Waimba kwaya wanaokata miuno na kunengua kanisani wanamsifu Mungu kweli?

Waimba kwaya wanaokata miuno na kunengua kanisani wanamsifu Mungu kweli?

Ila wafia dini kwa kuhamisha magoli hamjambo.
Mimi nakumbuka miaka ya zamani kidogo ilikuwa hairuhusiwi mwanamke kuvaa suruali au siketi fupi na kwenda nayo kanisani!
Cha ajabu miaka ya hivi karibuni wanawake wanavaa vichupi skin jeans na kwenda nazo kanisani na mmeanza kusema eti "Mungu haangalii mavazi, ila anaangalia roho"
Kweli magugu yanaota katitati ya nganooo safi
 
Ibada za pasaka zinaendelea; kwaya mbalimbali zinatumbuiza. Nimeenda kwenye kanisa mojawapo kusali naomba nisilitaje jina.

Waimbaji wananengua na kucheza mithili ya ngoma za kienyeji na kidunia.

Wengine wananengua miuno kabisa.

Sasa huku ni kumsifu Mungu kweli?
Kwani viuno vimeumbwa na nani?
 
Hii mada ya mavazi inahitajika mjadala mpana.

Neno la Mungu hali kuweka provision ya kuwa hilo vazi la Mwanaume likiwa pana basi itakuwa Sawa la hasha!

Imeandikwa: “ mwanamke asivae mavazi yampasayo Mwanaume “ maana ni machukizo machoni pa Mungu .

Hakuna provision yoyote kwamba iwapo yatakuwa mapana hayo mavazi ya kiume basi mwanamke akivaa itakubalika la hasha!
Wewe nikikupa pensi nyanya utavaa? Najua hutavaa kwa sababu sio vazi la mwanaume
 
Wewe nikikupa pensi nyanya utavaa? Najua hutavaa kwa sababu sio vazi la mwanaume


Mahala ambapo Neno limeweka wazi kuhusu nini kifanyike ni vyema tukatii badala ya kujaribu kutafuta excuses mbalimbali.

Imeandikwa; “ utii ni bora kuliko sadaka “

Hicho ulichoandika ndicho mojawapo ya excuse ambayo wengi hupenda kutafuta kujifichia humo!

Wengine watakwambia kuna suruari za kike na kiume lakini yote ni kutafuta excuse coz kwenye jamii tuliyonayo vazi la Mwanaume linajukana ni lipi hata mtoto Mdogo anafahamu.!

Halafu wengine tukajadili mambo haya hupata makasiriko ni kawaida sana kuona watu wa namna hiyo!
 
Unakuta mtu amevaa kama yuko night club [emoji848][emoji848][emoji848]

Na ni kwa bahari isiyo nzuri kwenye mahubiri ya siku hizi wahakemei kuhusu mavazi ya kihuni!

Wewe vaa utakavyo hata kama utaonekana kama aendaye night club ni Sawa hakuna wa kukukemea ilimradi uende na sadaka yako tu [emoji108][emoji108]

Mahubiri ambayo yameshika kasi na hufundishwa mara kwa mara siku hizi ni kuhusu utoaji sadaka!

Ya Utaua na ufalme badae!
 
Ukitaka kuvuta watu popote pale
  1. Kata viuno
  2. Zungumzia mahusiano au mapenzi
Waimbaji siku hizi wananengua kwa mashindano si kwamba wanapeleka ujumbe wa Mungu ila wanawatega watu

Wahubiri wanaofuatiliwa na watazamaji au wasikilizaji wengi ni wale wanaozungumzia sana ndoa, mahusiano, tabia za mabinti nk

Wabunge nao wanapenda sana kuvuta attention za watu kwa kukatika kwenye mikutano ya kisiasa na kuzungumzia mapenzi bungeni

Viongozi wa kisiasa kadhalika ...rejea ukatikaji wa Kangi Lug mbele ya mkubwa wake wa kazi nk

Hospitali nako unakuta TV ikionyesha nyimbo za vitovu nje wagonjwa wanafunua blanket, wengine wanasukumia net pembeni
Siyo siku hizi,walokole 1998 huko nilikokua,beat ya bongoman wanavisha injili Kisha wananengua jukwaani
 
Hili ni fundisho la upotoshi limeingizwa makanisani na freemason lengo ni kuwapotosha watu.
Biblia imeweka wazi juu ya mitindo yote kuanzia mavazi,kusifu na kuabudu.
Msienende kama mataifa,kama mtu anacheza dansi zisizo na staha za kukata viuno Ili kuchochea ashiki sio mafundisho ya Biblia hayo.
Je haikuandikwa nabii alicheza mpaka mavazi yakamvuka? Na sherehe ilichukua siku 7 au wewe una bible yako ilio tofauti na ninayo isoma Mimi?. Acha mabo ya wajenzi huru Ile ni office kama office zingine zilivyo au hujui makampuni ya ujenzi ya wageni yalio jaa hapa Tz?.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Baada ya Daud kumuua Goliati watu waliimba na kucheza., bali walicheza kama matokeo ya furaha baada ya ushindi wa vita, na wala hawakucheza wakiwa kwenye hema Takatifu.

1 #Samweli 18:6-7 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda. Nao wale wanawake wakaitikiana wakicheza, wakasema, Sauli amewaua elfu zake, Na Daudi makumi elfu yake.

Daudi baada ya kufanikiwa kulirudisha Sanduku la Bwana mahali pake, tunaona anacheza, #NOTE: Hakucheza Hekaluni na wala alipokuwa mbele ya Sanduku hakucheza ovyo bali alirukaruka tu kwa shangwe ; Ni kweli alicheza lakini alicheza kistaarabu na wala hapa hakujifunua nguo, Bali alikoenda kucheza hadi akajifunua nguo ni nyumbani kwake Na wala sio mbele za Sanduku la Bwana. Kwa hiyo kuna aina za uchezaji alizocheza Daudi

1. Aina ya uchezaji Mbele ya sanduku la BWANA: Daudi alipokuwa mbele za uwepo wa Mungu alicheza, lakini hakujifunua nguo yoyote, ina maana alicheza kwa Adabu na staha mbele za Mungu.

2 #Samweli 6:16-19 Ikawa, sanduku la Bwana lilipoingia mji wa Daudi Mikali, binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akiruka-ruka na kucheza mbele za Bwana; akamdharau moyoni mwake.Wakaliingiza sanduku la Bwana, na kuliweka mahali pake, katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.Kisha Daudi alipokwisha kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani akawabarikia watu kwa jina la Bwana wa majeshi. Akawagawia watu wote, mkutano wote wa Israeli, wanaume kwa wanawake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu. Basi watu wote wakaenda zao, kila mtu nyumbani kwake.
#NOTE: Program zote za kupokea sanduku zilimalizika salama na Daudi akawabariki watu salama na kila mtu akarudi nyumbani kwake, na wala haioneshi Daudi akijifunua nguo.


2. Aina ya uchezaji wa pili ni ule aliocheza akiwa nyumbani mbele ya wajakazi wake na si mbele za BWANA; Baada ya kumaliza program zote salama ndipo sasa Daudi wakati anarudi nyumbani kwake akaanza kucheza ovyo hadi kujifunua nguo.

2 #Samweli 6:20 Ndipo Daudi akarudi ili awabarikie watu wa nyumbani mwake. Na Mikali, binti Sauli, akatoka nje aende kumlaki Daudi, naye akasema, Mfalme wa Israeli alikuwa mtukufu leo namna gani, akijifunua mwili wake mbele ya vijakazi vya watumishi wake, mfano wa watu baradhuli mmojawapo, ajifunuavyo mwili wake mbele ya watu, asipokuwa na haya!
Uchezaji huu wa DAUD akiwa nyumbani ni tofauti na ule aliocheza mbele za BWANA na ndio maana Mikali akasema Daud anacheza mfano wa watu #BARADHULI,


Ukisoma Biblia yako yenye misamiati mwishoni mwa Biblia inasema #BARADHULI ni Mtu asiyefaa, au ni mtu #Mpumbavu sana.

Ina maana kwamba Daudi alivuka mipaka ya uchezaji wa siku zote na ndio maana hata mke wake alishangaa. Kwa hiyo na wale wanaocheza makanisani kwa kumuiga Daudi kwamba alijifunua hadi nguo nao ni MABARADHURI yaani ni #WAPUMBAVU.

Sasa aina hii ya uchezaji wa pili wa Daudi ndio uchezaji unaotumiwa na baadhi ya Wakristo ndani ya majengo ya ibada na ndio mtindo huohuo unaotumiwa na wacheza #Sengeli na #Bongofleva ambao hucheza hadi kujifunua nguo,ndani yake kuna viduku na unenguaji(kukata mauno).

Kwa hiyo hata wale ndugu zangu wanaosema wanacheza Makanisani kwa sababu Daudi alicheza hadi kufunua nguo wanakosea; Daudi alipokuwa mbele za Mungu hakucheza viduku, au kunengua na wala hakujifunua nguo, bali alipokuwa nyumbani ndipo alicheza hadi akajifunua nguo, kwa mantiki hiyo kama unamuiga Daudi kwa kucheza ovyo, basi hivyo viduku kachezee nyumbani sio Kanisani, maana hata Daudi alifanya hivyo pia na wewe jifunue nguo.

Lakini pia kwa wale wanaume mnaosema mnamuiga Daudi kwa kucheza basi nawaombeni mumuige Daudi pia kwa kutembea na wake za watu, maana Daudi alizini na mke wa Uria. Kwa hiyo si kila jambo ndani ya Biblia linahitaji utekelezaji hapana!! Kuna matukio mengine yaliandikwa ili kutuonya sisi tusiige,

1 #Wakorintho 10:11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.


Sasa kinacho sababisha watu kucheza ovyo ni kutokana na uwepo wa mrundikano wa vyombo vingi ambavyo vikipigwa hupelekea midundo yenye msisimuko wa mwili, Na ndipo sasa baada ya tukio hili la Daudi la kucheza ovyo hadi kujifunua nguo Mungu ikabidi atoe onyo juu ya vyombo vya musiki kwa wale wanaomuiga Daudi:


#Amosi 6:5 ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi;


Kwa hiyo kitendo alichokifanya Daud cha kupiga vyombo vingi vya musiki hadi ikampelekea kujifunua nguo Mungu hakukiafiki na ndio maana anaonya.
Popote milipo mkizungumzia habari za uzima wa mbinguni basi tambueni na mimi nipo, ikiwa mpo 2 au zaidi nami nitakuea katikati yenu. Kucheza kwa mtumishi wa Mungu mbele ya waabudu tafsiri yake ni kumtukuza mungu na kuirejesha sifa zake.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Licha ya kwamba tunamuona Daudi akicheza kwenye matukio mbalimbali, lakini katika suala la uimbaji ndani ya Ibada Daudi alikuwa makini na alipokea maelekezo kutoka kwa Mungu jinsi ya kuongoza kwaya ya Walawi, na hatuoni waimbaji hawa wakicheza kwenye Hema Takatifu wala Hekaluni, bali walisimama wakiwa na vyombo vyao waliimba kwa utulivu nyimbo za kumtukuza Mungu

2 #Mambo ya Nyakati 29:25 Akawasimamisha Walawi nyumbani mwa Bwana wenye matoazi, wenye vinanda, na wenye vinubi, kama alivyoamuru Daudi, na Gadi mwonaji wa mfalme, na Nathani nabii; kwani Bwana aliamuru hivi kwa manabii wake.
Hawa waimbaji hawakuimba wakiwa wanacheza viduku au kukatika viuno bali waliimba wakiwa wamesimama 2 #Mambo ya Nyakati 35:15 Nao waimbaji, wana wa Asafu #wakasimama mahali pao, kama alivyoamuru Daudi, na Asafu, na Hemani, na Yeduthuni mwonaji wa mfalme; nao mabawabu walikuwa katika kila lango; hawakuhitaji kuondoka katika huduma yao, kwa kuwa ndugu zao Walawi wakawaandalia.

KWANINI HAITAKIWI KUCHEZA NDANI YA MAJENGO YA IBADA?
1. Eneo la ibada sio sehemu ya kurukaruka kama Disko, ni mahali pa unyenyekevu palipotengwa maalumu kwa ajili ya mwanadamu kumuabudu Mungu na ndio maana tunatoka nyumbani kwenda kanisani. Kwa hiyo kinahitajika kicho.
#Waebrania 12:28-29 Basi kwa kuwa tunapokea ufalme usioweza kutetemeshwa, na mwe na neema, ambayo kwa hiyo tumtolee Mungu ibada ya kumpendeza, pamoja na unyenyekevu na kicho;maana Mungu wetu ni moto ulao.
#Habakuki 2:20 Lakini Bwana yumo ndani ya hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake.

2. Malaika wenyewe ambao ni watakatifu wanamuabudu Mungu kwa kuimba kwa unyenyekevu wakiwa wamefunika nyuso zao, na sio kwa kurukaruka:
#Isaya 6:2-3 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.

3. Ikiwa unapoenda kwa Baba yako mzazi au kwa bosi wako kuomba msaada unaenda kwa unyenyekevu na kicho, inakuwaje kwa Mungu uende kwa kucheza viduku na kunengua, ambaye yeye Mungu ni zaidi ya baba yako,na ni zaidi ya boss wako?
#Malaki 1:6 Mwana humheshimu baba yake, na mtumishi humcha bwana wake; basi, kama mimi ni baba yenu, heshima yangu iko wapi? Na kama mimi ni bwana wenu, kicho changu ki wapi? Bwana wa majeshi awauliza ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau jina langu. Nanyi mwasema, Tumelidharau jina lako kwa jinsi gani?

4. Je kuna mtu ambaye Alisha wahi kwenda kwa mzazi wake au kwa Boss wake kuomba mahitaji Fulani na akaenda kwa kupiga kelele na kwa kuchezcheza viduku?
Kucheza ndiko kunawafanya watu waimbe nyimbo za matusi na za kipuuzi,kwa sababu asiliia kubwa ya nyimbo za siku hizi hazina ujumbe wowote, bali zinapendwa kwa sababu ya style za kucheza na midundo iliyomo, #Zaburi 47:7 Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote, Imbeni kwa akili.
Mungu akubariki sana.

Uzi umejibiwa kiitifaki na kwa mifano mbali mbali.

Mwenye macho na ashuhudie Roho Mtakatifu awaambia Mataifa kupitia Jackwillpower.
 
Ni sawa kabisa na inapendeza sana
 
“tena Walawi waimbaji, wote pia, yaani Asafu, na Hemani, na Yeduthuni, na wana wao, na ndugu zao, hali wamevaa kitani safi, wenye matoazi na vinanda na vinubi, wamesimama upande wa mashariki wa madhabahu, na pamoja nao makuhani mia na ishirini wakipiga panda😉

— 2 Mambo ya Nyakati 5:12 (Biblia Takatifu)



Ufunuo wa Yohana 15 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
² Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu.
³ Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa.
 
Wasabato walidecide kwamba wasicheze kabisa. Kongole kwao.

Na madhehebu mwengine waliomua kucheza wacheze wanavyojisikia. Msikae mnapangia watu jinsi ya kucheza.
 
Hili ni fundisho la upotoshi limeingizwa makanisani na freemason lengo ni kuwapotosha watu.
Biblia imeweka wazi juu ya mitindo yote kuanzia mavazi,kusifu na kuabudu.
Msienende kama mataifa,kama mtu anacheza dansi zisizo na staha za kukata viuno Ili kuchochea ashiki sio mafundisho ya Biblia hayo.
kucheza kuna kipimo?

Tupe kipimo basi
 
ATHARI ZA KUCHEZA MBELE ZA MUNGU.

1. DHARAU [emoji116]

2 SAMWELI 6:16.
Ikawa, sanduku la BWANA lilipoingia mji wa Daudi Mikali, binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akiruka-ruka na kucheza mbele za BWANA; akamdharau moyoni mwake.

2. KUONEKANA MPUMBAVU (BARADHULI) [emoji116]

2 SAMWELI 6:20.
Ndipo Daudi akarudi ili awabarikie watu wa nyumbani mwake. Na Mikali, binti Sauli, akatoka nje aende kumlaki Daudi, naye akasema, Mfalme wa Israeli alikuwa mtukufu leo namna gani, akijifunua mwili wake mbele ya vijakazi vya watumishi wake, mfano wa watu baradhuli mmojawapo, ajifunuavyo mwili wake mbele ya watu, asipokuwa na haya!

3. NI UPUUZI NA MUNGU ATAADHIBU "AMOSI 5." [emoji116]

AMOSI 6:5.
Ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi.
 
Wasabato walidecide kwamba wasicheze kabisa. Kongole kwao.

Na madhehebu mwengine waliomua kucheza wacheze wanavyojisikia. Msikae mnapangia watu jinsi ya kucheza.
Wasabato hawajiamulia bali ni maagizo ya Mungu kupitia Biblia.

SOMA UJUMBE WOTE NO 49.
 
Back
Top Bottom