Wakazi wa Tarakea wachota maji Kenya

Hili ndio tatizo
Shirika la maji hawawezi kazi halafu hawataki wapinzani
Huu ni ushenzi kabisa ndio mana watoto wanakufa kisa maji machafu kabla hata hawajafika mitano
Tuna bahati kuishi kwenye nchi za umasikini wa kujitakia
Kule iringa chadema walichimba kisima mwenyekit ccm mtaa wakenda kubomoa
Daaah unajiuliza hivi hawa jamaa wanafikiri kwa kutumia nn?
 
Hawajui jinsi ni majirani
Hata mitandao husoma safari com.
Lkn ishu ya maji kwa tarakea ni tatizo. Na sehem kadha wa kadha rombo. Hii imechangiwa sana na ukataji wa miti ya mbao 90s kurudi nyuma kabla hawahamishia Iringa huko. Mito ilikua ikijaa maji yoote lkn siku hizi ni kisanga. Maji yakichimbwa bila shaka yapo ni basi tu kuna uzembe.
 
Kule iringa chadema walichimba kisima mwenyekit ccm mtaa wakenda kubomoa
Daaah unajiuliza hivi hawa jamaa wanafikiri kwa kutumia nn?
Hebu angalia upumbavu na akili za kimasikini na Husda
Hii kweli Mkuu?
Mbona watu wana roho mbaya hivi
Hajui waliochimba wamepata thawabu nyingi kwa kuwapa maji wengine
Huku mjinga mwingine anabomoa Daa so sad
 
Nikiambie? Mambo ya siasa yameharibu sana. Mfano kule Kahe wananchi walichangisha pesa nyingi sana. Mamilioni kwaajili ya utengenezaji wa ile barabara hao ya kiwanda cha vumbi. Lakini kwakua alikua mpinzani basi wakakataliwa. Just imagine.

Meanwhile tunakumbuka hata Mengi aliomba apewe uwekezaji sikumbuki ni kitu gani vile akagomewa kisa mswahili mwenzetu. BIla shaka ni gesi. Kwahiyo hatupendani.

Ukute pia kuna ulaji wa watu humo sasa wanaona Waha atawakatia mrija ndo maana wamemkataa.

Waha yuko vizuri sana. Ndiye mmiliki wa Rombo Green view ya hapo shekilango. Rafikiye na Mramba.
Pia huenda kuna mabifu ndani yake pia huwezi jua
 
Asante kwa kuelezea hili
Ni uzembe period
Wewe unajua zaidi sisi tunachangia tu
 
Inasikitisha mno yaani maji yamekuwa ya shida sana hadi kupelekea wakaji wa tarakea kwenda kuchota maji kenya halafu baadae utaskia ooh mama ana upiga mwingi 🤣🤣
Sasa huo si ndio ujirani mwema, Sumbawanga tulipata umeme zambia hata tulitibiwa zambia, mipaka hii ya wakoloni isikufunge akili kupita kiasi Afrika ni moja.
 
Asante kwa kuelezea hili
Ni uzembe period
Wewe unajua zaidi sisi tunachangia tu
Yes. Kuna eneo huko chini Mzee wangu alinunua. Kutokana na shida ya maji yeye amedrill kbs. Huo ukanda walitesekaga sana. Japo kwazee wangu siyo chini kihivyo. Na shamba lake la mdizi ni kubwa kwahiyo mdizi hazipati maji ya kutosha. Alifunga safari ya mbali kbs Asia huko kununua material. Amedrill na anawagawia majirani zake maji bure kbs. Na migomba shamba zima linamwagiliwa. So naona tatizo na wahusika wenyewe.

Niliona kama miaka mitatu hivi kipande cha shimbi wamechimba mifereji na mabomba pembeni lakini sijajua kama wameshafunguliwa maji. Nilisikia kama Rombo chini hivi. Huku ukanda wetu wa juu huwa haunaga chanhamoto za kihivyo za maji. Watu wahimizwe wapande miti zaidi milimano huko. Ubaya wake ni moto unaolipuka mara kwa mara inaharibu sana vyanzo vya maji.

Marangu wenzetu waligomaga kulipia bill za maji. Waliwaambia idara ya maji hawalipi kwasababu maji wamepewa burw na Mungu hivyo hawalipii. Na ukiangalia Marangu na mitaa yote sijui machame, kibosho, etc etc wana vyanzo vingi sana vya maji. Mifereji imepitisha maji mpaka nje kwako. Wengine unakuta hapo nje ana chemchem inapita. Rombo ni Semi Desert. Ukamda wa chini majirani na kenya. Hivyo Serikali itimize wajibu wake tuu
 
Asante sana kwa ufafanuzi wako, kwani na wengine waliochangia wataelewa pia.
Hongera kwa mzee wenu ila ana Baraka zake kwa Mungu pia
Kweli wajibu wa Serikali na pia wahimize upandaji wa miti zaidi
 
Waswahili roho mbaya sana tena ni zaidi ya wachawi
Sasa kuwa mpinzani ndio wanawafanyia hivyo

Tunayasikia sana haya hata marehemu alikuwa hivyo yeye akiona mpinzani anasema sileti maendeleo, kwa kweli alikuwa mtu wa ajabu sana kwa hilo

Na wengine wameendeleza hayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…