Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,470
- 40,593
- Thread starter
-
- #41
Nimeuelewa mchoro wako. Eneo nusu la uwanja (Half space) halipimwi kwa mapana bali kwa marefu. Hulitizami toka kushoto ama kulia bali toka chini kwenda juu ya mchoro wako.1)Ukitoka kwa golikipa pita katikati ya uwanja kuelekea kwa golikipa mwingine kule
2)Ukitoka kwa beki mbili nenda kwa namba saba maliza uwanja.
Half space ni katikati ya maeneo mawili niliyoeleza hapo juu. Hata ukitumia upande wa beki 3 na namba 11 pia ni half space kuna eneo ni half space.
Daaah mwanangu unachekaga kama mimi ninavyochekaga nikilisikiaga hili neno yaani wachambuzi uchwara bwana daaah inachekesha sasa wenyewe wakishalitamka hili ndo wanajiona boooonge la wachambuzi etiSiku hizi kuna double pivot....huwa nacheka mno nikisikia hii
Dah mna nongwa nyieUkimkuta Boniface Pawasa anachambua ndiyo utafurahi....!! Na mmoja wa wasafi anasauti ya kijuaji hivi halafu mbishi sana, Ki ukweli inachefua.
Unapojitwika ukamanda wa ufipa akili yako inakuwa fyongo.Shida yako muda mwingi unashinda umelewa machicha ya Lumumba!1
😀 😀
Hatari sana mkuuYes you know...
Ha! Ha! Ha! Ha! Ha!
Miongoni mwa sababu za code mixing ni kutafuta ufahari au ujiko kwamba na mimi nimo. Kiswahili kinajitosheleza mno,hawa wanapenda tu sifa kwa ile kuiga kutoka kwa wakoloni wetu.Code mix hizo na chanzo chake kikubwa ni kuto kuwa na lugha moja ya mawasiliano na kujifunzia hasa wakati wanasoma mashuleni kwahyo inapelekea mtu kuwa affected wakati wakutumia lugha kwahyo usiwalamu bari toa lawama kweny mfumo wako wa elimu na lugha ndio kweny Tatizo
Hiyo ni sawa na kutia vitunguu, nyanya na chumvi kwenye mboga,inaleta ladha flani hivi,cha muhimu ni kuwa tuanawaelewa...Huwa nakereka sana hawa jamaa wanaochambua soka la bongo wanavyopambana kufa na kupona kuongea kiingereza. Hivi hawawezi kuchambua mpira bila kuingiza hivyo viingereza vyao vya ugoko?
Badala ya kusema "Value" kwa nini wasiseme thamani?
Badala ya kusema "Flanks" kwa nini wasiseme eneo la kulia au kushoto?
Badala ya kusema "assists" kwa nini wasiseme amesaidia wengine kufunga?
Na vingereza vingine vingiiiiiiiii!!