Wakenya wanajua kuitumia ardhi kwa manufaa zaidi kuwazidi Watanzania?

Wakenya wanajua kuitumia ardhi kwa manufaa zaidi kuwazidi Watanzania?

Siku chache zilizopita, nilimtembelea mkulima mmoja wa matunda nchini Kenya. Taswira ya shambani kwake ilinipa ujumbe kuwa ni mkulima mwenye mafanikio mazuri.

Japo hana na eneo kubwa sana, analitumia kikamilifu eneo lililopo. Sidhani kama shamba lake lote linazidi ekari tano!

Aliniambia kuwa kwa kawaida, robo ekari humwingizia shilingi milioni moja hela ya Kenya kwa mwaka

Milioni moja ya Kenya ni kama milioni kumi na sita hela ya Tanzania.

Sitilii mashaka maelezo yake, ila najiuliza kama kuna Watanzania wanaopata mafanikio kama hayo kupitia kazi za shamba.

Na kwa kuwa bado sijamsikia Mtanzania mwenye mafanikio kama hayo, nimebaki najiuliza: Wakenya wenye uhaba wa ardhi wanajua namna bora ya kutumia ardhi kwa kilimo chenye tija kuwazidi Watanzania wenye ardhi bwerere?
Tatizo siyo ukubwa wa ardhi, tatizo ni ubora wa AKILI walizonazo hao watu wenye ardhi. Akili yako ikiwa mbovu, hata uwe na ardhi au rasilimali zingine nyingi au kubwa kiasi gani, bado ardhi au rasilimali hizo hazitakusaidia wala hazitakunufaisha.
 
Hiyo yote ni kazi bure kama hamna soko , soko kama ni la uhakika na purchasing power ipo ,hutaona mtu anaambiwa kalime , watu watakimbilia kumiliki ardhi bila kuambiwa wala kushinikizwa na watalima na kuzalisha mara dufu .
Tanzania soko la agricultural products ni bovu , wakulima wanakula loss Tu na sera mbovu za serikali zinazoharibu mfumo wa soko na ukiritimba hata kwenye kusafirisha nje ya nchi ,tumeona kwenye korosho ,mbaazi ,kahawa ,list ni ndefu mno
Mpaka sasa bado sijajua sababu ya Serikali kuingilia soko la kahae na korosho. Kwa nini mkulima asiruhusiwe kuuza mazao yake kwa bei na mahali atakayopenda, hata kama ni Ulaya?
 
Kenya serikali haiingilii soko na kuharibu bei na soko lipo stable + wanafanya export ya mboga ,nyama , matunda ,maua nk ,na mali nyingi hizo wanalangua Tanzania na sera za nchi yao zinaruhusu ,so soko ni la uhakika na sera bora thus ni tofauti na Tanzania
Wao wanawezaje kuipeleka huko kwao kutokea Tanzania lakini Watanzania wanashindwa kuwapelekea wao huko kwao Kenya au kupeleka kwa wateja "wengine" huko dunianai?
 
muda ukiwa sawa hakuna shaka niko dar nimekuja kufanya operation ya cataracs CCBRT jicho linasumbua, ila uwe a shmba, nakaa shamba huko huko
Pole sana mkuu. Ugua pole.

Mimi nayamudu mazingira yote:

1. Kukaa kwenye hoteli ya nyota tano

2. Kulala shambani kwenye banda la majani ambalo mlango wako ni kipande cha gunia

3. Kutumia usafiri wa ndege

4. Kutembea kwa miguu kwa masaa mengi bila kupumzika, hata zaidi ya masaa kumi, ikibidi.

5. Kuvaa kinadhifu

6. Kuvaa ",kishamba", ikibidi, na kutembea peku

7. Kulima muda mrefu kwa jembe la mkono, muhimu tu nisiwe na njaa. Naweza nikakaa shambani Asubuhi hadi Usiku

Kwa kifupi, ninayaweza mambo yote...
 
Mpaka sasa bado sijajua sababu ya Serikali kuingilia soko la kahae na korosho. Kwa nini mkulima asiruhusiwe kuuza mazao yake kwa bei na mahali atakayopenda, hata kama ni Ulaya?
Na ni cash crops zote .
Imagine bei ya kahawa hapo Uganda ni mara mbili ya bei ya Tanzania ,ila mkulima akivuna hawezi ruhusiwa kupakia kwenye fuso aende Kampala kuuza kahawa yake aliyovuna , ni mwiko .
Unakuta wakulima wamedumaa na mfumo wa kipumbavu wa ushirika ambao kwanza malipo ni madogo mno yasiyo endana na hali halisi na yanachelewa sana .
Huwezi kutoboa kwa mwendo huu
 
Wao wanawezaje kuipeleka huko kwao kutokea Tanzania lakini Watanzania wanashindwa kuwapelekea wao huko kwao Kenya au kupeleka kwa wateja "wengine" huko dunianai?
Wakenya wanalangua matunda na mbogamboga wanapeleka kwao kufanya package na kuuza nje ,mkuu kuuza mboga na matunda nje ya nchi sio kwamba unaamka tu na unajiamlia kuna utaratibu maalumu na makubaliano ambayo serikali ya nchi husika lazima ifanye na nchi unayoenda kuuza hizo bidhaa .
Sisi balozi zetu zimelala hazifungui masoko na kuingia mikataba ya kibiashara ya kumnufaisha mkulima directly ,sasa hilo ni tatizo .
Huwezi leo hii ukasema umelima zako Matango ,tikiti , spinach organic fresh kwenye greenhouses zako halafu unataka ukayauze UK bila pre agreement na vibali maalumu , haipo hiyo .Bidhaa yako yenye package na mambo ya Tanzania toka Tanzania haiwezi ingia UK bila makubaliano ya Tanzania na UK na vibali maalumu vya ukaguzi kuhusiana na hiyo bidhaa unayopelekea .
Hii haifanywi na raia ,ni kazi ya serikali kufungua hizi fursa
 
Sidhani kama ni lazima uamini
Ila Mimi nimeamini mkuu! Angalia
1. Ana wafanyakazi anaowalipa kila mwezi. Na hao wafanyakazi wanakula na kunywa kwa gharama za bustani. Kuna wanaoingja Asubuhi na kutoka Jioni na kuna wanaolala shambani kwenye nyumba zilizopo shambani.

2. Huwalipa wataalam kila anapiwaita kwa jambo fulani la kikazi.

3. Kaweka miundombinu ya uhakika.

4. Kuna gari la "maana" mahsusi kwa shughuli za shambani

5. N.k.
 
Wakenya wanalangua matunda na mbogamboga wanapeleka kwao kufanya package na kuuza nje ,mkuu kuuza mboga na matunda nje ya nchi si unaamka tu ,unajiamlia kuna utaratibu na makubaliano ambayo serikali ya nchi husika lazima ifanye na nchi unayoenda kuuza hizo bidhaa .
Sisi balozi zetu zimelala hazifungui masoko na kuingia mikataba ya kibiashara ya kumnufaisha mkulima directly ,sasa hilo ni tatizo .
Huwezi leo hii ukasema umelima zako Matango halafu unataka ukaya uze UK , haipo hiyo .Bidhaa yako yenye package na mambo ya Tanzania toka Tanzania haiwezi ingia UK bila makubaliano ya Tanzania na UK na vibali maalumu vya ukaguzi kuhusiana na hiyo bidhaa unayopelekea .
Hii haifanywi na raia ,ni kazi ya serikali kufungua hizi fursa

Kabisa mkuu,jamaa wameamka na wanachangamkia fursa
 
Wakenya wanalangua matunda na mbogamboga wanapeleka kwao kufanya package na kuuza nje ,mkuu kuuza mboga na matunda nje ya nchi si unaamka tu ,unajiamlia kuna utaratibu na makubaliano ambayo serikali ya nchi husika lazima ifanye na nchi unayoenda kuuza hizo bidhaa .
Sisi balozi zetu zimelala hazifungui masoko na kuingia mikataba ya kibiashara ya kumnufaisha mkulima directly ,sasa hilo ni tatizo .
Huwezi leo hii ukasema umelima zako Matango halafu unataka ukaya uze UK , haipo hiyo .Bidhaa yako yenye package na mambo ya Tanzania toka Tanzania haiwezi ingia UK bila makubaliano ya Tanzania na UK na vibali maalumu vya ukaguzi kuhusiana na hiyo bidhaa unayopelekea .
Hii haifanywi na raia ,ni kazi ya serikali kufungua hizi fursa
Ok! Ok! Nashukuru mkuu!!!

Naona kama wazo linanijia la kwenda kufungua biashara Kenya! Nitaona!!!
 
Back
Top Bottom