Uchaguzi 2020 Vyama vya upinzani msipogomea uchaguzi 2020 bila tume huru tutawashinikiza sisi wanachama

Uchaguzi 2020 Vyama vya upinzani msipogomea uchaguzi 2020 bila tume huru tutawashinikiza sisi wanachama

Hata sijui tatizo lipo wapi. Kwamba inakuwa vigumu sana kulieleza hili jambo lieleweke vizuri.

Aina yoyote ya uchaguzi utakaofanyika chini ya 'Tume ya Uchaguzi' iliyopo sasa uchaguzi huo unakabiriwa na uchakachuaji. Hili sote tunakubaliana juu yake.

"Uchakachuaji" utakuwa rahisi zaidi kuufanya kwa wapiga kura wengi kutojitokeza kwenda kupiga kura kwa hiari yao wenyewe.
Hii ni faida kubwa sana kwa CCM.

Na kama wapiga kura wamesusa kwenda kupiga kura, wakabaki tu wanapiga makelele huko nje ya utaratibu wa kupiga kura, hizi kelele hazina maana yoyote kwa mshindi wa uchaguzi huo wa kuchakachua.

Tofautisha hali hiyo na hii hapa chini:

"Uchakachuaji" utakuwa mgumu kufanywa na "Tume ya Uchakachuaji" kama mamilioni ya wapiga kura watajitokeza na kupiga kura zao, na huku wakionya bila ya kificho, kwamba kura zao zikichakachuliwa hapatatosha.

Hawa wengi waliojitokeza kupiga kura, kura zao ushahidi upo, unaonekana hata kama uchakachuaji utafanyika. Na wakikataa kunyang'anywa haki yao, suluhu ipo wazi kwa kuangalia tu kura zilizopo, na sio zisizokuwepo ambazo walizisusia wenyewe.

Sijaandika mahali popote kutowashirikisha watu wengine, mashirika mbalimbali na hata Jumuia za Kimataifa kuunga juhudi za wananchi hawa wakiongozwa na viongozi wao kukataa kuporwa haki yao ya msingi; haki ya kuwachagua viongozi wanaowataka wao wenyewe.

Sasa, unapoweka na vitisho vya "kupewa vilema", hapo ndipo unapomaliza kabisa na kuwakatisha tamaa hata hao ambao wako tayari kutetea haki zao!

Narudia tena kalamu1, kuliko wananchi kuendelea kupata vilema huku tume ikiendelea kuwa ile ile, huko ni kupoteza wakati, bora tume iwe huru kisha watu walinde kura zao kutoka mashinikizo mengine nje ya tume. Sio watu wapige kura kwa wingi, kisha tume imtangaze waliyeagizwa na mwenyekiti wa ccm, halafu vyombo vya dola vipokee amri ya kuwaua na kuwatia vilema wasiokubali kuporwa kura. Tume ikiwa huru tutahamasisha watu kupiga kura, na sio kinyume chake.
 
mada za kumkashf magu zmetosha sasa: haiwezekan kila kuamka na kulala ni negatives tu kwan hakuna mazuri yamefanyika? kwan kua upinzani inamaanisha unatakiwa kuangalia upande wa negatives tu?


cha ajab zaidi upinzani bado sana kushika nchi, jamaaa anawekeza nguvu kubwa vijijini maaana ndo kwenye watu wengi nyie mnawekeza nguvu online! this is purely bullshit

Hayo mazuri ni wajibu wake maana anapokea mshahara, ila hana uhalali wowote wa kutupatia viongozi kwa nguvu. Hata akiua hivyo vyama, tusiomkubali hatutamkubali tu, maana humu mitandaoni sio ofisi za chama chochote useme hivyo vyama ndio vinavyomkosoa huku mitandaoni, au uwepo wa hivyo vyama ndio vinafanya yeye akosolewe humu mitandaoni. Kama umeamua kumsifia hiyo ni haki yako, kama wengine walivyo na haki ya kumkosoa.
 
Halafu wewe, eti na wewe unaweza kujiita think tank ya chama fulani [emoji22]
1. Wakigomea uchaguzi unadhani watapata nini?
2. Wamegomea uchaguzi wa serikali za mitaa, wamepata manufaa gani zaidi ya kupoteza hata mitaa/vijiji/miji/wilaya walizokuwa wanaongoza? Nani amenufaika hapa?
3. Ukitaka kujadiliana na ccm ili kuleta change LAZIMA uwe una turufu ya aina fulani mkononi. Huwezi kwenda kwenye mjadala ukiwa mikono mitupu na umetanguliza '[emoji817]' yako tu ukategemea ccm will give a f**k!
Basi ngoja wagomee uchaguzi wasipate hata mbunge mmoja uone kama wataendelea kuwa hai kama vyama vya upinzani.
Kugomea uchaguzi nayo ni Demokrasia. Hakuna chama kinalazimishwa kusimamisha mgombea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaa hakuna tume huru ya uchanguzi, then upizani mukatae kusiriki kweye 2020 uchanguzi, ile kitu kitamufanya jiwe aanguka ni SANCTIONS, na mataifa yanayotupatia misaada, hio ikifanyike jiwe hana nguvu tena, kaa hukubaliani na mimi kuhusu hili, soma kile kilimfanya raisi msaafu wa kenya hapo 1992 kuondoa ibara ya 2A katika katiba ya kenya
Unategemea NCCR na DPP watagomea uchaguzi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mada za kumkashf magu zmetosha sasa: haiwezekan kila kuamka na kulala ni negatives tu kwan hakuna mazuri yamefanyika? kwan kua upinzani inamaanisha unatakiwa kuangalia upande wa negatives tu?


cha ajab zaidi upinzani bado sana kushika nchi, jamaaa anawekeza nguvu kubwa vijijini maaana ndo kwenye watu wengi nyie mnawekeza nguvu online! this is purely bullshit
Huko vijini amefanya vitu gani vya maana?
Mbona madarasa hakuna?
Mbona wazazi wanalazimika kuchangia Tsh.10, 000 kwa ajili ya walimu wa masomo ya sayansi?
Mbona huku vijini maji ni janga kubwa?
Mbona kila mtoto anayetakiwa kuanza kidato cha kwanza analazimika kwenda na kiti na meza yake?
CCM haikubaliki bali watu wamejaa woga mioyoni mwao tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Narudia tena kalamu1, kuliko wananchi kuendelea kupata vilema huku tume ikiendelea kuwa ile ile, huko ni kupoteza wakati, bora tume iwe huru kisha watu walinde kura zao kutoka mashinikizo mengine nje ya tume. Sio watu wapige kura kwa wingi, kisha tume imtangaze waliyeagizwa na mwenyekiti wa ccm, halafu vyombo vya dola vipokee amri ya kuwaua na kuwatia vilema wasiokubali kuporwa kura. Tume ikiwa huru tutahamasisha watu kupiga kura, na sio kinyume chake.
Hakuna asiyeitaka 'Tume Huru'. Hili sio tunalopishana juu yake wewe na mimi.

Tume huru haipo, na wala Magufuli hana mpango huo kabisa wa kuwa na 'Tume' mbadala ya hii iliyopo.

Uchaguzi utafanyika chini ya hii 'Tume'; sijaona popote unapoonyesha kwamba uchaguzi hautakuwepo.
Kufanyika kwa uchaguzi ni ushindi kwa CCM,; na juu ya hili sioni popote ukilikanusha.

Watu kutokwenda kupiga kura kama unavyopendekeza hakuzuii uchaguzi usiwepo.

Kuna sababu gani za "...watu walinde kura..." kama Tume Huru itakuwa ndio inasimamia uchaguzi? Watu wanatakiwa kulinda kura zao mahali ambapo hakuna Tume Huru.

Kwa ufupi, sioni chochote unachopendekeza kitakachozuia ushindi wa CCM. Hapo shida ipo wapi!
 
Hakuna asiyeitaka 'Tume Huru'. Hili sio tunalopishana juu yake wewe na mimi.

Tume huru haipo, na wala Magufuli hana mpango huo kabisa wa kuwa na 'Tume' mbadala ya hii iliyopo.

Uchaguzi utafanyika chini ya hii 'Tume'; sijaona popote unapoonyesha kwamba uchaguzi hautakuwepo.
Kufanyika kwa uchaguzi ni ushindi kwa CCM,; na juu ya hili sioni popote ukilikanusha.

Watu kutokwenda kupiga kura kama unavyopendekeza hakuzuii uchaguzi usiwepo.

Kuna sababu gani za "...watu walinde kura..." kama Tume Huru itakuwa ndio inasimamia uchaguzi? Watu wanatakiwa kulinda kura zao mahali ambapo hakuna Tume Huru.

Kwa ufupi, sioni chochote unachopendekeza kitakachozuia ushindi wa CCM. Hapo shida ipo wapi!

Sisemi kwamba hutaki tume huru, nasema bila tume huru ni wendawazimu kushiriki upigaji kura kwenye mazingira hayo. Sina tatizo na ccm kushinda, lakini ccm imekuwa ikishinda miaka yote hata watu waliposhiriki chini ya tume hii hii isiyo huru, na sasa ni even worse. Hivyo kuendelea kushiriki uchaguzi ujao kisha tutegemee matokeo tofauti kwangu ni jambo lisilowezekana. Ndio maana nasema bora hao ccm washinde bila ushindani, na tuugeuze huo uchaguzi usiwe mada, bali mada iwe ni tume huru ya uchaguzi. Hata wao ccm wakishinda huku watu wakiwa wamesusia uchaguzi kutokana na kutokuwa na tume huru ya uchaguzi, watajikuta kwenye wakati mgumu, kuliko kushiriki kisha watoe majimbo machache kwa wapinzani, halafu wafanye upotoshaji kama tume sio huru mbona kuna wapinzani wameshinda, ni bora kutokushiriki kabisa.

Naona unashangaa iwapo kukiwa na tume huru ya uchaguzi tutaendelea kulinda kura kwanini? Tume huru hailindi kura, bali inatangaza matokeo halali. Kwani we ukifunga CCTV camera kwako hutaweka walinzi au kufuga mbwa kwa ajili ya ulinzi? Kumbuka CCTV camera Ni kwa ajili ya kuona kinachoendelea na kukupa taarifa kwa uhakika kilichoendelea ili uchukue hatua, lakini CCTV haizuii wezi. Hivyo ulinzi wa kura ni lazima iwapo tume itakuwa huru na tutajitokeza kwa wingi kupiga kura na kuzilinda, kwani tutakuwa tunaamini tume ya uchaguzi itatangaza kwa haki.
 
Sisemi kwamba hutaki tume huru, nasema bila tume huru ni wendawazimu kushiriki upigaji kura kwenye mazingira hayo. Sina tatizo na ccm kushinda, lakini ccm imekuwa ikishinda miaka yote hata watu waliposhiriki chini ya tume hii hii isiyo huru, na sasa ni even worse. Hivyo kuendelea kushiriki uchaguzi ujao kisha tutegemee matokeo tofauti kwangu ni jambo lisilowezekana. Ndio maana nasema bora hao ccm washinde bila ushindani, na tuugeuze huo uchaguzi usiwe mada, bali mada iwe ni tume huru ya uchaguzi. Hata wao ccm wakishinda huku watu wakiwa wamesusia uchaguzi kutokana na kutokuwa na tume huru ya uchaguzi, watajikuta kwenye wakati mgumu, kuliko kushiriki kisha watoe majimbo machache kwa wapinzani, halafu wafanye upotoshaji kama tume sio huru mbona kuna wapinzani wameshinda, ni bora kutokushiriki kabisa.

Naona unashangaa iwapo kukiwa na tume huru ya uchaguzi tutaendelea kulinda kura kwanini? Tume huru hailindi kura, bali inatangaza matokeo halali. Kwani we ukifunga CCTV camera kwako hutaweka walinzi au kufuga mbwa kwa ajili ya ulinzi? Kumbuka CCTV camera Ni kwa ajili ya kuona kinachoendelea na kukupa taarifa kwa uhakika kilichoendelea ili uchukue hatua, lakini CCTV haizuii wezi. Hivyo ulinzi wa kura ni lazima iwapo tume itakuwa huru na tutajitokeza kwa wingi kupiga kura na kuzilinda, kwani tutakuwa tunaamini tume ya uchaguzi itatangaza kwa haki.
Kila sehemu unakwepa hoja moja ambayo naisisitiza. Hutaki kabisa kuiona wala kuigusia.

Wenye mamlaka na uwezo wa kuleta mabadiliko nchi hii ni wananchi wenyewe. Wananchi wakisema wanataka pawepo tume huru itakuwepo, hakuna anayeweza kuizuia.

Wananchi wakiamua kwenda kupiga kura kwa wingi, hata chini ya hii tume isiyokuwa huru na wakataka kura zao zisiharibiwe, hilo hakuna yeyote mwenye uwezo wa kulikataa.

Hoja hii ndiyo unayoikwepa, hutaki kabisa kuiona, na badala yake unaweka mikwara ya hao wananchi 'kupewa vilema'!

Uhakika ni kwamba hayo unayoyasimamia ndiyo anayoyataka CCM yatokee.
 
Halafu wewe, eti na wewe unaweza kujiita think tank ya chama fulani 😢
1. Wakigomea uchaguzi unadhani watapata nini?
2. Wamegomea uchaguzi wa serikali za mitaa, wamepata manufaa gani zaidi ya kupoteza hata mitaa/vijiji/miji/wilaya walizokuwa wanaongoza? Nani amenufaika hapa?
3. Ukitaka kujadiliana na ccm ili kuleta change LAZIMA uwe una turufu ya aina fulani mkononi. Huwezi kwenda kwenye mjadala ukiwa mikono mitupu na umetanguliza '💯' yako tu ukategemea ccm will give a f**k!
Basi ngoja wagomee uchaguzi wasipate hata mbunge mmoja uone kama wataendelea kuwa hai kama vyama vya upinzani.
suluhisho ni ni unadhani tuwaangalie tu ,tushiriki wajipe ushindi?
 
Kila sehemu unakwepa hoja moja ambayo naisisitiza. Hutaki kabisa kuiona wala kuigusia.

Wenye mamlaka na uwezo wa kuleta mabadiliko nchi hii ni wananchi wenyewe. Wananchi wakisema wanataka pawepo tume huru itakuwepo, hakuna anayeweza kuizuia.

Wananchi wakiamua kwenda kupiga kura kwa wingi, hata chini ya hii tume isiyokuwa huru na wakataka kura zao zisiharibiwe, hilo hakuna yeyote mwenye uwezo wa kulikataa.

Hoja hii ndiyo unayoikwepa, hutaki kabisa kuiona, na badala yake unaweka mikwara ya hao wananchi 'kupewa vilema'!

Uhakika ni kwamba hayo unayoyasimamia ndiyo anayoyataka CCM yatokee.

Kalamu naona unakuja na maelezo mazuri lakini yote ni nadharia tupu. Kwa kawaida wananchi wanaweza kuwa na uhitaji wa jambo fulani ikiwemo hata hiyo tume huru ya uchaguzi, lakini lazima kuwe na platform na uongozi wa kuratibu hilo. Na platform hiyo ni vyama vya upinzani na viongozi wake. Hiyo katiba mpya alipokubali JK ni baada ya shinikizo kutoka kwa cdm chini ya Dr. Slaa aliposhikia bango hoja hiyo, lakini toka hoja ilipokaliwa kimya na viongozi umeona tena hiyo hamasa, au wananchi hawataki tena hiyo katiba mpya?

Asikudanganye mtu, wananchi hata wawe na uhitaji wa jambo vipi, bila uratibu wa kundi au viongozi fulani na kupewa hamasa watabaki wakiongea chini chini. Niliwahi kukuambia ww sio mpiga kura bali ni mchambuzi na mjenga hoja mzuri za kisiasa lakini hujui uhalisia wa mazingira ya kura. Hilo la watu kupata vilema tena kwa uratibu wa vyombo vya dola kwenye hizi chaguzi zetu, wala sina shaka nalo. Sasa kuliko kuendelea kuhamasisha watu wakapige kura huku tume isiyo huru ikiwa na uwezo wa kutangaza nje ya mahitaji ya wananchi, kwangu naona ni matumizi mabovu ya raslimali muda.

Kama hakuna tume huru vya uchaguzi tutakuwa hapa hapa jukwaani kwa kudra za mola, kuhamasisha watu wasishiriki hata kujiandikisha kupiga kura. Kama hiki ninachosimamia ndio matakwa ya ccm wacha iwe hivyo. Kwakuwa ww huo sio msimamo wako, na wananchi wengi wako tayari kupiga kura bila tume huru ya uchaguzi na watazillinda, uje uwahamasishe wajiandikishe kupiga kura kama utaona hiyo idadi unayoisema.
 
Kalamu naona unakuja na maelezo mazuri lakini yote ni nadharia tupu. Kwa kawaida wananchi wanaweza kuwa na uhitaji wa jambo fulani ikiwemo hata hiyo tume huru ya uchaguzi, lakini lazima kuwe na platform na uongozi wa kuratibu hilo. Na platform hiyo ni vyama vya upinzani na viongozi wake.
'Tindo' niliisoma hii, kule chini sijafika.

Nadhani huwa hunisomi, kwa maana nshaliandika hili kila sehemu na hata kwenye mjadala huu nimeliandika na kutaja jinsi ilivyo kazi ngumu kufanyika; lakini ugumu wake kufanyika sio kwamba haiwezi kufanyika.
 
'Tindo' niliisoma hii, kule chini sijafika.

Nadhani huwa hunisomi, kwa maana nshaliandika hili kila sehemu na hata kwenye mjadala huu nimeliandika na kutaja jinsi ilivyo kazi ngumu kufanyika; lakini ugumu wake kufanyika sio kwamba haiwezi kufanyika.

Mkuu ww hii uliyoniquote sijaisoma kabisa.
 
Kudai tume huru ya uchaguzi sio kosa kudai mabadiliko ya katiba sio kosa baada ya maumivu ya jiwe na CCM yake kwa miaka 5/10 hatuko tayari kabisa kumpata jiwe mwingine kwa miaka kumi ijayo !! Never shall that be allowed to happen!!! It is an oath!!!
Hata wewe Mwenyewe kwa uwezo wako unaweza kuongoza hata mtaa. Zitto Kabwe anahangaika sana baada ya kukataliwa na Madiwani wa ACT Wazalendo Manispaa ya Kigoma. 😆😆😆😆😆
 
Haya mijamaa nusu yatakuwa mazombi tu c bure
Hayo mazuri ni wajibu wake maana anapokea mshahara, ila hana uhalali wowote wa kutupatia viongozi kwa nguvu. Hata akiua hivyo vyama, tusiomkubali hatutamkubali tu, maana humu mitandaoni sio ofisi za chama chochote useme hivyo vyama ndio vinavyomkosoa huku mitandaoni, au uwepo wa hivyo vyama ndio vinafanya yeye akosolewe humu mitandaoni. Kama umeamua kumsifia hiyo ni haki yako, kama wengine walivyo na haki ya kumkosoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom