Tetesi: Vyombo vya habari vya kimataifa vyaanza kuwasili Tanzania kuelekea Sep 1(UKUTA)

Tetesi: Vyombo vya habari vya kimataifa vyaanza kuwasili Tanzania kuelekea Sep 1(UKUTA)

Halafu kwa taarifa yenu hao wamekuja shuhudia kupatwa kwa jua wapate cha kuandika kwao sio hayo mnayofikiri yatatokea Not in Tanzania God bless us
 
Yani mtu unaota ICC hii iliyomgwaya Kinyata? Ndio unataka kutwambia Magu ataenda icc? Kwa lipi?

Kuweni wakweli jamani!
 
wenzako wanakuja kuangalia TUKIO LA KIHISTORIA LA KUPATWA KWA JUA ama wenyewe wanaita SOLAR ECLIPSE
 
Mfumo wa kuongoza Nchi usiufananishe na mfumo wa kuongoza Familia ...
Logically the child analogy has similar syllogism to CDM political behaviour; thus requiring similar shaping approach.

Uwezi kupata kila kitu kila saa its simple; na tabia hizo zikiendekezwa uwafanya watu waamini mambo ndio yanavyofanyika someone has to make a stop.
 
Sasa siasa ni hoja, je wapinzani waitolee wapi kama mikutano yote imepigwa marufuku? Mtafutano wooote huu ni kuwa watu wamezuiwa kutoa hoja na wameamriwa kuwa mazezeta hadi 2020.
Si kweli kinachopingwa ni campaign type of politics watu awawezi zunguka nchi nzima kupinga serikari iliyoko madarakani halafu wakaachwa sio Tanzania tu nchi yoyote siasa hizo uisha baada ya uchaguzi au kulazimisha kuonyeshwa kwa bunge live wakati hayo ni maamuzi ya serikari wasubiri washinde warudishe lakini si kulazimisha ni haki yao.
 
H
Acheni umbeya, hasa wa kuunganisha story na matukio.

Hao jamaa wameshuka kibao hapa Songwe airport Mbeya - wanaelekea Kitulo na maeneo mengine kushuhudia kupatwa kwa jua.

Msijifariji hakuna wa kuandamana, mzungu hawezi take risk ya kuleta mwandishi wake eneo ambalo kuna security alert, sana atatumia local journalists kwa ajili ya coverage.
Nafikiri huwajui wazungu na hufikiri sawa sawa hujaona waandishi kwenye maeneo yenye vita kali kuliko hii nchi km Syria, Iraq, Libya.. japo sina uthibtisho wa ujio huo wa waandishi
 
fikirieni nje ya box tarehe 1 sept kuna kupatwa kwa jua kwanini msiseme wanakuja ili kuchuku tukio hilo??hivo vyombo vya kimataifa vilishindwa kuweka kambi yao zanzibar ambako hali mpaka sasa ni tete ndo waje leo kisa tu ya ukuta??acheni upuuzi nyie...........
 
wakifukuzwa mgogoro utakuwa mkubwa zaidi
Hivi kuna mgogoro gani
na nani hasa
ni yupi wa kukaa naye Meza moja ?
CUF wamesambaratika
UKAWA wamewaondoa CUF katika umoja wao
waliobaki ni CHADEMA
kwa hiyo CHADEMA ndio UKUTA?
basi waandamane wao km wanatikisa kiberiti cha gesi
wasitusingizie Watanzania wengine
wao wanataka tu kutawala kabla ya 2025 kabla fedha ua UFISADI haijaisha
 
  • Thanks
Reactions: bdo
Si kweli kinachopingwa ni campaign type of politics watu awawezi zunguka nchi nzima kupinga serikari iliyoko madarakani halafu wakaachwa sio Tanzania tu nchi yoyote siasa hizo uisha baada ya uchaguzi au kulazimisha kuonyeshwa kwa bunge live wakati hayo ni maamuzi ya serikari wasubiri washinde warudishe lakini si kulazimisha ni haki yao.

Wangeruhusiwa kupanda majukwwani wananchi wachuje kati ya pumba na mchele. Pili serikali ingeweza kuwakamata na kuwafungulia mashtaka ya kuikashifu serikali na uchochezi. Hili lingeruhusiwa, wala hakuna mwananchi yeyote ambaye angepoteza muda wake kuandamana kwa ajili ya watu walioshtakiwa kwa mujubu wa sheria za nchi. Kinachogomba kwa sasa ni makatazo ya jumla bila kufuata sheria.
 
Chadema tunapita kwenye tanaru la moto,
Lakini Mungu haijawah kuliacha kundi lake lunaloshikilia ukweli liaibike mbele ya wadhalimu/ccm
 
Mfumo wa kuongoza Nchi usiufananishe na mfumo wa kuongoza Familia ...[/QUOTE
si majuzi mulikiwa unatumia mfano wa nchi kama familia mlipokuwa mnamkosoa Rais Kikwete?
 
Hao wanaofikiri Tanzania ni Yemen wameptea. Waende Iraq na Syria kwa matukio yao walikofanikiwa kupandikiza chuki. Uzuri hapa vyama vyote vimegoma kuunga uhuni wa chadema wa kutumiwa na walewale wanaotaka tuendelee kuwa masikini.
Taarifa zilizotufikia punde ni kuwa baadhi ya vyombo vya kimataifa hasa vya nchi za magharibi na mashariki ya mbali vimeanza kuwasili nchini ili kushuhudia tukio kubwa la kitaifa linalotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi unao kuja (Sept 1)

Uchunguzi uliofanywa na mchunguzi wetu unaeleza wazi kuwa vyombo hivyo vya habari vya kimataifa (CNN, BBC, SBBC, CCTV ALJAZERA, RT) vimewasili nchini baada ya taarifa zilizoripotiwa na ubalozi wa Marekani kwa raia wake ambapo imeelezwa kwamba taarifa za kijasusi zinasema kunaweza kutokea maandamano makubwa yanayoweza kupelekea mapigano na uvunjifu wa amani.

Pia wapo wachunguzi wengine wanasema maandamano haya yanasukumwa na baadhi ya mataifa yenye nguvu za ushawishi duniani.

Ikumbukwe kwamba vyama vya upinzani nchini vimeandaa maandamano ya amani yanayotarajiwa kufanyika Sept 1 kama yalivyopangwa huku kukiwa na mivutano mikubwa na serikali ambapo madai ya wapinzani yanahusisha serikali kukiuka katiba.

Source: Afisa uhamiaji (uwanja wa ndege JKNIA)

MY TAKE

Kwa mjibu wa nyaraka za MOSSAD, CIA, RAW na FSB juu ya elimu ihusuyo "kiwango cha hali ya hatari katika eneo la kiraia" ambacho hupimwa kwa kipimo kiitwacho Def Cond, inasema, "Pale majadiliano ya meza yanaposhindwa kuleta jibu chanya, wanamjadala hususia meza, ambapo katika kipimo husomeka Def Cond 0001".

Ikitokea kuwa hata huko walikoamua wanamjadala hao kupeleka hisia zao nako kukazuiwa, hasira ya wanamjadala hao huongezeka na kuwa Def Cond 0002. Hatua ya mwisho ya wanamjadala hawa huwa ni kwenda kwenye mahakama ya umma, hapa kipimo husomeka Def Cond 0003.

Hiki ni kipimo kikubwa katika medani ya kiusalama kwa mambo ya ndani, ambapo matokeo yake shughuli katika jamii husimama, serikali hushindwa kutawala wala kuongoza. Katika lugha nyingine huitwa mgogoro wa ndani,kisiasa,kikatiba nk...

Zingatia hali hii haizai vita, kwani ili vita kamili ya ndani izaliwe lazima hali ya hatari isomeki Def Cond 0006. Na ili vita kamili izaliwe katika ya taifa na taifa lazima hali ya hatari isomeke Def Cond 0008.

Ulimi ndio silaha izaayo vita, na ulimi ndio silaha imalizayo vita... Hakuna silaha kubwa duniani kama Ulimi wa binadamu.
 
Wangeruhusiwa kupanda majukwwani wananchi wachuje kati ya pumba na mchele. Pili serikali ingeweza kuwakamata na kuwafungulia mashtaka ya kuikashifu serikali na uchochezi. Hili lingeruhusiwa, wala hakuna mwananchi yeyote ambaye angepoteza muda wake kuandamana kwa ajili ya watu walioshtakiwa kwa mujubu wa sheria za nchi. Kinachogomba kwa sasa ni makatazo ya jumla bila kufuata sheria.
Watu wanafanya uchaguzi kwa sababu ya kupata 'political mandate' ya kuongoza nchi kutokana na namna sahihi kwao wao, mbinu zao, ilani yao etc. Na kufanikisha hilo inataka kuongoza jamii iliyo na amani na mshikamano.

Sasa aina maana kila maamuzi yatawapendezea watu wote lakini aiondoi uhalali waliopata kidemokrasia kufanya yale waliyodhamiria katika muda waliopewa na katiba. Kama ukubali kuna njia halali za kuponda sera za serikari yes kipindi hiki upinzani kazi yao ni kukosoa tu sio kuzuia maamuzi ya serikari iliyo namamlaka halali.

Kwa dhana hizi mikutano ya hadhara, au campaign za kutaka watu waandamane kuishinikiza serikari ni siasa ambazo azikubaliki duniani kwa mtindo wa demokrasia. Uamini subiri tarehe 1 uone kama kuna mtu atashutumiwa; wewe uwezi kugoma, utoke bungeni halafu utunge uongo wako utake kuusambaza kwenye mikutano ya hadhara huko sasa ndio kuchekeana na kukubali watu wakuaribie kazi uliyoipata kikatiba.
 
Hao wazungu wanataka kumjaribu wambie hajaribiwi
 
Taarifa zilizotufikia punde ni kuwa baadhi ya vyombo vya kimataifa hasa vya nchi za magharibi na mashariki ya mbali vimeanza kuwasili nchini ili kushuhudia tukio kubwa la kitaifa linalotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi unao kuja (Sept 1)

Uchunguzi uliofanywa na mchunguzi wetu unaeleza wazi kuwa vyombo hivyo vya habari vya kimataifa (CNN, BBC, SBBC, CCTV ALJAZERA, RT) vimewasili nchini baada ya taarifa zilizoripotiwa na ubalozi wa Marekani kwa raia wake ambapo imeelezwa kwamba taarifa za kijasusi zinasema kunaweza kutokea maandamano makubwa yanayoweza kupelekea mapigano na uvunjifu wa amani.

Pia wapo wachunguzi wengine wanasema maandamano haya yanasukumwa na baadhi ya mataifa yenye nguvu za ushawishi duniani.

Ikumbukwe kwamba vyama vya upinzani nchini vimeandaa maandamano ya amani yanayotarajiwa kufanyika Sept 1 kama yalivyopangwa huku kukiwa na mivutano mikubwa na serikali ambapo madai ya wapinzani yanahusisha serikali kukiuka katiba.

Source: Afisa uhamiaji (uwanja wa ndege JKNIA)

MY TAKE

Kwa mjibu wa nyaraka za MOSSAD, CIA, RAW na FSB juu ya elimu ihusuyo "kiwango cha hali ya hatari katika eneo la kiraia" ambacho hupimwa kwa kipimo kiitwacho Def Cond, inasema, "Pale majadiliano ya meza yanaposhindwa kuleta jibu chanya, wanamjadala hususia meza, ambapo katika kipimo husomeka Def Cond 0001".

Ikitokea kuwa hata huko walikoamua wanamjadala hao kupeleka hisia zao nako kukazuiwa, hasira ya wanamjadala hao huongezeka na kuwa Def Cond 0002. Hatua ya mwisho ya wanamjadala hawa huwa ni kwenda kwenye mahakama ya umma, hapa kipimo husomeka Def Cond 0003.

Hiki ni kipimo kikubwa katika medani ya kiusalama kwa mambo ya ndani, ambapo matokeo yake shughuli katika jamii husimama, serikali hushindwa kutawala wala kuongoza. Katika lugha nyingine huitwa mgogoro wa ndani,kisiasa,kikatiba nk...

Zingatia hali hii haizai vita, kwani ili vita kamili ya ndani izaliwe lazima hali ya hatari isomeki Def Cond 0006. Na ili vita kamili izaliwe katika ya taifa na taifa lazima hali ya hatari isomeke Def Cond 0008.

Ulimi ndio silaha izaayo vita, na ulimi ndio silaha imalizayo vita... Hakuna silaha kubwa duniani kama Ulimi wa binadamu.
Wacha waje hakuna shida.. mbona 2015 October 25 walikuja tele pia kwa matumaini hayo hayo waliokuja nayo sasa na mwisho wa siku wakaishia kuripoti mastaajabu yao ya hali ilivyokuwa kinyume na matarajio yao...
Tutaendelea kuwashangaza tena kama ilivyo ada na watarudi kama walivyokuja, sana sana watakua wamekuja kutalii kwa bajeti ya mabosi wao..

TZ yetu watuachie wenyewe... hatuendeshwi kwa hisia wala vichwa vya wendawazimu...
Non of the unthinkable will ever happen on this mother land..
 
H
Nafikiri huwajui wazungu na hufikiri sawa sawa hujaona waandishi kwenye maeneo yenye vita kali kuliko hii nchi km Syria, Iraq, Libya.. japo sina uthibtisho wa ujio huo wa waandishi
UKUTA sio global news, ukilinganisha na kupatwa kwa jua. Kupatwa kwa jua kunako tarajiwa has been covered kwenye hivyo media na makala kibao duniani ili hali huo UKUTA unaandikwa na Tanzania Daima, Mtanzania labda kidogo sana na Mwananchi.

Hizo criss za Libya and et al huwezi ukaringanisha na huu upupu wa akina nanilio, hadi mtu apewe DSA ya kuja kuandika kitu ambacho hakina maana, sawa na maigizo.

In fact sioni kama kutakuwa na maandamano, never hayatakuwepo.
 
Back
Top Bottom