Waarabu wanachezea mali alizowapa Mungu wakati duniani wapo Waislamu ambao hawapati hata mlo mmoja kwa siku

Waarabu wanachezea mali alizowapa Mungu wakati duniani wapo Waislamu ambao hawapati hata mlo mmoja kwa siku

Yamekuwa hayo tena? Osama si ndo alikuwa mmiliki wa alqaida!!!!!???? Na Alqaida si nimojawapo ya magenge ya kumpigania Allah!!!! Humtendei haki Osama kumbagaza
Alqaeda na makundi mengine yote yapo chini ya zionism, lengo ni kuuchafua uislamu ili ionekane ni dini ya magaidi.
 
'Eti wataulizwa na Mungu wao'!

Hivi kutatokea siku wanadamu watawekwa kikao cha hadhara na Mwenyezi Mungu aanze kuwahojiwa maswali ambayo tayari ana majibu yake?

Kwa nini Mungu mnamchukulia poa sana na kumvisha sura ya mtu yenye madhaifu kibao?

Kwa nini mnamtweza M/Mungu kiasi hiki?
Kama wewe ni muumini utakuwa unafahamu vyema kuhusu siku ya hesabu, siku ambayo kila nafsi itaeleza iliutumia vipi muda wake hapa duniani, na kila nafsi itajibu mbele za Mungu.
 
Alqaeda na makundi mengine yote yapo chini ya zionism, lengo ni kuuchafua uislamu ili ionekane ni dini ya magaidi.
Pamoja na boko haram na Alshabab? Lakini kila wakipga tukio wanaimba kale ka wimbo maarufu "Allahu Akbar"
 
Watoto wa mnyaazi mungu mnaweza kuchekesha maiti kabisa
 
Pamoja na boko haram na Alshabab? Lakini kila wakipga tukio wanaimba kale ka wimbo maarufu "Allahu Akbar"
Kusema hivyo kila mtu anaweza kusema, pia kama huamini kuhusu hayo ni vyema ukafanya tafiti zaidi.

Vipo vitabu vinavyoeleza kuhusu hayo makundi na ni nani anayafadhili, ninavyo na ukitaka nitakupa.
 
Kusema hivyo kila mtu anaweza kusema, pia kama huamini kuhusu hayo ni vyema ukafanya tafiti zaidi.

Vipo vitabu vinavyoeleza kuhusu hayo makundi na ni nani anayafadhili, ninavyo na ukitaka nitakupa.
Ok! Vipi kuhusu kikundi kinachojiita Islamic jihad?
 
Hakuna kikundi chochote ambacho kina husiana na uislamu halisi, hao wote ni wahuni tu.

Uislamu haujatuma watu kuuwa watu wasio na hatia, kujilipua au kuchoma makanisa.
Mmmhh! Watu wanadai imeandikwa kwenye Quran tukufu kwamba msiwe karibu na sisi na mtuchije kwa upanga.
 
Katika nchi za uarabuni, huko mwenyezi Mungu ametandika kwenye ardhi mali kubwa sana ya petroli. Wanaichezea na kuitumia wale wenye nafasi za juu au viongozi tu na baadhi ya watu wachache.

Na wala hawaendi nayo mali ile katika njia iliyo nyooka, wanaharibu na kuchezea ilhali wao ndyo waliopewa wajibu na Mungu kuwatupia macho waislamu dunia nzima. Inafika wakati wanakatazana au kupunguza uzalishaji kwa kuhofia kupungukiwa wakati sio wao waliyo iweka bali ni Mungu pekee.

Zipo baadhi ya nchi wanaweza kuzalisha mamilioni ya mapipa kwa wakati mmoja, kiasi ambacho kinaweza kutumika japo robo tu kusaidia Waislamu wengine duniani ambao hata mlo mmoja kwa siku ni taabu kupatikana.

Lakni wameharibu sana na kuchezea sana mali hizo kwa mambo ambayo ni batili, sasa hivi mashekhe huko uarabuni wanashindana kununua na kustawisha timu na wachezaji wa mpira, wanalipa mabilioni ya fedha kwa vilabu vya mpira wakati duniani wapo waislamu ambao hawana hata maji ya kunywa.

Wao ndyo viongozi na wenye dhamana ya kuwatizama Waislamu wengine duniani, na hizo mali hawakupewa kwa bahati mbaya ila kuzitumia katika njia yenye manufaa.

Wataulizwa na Mungu wao walitumiaje hizo mali kuimarisha uislamu na waislamu na watakosa la kujibu.
Nani kasema tz hakuna mafuta, hakuna gesi, hakuna neuclear.

Kupanga ni kuamua. Smart leadership make it all.

Poor leaders fail us.

Kupanga ni kuchagua.

Tunaweza kuondokana na janga la uongozi endapo tutaunga kwa waarabu mfumo wao wa utawala.

Kama ilivyo vya Switzerland, uae ni state zenye ukubwa kama wilaya za mkoa wa dsm.

Lkn mfumo wao ni wa serikali za majimbo yenye uhuru zaidi au uhuru kamili wa kujiamulia mambo yake wenyewe. Badala y mfumo wa serikali kuu.

Lkn pia itikadi ya nchi inaumiza.

Tz tumeamriwa na ccm tufate itikadi ya Uesherati (Secularism) badala ya kusimama na serikali ya Uadilifu.

Hivyo tutahitaji kuwa na serikali ya dini zote badala ya hii isipokuwa na dini
 
Huyo Mungu mwenyewe huwezi kuthibitisha kwamba yupo.

Ukibisha, thibitisha yupo.
Kafiri hata ukimficha kwenye chupa lzm atoe kidole kuonyesha kuwa bado yupo.
We Nani kakuuliza habari za Mungu km sio nyodo?

Jina lako na Tabia zako zinafanana kabisa.
Kiranga kwa lugha ya kimachinga NI Nyodo au kiherehere
Kwa Hizo Nyodo zako ungekuwa mwanamke saa hii Una watoto 20
 
Lkn pia itikadi ya nchi inaumiza.

Tz tumeamriwa na ccm tufate itikadi ya Uesherati (Secularism) badala ya kusimama na serikali ya Uadilifu.

Hivyo tutahitaji kuwa na serikali ya dini zote badala ya hii isipokuwa na dini
Mkuu hapa sijaelewa kabisa
 
Waislamu ni binadamu kama wengine, na Uarabuni ndyo chimbuko la dini yao, sasa siwezi kukaa kimya nikiona waarabu wanawatenga na kutowasaidia ipasavyo waislamu wenzao duniani.
Basi madai kwamba mitume wote walikuwa waislamu ni uongo ulio dhahiri.
 
Back
Top Bottom