Wafanyabiashara wa Kariakoo wagoma kuhama kupisha Wawekezaji




Shida ya watu kama nyie ni kukariri mambo hilo ni moja ya soko maarufu mjini Hong-Kong hilo eneo per square meter ni most expensive duniani. Sio mbali na hayo majengo ni downtown yao sasa yanafania ni vitu vilivyoangushwa maeneo ya Financial sector huko kwao.

Hivi unadhani capital city ya safe heaven as well as legit Financial services ina shortage ya mitaji ya kuvunja hizo dilapidated properties za street markets. Wanayaacha kwa sababu ya kulinda identity ya eneo na tamaduni za watu wao.

Sisi badala ya kutaka kuona kariakoo tunaondoa vibaka iwe sehemu salama ya watalii kuweza kuja kununua vitu vya kitanzania; kama kwingine duniani tunataka kuibadilisha.

Nimekuwekea na article ya kwanini giants supermarkets za west nyingi zilishindwa mainland China; kwanza upewi eneo la uwekezaji wa retail karibu na popular street markets ili kulinda long customs zao.

Embu waafrica acheni ushamba wa kudhani kila kitu lazima kibadilike.

Ukirudi huko kwenye huo mkataba unaotetea subiri hao wafanyabiashara waende mahakamani halafu mkataba udadavuliwe kwa terms z commercially contracts. Ndio utaelewa kwa hiyo notice waliyotoa NHC lazima walipe fidia ni mda mdogo mno; hapo watu wanahitaji si chini ya miaka miwili kuwatoa wenye maduka yao.

Mnatoa mambo vichwani mwenu tu na kubwabwaja as if kwenye hii dunia hakuna kanuni za kuishi na kufanya mambo.
 

We jamaa kwan umeshikilia maduka mangapi apo [emoji28]au ndio wale wale mnaokodisha mara mbili frem ...karibia frem nying kkoo za nhc watu wanalipa kodi zaid ya ile inayotakiwa
Na hii ni kutokana na madalali kama nyie
 
We jamaa kwan umeshikilia maduka mangapi apo [emoji28]au ndio wale wale mnaokodisha mara mbili frem ...karibia frem nying kkoo za nhc watu wanalipa kodi zaid ya ile inayotakiwa
Na hii ni kutokana na madalali kama nyie
It’s principles kutetea au kupinga kitu sio lazima uwe mnufaika wa moja kwa moja.

Na hiyo hatua ya NHC ni immoral
 
We unaongea huna Abc zozote za Biashara kila kitu unaleta siasa.

Kariakoo Majengo ya Wakinga, Wachaga, Waarabu yana ghorofa 5 ama 6 yanabomolewa sababu tu hayana Frame basement watu wanaanza upya.

Serikali inakosa mabilioni ya mapato eti bado frame zao ni laki kadhaa halafu mikubwa unakuta jengo zima lipo mtaaa mzima lina frame hata 10 hazifiki. Na wanaokodi wanauza vitu vya kipuuzi puuzi sababu anajua ata afford kodi, mtu anachukua Frame ya NHC anauza soda na Vitafunwa kama Keki na Biscuit.

Angalia jengo la swahili plaza lile ni ubia wa serikali na Mtu binafsi, Frame ya ndani ni 1.2M serikali inapata,

Hata mtu Binafsi ajenge achukue asilimia 50 bado Serikali itapata Mapato makubwa kuliko huu Upuuzi wa sasa.
 
Nyumba nyingi za NHC wamezulimumiwa watu binafsi na Nyerere, na nyingi zilikuwa za Watanzania wenye asili ya Asia.

Hakuishia hapo akatuzulumu Tanganyika yetu kwa lengo la "kuwameza"Wazanzibari sasa tumemezwa sisi, ujanja mwingi mbele giza.
Watanzania asilia wakati hata tofali,cement hawajatoa kwenye
Ujenzi wa nyumba hizo

Ova
 
Pole kwa kupewa notice ila njoo uwekeze huku chanika , fremu bei chee tu hata laki moja haifiki.Sio lazima mjazane hapo city center
 
Hayo ndo majibu ya serikali dhidi ya ule mgomo

Wanatafutiwa angle waumie

Tanzania hivi sasa ni ugali moto, mchuzi moto
 
Kuna sehemu nyingi za kujenga majengo ya kisasa na mazuri.

Kuna video nimeitafuta ya muda sijaipata wale wazungu walioenda tembelea kariakoo na kuporwa. Hiyo sio sehemu salama kwa sasa.

Lakini ikiboreshwa kwenye ulinzi hivyo hivyo ni kitengo cha utalii. Hawa wageni hawana shida ya kwenda malls kwao zipo za kumwaga kila kona. Ila street markets ni sehemu ya utalii sehemu kubwa duniani pia.

Sio kila kitu lazima ukibadili, halafu msukumo wa NHC ni kwa sababu ya eneo kuwa prime areas; lakini hawajali historia ya sehemu kubaki kama ilivyo.

Forodhani Zanzibar zamani ilikuwa ya wenyeji tu, sasa ni moja ya sehemu must see kwa watalii.

Embu tuache huu ushamba wa kuona eneo likiwa na maslahi tu basi livunjwe.
 
Hakuna kuchelewesha mambo

Mtanzania umpe mwaka mmoja si

Mradi utapotelea hewani,jambo kama

Likianza lianze

Ova
 

Kariakoo pia Kuna wapemba kibao
Lakini aliyelia na mama samia si mpemba ni mdanganyika
 
hawa watu wamezoeashwa sana, nyumba sio za kwao, ni za NHC, wenye nyumba wamewapa notice ili wajiandae hawajashitukizwa. wanatakiwa wafukuzwe ili hayo majengo 14 yavunjwe na hao wakorofi wasipate tena nafasi ya kupanga. wanasumbua. NHC boresheni nyumba zenu ili shirika liendelee kujiendesha kibiashara.
 
huyo mama anasema ana miaka 60 kwenye nyumba za NHC, miaka yote hajawapa watanzania wenzake wapange, na bado analeta jeuri anaamini hapo ni nyumbani kwake. sweken kabisa. anasema anaonewa, anasema ataenda wapi akifukuzwa, miaka 60 ameishi hapo hadi ameona kama ni kwake. NHC ijifunze, isipangishe mtu mmoja miaka yote hiyo, wanasahau kujenga na wanaamini hapo ndio wamefika ni pao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…