Wafungwa kula mlo mmoja kwa siku na hufanya kazi ngumu, hii ni haki?

Wafungwa kula mlo mmoja kwa siku na hufanya kazi ngumu, hii ni haki?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
1646750866291.png

Hizi jela zetu zimekuwa sehemu ya mateso na sio sehemu ya kumrekebisha mtu tabia.

Mfano hapa jela ya Mbeya Mjini watu wanafanya kazi asubuhi hadi saa nane mchana, hio kazi wanayofanya ni nzito ambayo uraiani anastahili malipo ya chini iwe kumudu milo miatu lakini wao wanapewa chakula mara moja tu saa tisa mchana, hicho chakula ni ugali maharage ambao haufikii hata nusu sahani, hapo ni mpaka kesho tena.

Unyanyasaji ni wa hali ya juu wafungwa ni kama watumwa kipindi cha ukoloni, nakumbuka hapa Mbeya kuna sehemu ya makaburi kulikuwa kuna nyasi ndefu ilibidi zifyekwe ila kulikuwa na nyoka wengi hio sehemu, ilibidi wafungwa ndio wafyeke (ukikataa unatembezewa kipigo kzito), pia nakumbuka rais Magufuli alitilia mkazo Wafungwa wawe wanapigwa mateke.

Pia hakuna haki kwa wafungwa wenye ndoa kukutana faragha, mfano kijana wa miaka 27 akifungwa miaka 30, ni kwamba katika hii miaka 30 hataruhusiwa kukutana kimapenzi na mke wake na hataweza kuwa na watoto, na hata akiamua kuwa na watoto baada ya kifungo, tayari umri utakuwa umeenda sana hata watoto watamwita babu. hapa ndipo ndoa huwa zinavunjika, binti anamkimbia mme wake kwasababu ya huu unyanyasaji.
 
Kwa nchi za uchumi wa kwanza milo yao ikoje? USA baby njooo
 
Mzungu alileta jela,mwafrika akazirithi na sheria zake za kutesa watu.Waafrija akili duni sana, wazungu walisha boresha sheria za jela huko kwao wameruhusu mpaka kulala na mke anapokuja kukutembelea jela sisi wafungwa ni kufi $&rana tu halifu eti tunapinga ushoga huku ushoga ukiendelea kwenye majela.
 
Ipo haja ya jela watu waruhisiwe kushiriki mapenzi na wake zao, mfano sabaya unamfunga Miaka 30 bado kesi zingine still ni kijana hana mtoto kwann asipewe haki ya kutungisha mimba Ili akitoka jela akute watoto wake ni wakubwa wamfae uzeeni.
 
Kuwafanyisha Kazi wafungwa bila kuwalipa ni utumwa na ni dhuluma pia ni kinyume na Sheria ya maadili ya kazi.

Inatakiwa mfungwa akifanya Kazi alipwe awekewe kwenye account yake Ili akitoka jela apate cha kuanzia.

Sio sahihi kuwatumikisha wafungwa maana biashara ya utumwa ilishakufa.
 
Gereza la Songwe ni gereza la kilimo na linamiliki mashamba makubwa sana ya mahindi na maharage, kwanini wanapewa chakula kidogo?
View attachment 2143225

Hizi jela zetu zimekuwa sehemu ya mateso na sio sehemu ya kumrekebisha mtu tabia.

Mfano hapa jela ya Mbeya Mjini watu wanafanya kazi asubuhi hadi saa nane mchana, chakula ni saa tisa mchana yani chakula ni ugali maharage ambao haufikii hata nusu sahan...
 
Yuko jirani yangu hapa Kimara B alikwenda kurushia mawe kanisa la walokole usiku wa manane kisa wanampigia makelele hawezi kulala. Asubuhi polisi wakaja kumbeba, utani utani kaja mtu mmoja kumuwekea dhamana , policcm wakasema wanataka wadhamini wawili, kisa mchungaji aliwapa ubani. Ilikua ijumaa, kufumba na kufumbua mshikaji Yuko gerezani.

Amesema kule kula kwa foleni, ugali na Maharage, siku ya kwanza walimpa Maharage 17 siku ya pili 14. Kujisaidia haja kubwa unasimamiwa na kijana mdogo na unaambiwa UFANYE haraka.

Kulala ndio ishu, maana mnakabana Kama mihogo na joto hili. Vidirisha viko juu kabisa haviingizi hewa.

Ameapa hata Kama walokole watapiga mziki mpaka saa Tisa usiku. Hatowagusa.
 
Back
Top Bottom