Wakati Watanzania wakibishana juu ya Bandari ya Bagamoyo, Kenya wafungua Bandari ya Lamu

Tanzania tumejaa masihara sana mdau berth 12 ni upuuzi mtupu kwa dunia ya leo tena ukizingatia tunahudumia nchi nyingi za pembeni yetu.....
 

Tanzania tayari tuna bandari sijui mapepe ya bandari nyingine ni ya nini wakati mizigo inatosha pale Dar pakipanuliwa vizuri. Lakini ni ujinga kujenga bandari nyingine kwa mikopo na kuwapa wageni waendeshe kwa faida zao. China anafikiria kufanya sehemu ile iwe kambi ya jeshi na dampo la vitu vya China. Yaani sisi tutoe miaka 100 na mizigo yote ihamie bagamoyo ina maana tutakuwa tumeuwa bandari ya Dar!. Hiyo bandari ikijengwa haitakuwa yetu kwa mikataba ya sasa itakuwa balozi ya china pale hata bendera itakuwa ya china. Je Kenya wametoa kwa miaka 100! ni ujinga mtupu
 
Haujamuelewa.... Tufundishe ni namna gani iyo bandari italeta faida wakati kuna bandari kibao na hatujawah kuona zikileta faida....

Then kwa nini ijengwe ingine kuliko kutanuliwa zilizopo?

Then kuna sababu hipi kuwa ni bagamoyo tu.... Kitaalamu au kibiashara??


Wajinga tupo weengi ukitaka tukueleww ni lazima kutuelekeza na sio kutulaumu tukipinga.

Berth ni kizungu tu kisikuchanganye..... Parking lot tu
 
Halafu kuna wajinga wanamuita Mbeba maono?? Kama Mwendazake alijuwa mbeba maono bassi alibeba maono ya vipofu. Na vipofu wenyewe Ni sisi Watanzania Milioni 60.

Kweli mtu aliyenakili (Plagiarist) andiko la PhD la mwenzie anaweza akawa na maono?

Magufuli alikuwa na akili za wastani tu, yaani karai au Grade "C", lakini alitaka tumtambue kama intellectual visionary leader.

No way, alikuwa ni BIG FAILURE
 
Lakn inasemekana bandari ya Bagamoyo isingekuwa na faida kwetu kama tungekubali ijengwe
Tujihadhari na China. China ya sasa sio ile ya wakina Mao -Tse - Tung na Choenlai. Hawa sasa ni mabepari wanaotaka kufanya Afrika koloni lao kwa mikopo ya miradi isiyolipa huku dhamana ikiwa kubwa sana. Djibouti na Zambia ni mifano ya nchi ambazo zimelizwa na hao Wachina. Kuwakataa Wachina ilikuwa ni kuona mbali! Hatukatai bandari bali tunakataa masharti ya mkataba!
 
Unataka wasifungue nyingine wakati Mombasa imechukuliwa na wachina?
Kwa hiyo na sisi tufungue nyingine? Pwani yetu ina bandari ngapi na Kenya inazo ngapi? Lengo ni kufungua tu, bila sababu? Foolish creature!
 
Foolish! Unadhani ukiongeza ndo unapata ufanisi? Mizigo inatengenezwa na berth? Mtu nguchiro?
 
Kwa hiyo kwa sababu Kenya wamezindua bandari mpya basi ni kigezo cha sisi kujenga bandari ya Bagamoyo? Je bandari za Dar es salaam, Tanga na Mtwara tumeziwezeshaje ili ziweze kutoa huduma nzuri na kubeba mizigo mingi?
 
Chadema ndege walipinga, reli walipinga, bwawa la nyerere walipinga, lakini kutwa macho kodo kusifia maendeleo ya Kenya
Hapo kuna mengi Boss! Wanasifia Kenya ili kuonesha hasira yao tu ya kikabila. Ukiwauliza malengo ya Bandari ya Lamu ni yapi, wao wanahesabu mizigo utadhani kuna meli zinasubilia bandari mpya. Ukiwauliza kama wana mizigo imekosa bandari, watasema iko mingi tu!
 
Kwa hiyo kwa sababu Kenya wamezindua bandari mpya basi ni kigezo cha sisi kujenga bandari ya Bagamoyo? Je bandari za Dar es salaam, Tanga na Mtwara tumeziwezeshaje ili ziweze kutoa huduma nzuri na kubeba mizigo mingi?
Sgr ikikamilika bandari yetu ya dar itakuwa na uwezo wa kuilisha mzigo wa kutosha??
 
Mkataba kwanza ukajadiliwe bungeni na akina Msukuma.
Halafu wataalam watuambie wananchi.
 
Mada ina lengo la kuwapa uoga watanzania.

Upanuzi wa bandari zote tulizonazo na uendelee kama kawaida.

Pwani yetu ni kubwa kuliko ya jirani zetu wa kaskazini hivyo hatuhitaji kujiona tumechelewa, hizo fursa zipo tu.
 
Mada ina lengo la kuwapa uoga watanzania.

Upanuzi wa bandari zote tulizonazo na uendelee kama kawaida.

Pwani yetu ni kubwa kuliko ya jirani zetu wa kaskazini hivyo hatuhitaji kujiona tumechelewa, hizo fursa zipo tu.
Unazungumzia vibandari hivi mbuzi vilivyoachwa na mkoloni?

Hivi vibandari haviwezeshi mimeli mikubwa kutia nanga, ni vidogo sana na hiyo ya Dar kina chake ni kidogo sana kuwezesha mimeli hiyo kutia nanga
 
Unazungumzia vibandari hivi mbuzi vilivyoachwa na mkoloni?

Hivi vibandari haviwezeshi mimeli mikubwa kutia nanga, ni vidogo sana na hiyo ya Dar kina chake ni kidogo sana kuwezesha mimeli hiyo kutia nanga
Hiyo ya bagamoyo ina mizengwe mingi kwa mujibu wa JPM inabidi tuwekwe sawa tusije kuuziwa mbuzi kwa mlio.

Afadhali hizi alizoacha mkoloni tunazozijua kwa undani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…