DOKEZO Wafanyabiashara wa ndizi mbivu Dar huchovya kwenye kemikali ili kuziivisha ndani ya muda mfupi. Afya za watu hatarini

DOKEZO Wafanyabiashara wa ndizi mbivu Dar huchovya kwenye kemikali ili kuziivisha ndani ya muda mfupi. Afya za watu hatarini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Dsm ni hatari.

Kuna siku nilipita soko la Makumbusho vibanda vya kuku. Nikakuta muuzaji na mwenzake (alijifanya msaidizi wa muuzaji), huyo mwenzake anamalizia kupakia kwenye mfuko kuku kadhaa walioandaliwa. Nikataka wanichinjie kuku wawili toka bandani. Yule mwenzake akadakia "bro si tungepunguza toka kwenye oda ya huyu ninayemfungia ili tusikucheleweshe? Ntabaki na-replace tu coz ninayempelekea hana haraka."

Nikasema poa. Jamaa akaenda kunichukulia mfuko ili achomoe wawili aniwekee. Yule jamaa aliyebaki akaniambia "bro, unaonekana mstaarabu, nafsi inanisuta, acha nikwambie ukweli. Huyo jamaa si muuzaji wangu bali huwa anapita kukusanya kwa bei chee kuku waliokufa hapa sokoni au wakati wa usafirishaji, anaenda kuwauzia wauza chips na mama ntilie kwa bei ndogo. Chagua tu bandani tu uchinjiwe."

Aisee nilichoka. Na hamu ya kuku ikaisha. Nikamwambia basi bro, nikampoza kidogo. Jamaa wakati anarudi na mfuko akaniona naondoka, nikamjibu sihitaji tena, wife kanipigia alishanunua mahali so mpelekee tu jamaa oda yake.

Muuzaji aliniambia wako wengi wanapita kukusanya. Hakuna soko kuku waliokufa wanatupwa.
Kama Watu wanathubutu kukaangia chipsi mafuta ya transformers, unadhani hao ni Binadamu halisi?

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Ahsante kwa taarifa lakini ngoja nishare ninachokijua kuhusu hii habari:

Kwanza kabisa matunda yote yanapokuwa kwenye uhalisia wake yani yakiwa kwenye mti wake yanakuwa na uwezo wa kutengeneza hormone au kichochoe kinachoitwa ethylene ambacho hufanya kazi ya kubadilisha baadhi ya vitu vilivyopo kwenye hilo tunda kama vile starch huwadilishwa kwenda kwenye sukari nyepesi yani simple sugar kama vile glucose n.k.

Sasa unapochuma hilo tunda maana yake imelitoa kwenye asili yake hivyo utahitaji hiyo ethylene ili matunda hayo yaweze kuiva kwa haraka na kwa wingi ingawa zipo njia za asili kama vile kuchimba shimo na kukoka moto ndani ya hilo shimo kisha zima huu moto na kisha weka ndizi zako na funika na majani ya ndizi na udongo kisha moto kidogo kwa juu na uuzima baadaye.

Baada ya siku sita ndizi zitakuwa zimeiva na hapo ni vitu viwili vimesababisha ziive, moja ni natural ethylene iliobaki kwenye ndizi pamoja na joto iliolitengeneza kwenye hilo shimo.

HIVYO HIYO ETHYLENE HAINA SHIDA
 
Na zile gari za embe pale mwandege zile embe za kazi gani? Hebu tupe elimu kidogo.
Embe moja juisi katoni mbili.
Soma boksi la juisi ujue vitu unavyokunywa na sisi kubungaa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango.
Nasikitia zaidi wazazi waonywesha watoto wao juisi za viwandani.
 
Nikila ndizi za kuvundika napata kwikwi kali mno saiv ndiz zangu ni zile og zenye sukari nyingi na vidoti vyeusi waniata malindi
 
Tangu 2012 sijawahi kula matikiti ya kipumbavu ambayo kila siku yapo mitaani wala hayana msimu, ila Mwanza na baadhi ya mikoa kanda ya ziwa yapo yenyewe ya kijani halisi kabisa.

Ngoja niendelee kujirundikia matunda, mazao na mimea ya asili huku porini kwangu.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
Hapa hapa mjini ila watu tunavuna
Nipo mjini ila kama shamba PXL_20241011_083019452.jpgza leo leo😂
PXL_20241009_065319963.jpg
PXL_20241009_065327715.jpg
 
Mtaan wanaweka maparachichi mabichi na ndizi na kuzifunika. Ndani ya siku mbili zinaiva.

Secondary chemistry walituambia ili tunda liive linahitaji acetylene cpd. Inawezekana hapo Dar mnatumia industrial acetylene, badala ya natural inayotoka kwenye matunda yenyewe.
 
Watu wanadanganyana sana kwenye vijiwe vya kahawa ,wanashindwa kujua ukichukua ndizi mbichi ukaiweka tu ndani bila hata kuifunika haichukui siku tatu ishaiva sasa ya nini uitose kwenye kemikali ,halafu ndizi kweli uiloweke kwenye kemikali ikitoka itakuwa salama? Si itakuwa nyonde nyonde na si kavu kabisa...ndizi ikiwekwa kwenye friji kama wanavyosema inakuwa nyeusi tiii sasa hawa wauza kahawa wanakwambia zinawekwa kwenye friza.
Inasikitisha sana akili za wabongo wengi
 
Watu wanadanganyana sana kwenye vijiwe vya kahawa ,wanashindwa kujua ukichukua ndizi mbichi ukaiweka tu ndani bila hata kuifunika haichukui siku tatu ishaiva sasa ya nini uitose kwenye kemikali ,halafu ndizi kweli uiloweke kwenye kemikali ikitoka itakuwa salama? Si itakuwa nyonde nyonde na si kavu kabisa...ndizi ikiwekwa kwenye friji kama wanavyosema inakuwa nyeusi tiii sasa hawa wauza kahawa wanakwambia zinawekwa kwenye friza.
IMG-20241014-WA0000.jpg
 
Hii tetesi itazaa taharuki kubwa sana, kwa vyanzo vya uhakika vitakapo sema ndio itakuwa taarifa rasmi. Iko hivi
👇

Ndizi Mbichi zikiwasili DSM zikiwa mikononi mwa wawekezaji wa biashara hio huvundika kwa namna ya kuchovya kwenye maji yaliyowekwa vimiminika (chemicali) na hivyo ndizi kuiva ndani ya siku 2 masaa 48, japo wenyewe hao wahuni husema ndizi inaiva ndani siku 4 wakati hizo siku 4 ni utamaduni alisia wa ndizi kuiva kwa siku 4.

Hao wahuni inasemekana hutumia liquid za ethene na oxygen (not sure) mtajua wenyewe.

Na hapa Pro. Janabi ajitokeze kukemea na kusema kuhusu madhara ya huo uuaji.

Nasisitiza hii ni tetesi, japo ninayo video ya mwandishi aliyefanya utafiti na mahojiano na wahusika sipaswi kuweka hadi pale itakapokuwa viral na moderators wenyewe wataweka pasipo shaka.

Hii ndio mixer (Acetylene+ Calcium carbide+ water)

Chukua tahadhari ya dhati kabisa.

Kufa kufaana ndio uninja wa Waafrika.

Wadiz
wacha uongo,
 
Tangu 2012 sijawahi kula matikiti ya kipumbavu ambayo kila siku yapo mitaani wala hayana msimu, ila Mwanza na baadhi ya mikoa kanda ya ziwa yapo yenyewe ya kijani halisi kabisa.

Ngoja niendelee kujirundikia matunda, mazao na mimea ya asili huku porini kwangu.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
Hata ukifanyaivo nakwambia utakufa tuuu
 
Najibu Kama Mwl wa Kemia na Bailojia

'Ethene‘ ndo huivisha matunda na imo kwenye mmea kama kichocheo 'phytohormone' ambayo kazi yake ni kuivisha tunda.

'Ethene' ama ‘ethylene’ ni kemikali ogania kundi la hidrokaboni familia ya 'alkini'. Inapatika katika uasili na inaweza kutengenezwa na binadamu.

Miongoni matumizi ni kuivisha matunda: kiasilia na isivyoasilia (artificiall ripening).

Wafanyabiashara hutoa matunda shambani yakiwa bado mabichi, hii ina faida: usafirishaji na utunzaji. Muda mwafaka ukifika muuzaji atalazimika kuvundika ili matunda yaive na ndipo matumizi ya kichocheo hiki hutumika.

Kuivisha matunda isivyoasilia kwa kutumia kemikali ya 'ethene' kiafya haina shida; shida ipo kwenye vyanzo vya hiyo 'ethene'.

Kuna baadhi ya wafanyabiashara wanazijua njia za asili za kuzalisha ethene na kuharakisha uivaji wa matunda k.v kutumia mbegu za maparachichi ambazo huzalisha ethene na kuharakisha uivaji wa matunda husika.

Maswali ya hii ni salama au sisalama, yako juu ya njia ya kuivisha matunda, vyanzo vya kemikali husika, inatoka wapi? Na namna ya kuitumia. Weledi wa wavundikaji uko vipi? Rafu ziko hapo!

Nashauri:
 

Attachments

  • Screenshot_20241015-002656.png
    Screenshot_20241015-002656.png
    102.9 KB · Views: 3
Biashara ya ndizi mbivu Imekuwa kubwa sana hivyo wauzaji wanaangalia faida na si afya ya mlaji
 
Sio kweli ndizi huivishwa haraka na parachichi kama huku Rombo wanakata Kata parachichi lililoiva kwenye Tenga la ndizi mbichi Hadi wakifikia Dar zimeshaiva kununua parachichi saa nyingine mbovu au za kuokota mgombani ni rahisi kuliko kununua hizo kemikali ambazo umeshindwa kudhibitisha lingine msiongee vitu kama hujui hata kemikali inaitwaje na wanawekea wap Kuna ndugu zetu wanategemea biashara hiyo kula kusomesha kuvaa na kuishi mjini kwahiyo usiwaharibie
 
Back
Top Bottom