Wahhab kundi lenye itikadi kali ndani ya uislamu

Wahhab kundi lenye itikadi kali ndani ya uislamu

Sasa wewe, utaratibu wako wa maisha unaengemeza wapi? Labda nikuulize kama ni mwanaume umetahiriwa? Na kama ni ndio umepata wapi huo utaratibu? Kuna mengine mengi kama kuona, kuzikakana, majina tuliyo nayo n.k. yameegemea kwenye dini fulani. Ukisema huamini katika dini unakuwa unatudanganya.
labda nikuulize wewe huyo mungu wako ni wa dini gani
 
Unao ushahidi ? Wenzako kina nani ?
Labda huwajui ,Mimi nipo magrupu ya wahabi na salafi

Zipo nyingi Tena mnachukiana hatari
Screenshot_20250308-123715_1.jpg
 
Waislamu bila kujali ni Wasunn,Wahabi,Washia,Wahamadia ni walewale! Wote wanatumia Quran ile ile na Sunna za mtume yule yule.
Ni hatari kwa ulimwengu huu.
Nipo Grupu la mashia,suni, masalafi na wahhabi

Hao jamaa Wana chuki sio ya nchi hii Tena wao kwa wao ,nimegundua Wana chukua


Soma hii ya 👇👇

KWANINI MAWAHABI HAWAPENDI KUNASIBISHWA NA JINA LA SHEKH WAO SHEKH MUHAMMAD BIN ABDILWAHAAB ?

Wapo wanaosema haifai kuwaita Mawahabi au Wahabiya kwasababu ni jina la Allaah.

Madai haya sio ya kweli kwasababu, kwanza Allaah ni AL WAHAAB. Kwahiyo hata mtu akiitwa Wahab sio tatizo kisheria.

Pili kuna dhehebu katika Ahli sunna linaitwa Dhwaahiriyah ambapo Allaah anaitwa AL DHWAAHIR. Lakini hakuna Shekh wa Kiwahabi aliekataza matumizi ya jina hili.

Wapo wanaosema kwanini wasiitwe Muhammadiya kwasababu jina la kwanza la Shekh ni Muhammad na la pili ndio Abdulwahaab.

Hoja hii sio sahihi kwasababu, hata majina ya wafuasi wa maimamu wetu wanne wa Fiqhi hawaitwi kwa majina ya kwanza ya maimamu hawa.

Hanafiyah
Hanbaliyah
Maalikiyah
Shaafiyah

Majina yote hayo sio majina ya kwanza ya maimamu wetu wa nne.

Naomba tusaidiane kutafuta sababu kwanini Mawahabi hawapendi kuitwa kwa jina hili.

Kwa mtazamo naona baadhi ya matukio ya Kihistoria ya Shekh Muhammad bin Abdilwahaab, yanawafanya wafuasi wake wasijiamini kwa jina la Shekh wao.

Shekh Ibn Baz anasema, daawah ya Shekh Muhammad bin Abdilwahaab imeelezwa wazi katika vitabu vyake. Moja ya kitabu alichokitaja hapo ni Al Duraru Saniyya Fi Ajwibat Al Najdiyya

Sasa katika kitabu hicho Shekh Muhammad bin Abdilwahaab amenukuliwa akisema maneno haya

(وأنا أخبركم عن نفسي والله الذي لا إله إلا هو، لقد طلبت العلم، واعتقد من عرفني أن لي معرفة، وأنا ذلك الوقت، لا أعرف معنى لا إله إلا الله، ولا أعرف دين الإسلام، قبل هذا الخير الذي من الله به؛ وكذلك مشايخي، ما منهم رجل عرف ذلك.‏فمن زعم من علماء العارض أنه عرف معنى لا إله إلا الله، أو عرف معنى الإسلام قبل هذا الوقت، أو زعم من مشايخه أن أحدا عرف ذلك، فقد كذب وافترى، ولبس على الناس، ومدح نفسه بما ليس فيه).

الدرر السنية في الأجوبة النجدية51/10


"Na mimi nawapa habari kuhusu nafsi yangu, naapa kwa jina la Allaah ambae hakuna apasae kuabudiwa kwa haki ila yeye, hakika nimetafuta elimu na nikaitakidi nina maarifa. Na mimi katika wakati huo nilikuwa sijui maana ya Laa ilaaha illa Allaah, wala nilikuwa sijui Uislamu, kabla ya kheri hii ambayo Allaah amenineemesha Na hivyo hivyo Mashekh wangu hakuna katika wao mtu aliekuwa anajua hayo (Maana ya Laa ilaaha illa Allaah na Uislamu). Na atakae dai miongoni mwa wanazuoni kwamba anajua maana ya Laa ilaaha illa Allaah au anajua maana ya Uislamu kabla ya wakati huu, au akadai miongoni mwa Mashekhe zake kwamba yupo yoyote anajua hilo (maana ya Laa ilaaha illa Allaah) basi atakuwa amezua na akawadanganya watu na amejisifu kuwa na elimu ambayo hakuwa nayo"

Kitabu: Al Duraru Saniyya Fil Ajwibat Al Najdiyya Juzuu ya 10 ukurasa wa 51.

Kwahiyo Shekh anaamini yeye ndio alikuja kuwafundisha Uislamu na maana ya Laa ilaaha illa Allaah, waislamu wote katika zama zake.

Na mtazamo huu ndio wameurithi Mawahabi wote, wanaamini waislamu wengi wamepotea isipokuwa wao.
 
Umecopy na kupastee mzee Baba....hutaki ata kuumiza kichwa,wa bongo bhna

Hizo sifa unazosema za wahab ndo sifa za kila muislam anatakiwa awe nazo...

Nyongeza mashia sio waislam
Kwa nn msiwauwe kwanza hao?
 
Pamoja na hayo. Waislamu duniani wanamchango gani kwenye dunia? Bidhaa 99.9%, mifumo, teknolojia, siasa na elimu tunatumia za makafiri
Kiufupi sioni mchango wa waarabu kwenye hii dunia maana hadi kanzu, baibui na nikabu vitambaa vyake vinatoka China (waabudu dragon)
1. Iran ni Nchi ya Tatu Duniani Nyuma ya Urusi na Usa kwenye Kutoa ma Injinia Duniani, Ma Injinia wake wanajulikana Dunia nzima mpaka Nchi kama Usa wanaaminiwa kuongoza project kubwa, mfano Project ya Mars. Drone zao zimechachafya vita ya Ukraine huko, wao ndo wamefanya leo ukifanyiwa Upasuaji wa Kichwa possibility ya kufa ni ndogo etc ipo top 20 kwenye nchi zenye Mchango mkubwa wa kisayansi Duniani, wanashika hadi nafasi ya 15

2. Saudi Arabia hasa Chuo chake cha mafuta ni Chuo cha pili kwa ubora wa mafuta duniani, wamegundua mambo mengi na mwaka 2023 ime rank chuo cha 3 Duniani kupewa Patents Usa.


Hao Saudi Arabia wana wanasayansi wao wengine kama Hayat Sindi Mgunduzi wa Mobile laboratory Zisizo tumia umeme, leo hii Unaenda pharmacy kununua Vikaratasi vya kupima mimba, Ukimwi, Hormony etc unajipima mwenyewe nyumbani huyu dada Ana mchango mkubwa kwenye Hio sector.

Saudi wapo top 30 ya Nchi zenye Output kubwa za Kisayansi

3. Uturuki tunaijua, Leo hii tunaona kina Antonio Conte wanaenda Uturuki kufanyiwa Upasuaji wa kuondoa Kipara, Tumeona Pfitzer Chanjo ya COVID ikitumia Technology ya Waturuki, Silaha zao zimefanya Vizuri Ukraine etc nayo ipo top 20 ya Nchi zenye Output kubwa Kisayansi.

Katika Nchi 30 ambazo zinaongoza publication za Kisayansi Duniani kuna Nchi 7 za kiisilamu Iran, Saudi, Uturuki, Indonesia, Malyasia, Egpty na Pakistan.

So sio kweli kwamba 99.9% ya invention hazitoki kwa waisilamu.
 
Mbona wanasema mnafanya bidaaView attachment 3263450
Elewa ninachozungumzia mimi sipo upande wa dhehebu lolote hapo

Nimesema kuwa duniani ukitekeleza kama ilivyoandikwa kwenye sheria utaonekanwa mbaya

Mfano siku TRA wakitekeleza sheria ya kukamata na kufungua biashara pamoja na faini kama ilivyoandikwa kwenye katiba lazima kuna kundi litapiga kelele Sana

Hivyo hivyo katika dini, ukitekeleza kama ilivyoandikwa katika dini kwa vitendo lazima utaitwa gaidi, sijui bidaa na mambo kama hayo

Nikahitimisha kwa kusema dini zote duniani zinafuata misingi ya kijamaa ambayo ili dini au dhehebu fulani liweze kutekeleza sheria zake ni lazima liwe katika jamii wanaoiamini dini au dhehebu hilo vinginevyo ni vita
 
Waislamu bila kujali ni Wasunn,Wahabi,Washia,Wahamadia ni walewale! Wote wanatumia Quran ile ile na Sunna za mtume yule yule.
Ni hatari kwa ulimwengu huu.
Ni hatari kivipi weyee,kwani we ulitaka waislam watofautiane kama dini nyinginezo?, waislamu ni wamoja kote, tofauti ni ndogo tu kimitazamo na kimapokeo.
 
Umecopy na kupastee mzee Baba....hutaki ata kuumiza kichwa,wa bongo bhna

Hizo sifa unazosema za wahab ndo sifa za kila muislam anatakiwa awe nazo...

Nyongeza mashia sio waislam
kama washia sio waislam ni kina nani? BAKWATA nao ni kina nani maana wanatofautiana na wale kina Ponda.
 
Kwa kifupi makundi yote ya kiislam ni ukafiri mtupu, hakuna Mungu hapo, ni mila, desturi na tamaduni za kipagani za waarabu wa mashariki ya kati ulikoanzia uislam
 
Tumeona kundi la osama bin laden la al qaeda na isis wanafuata itikadi kali za wahab, je makundi mengine kama al shabaab, boko haram na washenzi wengine wanaojinasibu ni waislam huku wakifanya ugaidi wanafuata uislam upi? Mara kuna wasuni, mara washia, mara waislamiya, mara mabohara hawa wote ni waislam wa aina gani? Maana kuna wengine hawafanyi ugaidi kabisa. Kwa mgawanyo huu ni mataifa yapi ni washia na yapi ni wasuni, waismailia na mabohara? Kuna waislam wengine wanaitwa ansar sunni nao ni wa aina gani hawa? Wapo hata tanzania huwahi kufunga na kufungua wakitofautiana na waislam wa BAKWATA
 
Ni hatari kivipi weyee,kwani we ulitaka waislam watofautiane kama dini nyinginezo?, waislamu ni wamoja kote, tofauti ni ndogo tu kimitazamo na kimapokeo.
Wamoja ,hapo hapo unasema tofauti ni ndogo

Washia na wasuni Hadi wanauana unasema tofaut ni ndogo

Salafi na wahhabi wanatoleana maneno makali na wote ni wasunni ,unasema tofaut ni ndogo

Mimi nakaa na wahabi na masufi jinsi wanavyoitanq na kuchukiana kisa kupishana mafundisho
 
Tumeona kundi la osama bin laden la al qaeda na isis wanafuata itikadi kali za wahab, je makundi mengine kama al shabaab, boko haram na washenzi wengine wanaojinasibu ni waislam huku wakifanya ugaidi wanafuata uislam upi? Mara kuna wasuni, mara washia, mara waislamiya, mara mabohara hawa wote ni waislam wa aina gani? Maana kuna wengine hawafanyi ugaidi kabisa. Kwa mgawanyo huu ni mataifa yapi ni washia na yapi ni wasuni, waismailia na mabohara? Kuna waislam wengine wanaitwa ansar sunni nao ni wa aina gani hawa? Wapo hata tanzania huwahi kufunga na kufungua wakitofautiana na waislam wa BAKWATA
Vikundi vyote vya kigaidi na itikadi Kali ni wahhabi
 
HAWA NI WAISLAMU WOTE DHAHEBU MOJA ,WOTE SUNII ILA NDANI YA SUNNI KUNA ITIKADI HIZI WAHABI NA SALAFI

LAKINI ONA CHUKI BAINA YAO ,WAPO TAYARI HATA KUTOANA ROHO

Gii2q6hWcAA-UzF.jpeg
Gii2q6YWIAAyCWI.jpeg
 
Back
Top Bottom