Wafungwa kula mlo mmoja kwa siku na hufanya kazi ngumu, hii ni haki?

Wafungwa kula mlo mmoja kwa siku na hufanya kazi ngumu, hii ni haki?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hapana huwezi kufa ila cha moto utakiona
Hatopata shida yeyote,
Kuna watu watalala njaa ili yeye ashibe vizuri anawiri..

Azidi kupendeza.
 
Unamuongelea mtu ambaye ameua watu hapa.

Yaani akili yangu inakubaliana na ulichoandika ila inamuwaza huyu tunayetakiwa kumbadilishia mazingira.

Yeye angetufanyia hivyo?
 
Tena mahindi na maharage daily. No mboga mboga, no matunda.

Ni zaidi ya ukatili kwa kweli.
Nasikia sasaivi kila jela inautaratibu wa kila wiki kula japo mboga za majani
 
Yuko jirani yangu hapa Kimara B alikwenda kurushia mawe kanisa la walokole usiku wa manane kisa wanampigia makelele hawezi kulala. Asubuhi polisi wakaja kumbeba, utani utani kaja mtu mmoja kumuwekea dhamana , policcm wakasema wanataka wadhamini wawili, kisa mchungaji aliwapa ubani. Ilikua ijumaa, kufumba na kufumbua mshikaji Yuko gerezani.

Amesema kule kula kwa foleni, ugali na Maharage, siku ya kwanza walimpa Maharage 17 siku ya pili 14. Kujisaidia haja kubwa unasimamiwa na kijana mdogo na unaambiwa UFANYE haraka.

Kulala ndio ishu, maana mnakabana Kama mihogo na joto hili. Vidirisha viko juu kabisa haviingizi hewa.

Ameapa hata Kama walokole watapiga mziki mpaka saa Tisa usiku. Hatowagusa.
😃😃😃😃😃😄
 
Yuko jirani yangu hapa Kimara B alikwenda kurushia mawe kanisa la walokole usiku wa manane kisa wanampigia makelele hawezi kulala. Asubuhi polisi wakaja kumbeba, utani utani kaja mtu mmoja kumuwekea dhamana , policcm wakasema wanataka wadhamini wawili, kisa mchungaji aliwapa ubani. Ilikua ijumaa, kufumba na kufumbua mshikaji Yuko gerezani.

Amesema kule kula kwa foleni, ugali na Maharage, siku ya kwanza walimpa Maharage 17 siku ya pili 14. Kujisaidia haja kubwa unasimamiwa na kijana mdogo na unaambiwa UFANYE haraka.

Kulala ndio ishu, maana mnakabana Kama mihogo na joto hili. Vidirisha viko juu kabisa haviingizi hewa.

Ameapa hata Kama walokole watapiga mziki mpaka saa Tisa usiku. Hatowagusa.
Kimara B kwa mchungaji gani huyo mwanjelwa road au huko jirani kabisa na shule ya msingi?.
 
View attachment 2143509

Hizi jela zetu zimekuwa sehemu ya mateso na sio sehemu ya kumrekebisha mtu tabia.

Mfano hapa jela ya Mbeya Mjini watu wanafanya kazi asubuhi hadi saa nane mchana, hio kazi wanayofanya ni nzito ambayo uraiani anastahili malipo ya chini iwe kumudu milo miatu lakini wao wanapewa chakula mara moja tu saa tisa mchana, hicho chakula ni ugali maharage ambao haufikii hata nusu sahani, hapo ni mpaka kesho tena.

unyanyasaji ni wa hali ya juu wafungwa ni kama watumwa kipindi cha ukoloni, nakumbuka hapa Mbeya kuna sehemu ya makaburi kulikuwa kuna nyasi ndefu ilibidi zifyekwe ila kulikuwa na nyoka wengi hio sehemu, ilibidi wafungwa ndio wafyeke (ukikataa unatembezewa kipigo kzito), pia nakumbuka rais Magufuli alitilia mkazo Wafungwa wawe wanapigwa mateke.

Pia hakuna haki kwa wafungwa wenye ndoa kukutana faragha, mfano kijana wa miaka 27 akifungwa miaka 30, ni kwamba katika hii miaka 30 hataruhusiwa kukutana kimapenzi na mke wake na hataweza kuwa na watoto, na hata akiamua kuwa na watoto baada ya kifungo, tayari umri utakuwa umeenda sana hata watoto watamwita babu. hapa ndipo ndoa huwa zinavunjika, binti anamkimbia mme wake kwasababu ya huu unyanyasaji.
Jela sio sehemu ya kula bata weweeee amka

Sent from my PBBM00 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom