Wafanyabiashara wa Kariakoo wagoma kuhama kupisha Wawekezaji

Wafanyabiashara wa Kariakoo wagoma kuhama kupisha Wawekezaji

Wawalipe fidia za loss of income kwa miaka kadhaa ndio watu wanavyofanya na gharama fixtures and fittings za maduka yao; sio kupenda mambo rahisi.

Yaani unachukulia poa tu kisa jengo mali yako utadhani watu awakutafuta hizo hela za kuwekeza hapo.
Kwani mikataba yao inasemaje? Kusoma hawawezi sasa hata kusikiliza hawawezi!
 
Nchi imekuwa ya hovyo sana. Mwenye nyumbani anataka kuboresha nyumba yake hivyo anakupa notisi ya kuhama kwa mujibu wa mkataba wewe unakimbilia kwa Rais azuie uboreshaji ili wewe uendelee kuitumia!

Upuuzi mtupu!
Raisi asipozuia wajiandae kulipa mabillioni ya fidia hao wafanyabiashara wakitafuta mwanasheria mzuri.

👋
 
Wafanyabiashara wa maduka kutoka soko la Kariakoo wamefika makao makuu na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupinga notice walizopewa na shirika hilo kwa kuwataka kuhama ndani ya siku 90 kupisha mwekezaji mpya katika eneo hilo.

Wafanyabiashara hao wamesema, wao hawapingi maendeleo lakini muda uliotolewa na NHC ni mfupi sana na wamemuomba Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuingilia kati sakata hilo ili waweze kupata haki yao kwani muda waliopewa ni mfupi sana kwa wao kuhama kutokana wao kuwa na madeni na mikopo.


====

View attachment 2657014
NOTISI YA SIKU TISINI (90) YA KUSITISHA MKATABA WA UPANGAJI WA NYUMBA NA 005 KWENYE KIWANJA NA 23 KITALU NA 31 MTAA WA TANDAMTI NA SWAHILI

Tafadhali husika na somo hapo juu;

Unafahamishwa kuwa Shirika la Nyumba la Taifa limeanza rasmi utekelezaji wa Sera va Ubia na wawekezaji binafsi na taasisi mbalimbali ambayo ilizinduliwa rasmi mwezi Novemba 2022.

Hivyo basi Shirika la Nyumba la Taifa lina mpango wa kuanza ujenzi kwenye Kiwanja tajwa hapo juu ambapo wewe ni mpangaji, hivyo tunakutaarifu kwamba unapewa NOTISI ya siku tisini (90) kuanzia tarche 02/06/2023 mpaka tarehe 31/08/2023 kusitisha mkataba baina yako na Shirika la Nyumba la Taifa kwenye nyumba tajwa hapo juu.

Shirika limerejea kipengele namba 4.1 (c). (d) na 7.2 cha Mkataba wa Upangaji kinachompa mamlaka mpangishaji kuvunja mkataba ndani ya siku tisini (90) pale anapohitaji jengo lake kwa ajili ya matumizi mengine.

Kwa maelezo hayo, unapewa NOTISI ya siku tisini (90) ya kutakiwa kuhama katika nyumba unavoishi ili kupisha uendelezaji unaokusudiwa kufanyika katika kiwanja hicho.

Unaruhusiwa kuomba upangaji upya baada ya jengo jipya kukamilika kulingana na masharti ya kipindi hicho.

Mbo
Pia soma: Wapangaji nyumba za NHC Kariakoo walalamika notisi za kuhama bila mazungumzo, wadai NHC wamempa dili mwekezaji mpya kimyakimya
Mbona walishindwa kuendeleza bilicanas ya mbowe licha ya kuivunja
 
Wakavunje Michenzani Zanzibar kuna majengo nayo yamechoka mbaya na yakizamani; na wapangaji ZHC wanamikataba kama hiyo.

Zanzibar inapokea watalii wengi sana wakijenga nyumba mpya za kisasa na gated community; awawezi kukosa wazungu wakuwapangisha kama holiday let mwaka mzima kwa hela nyingi sana za kigeni.

Point hapo ni kwamba hela ina mipaka uwezi ku disrupt maisha ya watu kisa eneo unadhani linathamani zaidi; na wala huna alternative ya kuwapeleka watu unaowatoa kwenda kwingine huo ni unyanyasaji.
Hivi ni NHC waliwaweka hapo au walijipeleka wenyewe tena kwa kubembeleza!
 
Wengi hapo wanawaza kukosa nafasi za maduka mradi utakapokamilika ,maana wataaanza kuomba kupangishwa kama wapangaji wapya. Hivyo Kuna uwezekano Wengi wakakosa Kwa sababu mkatabata baina Yao utakuwa umeisha,hivyo Kila atakayetaka kuwa mpangaji sharti afuate taratibu za Shirika ambapo utalipia miezi mitatu mbele halafu ndio uanze kulipia Kodi Yako ya Kila mwezi.
 
Biashara 1000 zinaweza kuwa zimeajiri watu wangapi kila duka. Ukishawatoa hao wenye maduka na wafanyakazi wao hao watu wanaenda kula wapi?

Haya tupe jibu wewe mwelewa?
Ebo hiyo siyo hoja, mwenye nyumba anataka nyumba yake! Hama kajenge nyumba yako ufanye hizo biashara zako!

Unafanya biashara kwa kutegemea nyumba ya mwenzako, ujinga gani huo!
 
Wakavunje Michenzani Zanzibar kuna majengo nayo yamechoka mbaya na yakizamani; na wapangaji ZHC wanamikataba kama hiyo.

Zanzibar inapokea watalii wengi sana wakijenga nyumba mpya za kisasa na gated community; awawezi kukosa wazungu wakuwapangisha kama holiday let mwaka mzima kwa hela nyingi sana za kigeni.

Point hapo ni kwamba hela ina mipaka uwezi ku disrupt maisha ya watu kisa eneo unadhani linathamani zaidi; na wala huna alternative ya kuwapeleka watu unaowatoa kwenda kwingine huo ni unyanyasaji.
Alokwambia kuwa nyumba za michenzani ni za kupanga nani? Tulivunjiwa nyumba zetu, zikajengwa flats na tukapewa flats kama mali zetu na documemts zote tunazo. Flats za serikali ambazo ni za kupanga ni zile za mwisho kumalizwa kujengwa na mtoto wa marehemu Karume. Hizo labda wataweza kuzivunja ila kutoka block number 1 hadi 8 watahitaji kutupa compensation na kama flats za kilimani watajikuta na upinzani wa kqweli kwa sababu flats zile si mali ya serikali.
 
Shida ni moja tu, watanzania tunaposaini mkataba wala hatujali yaliyomo ndani ya mkataba. Tunachoangalia ni pesa ngapi tutapata kwa mwezi/mwaka n.k.

Hayo ndio yanayotukuta katika mkataba wa DP world. Mtu anakwambia eti tutapata trilioni 31 badala ya trilioni 7 tunazopata leo. Wenye akili huangalia mkataba unasemaje? Kwenye hili NHC Kariakoo litatupa akili nzuri ya kujadili mkataba wa DP WORLD. Watanzania amkeni!!!!!!!!
Wanatwambia Mapato kutoka tril 31 hadi 67 bila kutwambia Matumizi ni sh ngapi na tutagawana shi ngapi ma DP
 
Wengi hapo wanawaza kukosa nafasi za maduka mradi utakapokamilika ,maana wataaanza kuomba kupangishwa kama wapangaji wapya. Hivyo Kuna uwezekano Wengi wakakosa Kwa sababu mkatabata baina Yao utakuwa umeisha,hivyo Kila atakayetaka kuwa mpangaji sharti afuate taratibu za Shirika ambapo utalipia miezi mitatu mbele halafu ndio uanze kulipia Kodi Yako ya Kila mwezi.
Kwani kulipia hiyo miezi mitatu mbele unadhani ni tatizo kwao Mkuu?Ikiwa Kodi zao wanalipa kwa Mwaka?

Hapo kinachowafanya wapate sintofahamu ni Issue za vilemba...
 
Ebo hiyo siyo hoja, mwenye nyumba anataka nyumba yake! Hama kajenge nyumba yako ufanye hizo biashara zako!

Unafanya biashara kwa kutegemea nyumba ya mwenzako, ujinga gani huo!
Umeishiwa hoja

Subiri waende mahakamani uone kama watatolewa.

Uwezi kuwa na mkataba wa kukodisha mtu shamba ata kama umesema unaweza vunja muda wowote. Ukifanya hivyo huyo mkulima ata shinda kesi hizo terms zako utaambiwa ni batili, uwezi kukodisha shamba bila mkulima kuvuna; hizo ndio customary implied terms za mkataba.

Kila industry ina customary norms zake ndio maana nakueleza unaropoka tu; subiri waende mahakamani uone kama serikali aitotozwa billions za fidia; huo muda ni mdogo sana.
 
Back
Top Bottom