Wafungwa kula mlo mmoja kwa siku na hufanya kazi ngumu, hii ni haki?

Wafungwa kula mlo mmoja kwa siku na hufanya kazi ngumu, hii ni haki?

Kuna waziri wa Mambo ya ndani mzanzibar aliwahi kuulizwa bungeni
1. kwanini wafungwa wanakula Mara moja?

Waziri. Wanakula Milo mitatu Ila ili kuokoa muda wanaopewa hiyo Milo kwa wakati mmoja.

2. Kwanini wafungwa wanafanyana mapenzi kinyume na maumbile huku serikali ikilifumbia macho?
Waziri.

Kwani huku uraiani hakuna mashoga na mabasha?
 
Kwani kule unakwenda Holiday ?

Jela sio Sehemu ya kwenda, ile sio Hoteli au unashauri tuongezewe Tozo ili Jela wapate milo minne (kwanini wasilime bustani na kuzalisha ili wapate milo hata kumi na ziada wauze) au better still kujitahidi kutokwenda huko....
 
View attachment 2143225

Hizi jela zetu zimekuwa sehemu ya mateso na sio sehemu ya kumrekebisha mtu tabia.

Mfano hapa jela ya Mbeya Mjini watu wanafanya kazi asubuhi hadi saa nane mchana, chakula ni saa tisa mchana yani chakula ni ugali maharage ambao haufikii hata nusu sahani.

pia unyanyasaji wa vipigo ni wa hali ya juu, nakumbuka rais Magufuli alitoa amri Wafungwa wafanyishwe kazi usiku na mchana na wapigwe mateke

Pia kwa wale waliooa, wakiingia jela ndoa huwa zinaharibika moja kwa moja, mtu ukiingia jela huwezi kuwa faragha na mke wako mpaka umalize kifungo, ni wanawake wache sana wanaweza kuwa waaminifu katika hi hali.

Hii hali sio hali aisee.
Mume/mke akienda jela aliyeachwa ana haki ya kuomba talaka. According to roman catholic. Ukikuta kakuvumilia basi shukuru mungu
 
Tatizo kubwa ni wale maaskari jela gereza kama la songwe wanalima sana ila bado chakula ni cha manati askari wanaiba mahindi na maharage wanachukua magunzi wanasaka wanamix na unga ndio ugali hakika magereza yote nchini chakula ni mlo mmoja na hautoshi kisa tamaa za mabwana wale.
 
Nafikiri tuliiga jela ilivyokuwa enzi za mkoloni bila kutambua kwamba mkoloni alifanya vile kwa makusudi ya kumkandamiza mtu mweusi.......kwa wale waliowahi kufika magereza ya huko majuu watupe uzoefu wao kwenye hili.
 
Kuwafanyisha Kazi wafungwa bila kuwalipa ni utumwa na ni dhuluma pia ni kinyume na Sheria ya maadili ya kazi.
Inatakiwa mfungwa akifanya Kazi alipwe awekewe kwenye account yake Ili akitoka jela apate cha kuanzia.
Sio sahihi kuwatumikisha wafungwa maana biashara ya utumwa ilishakufa.
Hilo la wafungwa kulipwa pesa na kuwekwa kwnye ACC zao ni ngumu sn kwa Tanzania.

Kama mahabusu ana kaa week anatoka na kukuta Askari kajimilikisha simu pamoja na viatu vya mtuhumiwa.

Unadhani ya gerezani unapokaa miaka pesa zako itawezekana kubaki salama?

Sent from my M2101K7BG using JamiiForums mobile app
 
Mfungwa kufanya Kazi ni makosa ni kinyume na sheria za Kazi
Kwa hiyo mfungwa anaondolewa uhuru wa kuchangamana na wengine tu, na serikali au waliomfunga wanatakiwa kumgharimia kwa kila kitu bila yeye kujishughulisha kufanya kazi yoyote ile, wataalamu wa sheria kujeni kutoa udadavuzi zaidi..........
 
Ipo haja ya jela watu waruhisiwe kushiriki mapenzi na wake zao, mfano sabaya unamfunga Miaka 30 bado kesi zingine still ni kijana hana mtoto kwann asipewe haki ya kutungisha mimba Ili akitoka jela akute watoto wake ni wakubwa wamfae uzeeni.
Mfungwa atungishe mimba, nani atalea huyo mtoto? Wewe uko tayari kutoa binti yako akatungishwe mimba na mfungwa? Kumbafu wewe.
 
Jela za Tz ni mateso.
Kuna mshua mmoja alishawahi kuwa uko,aliwahi kuniambia ukisikia siku nduguyo amekamatwa palepale akiwa mahabusu ya polisi jitahidi kumtoa kwa kumpa dhamana yoyote hata nyumba yako weka rehani kisha akiwa nje fanya mipango yoyote ile kesi iishie ukuuku chini kabla ya kufika mahakamani,mpaka hapo kuna cha kujifunza
 
Yuko jirani yangu hapa Kimara B alikwenda kurushia kanisa la walokole usiku wa manane kisa wanampigia makelele hawezi kulala. Asubuhi polisi wakaja kumbeba, utani utani kaja mtu mmoja kumuwekea dhamana , policcm wakasema wanataka wadhamini wawili, kisa mchungaji aliwapa ubani. Ilikua ijumaa, kufumba na kufumbua mshikaji Yuko gerezani.

Amesema kule kula kwa foleni, ugali na Maharage, siku ya kwanza walimpa Maharage 17 siku ya pili 14. Kujisaidia haja kubwa unasimamiwa na kijana mdogo na unaambiwa UFANYE haraka.

Kulala ndio ishu, maana mnakabana Kama mihogo na joto hili. Vidirisha viko juu kabisa haviingizi hewa.

Ameapa hata Kama walokole watapiga mziki mpaka saa Tisa usiku. Hatowagusa.
Duuh pole yake
 
Kuna waziri wa Mambo ya ndani mzanzibar aliwahi kuulizwa bungeni
1. kwanini wafungwa wanakula Mara moja?

Waziri. Wanakula Milo mitatu Ila ili kuokoa muda wanaopewa hiyo Milo kwa wakati mmoja.

2. Kwanini wafungwa wanafanyana mapenzi kinyume na maumbile huku serikali ikilifumbia macho?
Waziri.

Kwani huku uraiani hakuna mashoga na mabasha?
Cheo kinamzuzua huyo waziri
 
Huu ni zaidi ya unyanyasaji na uvunjifu wa haki za kibinadamu.

Wale human rights watch dogs wapo wapi!?
 
Mijitu myeusi ni mijinga sana. Especially politicians.
Mzungu alileta jela,mwafrika akazirithi na sheria zake za kutesa watu.Waafrija akili duni sana, wazungu walisha boresha sheria za jela huko kwao wameruhusu mpaka kulala na mke anapokuja kukutembelea jela sisi wafungwa ni kufi $&rana tu halifu eti tunapinga ushoga huku ushoga ukiendelea kwenye majela.
 
Back
Top Bottom