Wabunge wa Viti Maalum (CHADEMA) na kisa cha asiyefanya kazi na asile

Wabunge wa Viti Maalum (CHADEMA) na kisa cha asiyefanya kazi na asile

Hivi CHADEMA mlikuwa mnatafuta kurudisha kwa wananchi nchi yao iliyoporwa na CCM au mlikuwa mnatafuta posho na marupurupu ya ubunge? Comredi Mbowe, nimekuwa ninaamini seriousness yako katika ukombozi wa Mtanzania kuliko hicho kingine, labda kama sikuwa sahihi! Kweli katika uchaguzi ule ambao hata mtoto mdogo anajua ni uchafuzi mtakubali kula ruzuku haramu? Mlikuwa mnamaanisha au mlikuwa mnadanganya umma kuwa ninyi ni watu makini?

Wewe mwenyewe ulinyanganywa Bilicanas, ukavunjiwa Green houses zako, ukachajiwa kodi kubwa pale Protea, umehatarisha maisha yako mara nyingi, umefungwa gerezani, na hayo na mengine yakafanya watu wakuamini na kuiamini Chadema. Ulikuwa unatafuta watu wawe wabunge wa kuteuliwa? Sasa kuwepo ama kufa kwa Chadema kumefika. Chaweza kufia mikononi mwako na mtaitwa wasaliti wakubwa wa matumaini ya WaTz.

Fukuza wasaka tonge wote bila kujali ni akina nani. Hawafai kabisa kuwepo katika kikosi cha ukombozi wa nchi! Eti watapewa unaibu Waziri! Kweli? Ndicho mlichokuwa mnapigania? Kweli ndicho kilisababisha Lissu akapigwa risasi zile na bado akarudi kusimama jukwaani kuleta matumaini ya kurudisha haki, uhuru, na maendeleo? Usipochukua hatua sasa ya kuonyesha msimamo, huu ndio utakuwa mwisho wa Chadema. Na itaonekana kuwa wote mlikuwa mnacheza tu bila kumaanisha. Labda Lissu tu ndiye alikuwa anamaanisha.
 
Kama huzijui siasa za ndani ya CHADEMA unaweza kudhani kuna suala la kisiasa ambalo Halima Mdee anaweza kulifanya bila ridhaa ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe! Haiwezekani.

Halima Mdee ni mmoja wa watu ndani ya CHADEMA ambao ni sehemu ya Freeman Mbowe. Mwingine ni Godbless Lema na genge lake!

Kwa maana nyingine, ukimgusa kisiasa Halima Mdee unakuwa umemgusa kisiasa Mbowe! Yote anayofanya kisiasa Halima Mdee yanakuwa ni mkono wa Mbowe!

Kitu ambacho nampa hongera Mbowe ni uwezo wake wa kutumia ''wakala'' katika kutimiza malengo yake ya kisiasa. kwa wasiojua wanaweza kudhani wanapambana na ''mtu fulani'' ndani ya CHADEMA bila kujua kama wanapambana na Freeman Mbowe kwa kupitia ''wakala''.

Mbowe ndani ya madaraka anatumia nadharia inayosema, '' Always say less than necessary'' kama inavyobainishwa katika sheria ya 4 ndani ya kitabu kinachoitwa The 48 Laws of Power kilichoandikwa na Mmarekani, Robert Greene.

Kuna msema pia usemao, ''Ukiona kifaranga kipo juu ya chungu ujue chini kuna mama yake''. Hii ina maana kuwa, ukimuona Halima Mdee anatamba juu kisiasa ujue Freeman Mbowe yuko chini yake!

Muda ni mwalimu mzuri anayetoa mafunzo ya ukweli kwa wale wazito kujua au kung'amua ukweli wa mambo!
Ndiyo maana mimi huwa namkubali Mbowe kama kiongozi madhubuti. Hata katika uchaguzi ulopita alijua hakuna wa kumg’oa JPM ila akamtoa kama sadaka Tototundu. Tototundu kwa vile he is not that much intelligent, akaingia kingi.

Kwa hili la akina Halima, kiongozi asiye na mihemko lazima angefanya Mbowe alivyofanya. Usisahau chama ni gharama lazima utafute pesa ya kukiendesha. Achana na vichelema akina Retired Salary Slip even Tundu Lissu ni mihemko na uanaharakati unawasumbua
 
Naona umepata mwanya wa kuichamba Chadema Kwa hili la akina Mdee. Chuki yako haikusaidii wewe kujenga taaluma yako ya uandishi wa habari. Kama kukengeuka Chadema wanafuata nyayo zako wewe unayelamba viatu vya watawala wakuchague UDC. Nyani haoni kundule

🤣🤣🤣 mnajishtukia tu maandishi ni yaleyale ya Pasco.

gwajiBOY wa kamati kuu ndio yule yule wa green area.
 
Kama huzijui siasa za ndani ya CHADEMA unaweza kudhani kuna suala la kisiasa ambalo Halima Mdee anaweza kulifanya bila ridhaa ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe! Haiwezekani.

Halima Mdee ni mmoja wa watu ndani ya CHADEMA ambao ni sehemu ya Freeman Mbowe. Mwingine ni Godbless Lema na genge lake!

Kwa maana nyingine, ukimgusa kisiasa Halima Mdee unakuwa umemgusa kisiasa Mbowe! Yote anayofanya kisiasa Halima Mdee yanakuwa ni mkono wa Mbowe!

Kitu ambacho nampa hongera Mbowe ni uwezo wake wa kutumia ''wakala'' katika kutimiza malengo yake ya kisiasa. kwa wasiojua wanaweza kudhani wanapambana na ''mtu fulani'' ndani ya CHADEMA bila kujua kama wanapambana na Freeman Mbowe kwa kupitia ''wakala''.

Mbowe ndani ya madaraka anatumia nadharia inayosema, '' Always say less than necessary'' kama inavyobainishwa katika sheria ya 4 ndani ya kitabu kinachoitwa The 48 Laws of Power kilichoandikwa na Mmarekani, Robert Greene.

Kuna msema pia usemao, ''Ukiona kifaranga kipo juu ya chungu ujue chini kuna mama yake''. Hii ina maana kuwa, ukimuona Halima Mdee anatamba juu kisiasa ujue Freeman Mbowe yuko chini yake!

Muda ni mwalimu mzuri anayetoa mafunzo ya ukweli kwa wale wazito kujua au kung'amua ukweli wa mambo!
Chama chochote kile cha siasa huwa kina makundi madogomadogo ambayo kila kundi walio ndani yake wana strong bond kati yao na huwa wana msimamo mmoja kwa kila jambo hata kabla ya vikao rasmi vya chama. Pia kuna mahusiano ya kingono huwa yanakuwepo ndani ya makundii hayo na pia kati ya mfuasi wa chama kimoja na mfuasi wa chama kingine. Uhusiano huo wa kingono ndio hudrive decision mbali mbali au uungaji hoja fulani fulani inayotolewa na mpenzi mwenza.

Katika nchi za dunia ya tatu wengi wa wanasiasa wanawake huwa na wapenzi wanaume wanasiasa ambao huwasaidia kuwanyanyua kisiasa.
 
Chadema ipo katka bonde la uvuli wa mauti,inaelekea pabaya Sana just imagine kura zilipigwa kwa uwazi ukashindwa na ukapewa priority ya viti maalum Bado unakaidi utaki Sasa unataka nn kwa mfano,mi nampongeza Halima mdee na wengin kwa kukubali mapendekezo ya katiba
 
Mkuu uneniwahi kuandika huu uzi!

Maamuzi ya akina Mdee yana baraka zote za chama, anachofanya Mnyika huko Twitter ni kubuy time ili kuficha aibu kwa wafuasi wao waliomeza maji ya bendera y chama chao.
 
Nimepitia mabandiko yote kuhusu hili sakata lakini hili la Msemakweli lina ukweli.Hapa Mbowe kacheza mchezo wa kuwazunguka viongozi wote wa juu,na mimi naongezea ,kwa maslahi yake mwenyewe.Ameona asipoteze vyote.
Inahitaji akili ya kawaida tu kung'amua kilichoko nyuma ya pazia!
 
Mkuu kwa huu uzi wako chukua soda na kuja kulipa aisee.

Hawa kina salary slip wanatumika kama makarai tu ila hawajui A wala B
 
Nimeandika hata jana, Mbowe,Mnyika,Mdee lao moja.

Kwa mliofuatilia mahojiano ya wabunge baada ya kuapishwa jana, wanasema tunakishuru Chama kwa kutupa nafasi, tena kwa msisitizo wakirudia Mara kwa Mara Chama kuwapa nafasi.

Hakuana mbunge alieenda pale bila baraka za Mbowe.

Sitashangaa kuona Mbowe ameingia nao makubaliano kama awamu iliyopita kila Mbunge kukatwa asilimia ya mshahara kuchangia Chama lakini zote zikiishia mfukoni mwa Mbowe,Mnyika na akina Mrema pale Makao makuu.
 
Ila kwa hili Mbowe ni mjanja. Pamoja JPM kubana matumizi sanaa, bado Mbowe ataendelea kulamba bingo kama kawa. This man is so smart.
 
Back
Top Bottom