Wafungwa kula mlo mmoja kwa siku na hufanya kazi ngumu, hii ni haki?

Wafungwa kula mlo mmoja kwa siku na hufanya kazi ngumu, hii ni haki?

Yuko jirani yangu hapa Kimara B alikwenda kurushia kanisa la walokole usiku wa manane kisa wanampigia makelele hawezi kulala. Asubuhi polisi wakaja kumbeba, utani utani kaja mtu mmoja kumuwekea dhamana , policcm wakasema wanataka wadhamini wawili, kisa mchungaji aliwapa ubani. Ilikua ijumaa, kufumba na kufumbua mshikaji Yuko gerezani.

Amesema kule kula kwa foleni, ugali na Maharage, siku ya kwanza walimpa Maharage 17 siku ya pili 14. Kujisaidia haja kubwa unasimamiwa na kijana mdogo na unaambiwa UFANYE haraka.

Kulala ndio ishu, maana mnakabana Kama mihogo na joto hili. Vidirisha viko juu kabisa haviingizi hewa.

Ameapa hata Kama walokole watapiga mziki mpaka saa Tisa usiku. Hatowagusa.

Ahhahahha Dah
 
Dah tudai katiba mpya siku samia na wenzake wakifungwa ndio hapo hapo sheria zitabadilishwa
 
Ila gerezani kuna binadamu wana roho ngumu sana...
 
Ni sawa kabisa, tena wanapaswa na kutandikwa na viboko juu ili wasirudie kufanya makosa tena!
 
View attachment 2143509

Hizi jela zetu zimekuwa sehemu ya mateso na sio sehemu ya kumrekebisha mtu tabia.

Mfano hapa jela ya Mbeya Mjini watu wanafanya kazi asubuhi hadi saa nane mchana, hio kazi wanayofanya ni nzito ambayo uraiani anastahili malipo ya chini iwe kumudu milo miatu lakini wao wanapewa chakula mara moja tu saa tisa mchana, hicho chakula ni ugali maharage ambao haufikii hata nusu sahani, hapo ni mpaka kesho tena.

unyanyasaji ni wa hali ya juu wafungwa ni kama watumwa kipindi cha ukoloni, nakumbuka hapa Mbeya kuna sehemu ya makaburi kulikuwa kuna nyasi ndefu ilibidi zifyekwe ila kulikuwa na nyoka wengi hio sehemu, ilibidi wafungwa ndio wafyeke (ukikataa unatembezewa kipigo kzito), pia nakumbuka rais Magufuli alitilia mkazo Wafungwa wawe wanapigwa mateke.

Pia hakuna haki kwa wafungwa wenye ndoa kukutana faragha, mfano kijana wa miaka 27 anafungwa miaka 15, wakati huo bado hana mtoto ila kaacha mke uraiani, hapo ni kwamba hataweza kumtungisha mimba mke wake mpaka kifungo kiishe atakapokuwa na miaka 40+, kwa hali hii ni wazi kabisa jela inatengeneza mazingira ya mwanamke kumkimbia mme wake aende kuzalishwa na kuolewa na mwanaume mwengine. hali hii nayo inapelekea jela ziwe sehemu za kutengeneza mashoga.
Afu wanakulazimisha uvae pensi hata kama miguu miembamba kama miwa
 
Kuna jamaa hapa Dar alifungwa kwa kosa la wizi wa kalamu. Siku anatoka alikuta mke wake mpenzi amezaa na best friend wake.

Ma besti Hawa tuwaangalie Sana.
 
Mume/mke akienda jela aliyeachwa ana haki ya kuomba talaka. According to roman catholic. Ukikuta kakuvumilia basi shukuru mungu
Solution ni kuoa kimwanamke kisicho na chura. Yaani akivaa Dera hujui mbele Wala nyuma
 
Kwa kweli hiyo si haki, kama watu wanafanya kazi maana yake wanazalisha, na kama wanazalisha wanapaswa wapewe angalau milo mitatu ya kushiba, maana hata wangekodi vibarua si bado wangewalipa?!
 
Pole kwa wale waliosingiziwa.....
Na mtu yoyote anaweza kuingia huko ( hata mimi).
Ila Wengi wanastahili hiyo adhabu, wengi wao ni hatari kwa raia wema.
Kumnyima mtu uhuru wake ni adhabu tosha, hiyo ya kumnyima chakula ni ukatili sasa..
 
Ipo haja ya jela watu waruhisiwe kushiriki mapenzi na wake zao, mfano sabaya unamfunga Miaka 30 bado kesi zingine still ni kijana hana mtoto kwann asipewe haki ya kutungisha mimba Ili akitoka jela akute watoto wake ni wakubwa wamfae uzeeni.
Hili jambo la Msingi sana, kwa kesi ya Sabaya ni muhimu akaruhusiwa walau kutungisha mimba hata tatu ikiwezekana, we mtu umfunge miaka 30 na hana mtoto wa umri ule kweli, ni zaidi ya uonevu, wafungwa wapewe haki ya kutungisha mimba..
 
Uhuru ni pamoja na Kula utakavyo, mda utakao.
Milo mitatu kwa siku ni haki ya binadamu yeyote, na hakuna mwenye haki ya kukuondolea, unless iwe stated specifically kwa hiyo ndio adhabu yako; either akuache ujitafutie mwenyewe, au kama amekufunga basi akuhudumie milo mitatu, maana kazi hata huko jela watu wanafanyishwa kama punda, kwanini wasilishwe ipasavyo?
 
Milo mitatu kwa siku ni haki ya binadamu yeyote, na hakuna mwenye haki ya kukuondolea, unless iwe stated specifically kwa hiyo ndio adhabu yako; either akuache ujitafutie mwenyewe, au kama amekufunga basi akuhudumie milo mitatu, maana kazi hata huko jela watu wanafanyishwa kama punda, kwanini wasilishwe ipasavyo?
Tunatofautiana namna tunavyowachukulia wafungwa...
 
Back
Top Bottom