Wadau waulizia alipo Mwana CCM Thadei Ole Mushi

Wadau waulizia alipo Mwana CCM Thadei Ole Mushi

Nimeona X-Mayor wa Ubungo Bwana Jacob akiripoti kwamba OLe MUSHI anaumwa na inasadikiwa amepewa sumu. Inaelezwa kuugua kwake ni siri na yupo Sehemu ya siri; wanadai wanasiasa wenzake wamemtenga na hakuna juhudi za kumfikisha hospital.

Nitoe rai kwa wanaohusika au familia watoke adharani kusema na jamii kuondoa uzushi huu unaolenga kubomoa taswira njema ya serikali ya kuwalinda wakosoaji wake. Serikali imejipambanua wazi kwamba haitishwi na wakosoaji hivyo ni vigumu wakosoaji wakapata madhara kiafya kisa wamesema vibaya chama au serikali.

Lakini pia nitoe wito kwa wanachama wa CCM kujiamini na kutosubiri maelekezo yakumsaidia binadamu anapopatwa na matatizo. Wenzenu CHadema wamewezaje kuwa wasemaji wema kwa wana CCM wanapougua au kupata majanga? Kwanini CHadema wawe wakwanza kutoa taarifa za msaada kwa mwana CCM?

Nape alipopata msaada marafiki wote wakamkimbia wakabaki wana harakati na CHadema kumsemea, same applies to mzee Kinana na hata akina polepole. Ninyi wahanga wanufaika wa siasa mnakosaje kujifunza kwa wenzenu?

Siasa zinapofika mahali zikakunyima uhuru wa kwenda msibani ,hospital au kwa mwanadamu mwenzako anayepitia kadhia flan basi hizo fikra za siasa zimekutenga na roho wa Mungu.

Kama ni kweli Ole MUSHI unaumwa tukutakie afya njema . Usisite kujitokeza kuomba msaada maana watu wema bado wapo na wanasubiri wito wako.
Ccm na tuvikundi vyenu ,mpo na matatizo sana, mwanaccm kuikosoa au kua na msimamo tofauti haijawai kuwa na afya kwa mwanachama husika, hii tabia haijaanza leo ndani ya ccm bali tangu kipindi cha Nyerere, sema kwa sasa mmezidi,

Leo huwezi kutuaminisha kwamba ni vigum wanachama wenu kuweza dhuliwa na wanaccm wenzake, inawezekana sana , kati ya chama chenye mambo ya kutendeana vibaya wanachama kwa wanachama, kufitiana, kubaguana Afrika basi ccm ni no moja,

Na kwa kweli nchi hii ukitaka ishi maisha ya amani moyoni bila kujali nafasi yako katika jamii, kaa mbali na ccm ,wasikuzoee na usiwazoee, kaa bila chama au chagua majukwaa huru, kupitia vyama vingine ila sio ccm.

Wanaccm ni nyama zinazotembea ila roho ya ubinadam, hofu ya Mungu kwao ni kama ardhi na mbingu hamna kitu pale,

Alafu unamkuta kijana , au mtu na akili yake eti ukitaka kutoboa lazima uwe ccm , pumbavu, fuatilia vizuri kuanzia wafanyabiashara wakubwa, wadogo , hao wajifanyao wanachama kindakindaki nini kipo nyuma yao , kama sio kulinda madili yao kupitia mgongo wa uanachama wa ccm (wizi ,ujangili n.k)

Be strong wewe, ccm sio Mungu, baba yako au mama yako , maisha na mafanikio yako yapo mikononi mwa Mungu wala sio ccm
 
CCM KWANINI MNATAKA KUMUUA THADEI OLE MUSHI......!

Nimepokea kwa masikitiko na mshangao mkubwa sana taarifa ya shambulio la ghafla linaloaminiwa kuwa la "SUMU" dhidi ya mwana CCM machachari na mkosoaji wa Serikali ya CCM ndugu yetu Thadei Ole Mushi

Baada ya kupata taarifa za siri kuhusu kulishwa/kunyweshwa au kushambuliwa kwa sumu ndugu Thadei Ole Mushi

Mimi Boniface Jacob nimefanya jitihada za kumtafuta Thadei Ole Mushi na kuchunguza ukweli wa taarifa hizo

Nimejiridhisha kwamba Thadei Ole Mushi yuko katika hali mbaya inayoonekana siyo ya kawaida kwake

Yupo mkoani Dodoma (sehemu ni siri) akiwa na mke wake ambaye nimepatiwa namba yake na mtoa taarifa wangu.

Kinacho nisikitisha ni ndugu Thadei Ole Mushi kukosa msaada wa kuletwa hospitali kubwa kama Muhimbili jijini Dar es Salaam

Wakati nikiwa nimejiridhisha kuwa Thadei Ole Mushi hayupo katika hali ya kawaida, ndugu na watu wale wa karibu wa Thadei Ole Mushi wanaonekana kujitahidi kumficha na kuficha taarifa za ugonjwa wa Thadei Ole Mushi na wakati mwingine kuogopa kutoa taarifa za nini kimemkuta ndugu yetu.

Thadei Ole Mushi ni mwana CCM kindakindaki na mkosoaji mkubwa wa chama chake na serikali yake ya CCM, lakini haiondoi ukweli kuwa Thadei Ole Mushi ni mtu muhimu kwa CCM na siasa za Tanzania kama mchambuzi wa siasa nilifikiri CCM na Serikali yake ilitakiwa kutoa umuhimu mkubwa kwa Afya ya Thadei Ole Mushi hata kama hawakubaliani naye baadhi ya misimamo na mawazo yake.

Nikifikiri Jinsi Thadei Ole Mushi alivyokaribu na baadhi ya viongozi wa CCM na Serikali kama katibu Mkuu wa CCM Bw. Daniel Chongolo, wabunge kama akina Charles Kimei, wakuu wa Mikoa kama Anthony Mtaka, Mawaziri na manaibu kama Ridhiwani Kikwete bado nashangaa kwanini Thadei Ole Mushi atelekezwe wakati muhimu kama huu wa kupigania Afya yake.

Kwa namna ambavyo marafiki zake wa CCM na viongozi Serikali wanavyo muacha Thadei Ole Mushi kwa kumuacha apambane na hali yake ni dhahiri huenda wabaya wa Thadei Ole Mushi wapo CCM au kutoka ndani ya serikali ya CCM

Ni wakati sahihi sasa familia ya Thadei Ole Mushi itoke hadharani ituambie nini kimemkuta ndugu yetu katika siasa na mtanzania mwenzetu haraka na mapema tuweze kushiriki kunusuru uhai wake kabla hatujaijumuisha familia yake kama sehemu ya watu wabaya wa Thadei Ole Mushi.

Sisi Watanzania tupo tayari kumpambania na kumuokoa ndugu yetu Thadei Ole Mushi

Mtoeni mlipomficha, mpelekeni hospitali na kama gharama za matibabu ni kubwa tujulishwe tuweze kuchangia haraka sana.

Boniface Jacob
 
Alijianika mno

Walivyo CCM muda huu atakuwa wanahesabu kunyanzi za mfuko wake wa gololi huko kusikojulikana.

Ni jinai mwanaCCM kuikosoa CCM hadharani, ataambiwa atumie vikao halali. Ukiuliza vikao vipi hivyo kwa asiye kiongozi? Ataishia kupimwa mkojo[emoji1787]

Ccm sio chama cha siasa bali ni genge la walaghai na matapeli[emoji28][emoji28]
 
Karibu kila mahali na mitandaoni kote wadau mbali mbali wanaulizia aliko Mchambuzi Mahiri na Mtetezi kabambe wa siasa za CCM, Bwana Thadei Ole Mushi.

Kwani ni kipi kimemtokea huyu Jamaa?

View attachment 2781579
Wana jamiiforums ni familia moja imara na yenye upendo dhabiti, ni jambo la heri kuulizia ili kufahamu alipo au ni nini kimemsibu mwenzetu. Huo ndio utamaduni na upendo wa wana jamiiforums!
 
CCM KWANINI MNATAKA KUMUUA THADEI OLE MUSHI......!

Nimepokea kwa masikitiko na mshangao mkubwa sana taarifa ya shambulio la ghafla linaloaminiwa kuwa la "SUMU" dhidi ya mwana CCM machachari na mkosoaji wa Serikali ya CCM ndugu yetu Thadei Ole Mushi

Baada ya kupata taarifa za siri kuhusu kulishwa/kunyweshwa au kushambuliwa kwa sumu ndugu Thadei Ole Mushi

Mimi Boniface Jacob nimefanya jitihada za kumtafuta Thadei Ole Mushi na kuchunguza ukweli wa taarifa hizo

Nimejiridhisha kwamba Thadei Ole Mushi yuko katika hali mbaya inayoonekana siyo ya kawaida kwake

Yupo mkoani Dodoma (sehemu ni siri) akiwa na mke wake ambaye nimepatiwa namba yake na mtoa taarifa wangu.

Kinacho nisikitisha ni ndugu Thadei Ole Mushi kukosa msaada wa kuletwa hospitali kubwa kama Muhimbili jijini Dar es Salaam

Wakati nikiwa nimejiridhisha kuwa Thadei Ole Mushi hayupo katika hali ya kawaida, ndugu na watu wale wa karibu wa Thadei Ole Mushi wanaonekana kujitahidi kumficha na kuficha taarifa za ugonjwa wa Thadei Ole Mushi na wakati mwingine kuogopa kutoa taarifa za nini kimemkuta ndugu yetu.

Thadei Ole Mushi ni mwana CCM kindakindaki na mkosoaji mkubwa wa chama chake na serikali yake ya CCM, lakini haiondoi ukweli kuwa Thadei Ole Mushi ni mtu muhimu kwa CCM na siasa za Tanzania kama mchambuzi wa siasa nilifikiri CCM na Serikali yake ilitakiwa kutoa umuhimu mkubwa kwa Afya ya Thadei Ole Mushi hata kama hawakubaliani naye baadhi ya misimamo na mawazo yake.

Nikifikiri Jinsi Thadei Ole Mushi alivyokaribu na baadhi ya viongozi wa CCM na Serikali kama katibu Mkuu wa CCM Bw. Daniel Chongolo, wabunge kama akina Charles Kimei, wakuu wa Mikoa kama Anthony Mtaka, Mawaziri na manaibu kama Ridhiwani Kikwete bado nashangaa kwanini Thadei Ole Mushi atelekezwe wakati muhimu kama huu wa kupigania Afya yake.

Kwa namna ambavyo marafiki zake wa CCM na viongozi Serikali wanavyo muacha Thadei Ole Mushi kwa kumuacha apambane na hali yake ni dhahiri huenda wabaya wa Thadei Ole Mushi wapo CCM au kutoka ndani ya serikali ya CCM

Ni wakati sahihi sasa familia ya Thadei Ole Mushi itoke hadharani ituambie nini kimemkuta ndugu yetu katika siasa na mtanzania mwenzetu haraka na mapema tuweze kushiriki kunusuru uhai wake kabla hatujaijumuisha familia yake kama sehemu ya watu wabaya wa Thadei Ole Mushi.

Sisi Watanzania tupo tayari kumpambania na kumuokoa ndugu yetu Thadei Ole Mushi

Mtoeni mlipomficha, mpelekeni hospitali na kama gharama za matibabu ni kubwa tujulishwe tuweze kuchangia haraka sana.

Boniface Jacob
 
Jamaa ameonekana leo kwenye page yake ya facebook.
 

Attachments

  • IMG_20231015_163202.jpg
    IMG_20231015_163202.jpg
    56.5 KB · Views: 6
Kada wa chama cha mapinduzi Ole Mushi amejitokeza kwenye Ukurasa wake wa Facebook na Kukanusha kuhusu kulishwa Sumu

Hivi karibuni kuliibuka sintofahamu kuhusu alipo kada huyu ambaye alipotea kwa muda kwenye mitandao ya kijamii, Kada huyu ambaye alikuwa mkosoaji pia wa baadhi ya Viongozi wa chama Chake cha CCM.

Hata hivyo Jana iliibuka taarifa kuwa Ole Mushi alilishwa sumu na watu wasiojulikana, Kabla ya yeye kuibuka kwenye mtandao wa Facebook na mada ya kumpinga Martin Maranja kuhusu Kuongezeka kwa Deni la Taifa.

'' Ufafanuzi wa mimi kulishwa Sumu'

Naomba kuwapa taarifa kuwa jambo hili ni Uzushi usiokuwa na Maana lililoibuliwa na watu kwa nia wanazozijua wao wenyewe. Mimi nipo salama kabisa japokuwa nilikuwa nimepumzika kidogo kuandika kwenye Social Media.

Hata hivyo nawashukuru nyote kwa kuonyesha upendo wenu kwa kunitafuta hapa na pale pindi mlipoona nipo Kimya kwa Muda Mrefu. Kunitafuta kwenu bila kuchoka kumenionyesha pia thamani yangu katika kuwasiliana na ninyi kupitia Ukurasa huu. Niwape taarifa kuwa nimerudi na tutaendelea kusomana hapa katika majadiliano ya mambo mbalimbali yayohusu jamii yetu kwenye nyanja zote (Siasa, Uchumi, Michezo nk)

Kidumu Chama cha Mapinduzi.

Ole Mushi
0712702602
 
Mleta mada, una uhakika kaandika yeye mwenyewe au unaamini kaandika mwenyewe kisa ni ukurasa wake?
Think beyond your nose na hatakama ni kweli kaandika, unaamini kaandika pasipo maelekezo ya nini aandike?
Think big even if you are not big.
 
Back
Top Bottom