Wakili Ishabakaki: Idris Sultan anahojiwa kwa kuicheka picha ya Rais

Wakili Ishabakaki: Idris Sultan anahojiwa kwa kuicheka picha ya Rais

Kavunja kifungu gani cha sheria hiyo?

Kavuka mpaka gani huo wa uhuru?

Mimi naona kama vile nyote mko ktk hali ya kujikana na kutojikubali wenyewe kama mlivyo..!!

Huyo anayeonekana kwenye picha ni mtu anaitwa John Pombe Magufuli....

Suti hiyo aliyovaa ni ya kwake. Wengine watacheka isivyompendeza + pozi lake la Kichato - Chato. Wengine watampigia makofi na kumpongeza...

What's wrong with that?

Itafika wakati mtaanza hata kukimbia vivuli vyenu wenyewe na pengine hata kujaribu kuvipeleka polisi maana mtakuwa mmemkamata kila mtu...!!
Ile ni kama dhihaka mkuu
Huwa tunapinga lkn syo kwa level ile

Ova

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Akajifunze kwanza, anajifanya mwehu, kwa mfano angekuwa mwingine anaicheka na kudhihaki picha ya baba yake yeye, angefurahi?

Yafaa akale Idd El fitr huko kwanza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtoto wangu alicheka nilivyomwonyesha picha yangu fulani ya utotoni, akaniambia baba kumbe ulikuwa mshamba na wewe nikamwambia ndio ujanja nimeupata baada ya kumaliza chuo na kipato changu kuwa kizuri. Sikujua kumbe alikuwa anafanya makosa....maana mi nilichukulia kama mzaha tu! Itabidi nimtafute Mambosasa amuweke cello kwa kunidhalilisha babake.
 
Nchi hii imekuwa sawa na North Korea. Anyway sasa kwa nini wamekaa naye rumande kwa siku 3 bila kumfikisha Mahakamani?
 
sawa lakini huo ujinga wake akafanye kwa billnas ndo saizi yake sio kwa kiongozi wa nchi jamani
Inaelekea unanijibu bila ya kusoma na kuelewa, ubongo wako ndiyo unaoendesha tabia zako na kunaidara nyingine ndani ya ubongo wako unaoweka imaginations.
 
Picha ya rais ni ile inayotolewa rasmi nadhani kupitia idara ya habari,ambayo ndiyo hutumika katika ofisi mbali mbali nchini.



Sent using iphone pro max
 
Hayo unatakiwa kuyafanya ukishabadilisha katiba ya 1977.
Kwa sasa rais anayo nguvu sana na unatakiwa kutumia akili sana. Narudia tena hapa siyo USA. Hii ni Tanzania na katiba yetu mama ni ya mwaka 1977. Kaisome vizuri na utajua madaraka ya Rais yalivyo makubwa.
 
Huyu ni wakumsamehe tu alisquander 500m kwa miezi sita...au Bashite ana beef nae kwa ajili ya Sepenga?
 
Washauri wa Idriss sijui ni akina nani! Ile video tokea nilipoiona nilijua itamletea shida, kwa jinsi picha zile za ‘TBT’ za Rais zilivyoenea mitandaoni huku wengi wakifanya dhihaka haikufaa yeye kujifunga kibwebwe kuchekelea waziwazi.

Kwa hili umelivagaa Idriss, umepatikana...
Ni wazi Rais hakupendezwa na dhihaka zile, utayabeba machungu yake wewe mwenyewe!

Ukiponea hili uache kiherehere cha kurukia mambo, cheap stunts zitakuponza!


Sent from my iPhone using JamiiForums
Sijaona picha yoyote; lakini nashangaa sana hata wewe kuandika uliyoandika hapa.

Ameitemea mate, ameivunjavunja ama kuipaka matope na kuiharibu?

Kuna sheria yoyote inayozuia mtu kucheka? Na kama amecheka kwa kufurahia kuiona picha hiyo, ni kosa?

Halafu mkuu 'Nifah', unashangila kabisa mtu kuwekwa rumande, siku kadhaa, kweli huoni kasoro yoyote hapo?

Ndio, hata mimi sipendezwi rais au hata picha yake idhihakiwe. Kama kahisiwa kufanya kosa/kuvunja sheria, kumweka rumande kama adhabu yake ni kosa pia. Haya ndio tunayotakiwa kuyakataa.

"Dhihaka" ni kufanya nini?

Tunakwenda taratibu sana, lakini najua siku moja tutafika mahali na kushangaa watu walikuwa wanawekwa rumande kwa sababu za "kucheka"?
 
Ile picha inachelesha sana aiseee
Jamaa anaonekana alikuwa mshamba tangu miaka hiyoooo

Magufuli ni changer kwenye kila eneo.

Hatimaye ametokomeza Corona Tanzania nzima

Watanzania tunamhitaji kwa miaka 50 ijayo

Wapinzani wote say yeeeeiiiiyeeeee

Kwa nionavyo mimi kwanza tuangalie hiyo picha ilikuwa ya miaka gani? Je kwa wakati huo style ya mavazi ilikuwa ipi? Uwezi sema alikuwa mshamba kumbe kipindi hicho kuvaa suti kubwa ndo ilikuwa fashion. Mitindo mingi hapa duniani ujirudia. Hata hiv sasa hizi model au suruali zisizo gusa kisigino ilikuwa ni Mitindo ya zamani miaka ya themanini na kitu baada ya buga. Huu mtindo uliitwa "Mdomo wa chupa" wengine waliita "Dont touch" au Dont touch my shoes. So sioni ubaya wa hiyo suti bali tuangalie nyakati na kuona wakati huo ilikuwa ni sawa kwake kuvaa hivyo kama ndo ilikuwa fashion. Hata Idrisa atakuja chwekwa na wajukuu zake Kwa nguo anazovaa sasa na kuona ni model. Uenda wakati ujao itakuwa si fashion. Hivyo tuache kusema Rais wetu alikuwa mshamba. Pia watanzania tumekuwa tunahusudu kila utamaduni wa nje. Ati kwakuwa Marekani au Ulaya wanafanya basi basi tufanye. Nini maana ya utamaduni au mila ktk Taifa? au watu fulani? Usasa si kuiga kila kitu kutoka nje. Utamaduni wetu ni heshima Kwa wakubwa na Uwezi mcheka baba yako waziwazi hata kama kateleza kaanguka. Itabidi uingie chumbani uanze kucheka si kumcheka mbele za watu. Huu ndo utamaduni na mila zetu. Kwanini tuige kila kitu? Alichofanya Huyu mchekeshaji si ubunifu. Ni kumkosea heshima Rais wa nchi. Hii ni namna alivyowasilisha ujumbe wake. Mfano angeongelea Mitindo ya zamani na kuweka picha si mbaya sana. Ila Kwa uwasilishaji huo kunaudhalilishaji na kutokuwa na adabu. Je anaweza kuchukua picha ya baba yake na kuiweka mtandaoni na kuanza mcheka? Nadhani ukoo au wanandugu wangemuita na kumwambia si vizuri. Usasa au maendeleo si kuiga na kuona wafanyavyo Marekani basi nasi tufanye. Huo ni utumwa wa kifikra na pia utumwa wa utamaduni, mila na desturi. Ulaya unaweza kaa na chupi, mzazi mbele ya watoto wako ni kitu cha kawaida je kwa Watanzania tuwe hivyo kisa wazungu wanafanya? Watanzania tumekuwa tunajidharau na kutojiamini ndo maana nchi nyingi wanatudharau. Tunajiona hatufai bali vya wengine ndo vinafaa. Nimebahatika kuishi sehemu mbalimbali duniani Sijawahi ona Taifa wanaojidharau wao wenyewe kama Tanzania. Wanafikiri usasa ni kuiga wazungu wafanyacho. Tuangalie Afrika kusini, Tuangalia Swatini mavazi yao. Lakini wanajikubari. Wanajivunia utamaduni wao. Hata wakati fulani Rais Jacob Zuma aliyatinga. Angalia Ethiopia wana mila zao hawaziachi. Eti Leo wanaharakati wa Tanzania ni kushabikia mtu ambae hana maadili na kutoheshimu mila zetu. Hizo nguvu wanazotumia mitandaoni kwanini wasitumie kuitangaza Tanzania Kwa mema na mazuri na utamaduni wetu. Katika wachekeshaji bora duniani Sijawahi ona uchekeshaji wa namna hii. Huu mtindo ulozuka wa kuonesha dharau na hata udharirishaji kwa kiongozi wa nchi si tamaduni na mila za mtanzania. Wanao fanya hivyo wajaribu kuanza na udharirishaji wa wazazi wao ili waone ndugu au koo watasemaje. Tuwe na uzalendo Kwa nchi yetu na kumheshimu Rais wetu hata kama atukumpigia kura. Au hatumuungi mkono basi tumheshimu. Namalizia kwa kusema Wanao jiona leo wao ni wajanja na wakisasa kesho wataonwa na wao ni washamba na wamepitwa na wakati. Jitafakari wakati huo utaochekwa na watoto wako au wajukuu zako, utawaza nini? Nadhani tunao cheka kwa kebehi na kudharau uenda sisi ndo washamba zaidi. Hatujui nyakati, mitindo, na Pia hatujui mila na desturi zetu za kuheshimu wakubwa. Tunadhani usasa ni kufanya wafanyacho wazungu au mataifa mengine. Kwa hili nami naomba nicheke Ha ha ha ha!
 
JF na vituko vyake, Great Tinkers wameamini maneno yaliyotolewa BBC, Je, Mashitaka ni nini? Je, wameona kilichoandikwa kwenye shitaka? Kama hawajaona basi ni kujadili majungu na propaganda. Nchi haiendelei kwa wale wanaojiona Great Tinkers kujadili majungu na propaganda.
Wewe hujui kitu unaropoka. Wakili alishaongea kuwa ni shitaka la kumdhalilisha rais. Wewe una bisha kitu gani? Uwe na uhakika wa unachosema kabla hujaandika utumbo wako hapa. Hata kama umetumwa na Polepole basi uwe unatumia akili kiidogo.
 
Yaani tunapoteza rasilimali kufuatilia vitu vidogo na vya kipumbavu kabisa wakati kuna mambo muhimu sana ya kufuatilia. Yaani hii inaonyesha ni jinsi gani vyombo vya usalama na hata serikali ilivyo na vipaumbele kwenye mambo ya kijinga na yasio na tija kwenye kulipeleka taifa mbele kiuchumi au hata kiusalama. Wanatumia nguvu nyingi kwenye mambo madogo yanayofaa kupuuzwa.
 
Acheni siasa, ile ni dhihaka na sio vinginevyo. Tupingane na Rais katika mambo ya msingi ila sio kumdhihaki.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Dhihaka ni Nini?
 
Kwa nionavyo mimi kwanza tuangalie hiyo picha ilikuwa ya miaka gani? Je kwa wakati huo style ya mavazi ilikuwa ipi? Uwezi sema alikuwa mshamba kumbe kipindi hicho kuvaa suti kubwa ndo ilikuwa fashion. Mitindo mingi hapa duniani ujirudia. Hata hiv sasa hizi model au suruali zisizo gusa kisigino ilikuwa ni Mitindo ya zamani miaka ya themanini na kitu baada ya buga. Huu mtindo uliitwa "Mdomo wa chupa" wengine waliita "Dont touch" au Dont touch my shoes. So sioni ubaya wa hiyo suti bali tuangalie nyakati na kuona wakati huo ilikuwa ni sawa kwake kuvaa hivyo kama ndo ilikuwa fashion. Hata Idrisa atakuja chwekwa na wajukuu zake Kwa nguo anazovaa sasa na kuona ni model. Uenda wakati ujao itakuwa si fashion. Hivyo tuache kusema Rais wetu alikuwa mshamba. Pia watanzania tumekuwa tunahusudu kila utamaduni wa nje. Ati kwakuwa Marekani au Ulaya wanafanya basi basi tufanye. Nini maana ya utamaduni au mila ktk Taifa? au watu fulani? Usasa si kuiga kila kitu kutoka nje. Utamaduni wetu ni heshima Kwa wakubwa na Uwezi mcheka baba yako waziwazi hata kama kateleza kaanguka. Itabidi uingie chumbani uanze kucheka si kumcheka mbele za watu. Huu ndo utamaduni na mila zetu. Kwanini tuige kila kitu? Alichofanya Huyu mchekeshaji si ubunifu. Ni kumkosea heshima Rais wa nchi. Hii ni namna alivyowasilisha ujumbe wake. Mfano angeongelea Mitindo ya zamani na kuweka picha si mbaya sana. Ila Kwa uwasilishaji huo kunaudhalilishaji na kutokuwa na adabu. Je anaweza kuchukua picha ya baba yake na kuiweka mtandaoni na kuanza mcheka? Nadhani ukoo au wanandugu wangemuita na kumwambia si vizuri. Usasa au maendeleo si kuiga na kuona wafanyavyo Marekani basi nasi tufanye. Huo ni utumwa wa kifikra na pia utumwa wa utamaduni, mila na desturi. Ulaya unaweza kaa na chupi, mzazi mbele ya watoto wako ni kitu cha kawaida je kwa Watanzania tuwe hivyo kisa wazungu wanafanya? Watanzania tumekuwa tunajidharau na kutojiamini ndo maana nchi nyingi wanatudharau. Tunajiona hatufai bali vya wengine ndo vinafaa. Nimebahatika kuishi sehemu mbalimbali duniani Sijawahi ona Taifa wanaojidharau wao wenyewe kama Tanzania. Wanafikiri usasa ni kuiga wazungu wafanyacho. Tuangalie Afrika kusini, Tuangalia Swatini mavazi yao. Lakini wanajikubari. Wanajivunia utamaduni wao. Hata wakati fulani Rais Jacob Zuma aliyatinga. Angalia Ethiopia wana mila zao hawaziachi. Eti Leo wanaharakati wa Tanzania ni kushabikia mtu ambae hana maadili na kutoheshimu mila zetu. Hizo nguvu wanazotumia mitandaoni kwanini wasitumie kuitangaza Tanzania Kwa mema na mazuri na utamaduni wetu. Katika wachekeshaji bora duniani Sijawahi ona uchekeshaji wa namna hii. Huu mtindo ulozuka wa kuonesha dharau na hata udharirishaji kwa kiongozi wa nchi si tamaduni na mila za mtanzania. Wanao fanya hivyo wajaribu kuanza na udharirishaji wa wazazi wao ili waone ndugu au koo watasemaje. Tuwe na uzalendo Kwa nchi yetu na kumheshimu Rais wetu hata kama atukumpigia kura. Au hatumuungi mkono basi tumheshimu. Namalizia kwa kusema Wanao jiona leo wao ni wajanja na wakisasa kesho wataonwa na wao ni washamba na wamepitwa na wakati. Jitafakari wakati huo utaochekwa na watoto wako au wajukuu zako, utawaza nini? Nadhani tunao cheka kwa kebehi na kudharau uenda sisi ndo washamba zaidi. Hatujui nyakati, mitindo, na Pia hatujui mila na desturi zetu za kuheshimu wakubwa. Tunadhani usasa ni kufanya wafanyacho wazungu au mataifa mengine. Kwa hili nami naomba nicheke Ha ha ha ha!
I ddnt see this long shit coming
 
Hivi ni mimi tu sijaona hiyo video ya idriss au tuko wengi?

Yani sielewi chochote acha tu nisome comments sina namna.
 
Inaelekea unanijibu bila ya kusoma na kuelewa, ubongo wako ndiyo unaoendesha tabia zako na kunaidara nyingine ndani ya ubongo wako unaoweka imaginations.
nimekuelewa, hoja yangu ni kwamba huo ubongo wake unaoendesha tabia zake unaona wa kumfanyia hizo komedi ni rais tu maana hii ni mara ya pili anapata shida kwa makosa yanayofanana.
 
Back
Top Bottom