, kwenda kushiriki chaguzi ambazo hujuma ziko wazi ni kupoteza muda. Tudai tume huru kwa nguvu zote, na tuonyeshe taifa na dunia hakuna uchaguzi bali ubatili. Ni bora kutokushiriki uchaguzi kuliko kushiriki uchaguzi ambao watu wataishia kupata vilema.
Hata sijui tatizo lipo wapi. Kwamba inakuwa vigumu sana kulieleza hili jambo lieleweke vizuri.

Aina yoyote ya uchaguzi utakaofanyika chini ya 'Tume ya Uchaguzi' iliyopo sasa uchaguzi huo unakabiriwa na uchakachuaji. Hili sote tunakubaliana juu yake.

"Uchakachuaji" utakuwa rahisi zaidi kuufanya kwa wapiga kura wengi kutojitokeza kwenda kupiga kura kwa hiari yao wenyewe.
Hii ni faida kubwa sana kwa CCM.

Na kama wapiga kura wamesusa kwenda kupiga kura, wakabaki tu wanapiga makelele huko nje ya utaratibu wa kupiga kura, hizi kelele hazina maana yoyote kwa mshindi wa uchaguzi huo wa kuchakachua.

Tofautisha hali hiyo na hii hapa chini:

"Uchakachuaji" utakuwa mgumu kufanywa na "Tume ya Uchakachuaji" kama mamilioni ya wapiga kura watajitokeza na kupiga kura zao, na huku wakionya bila ya kificho, kwamba kura zao zikichakachuliwa hapatatosha.

Hawa wengi waliojitokeza kupiga kura, kura zao ushahidi upo, unaonekana hata kama uchakachuaji utafanyika. Na wakikataa kunyang'anywa haki yao, suluhu ipo wazi kwa kuangalia tu kura zilizopo, na sio zisizokuwepo ambazo walizisusia wenyewe.

Sijaandika mahali popote kutowashirikisha watu wengine, mashirika mbalimbali na hata Jumuia za Kimataifa kuunga juhudi za wananchi hawa wakiongozwa na viongozi wao kukataa kuporwa haki yao ya msingi; haki ya kuwachagua viongozi wanaowataka wao wenyewe.

Sasa, unapoweka na vitisho vya "kupewa vilema", hapo ndipo unapomaliza kabisa na kuwakatisha tamaa hata hao ambao wako tayari kutetea haki zao!
 
mada za kumkashf magu zmetosha sasa: haiwezekan kila kuamka na kulala ni negatives tu kwan hakuna mazuri yamefanyika? kwan kua upinzani inamaanisha unatakiwa kuangalia upande wa negatives tu?


cha ajab zaidi upinzani bado sana kushika nchi, jamaaa anawekeza nguvu kubwa vijijini maaana ndo kwenye watu wengi nyie mnawekeza nguvu online! this is purely bullshit
 
Cha kusikitisha si Chadema wala chama chochote kinachoonyesha kuwa na mikakati ya kudai tume huru let alone katiba mpya. Vyama havina political strategists, wanafanya tu vitu kwa mazoea.
Bila tume huru, na mimi nasisitiza sitasimama juani eti kusubiri kupiga kupiga kura. Siwezi kuwapa legitimacy wapuuzi wanaotutesa miaka na miaka.Wafanye uhalifu wao but not under my name.
 
Back
Top Bottom