Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Wahenga wenzangu njoo tukumbushane vipindi vilivyobamba RTD enzi hizoo

Taarifa ya habari ilikuwa na watangazaji maalumu kwa matukio maalum. Nyerere akiteua au akitumbua itasomwa na David Wakati. Kama hayupo ni wakina Jacob Tesha, Juma Ngondae, Abdul Ngarawa au Mgosi Godfrey Mngodo. Na mara nyingi inakuwa saa 2 usiku.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumbuizo Asilia - Michael Katembo , Khalid Ponera baadae Malima Ndelema

Starehe na BP - Julius Nyaisangah

Misakato - Julius Nyaisangah

Ugua pole - Walikuwa wanazunguka hospitali mbalimbali nchini kupitia wawakilishi wa mikoani na wale wa Dar

Nipe Habari - Siwatu Luanda

Mama na Mwana - Deborah Mwenda

Club Raha Leo Show - Julius Nyaisangah, Enock Ngombale na Geofrey Erneo

Kijaruba - Abdallah Mlawa

Mchana Mwema/Pokea Salamu - Christine Chokunegela na wenzake wengi

Chaguo la msikilizaji - Malima Ndelema

Mkoa kwa Mkoa - Michael Katembo, Nadhir Mayoka, Malima Ndelema

Disco Show - Julius Nyaisangah

General tyre na gari lako - Samadu Hassan

Ngano za Muziki - Salama Mfamao, Siwatu Luanda na wengine

Majira ya asubuhi na saa 3 usiku...

Watoto wetu - Watangazaji wa kike..

Mikingano - Salum Seif Nkamba 'SS Nkamba'

Mkulima wa Kisasa - Malima Ndelema

Michezo/Matangazo ya Mpira - Mshindo Mkenyenge, Omary Jongo, Ahmed Jongo 'Father', Dominick Chilambo, Mikidah Mahmoud, Charles Hillary, Juma Nkamia, Salim Mbonde, Abdallah Idrissa Majura na wengine..

Taarifa ya Habari - Julisu Nyaisangah, Charles Hillary, Betty Mkwasa, Sarh Dumba, Halima Kihemba, Jacob Tesha, Sekione Kitojo, Tido Mhando, Mikidad Mahmoud, Christine Chokunegela, Abdallah Mlawa, Abdul Ngalawa, Eddah Sanga, Aboubakary Liongo, Iddi Rashid Mchatta na wengine...

Mazungumzo baada ya Habari - Abdul Ngalawa, Mikidad Mahmoud

Pia walikuwepo wawakilishi wa Kanda/mikoa

Nyanda za Juu Kusini - Idrissa Sadallah, Martha Ngwila

Kanda ya Mashariki - Halima Kihemba , Penzi Nyamungumi, Monica Lyampawe..

Kanda ya Magharibi - Titus Philipo

Kigoma - Chisunga Stephen

Songea - Abisai Stephen

Lindi - Angalieni Mpendu

Ziwa Victoria - Dominick Chilambo, Nathan Rwehabura

Kanda ya Kati - Ben Kiko, Ahmed Kipozi, Sangi Kipozi, Hendrick Michael Libuda, Daniel Msangya, Wilson Malosha, Hellen Masele na wengine

Mtwara - Cassim Mikongoro

Kanda ya Kaskazini - Ahmed Jongo

Zanzibar - Yusuph Omary Chunda na Makame Abdallah

Hawa ni kwa uchache tu....


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwendraa af unajua utoto mpaka miaka 17. Ulivyo kapenda sifa unataka kutuambia hiyo miaka tayari ulikuwa unatumia topaz...sifa zitakuua nyonyo

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakumbuka kipindi hicho kulikuwa ma nyembe zinaitwa "Perma Sharp" kiwanda kilikuwa pale PUGU ROAD ambayo kwa sasa tunaita NYERERE ROAD, kiwanda hicho kilikuwa kinatazamana na kiwanda cha betri wakati huo kinaitwaNATIONAL, kwa kinaitwa PANASONIC.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wahengaa.. Idhaa ya Taifa ilikuwa inapiga nyimbo za kiswahili tu, idhaa ya biashara ndio ilikuwa inachanganya na miziki ya ki Zaire, hapa Lipua Lipua, Orch Veve, Kiam na nyinginezo, kweli maisha ni safari.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1. Tunakuletea Chakula na Lishe- Ranfred Masako
2. Wananchi Tujifunzeni Ushirika- Ibrahim Chemgege
3. Rushwa- Augustine Buluba
4. Jeshi letu la Polisi- Ramadhan Mhina
5. IDM Mzumbe- Zainabu Mwatawala
6. Bwana Umeme- ???
 
Back
Top Bottom