Uchaguzi 2020 Wakazi wa Dar es Salaam kweli na nyie mtamnyima Magufuli kura?

Uchaguzi 2020 Wakazi wa Dar es Salaam kweli na nyie mtamnyima Magufuli kura?

Ccm wenyewe wanajua kama watu wa dar hawajawahi kuiamini ccm. Ccm dar labda sana sana waibe kura. Dar ccm inachukiwa kwa sababu ya bomoa bomoa, watu kama wa kimara unategemea wawape kura ccm
 
Wana JF habari. Mi sio mwanasiasa Ila Uchaguzi tunaoshiriki ni wengi japokuwa wengine huwa hawapigi kura Ila maneno wanayo mengi kwenye vijiwe.

Kuelekea tarehe 28.10.2020 siku ya jambo la watu Fulani.
Bado najiluliza Kama wana Dar es Salaam nao watashindwa kumpa kura JPM..

Tunatambua wale jamaa wa Buhaya wao hawana masihara kabisa hapati kitu pale mheshimiwa .

Ila sasa kwa wana Dar es Salaam habari katika television zetu zilipambwa kwa kiasi kikubwa na maendeleo ya mkoa huo.

1. SGR(Railway)
2. Mbezi Stand
3. Ubungo FlyOver
4. Kinyerezi
5. The Port
6. Airport

Na mengine mengi ni heri wana Kaskazini wamnyime Ila sio wana Dar..

Ila ngoja tuone wana DSM wanalichukuliaje hili?
Unafikiri Dar wanaishi mapoyoyo kama wa Kongwa kwa Ndugai?
 
Mwenyezi Mungu ni wa haki hivyo hupendezwa na matendo ya haki.

Udhalimu ni machukizo na huambatana na adhabu na ugumu ktk namna tofauti tofauti!

Tumuogope Mungu sana!
 
Dar Es Salaam tumeokotana sana beach tukiwa maiti kwenye viroba.
Na tumetekwa sana ndani ya nchi yetu huru..?!
Magufuli hafai ni Muuaji mkubwa.
Oktoba 28 kura zote za DSM, ni kwa mbeba maono #NIYEYE
 
Saa nne asubuhi Magufuli namba moja Dar es salaam

1602460886894.png
 
Wana JF habari. Mi sio mwanasiasa Ila Uchaguzi tunaoshiriki ni wengi japokuwa wengine huwa hawapigi kura Ila maneno wanayo mengi kwenye vijiwe.

Kuelekea tarehe 28.10.2020 siku ya jambo la watu Fulani.
Bado najiuliza Kama wana Dar es Salaam nao watashindwa kumpa kura JPM..

Tunatambua wale jamaa wa Buhaya wao hawana masihara kabisa hapati kitu pale mheshimiwa .

Ila sasa kwa wana Dar es Salaam habari katika television zetu zilipambwa kwa kiasi kikubwa na maendeleo ya mkoa huo.

1. SGR(Railway)
2. Mbezi Stand
3. Ubungo FlyOver
4. Kinyerezi
5. The Port
6. Airport

Na mengine mengi ni heri wana Kaskazini wamnyime Ila sio wana Dar..

Ila ngoja tuone wana DSM wanalichukuliaje hili?
Kwa nini mnaziba masikio na kung'ang'ania vitu badala ya watu?

Hivyo vitu vitano ni vichache kulinganisha na walivyofanya wakoloni, mbona waliondolewa?
 
Wagombea wa CCM huwa wanatuambia Tuache Kutegemea Kuajiriwa Na Serikali, Tujitegemee Na Tujiajiri Wenyewe!! Wakati Wao Wanatuomba Kura Ili Tuwape Ajira Waajiriwe Na wananchi.

TUSAIDIANE MAWAZO HAPA VIJANA WENZANGU, HAWA WATU ZIMO KWELI VICHWANI MWAO ?
Wanazo sana akii tatizo wanatuona sisi mazwazwa
 
I relevant ndio nini? Even to type an english word is a problem to you, how then can you urge with me? Show how irrelevant they are fella. Yaonekana you're very simple minded person mpaka kushindwa kuanalyse hayo unayosema mengi, sasa mimi na wewe nani ana poor understanding capacity.?
Kama kukosea ku type tu ndio mtu awe ana matatizo makubwa hivyo, basi angalia na wewe hilo neno uliloliandika urge
 
Hata Buhaya watampa kura nyingi tu. Pesa za tetemeko zimeboresha shule ya sekondari imekuwa ya kisasa na kuna meli zipo ziwa Victoria zinafanya kazi nzuri.

Watu wa Dar hatuna sababu ya msingi ya kumkataa Magufuli, tuna sababu ya kuwakataa wabunge wanaokwenda bungeni kuvaa vitambaa midomoni na kutoka nje ya ukumbi wakiwa wameshachukua posho ya siku.
Bora hao kuliko hao wetu wa Ndio mzee Rubber stamps.. Wakiulizwa Umeoga? Ndio. Hujaoga? Ndio. Enzi za kina Mzindakaya ilikuwa komesha huwezi fananisha na hizi punda akina Kibajaji
 
watanzania wote kwa umojawetu hajaalishi upo wapi, hakikisha tarehe ishirini na nane unakataa ccm, hawandio chanzo cha umasikini Tanzania, wameua kilimo cha kahawa huko mbozi, wamua mbaazi, wameua korosho, wameaua mji wa dar, maduka ya kubadilishia fedha za kigeni, sijui vitambulisho ya mjasiriaa mali mabayo habita hata sifa ya kuitwa vitambulisho, mambo mengi maovu yamefanywa dhidi ya watanzania, tukatae kwa kumpigia kura Lissu, twende naye tupate utawala wa sheria wa kusheshimu taasisi zilizowekwa kisheria.
 
Kwa nini mnaziba masikio na kung'ang'ania vitu badala ya watu?

Hivyo vitu vitano ni vichache kulinganisha na walivyofanya wakoloni, mbona waliondolewa?
Mkoloni asingenyanyasa watu Hadi leo tungekuwa nae akituletea maendeleo
 
Katika mikoa iliyoathirika na serikali ya awamu ya tano ni Dar es salaam. Kuhamisha makao makuu ya nchi kwenda Dodoma ni pigo la historia kwa wakazi wa Dar es salaam. Balozi zote zitaamua Dodoma,ikulu Dodoma,wizara zote Dodoma, mashirika ya kimataifa Dodoma, mashirika ya umma Dodoma,wafanyakazi wote Dodoma,uwanja wa ndege wa msalato Dodoma. Sasa akawadanganya kuondoa foleni dar kwa kujenga flyover,sio kweli kwanza foleni dar haitakuwepo kwani serikali inaondoka kwenda Dodoma. Kwa mantiki hiyo uchumi wa dar ikifika mwaka 2025 wananchi wengi watakuwa omba omba kwani miradi yao mingi itakuwa imekufa au haipo tena.
Magufuli amehamishiwa makao makuu Dodoma kwa makusudi kwa kutambua kuwa watu wengi waliiba fedha serikalini awamu zilizopita na kuwekeza Dar,Sasa walioiba washindwe kuwekeza Dodoma na miradi iliyopo dar ife. Kwa kifupi Dar hali itakuwa mbaya sana .tunadanganywa dar itakuwa jiji la biashara biashara ipi itajwe? Utawala huu utaacha historia dar kuweni nao makini sana.
Ndoto za mchana hizo,alisema atakaebaki dar ni mwanaume matokeo yake kakimbia mwenyewe,dodoma kuna fursa gani Hadi iishinde dar, population ndio uchumi wa jiji lolote.
Dodoma bado Sana kuifikia hata Mwanza au Mbeya tu sembuse dar
 
Back
Top Bottom