Wakati Urusi bado wanahangaika na HIMARS, sasa USA kutuma 'VAMPIRE' Ukraine

Wakati Urusi bado wanahangaika na HIMARS, sasa USA kutuma 'VAMPIRE' Ukraine

Hiki ndicho kitu Marekani anakipenda siku zote. Kutengeneza migogoro ya kivita duniani kote, ili wamiliki wa viwanda vya silaha wa Kimarekani wapate soko la kuuzia bidhaa zao.

Na wakati huo huo tenda za kuijenga upya hiyo nchi iliyo haribiwa na vita lazima yapewe makampuni ya Kimarekani!

Kiufupi tu Marekani ni Taifa la kijinga sana. Kamwe huwezi kuona vita inapiganwa nchini kwake! Yenyewe inapenda kuchochea vita kwenye nchi nyingine, halafu wakati mnauana, yenyewe inawauzia silaha na kuchukua yenda za ujenzi! Na kama kuna mafuta, inabeba kupeleka Marekani.

Yule Mchekeshaji Zelenysky anatumika pasipo yeye mwenyewe kujua.
Fahamu hili
20220826_180257.jpg
 
No at all, Russia with her advanced weapons in repository, can set ablaze most part of Ukraine and cause many people lives to perish let alone casualties etc, mind you, Russia will never ever accept defeat in this operation . By NATO and The US supplying weapons to Ukraine it is just like fuelling the crisis and it is Ukraine which, so far, suffers a lot. Russia uses her high-tech weapons in calculations.
Huelewei unachosema
20220826_180257.jpg
 
Congress wamempa Biden dola bilioni 40 za kuanzia atumuie kwa ajili ya Ukraine, bajeti ya mwaka ya ulinzi tu ya US ni dola bilioni 750.
Vita vya Iraq US ilikuwa inatumia dola milion 300 kwa siku kwa miaka 20.
Hawafilisiki leo wala kesho hao.
Sio kwa Urusi! Hapo Marekani atatoa mikopo mingi kwa Ukraine ila akija kushtuka Ukraine yenyewe haitokuwepo tena.
Yani kwa kifupi Marekani atakula hasara kubwa itakayopelekea anguko lake
 
Mfano wa hao watu wanaoitwa "finance capital" ni kina nani?
Wataje watatu tu.
Mkuu, sera zilikwishatengenezwa miaka zaidi ya 20 sasa kuhusu kuifanya Russia iwe kainchi chenye kuwategemea wao NATO na Marekani.

Hiyo ya kusogea kidogokidogo pembezoni kwa Russia kutaka kuizunguka, kisha kuivamia na kuigawa mazima na baadae kupora rasilmali zake yabaki kuwa ndio sera pekee kwa sasa.

Hiyo ndo sababu Marekani na NATO wataendelea kusaidia silaha hadi hapo wanaaamini Russia itaanguka na itachukuliwa nao na Ukraine ndio awe mbadala wa Russia.

Tufahamu kuwa sasa hivi NATO na Marekani wamesema wazi kuwa maadui wao ni Russia na China hivyo lazima waongeze bajeti zao za ulinzi kwa ajili ya kukabiliana nao, ni vita ya kugombania maeneo yenye rasilimali na kuyamiliki kwa nguvu au "Hegemovy".

Lakini hapohapo kuna mambo mawili makubwa kuhusiana na vita hii ya Ukraine ambayo Zelenski anatumika.

Kwanza, ni makubaliano ya siri kati ya Marekani na NATO ambao viongozi wake wanakutana kuamua sera mbalimbali za dunia kwa siri huku wakificha ukweli halisi malengo ya walo nyuma yao ambao wana hisa katika rasilimali na uchumi wa dunia hii.

Pili, mzizi khasa wa vita hii ni lazima ueleweke baina yetu kwamba, huu ni mgawanyo wa dunia baina ya mataifa makubwa ambazo tangu mwaka 1991 USSR ilipoanguka wanataka kuizunguka Russia na kumuondoa raisi Putin na kuhodhi rasilimali za nchi hiyo bure kwa niaba ya hao watu ambao huitwa "finance capital".

Hawa watu wapo na ndo hupanga mipango ya dunia hii, ila safari hii wamekumbana na Vladmir Putin, jambo ambalo ni mtihani mkubwa kwa kujipa kazi ya kukabiliana na hawa jamaa.
 
Kumbe Hypersonic na thermobaric bombs ni silaha za vita vya pili vya dunia![emoji1787]

Kitu Mrusi hajatumia Ukraine ni mabomu ya nyuklia tu wewe kilaza.
Hapana .mrusi anajifanya .kama vita imemshinda .hii si kweli ebu jaribu kufikiria toka wa magharibu watume machuma yao ukrein nn kimebadilika? Mrusi anakuambia silaha anazotumia sasa nizile toka vita kuu ya pili. Zana zake mpya hajazigusa kabisa anasubiri wa magharibi wamalize kutoa zakwao ndiyo muone mrusi anafanya nn ukrain .
 
Bullshit na mawazo ya kijima ya kumhesimu mkubwa tu.

Mbona Finland imepeleka maombi ya kujiunga na NATO na huyo mkubwa hajamvamia mpaka sasa hivi?
Wewe ni team America. Tutaishia tu kubishana na kamwe hatutaelewana.
 
Uongo mtupu,

1.Zelenskyy haiwezi kuiingiza Ukraine NATO, Bunge la Ukraine ndilo lenye mamlaka hayo.

2.Ukraine pia haiwezi kuingia tu NATO bila nchi wanachama wote wa NATO kuridhia kupitia mabunge ya nchi zao.

3.Mbona Finland imepeleka maombi ya kujiunga NATO na mchakato wa kuifanya mwanachama umeanza ila Putin hajaivamia mpaka sasa??
Mwaka huu wa 2022 huyo Zelenysky alipanga kuiingiza Ukraine kwenye Umoja wa Ulaya na NATO! Jambo ambalo Putin alishalipinga tangu mwanzo. Ila sasa kwa sababu huyo Zelenysky alishajazwa upepo na Marekani, akajifanya mkaidi.

Na mwisho wa siku Putin akaja na hii oparesheni yake maalum ya kutaka kuiindoa kimabavu hiyo Serikali ya Ukraine yenye mafungamqno na nchi za magharibi na Marekani.
 
... uko tayari ku-surrender uhuru wa familia yako simply jirani yako hataki ufanye kitu fulani chenye manufaa kwa family yako?
Kwani kungetokea nini iwapo hiyo Ukraine ingebakia kuwa neutral State kama alivyotaka Urusi?

Na hasa umichukulia uhasama wa muda mrefu uliopo kati ya Urusi na Marekani, na baadhi ya nchi za Ulaya Magharibi! Na hasa Uingereza?
 
Hiki ndicho kitu Marekani anakipenda siku zote. Kutengeneza migogoro ya kivita duniani kote, ili wamiliki wa viwanda vya silaha wa Kimarekani wapate soko la kuuzia bidhaa zao.

Na wakati huo huo tenda za kuijenga upya hiyo nchi iliyo haribiwa na vita lazima yapewe makampuni ya Kimarekani!

Kiufupi tu Marekani ni Taifa la kijinga sana. Kamwe huwezi kuona vita inapiganwa nchini kwake! Yenyewe inapenda kuchochea vita kwenye nchi nyingine, halafu wakati mnauana, yenyewe inawauzia silaha na kuchukua yenda za ujenzi! Na kama kuna mafuta, inabeba kupeleka Marekani.

Yule Mchekeshaji Zelenysky anatumika pasipo yeye mwenyewe kujua.


Well said binafsi nawashangaa JF Members wanao support Ma-Gringo hawa wauuaji, wakatiri, wafitini,roho za kutu walio kubuhu kwenye vices zote ovu hapa Duniani!!

Wao ndio walio changia sana kwenye vita hii inayo endelea nchini Ukraine walimvimbisha kichwa Zelensky ili apuuzie makubaliano ya Minsk vile vile NATO specifically USA ikapuuzia/dharau concerns za Urusi kuhusu kuwakikishiwa usalama wa Taifa lake baada ya kuona NATO alliance inajisogeza sogeza na kuizingira mipaka yote ya Urusi, kufanya mazoezi mara kadhaa kwa mwaka wakiwa mipakani mwa Urusi kwa lengo la kujaribu kuwa tisha tisha Warusi, yaani ujeuri wa Merikani unaifanya kusahau kwamba Urusi ni a thermonuclear Super Power yenye uwezo mkubwa wa kuifuta kwenye uso wa Dunia Taifa lote la Merikani in no time - Urusi iliwaonya Wamerikani kidiplomasia mara nyingi tu lakini Merikani ikampuuzia tu kutokana na ujeuri na dharau za kitoto,walifikiri Urusi haiwezi kufanya lolote kukomesha ujinga/uchokozi wao, Wamerikani walivyo watu wa ajabu Urusi ikipeleka silaha kwenye mipaka ya Mexico na Merikani, Cuba,Venezuela, Nicaragua na Canada na kuanzisha mazoezi ya kijeshi ikishirikiana na mataifa tajwa hapo juu, nawa hakikisheni siku hiyo Merikani itaitisha kikao cha dhalula cha Umoja wa mataifa kuishutumu Urusi kwa hatarisha amani Duninani lakini wao kuwafanyia ujinga kama huo huo Warusi wao wanaona hilo balabala.

Vita ya Ukraine ndio Merikani imeona imepata golden opportunity ya kutekeleza njama/malengo yake ya miaka mingi dhidi ya Urusi kwa kulitumia taifa kubwa kieneo Barani Ulaya lenye wanajeshi wengi pamoja na silaha nyingi ndio maana Amerika imeshupalia Taifa la Ukraine lipigane a proxy war kwa niaba ya Merikani walishirikiana na wamiliki wa viwanda vinavyo unda silaha(MIC) - wamiliki wa viwanda hivyo huko Merikani ni kama Serikali ndani ya Serikali hao ndio wanamwendesha puta Biden afanye wapendalo si wao wala Biden wenye uchungu wa kweli kuhusu Ukraine na raia wake, wanacho fanya ni maigizo tu akili zao zote zipo kwenye uuzaji wa silaha kwa wingi na kutaka kusambaratisha taifa la Urusi wako, overly obsessed na Urusi, lakini wanagwaya kupigana na Warusi moja kwa moja ndio maana wanawatumia watu/mataifa mengine kabisa kutekeleza malengo yao ya siri.

Watu wangapi wanajua kwamba mwanae Biden alikuwa mshauri mkubwa wa Serikali ya Ukraine wakati baba yake akiwa makamu wa Rais Obama, akamilikishwa kampuni ya Ukraine inayo deal na biashara ya mafuta na gesi - huu ni ushahidi tosha wa kudhilisha kwamba familia ya Biden wana vast vested interest kwenye taifa la Ukraine - hivyo Rais Biden atalazimika kufanya lolote ili kuhalikisha maslahi ya familia nchini Ukraine yanalindwa these are some of reasons why Biden ana chuki binafsi kwa Putin,swali ni: wangapi wanajua ukweli huo.
 
Kwani kungetokea nini iwapo hiyo Ukraine ingebakia kuwa neutral State kama alivyotaka Urusi?

Na hasa umichukulia uhasama wa muda mrefu uliopo kati ya Urusi na Marekani, na baadhi ya nchi za Ulaya Magharibi! Na hasa Uingereza?
... "kama alivyotaka Urusi"! Kama thinking zenyewe ndio hizo ni hatari sana! Kuna mktaba wowote baina ya Ukraine na Urusi ambao Ukraine ameuvunja? Au ni kwa kuwa Putin hataki tu? In short, Russia hana justification yoyote ya kuivamia Ukraine.
 
... "kama alivyotaka Urusi"! Kama thinking zenyewe ndio hizo ni hatari sana! Kuna mktaba wowote baina ya Ukraine na Urusi ambao Ukraine ameuvunja? Au ni kwa kuwa Putin hataki tu? In short, Russia hana justification yoyote ya kuivamia Ukraine.
Justification zipo kiusalama zaidi kilaza huwezi elewa. Ni sawa tu na ndugu yako akitaka kukuingiza matatizoni ukaamua kumchukulia hatua wengi watakuona huna maana ila kumbe unalinda usalama wako.
 
Hiki ndicho kitu Marekani anakipenda siku zote. Kutengeneza migogoro ya kivita duniani kote, ili wamiliki wa viwanda vya silaha wa Kimarekani wapate soko la kuuzia bidhaa zao.

Na wakati huo huo tenda za kuijenga upya hiyo nchi iliyo haribiwa na vita lazima yapewe makampuni ya Kimarekani!

Kiufupi tu Marekani ni Taifa la kijinga sana. Kamwe huwezi kuona vita inapiganwa nchini kwake! Yenyewe inapenda kuchochea vita kwenye nchi nyingine, halafu wakati mnauana, yenyewe inawauzia silaha na kuchukua yenda za ujenzi! Na kama kuna mafuta, inabeba kupeleka Marekani.

Yule Mchekeshaji Zelenysky anatumika pasipo yeye mwenyewe kujua.

Hata Putin naye anatumika pasipo yeye kujua, waukraine na warusi wanakufa kwa faida ya Marekani.
 
Justification zipo kiusalama zaidi kilaza huwezi elewa. Ni sawa tu na ndugu yako akitaka kukuingiza matatizoni ukaamua kumchukulia hatua wengi watakuona huna maana ila kumbe unalinda usalama wako.
... nakuheshimu sana humu jamvini bro; tumia lugha ya staha. Kwa hiyo tangu Russia kuivamia na kuimiliki Crimea back 2014 ilikuwa ni kulinda usalama wake (Russia) au alikuwa na mengine?
 
Ukraine haijwahi kuacha kuwa neutral state.

Kwa nini Putin anataka Ukraine tu ndio iwe neutral state ila sio nyingine kama Finland, Estonia, Latvia au Japan anazopakana nazo?
Kwani kungetokea nini iwapo hiyo Ukraine ingebakia kuwa neutral State kama alivyotaka Urusi?

Na hasa umichukulia uhasama wa muda mrefu uliopo kati ya Urusi na Marekani, na baadhi ya nchi za Ulaya Magharibi! Na hasa Uingereza?
 
Hiki ndicho kitu Marekani anakipenda siku zote. Kutengeneza migogoro ya kivita duniani kote, ili wamiliki wa viwanda vya silaha wa Kimarekani wapate soko la kuuzia bidhaa zao.

Na wakati huo huo tenda za kuijenga upya hiyo nchi iliyo haribiwa na vita lazima yapewe makampuni ya Kimarekani!

Kiufupi tu Marekani ni Taifa la kijinga sana. Kamwe huwezi kuona vita inapiganwa nchini kwake! Yenyewe inapenda kuchochea vita kwenye nchi nyingine, halafu wakati mnauana, yenyewe inawauzia silaha na kuchukua yenda za ujenzi! Na kama kuna mafuta, inabeba kupeleka Marekani.

Yule Mchekeshaji Zelenysky anatumika pasipo yeye mwenyewe kujua.
Wazungu nao wameonesha utahiira wao kwenye hili. Wameshindea kuwa na misimamo yao binafsi. Hawana tofauti na huku Africa
 
Back
Top Bottom