Wafanyabiashara Stendi ya Magufuli wataka mabasi yote yashushe na kupakia abiria hapo stendi ili wapate wateja

Ok sasa kila abiria atashushwa anapoishi Dar es Salaam hii?! mhmm haya ngoja nikae na ujinga wangu.
Ndio mtu ashushwe kwenye wilaya yake anapoishi

Mtu anaishi wilaya ya Kinondoni basi linatoka Moshi au Arusha linapita wilaya ya Kinondoni anapoishi liende likamshushe wilaya ya ubungo halafu aanze kutafuta Usafiri wa kutoka wilaya ya ubungo arudi nyuma kwake wilaya ya Kinondoni huo ni ujinga wa kiwango Cha lami
 
Acha taralira zako ndugu. Na treni na ndege unasemaje?
 
Mbona ndege huwa hamuombi mshushwe kwenu mnakubali kwenda airport? Utaratibu wa vituo ni muhimu sana, mkifanya shaghala baghala msilalamikie mfumo na utaratibu wa serikali.

Sasa Stand ya bus ya nini kama unaweza panda na kushuka popote?
Acha kufananisha abiria wa ndege nawa kwenye bus abiria wengi wapanda ndege wana vipato vizuri ndo maana wanakodi magari au kuja na magaria yao ila abiria wengi wa ma bus vipato vyetu ni vya kawaida sana, Kingine airport ni sehemu salama sio pale magufuri pamejaa wezi na matapeli.
 
Ujinga mtupu let nature work, huwezi kumlazimisha abiria kununua bidhaa, semeni mnataka bajaji na daladala zenu zipige pesa kama mnavyotoza abiria kiingilio cha stand wakati wana ticket, wizi mtupu
 
Kwani hapo mbezi hakuna watu wanaoishi hapo?
Hao ndio watapanda na kushuka hapo stendi kuu.
Au hakuna watu wanaosafiri wanaoishi Mbezi ?
Yaani basi la lindi limpitishe abiria nyumbani kwake Vikindu, na likamshushe Mbezi ilimradi tu anunue maji na tishu
Halafu aanze kutafuta usafiri mwingine wa kurudi Vikindu.

Kama hapo mbezi hakuna abiria wanaoishi hapo, basi aliyejenga hiyo stendi alikuwa mwehu.
 
Mbona ndege huwa hamuombi mshushwe kwenu mnakubali kwenda airport? Utaratibu wa vituo ni muhimu sana, mkifanya shaghala baghala msilalamikie mfumo na utaratibu wa serikali.

Sasa Stand ya bus ya nini kama unaweza panda na kushuka popote?
Mfano wa ndege ni irrelevant.
 
kurasa zote nimesoma sijaona aliyeongelea sababu za mabasi kukwepa stendi ya mkoa
Kwenye soko huru na lenye ushindani, huwezi kulazimisha washindani wa kibiashara wafanye biashara kwa mbinu moja. Ndio maana stendi zipo nyingi, Kigamboni, magomeni, Urafiki, chanika etc. kulazimisha stendi iwe mmoja ni impracticable.
 
1. Kwani mtu anayeshuka uwanja wa ndege na anakaa Kunduchi huwa anafikaje nyumbani...?

2.Kwanini gari ziende Shekilango au Mnazi mmoja .....?
 
Huu ni upumbavu wanawalipia nauli ,wajinga kweli hawa
 
Kwenye soko huru na lenye ushindani, huwezi kulazimisha washindani wa kibiashara wafanye biashara kwa mbinu moja. Ndio maana stendi zipo nyingi, Kigamboni, magomeni, Urafiki, chanika etc. kulazimisha stendi iwe mmoja ni impracticable.
Miundombinu ya usafiri mkubwa na uchukuzi(Uwanja wa ndege, stendi za Mabasi,Bandari kavu)huwa inatakiwa iwe nje kidogo ya mji....ili
  • kuondoa msongamano wa magari barabarani...
  • Kupunguza uharibifu wa barabara za ndani ya mji
 
Biashara zenyewe ni maji ya kunywa, sambusa, Mikate ya zaidi ya siku 4 toka izalishwe, etc magazeti ya zamani na vitabu visivyo na tija! Chaja na vifaa vingine vya simu visivyo na ubora na pombe za kwenye vichupa vya plastic.Kuingia ndani ni Tzs 500 kwa abiria:
 
Yakipaki nje hayalipi, na sio utaratibu. Abiria wanatakiwa kupanda na kushuka ndani ya bus stand terminal.
Sikubaliani na hili. Hakuna basi linapaki nje ya stendi ya Magufuli, labda Kama unamaanisha stendi nyingine tofauti na ya Magufuli. Tulikosea kuhamisha stendi ubungo bila kutafakari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…