Hapana mkuu, swala la kesi ya kujibu lilishaamriwa mwanzoni kabisa baada ya rufaa ya Mbowe akipinga kuwa mahakama hii sio sahihi kusikiliza kesi hii na kuwa hati ya mashitaka ilikuwa na makosa. Kama upande wa mashitaka umesikilizwa na hautaondoa kesi, basi upande wa utetezi utasikilizwa pia. Swala la kuwa na kesi ya kujibu ni la DPP na hatua hii imevukwa - Sasa ni DPP kufuta kesi au wahitakiwa kukutwa au kutokutwa na hatia.Uwezekano mkubwa watakuwa hawana kesi ya kujibu baada ya Jamhuri kumaliza ushahidi.
Mbona unauliza maswali ya kijinga au ndio na wewe unataka kuwaburudisha wenzako humu kwa kumuiga Kibatala? Lissu keshatiwa ulemavu na nyie wafuasi wake(wanafki) hamkurusha hata jiwe ajabu mnafurahia kufa kwa Jiwe yani hicho ndio mlichoweza kufanya.Kama kila mtu atakufa kwanini mlimpiga risasi 30?
Si mngeshauriana kwamba tusimpige risasi kwakuwa kila mtu atakufa
Aseee! Hata hivyo uachwe ulivyo!Mbona unauliza maswali ya kijinga au ndio na wewe unataka kuwaburudisha wenzako humu kwa kumuiga Kibatala? Lissu keshatiwa ulemavu na nyie wafuasi wake(wanafki) hamkurusha hata jiwe ajabu mnafurahia kufa kwa Jiwe yani hicho ndio mlichoweza kufanya.
Jiwe sasa hayupo ila mambo yanaendelea kama kawaida Mbowe kapewa kesi ya ugaidi ila nyie wafuasi(wanafki) mnanyokifanya ni kuburudika na maswali ya Kibatala mwenzenu anakonda mule na wakiamua wanamfunga na hayo maswali ya Kibatala hayatokuwa na msaada wowote na burudani yenu itaishia hapo.
Unapotosha! Hatua ya kukutwa na kesi ya kuh=jibu aua hapana haijafikiwa!Hapana mkuu, swala la kesi ya kujibu lilishaamriwa mwanzoni kabisa baada ya rufaa ya Mbowe akipinga kuwa mahakama hii sio sahihi kusikiliza kesi hii na kuwa hati ya mashitaka ilikuwa na makosa. Kama upande wa mashitaka umesikilizwa na hautaondoa kesi, basi upande wa utetezi utasikilizwa pia. Swala la kuwa na kesi ya kujibu ni la DPP na hatua hii imevukwa - Sasa ni DPP kufuta kesi au wahitakiwa kukutwa au kutokutwa na hatia.
Unaamini Mbowe ana makosa?We endelea kushabikia umbeya wa kiasiasa maana si ndio mnaloliweza. Hilo la Lissu ni la awamu ya Magufuli na awamu hii imeanza na Mbowe na safari ndio kwanza imeanza.
Tuendelee kuburudishwa na Kibatala.
Muhimu ni kuburudika tu maswali ya Kibatala, hayo ya kwamba ana makosa au hana hakuna tofauti.Unaamini Mbowe ana makosa?
Aseee - umepania mtu afungwe! Na je asipofungwa itakuwaje?Muhimu ni kuburudika tu maswali ya Kibatala, hayo ya kwamba ana makosa au hana hakuna tofauti.
Kwa sababu hata akifungwa na hali hana makosa unadhani kuna chochote kitatokea?
Roho mbaya sana maana aliona kuwa Rais hakujamtosha akatamani awe IGP.Mwingine alisema "i wish i could be igp"
Itakuwa wenyewe wameamua tu wasimfunge na si kwamba watanzania wamefanya lolote au maswali ya Kibatala yamezuia wasimfunge, hivyo ni suala la wenyewe tu kuamua sie tuendelee kuburudishwa na Kibatala hiyo ndio nafasi yetu kwenye hii kesi au mchango wetu.Aseee - umepania mtu afungwe! Na je asipofungwa itakuwaje?
Hii picha inaonekana ilishapangwa tangu jana au asubuhi, kwa sababu alianza na hoja ya kutojisikia vizuri, akasema ataendelea "hivyo hivyo"
AMRI ya Mahakama kumtafuta POPOTE shemeji yako Bashite ni umbeya? UVCCM hebu jaribu kuwa serious kidogo basi.We endelea kushabikia umbeya wa kiasiasa maana si ndio mnaloliweza. Hilo la Lissu ni la awamu ya Magufuli na awamu hii imeanza na Mbowe na safari ndio kwanza imeanza.
Tuendelee kuburudishwa na Kibatala.
Mlemavu lakini anakula ugali na kudunda. yuko wapi aliyemtia ulemavu,amegeuka ugali na funzaLissu keshatiwa ulemavu na nyie wafuasi wake(wanafki) hamkurusha hata jiwe
Wengi walikuulizai kama unavyosema watu watafute suluhisho ili atoke. Hebu jibu kama unavyoulizwa.Hii kesi ya Mbowe ni matokeo tu tatizo lililopo siku nyingi na mengi yashatokea, point si kutoka Mbowe tu bali hili tukio la Mbowe haliwafikirishi ndio kwanza mnafurahia maswali ya Kibatala na mtu anakuuliza sasa ulitaka tufanyaje? Yani ni wazi hii kesi ya Mbowe bado nayo haijawagusa kiasi kufikia kuona hii sasa basi yatosha.
Tuendelee kuburudishwa na Kibatala.
Hebu soma yote kwa ufahamu kwa kila anaekukoti kabla ya kujibu.Mimi nalitazama hili suala kwa fikra za kwamba tulipofika sio kuzuri ila bado watu hawajazinduka ndio kwanza wanafurahia maswali ya Kibata.
Yani unaona kabisa kwamba hili nalo litapita kama yalivyopita mengine.
Yeah ni umbeya.AMRI ya Mahakama kumtafuta POPOTE shemeji yako Bashite ni umbeya? UVCCM hebu jaribu kuwa serious kidogo basi.
Wewe unajadili matatizo yanayowakumba wapinzani,nchi, au kesi ya kubumba aliyoshizingiziwa mbowe?Yeye kutoka sio suluhisho, hii kesi ni mfululizo tu wa matatizo tuliyonayo na Mbowe sio wa kwanza kupewa kesi za aina hiyo.
Hivyo Mbowe kutoka sio suluhisho la tatizo tulilonalo.
Ni kwa sababu hamjaelewa ninachokikusudia mkuu, mimi sipo hapa kupiga umbeya wa kisiasa hayo nawachia nyie.Hebu soma yote kwa ufahamu kwa kila anaekukoti kabla ya kujibu.
Unachokotiwa na unachojibu ni vitu viwili tofauti ndugu.
Mimi nataka muyatafakari hayo matatizo ya aina zote iwe ya nchi,wapinzani au kesi za kubambikiwa kwa yeyote yule maana haijaanza kwa Mbowe tu.Wewe unajadili matatizo yanayowakumba wapinzani,nchi, au kesi ya kubumba aliyoshizingiziwa mbowe?
Basi kwafaida ya wote hicho unachokikusudia kieleze au unaogopa kueleza?Ni kwa sababu hamjaelewa ninachokikusudia mkuu, mimi sipo hapa kupiga umbeya wa kisiasa hayo nawachia nyie.
Mkuu unaelewa kwamba point yangu si kutoka kwa Mbowe tu maana nimesema kwamba Mbowe si mtanzania wa kwanza kupewa kesi kama hiyo na hali ilivyo anaweza asiwe wa mwisho pia kupewa kesi za aina hiyo.Wengi walikuulizai kama unavyosema watu watafute suluhisho ili atoke. Hebu jibu kama unavyoulizwa.
Watu hawafurahii jinsi kibatala anaavyouliza maswali kinachoshangaza ni kwamba walliofungua kesi na mashahidi ni hawo hawo lakni huwo ushahidi wanaoutoa hauendani na hoja zilizopo mahakamani ndio ukaona mashahidi wote wanapuyanga kytokana na ushahidi wanaoutoa wakimaliza kujibu waliyomezeshwa yaliyobakia ni sifahamu n.k..
Swali kama mdau unaechukia mbowe kufungwa hebu lete njia mbadala watu watumie ambayo anaweza kutoka bila ya shida yoyote.