Wadau wapinga Rais Samia na Makamu wake kuingia na Viti binafsi Kanisani, yadaiwa ni kujikweza

Wadau wapinga Rais Samia na Makamu wake kuingia na Viti binafsi Kanisani, yadaiwa ni kujikweza

Wewe hupaswi kuwalaumu hao viongozi moja kwa moja.

Erythrocyte!
Umeandika as if walikuja wamebeba viti vyao,wakati ukweli ni kwamba kama ni kasoro imetokea.na kama ni kulaumiwa ni hao waliokuwa na jukumu la maandalizi na sidhani kama ni maagizo ya Mheshimiwa Rais wala Makamu wake.
Wao wameingia na kuelekezwa mahali walipoandaliwa kukaa.

Baadhi ya vitu sio lazima uvipinge kwa sababu havina tija kwa maendeleo chanya wala havitowi fundisho lolote kwa jamii.
Pia kuwa pingapinga sio alama ya elimu bali ni dalili za ubishi usio na tija pia.

Rais akipanda basi mnasema kadharauliwa,je kipi afanye ili awafurahishe?

Mtaendeleza bifu la kukaa benchi mpaka 2025?

Si mtafika mmechoka Sana?

Mnyonge mnyongeni ila haki yake apewe.
Sasa hoja yako ni ipi? Mbona unashambulia badala ya kutoa facts?
 
Acha makelele yako Hapa kwani kipi walichozuia kisiendeelee katika ibada hiyo, wewe unafikiri Rais Ni sawa na Rais wa bendi ya mziki, Rais wa nchi lazima alindwe kwa gharama ya aina yoyote Ile kuhakikisha kuwa usalama wake unakuwa Ni salama muda wote kwa uweza mwa mwenyezi Mungu mtoa njia na maarifa kwa mwanadamu
Mwashambwa karibu sana
 
Hao ni marais wa nchi kuna suala zima la ulinzi. Vipi kama viti vya hapo hapo kanisani vikawekewa mabomu na yakawamaliza?. Huoni kama huo ni uzembe wa ulinzi.

Hii amani inatudanganya sana, tunashindwa kufikiria kwa kina.
Kwenye hii hoja, wewe ndio hujafikiria kwa kina! Kwamba waweke mabomu kwenye mabenchi au viti vya kanisani ?

Ina maana usalama wa taifa hawana vifaa vya kutambua hivyo viashiria?

Kama wana nia ya kumdhuru, watashindwa kutumia vitu vingine kama mic, podium, nk ikiwa watawaza kuweka kwenye hivyo viti??

Kwa kifupi, huo ni ukoloni usio na maana yoyote! Protocol nyingine ni za kitumwa ndio maana hata baadhi ya marais ya nchi nyingine wanazipotezea kama hazina tija yoyote!

Kubeba kiti maalum hadi kwenye nyumba za ibada, wakati viti vingine vipo, huo ni u-tu-mwa!
 
Nadhani inahusu usalama zaidi kuliko hivyo ulivyoiweka
 
Kwenye Ibada Maalum ya kumbukumbu ya miaka 23 ya kifo cha Mwalimu Nyerere , iliyofanyika huko Mkoani Kagera , Viongozi kadhaa wa Kitaifa wamehudhuria, akiwemo Mh Rais Samia Suluhu na Makamu wake , Dr Philipo Mpango , Tunawapongeza kwa jambo hilo .

Sitaki kurudia yaliyotokea ili nisiwachoshe , lakini Kitendo cha Rais na Makamu wake kuingia na Viti vyao vya enzi ndani ya kanisa kimepingwa na wadau wengi , huku wakitahadharisha viongozi kuacha kujiona ni wa kipekee , Ukweli ni kwamba HAWANA UPEKEE WOWOTE , ukiachilia mbali vyeo walivyo navyo hawana tofauti yoyote nyingine na sisi wengine .

Kitendo cha kuingia na Masofa yao Kanisani ni DHARAU KWA WAUMINI na Kanisa kwa ujumla , na kinapaswa kukemewa ili kisirudiwe tena , kama hawataki kukaa kwenye mabenchi ya kanisa , basi wasiingie kwenye Makanisa , waishie nje na hotuba zao .

Ziko Picha kadhaa zikiwaonyesha Joe Biden wa Marekani na Haikainde Hichilema wa Zambia wakiwa wameheshimu madhabau na kukalia Mabenchi ya kanisa , mbona walishiriki ibada na wakamaliza kwa amani tu , Hawa viongozi wetu wana upekee gani hawa ?

View attachment 2387287

Angalizo : Sina chuki yoyote na viongozi hawa .
Siyo chuki we una Una ugonjwa wa akili. Hao wadau ni kina nani.
 
Kwenye Ibada Maalum ya kumbukumbu ya miaka 23 ya kifo cha Mwalimu Nyerere , iliyofanyika huko Mkoani Kagera , Viongozi kadhaa wa Kitaifa wamehudhuria, akiwemo Mh Rais Samia Suluhu na Makamu wake , Dr Philipo Mpango , Tunawapongeza kwa jambo hilo .

Sitaki kurudia yaliyotokea ili nisiwachoshe , lakini Kitendo cha Rais na Makamu wake kuingia na Viti vyao vya enzi ndani ya kanisa kimepingwa na wadau wengi , huku wakitahadharisha viongozi kuacha kujiona ni wa kipekee , Ukweli ni kwamba HAWANA UPEKEE WOWOTE , ukiachilia mbali vyeo walivyo navyo hawana tofauti yoyote nyingine na sisi wengine .

Kitendo cha kuingia na Masofa yao Kanisani ni DHARAU KWA WAUMINI na Kanisa kwa ujumla , na kinapaswa kukemewa ili kisirudiwe tena , kama hawataki kukaa kwenye mabenchi ya kanisa , basi wasiingie kwenye Makanisa , waishie nje na hotuba zao .

Ziko Picha kadhaa zikiwaonyesha Joe Biden wa Marekani na Haikainde Hichilema wa Zambia wakiwa wameheshimu madhabau na kukalia Mabenchi ya kanisa , mbona walishiriki ibada na wakamaliza kwa amani tu , Hawa viongozi wetu wana upekee gani hawa ?

View attachment 2387287

Angalizo : Sina chuki yoyote na viongozi hawa .
Uzuri wa mleta hoja ni anajadili kistaarabu. Naomba kukuuliza, ni wadau gani waliopinga? Facts.🙏🙏🙏
 
Hii nchi watu wana obsession na mambo yasiyo na msingi.

Kiti gani Rais amekalia, inageuka topic.

Watu wanadhani Rais anaamka asubuhi na kusema leo nataka nikakalie kiti fulani! Never, hizo ni kazi za watu.
 
Hahaaaa ww hata historia ya dini yako huijui kubishana na ww ni ujinga....kasome tena vitabu ndo utajua ...swali dogo tu nambie msikiti walio kua wanasali waislam kabla ya mtume uko wapi.
Mingi tu, Hata pale Jerusalem kwenye msikiti wa Nabiii suleiman waliswali
 
Back
Top Bottom