Wakili Kibatala anajua sana alifanyalo. Ni lazima akuchanganye tu

Wakili Kibatala anajua sana alifanyalo. Ni lazima akuchanganye tu

mtoa mada nafikiri hujui kitu kuhusu sheria kibatala ni kama mwanamke wa kizaramo huwezi kumshinda kwa kushindana naye kuongea lakini kinachotakiwa pale ni point za shahidi kueleweka tu hayo maswali ya kumchanganya hayana point yoyote chamuhimu kimeshapatikana maelezo ya shaghidi yaliyobaki ni kama yale tunaitaga mazungumzo baada ya habari yaani anapoteza muda tu mbowe tayari yuko kitanzini hata kibatala anajuwa lakini anajifanya kupoteza muda wa watu tu hana kitu kibatala kama mwanamke wa kizaramo tantalila nyingiiiii lakini hakuna point za maana
Another street lawyer🤣🤣
 
Sasa wewe mtu mzima tena afisa mkubwa wa Police 👮 yakimtokea hayo urafurahi.
Tatizo kweny maswali hata ukipewa desa...

Kweny cross examination hakuna kuingia na majawabu ya kumezeshwa lazima utatolewa know out....sema ma afande wanakubali kwasababu ya kulinda Ugali wao
 
Siku ingine tena ya kumsikiliza Wakili Msomi Kibalata akileta madude yake!
 
Hii ni project ya muda mrefu aliyoifanya Mbowe kurecruit vijana wasomi akianza na lissu km mentor wa Hawa kina kibatala naona wanazidi kuongezeka kina nashon nkungu,dickson matata etc wanavutia kuwasikiliza hd unatamani kuwasomesha wanao law
Na siku zote ukitaka kuonyesha kipaji chako cheza timu pinzani
 
Hii ni mbinu sahihi kabisa na imefanywa makusudi kwa sababu hizi;
1. Urio ndio alikuwa mtoa habari mkuu wa kesi nzima.
2. Mkaguzi Swila ndiye aliyekuwa mpelelezi wa kesi hii. Yeye ndio aliyefungua kesi, kupewa maelekezo na Kinga, kuomba vyombo vya uchunguzi kufanya kazi zake na hata kumhoji mtoa taarifa na hata kuandika maelezo ya Kingai.

Baada ya watu hawa, kesi itakwenda haraka sana ili utetezi nao ulete mashahidi wao. Ninahofia kuwa kutakuwa na mashahidi wa utetezi wengi waliohusishwa na Kaaya, Urio na kesi ya ugaidi kuliko Mbowe. Nina dhana kuwa uchunguzi dhidi ya makomandoo inatokana na zile mambo za Kibiti - Mbowe aliingizwa tu baada ya kuona amewasiliana na Urio ambaye alikuwa na kazi ya kuchoma makomandoo wote wasio kazini!!
OK, ni kama nimekusoma hivi.

Na kwavile makomandoo wenyewe wana majina ya dini yetu ya Ijumaa! Hapa hakuna kesi isipokuwa kutaka kuvurugiana maisha na kupotezeana muda tu.
 
Sio kwa sasa tu hamjawahi kuwa na la kufanya, Lissu yule pale katiwa kilema kuna ambalo mlifanya? Ila kama ulivyosema tuendelee kufurahia maswali ya Kibatala na huyo Mbowe muache aendelee kukonda sasa akihukumiwa kabisa sijui itakuaje.
Shemeji yako Bashite siku atakapojitokeza Mahakamani tu, suala la Lissu litaanzia hapo pia. Unadhani ni kwanini yuko MAFICHONI? Time will tell..
 
Mimi nilitaka wamfikirie mwenzao kule anakonda na wafikirie ni jinsi gani ya kupata suluhisho la kuondokana na haya manyanyaso yote haya ila ajabu ndio kwanza wanafurahia maswali ya Kibatala.
Hata kama hawana la kufanya ila ndio wafurahie maswali ya Kibatala wakati mwenzao hadi sasa keshakonda na wakiamua wanaweza kumfunga na hayo maswali ya Kibatala ndio yatakuwa na msaada upi sasa?

Kule utakonda ww mzee wao wanapelekewa msosi mzr kila siku
 
Huyu bwana stahili yake ni kukuhoji kwa muda mrefu sana. Yaani kielelezo kimoja kinaweza kwake kikawa na maswali Zaidi ya 25. Ana utaratibu wa kuhoji mpaka kufikia muda wa kuhairisha ili siku inayofuata aje na nguvu mpya na mawazo mapya. Amekuwa sana na utaratibu huo ambao kwa kweli umekuwa ukiwachanganya sana mashahidi.
Mwenye picha ya insp swila atuwekee hapa tafadhari, maana tunahitaji kuona hadi sura yake.
 
Huyu bwana stahili yake ni kukuhoji kwa muda mrefu sana. Yaani kielelezo kimoja kinaweza kwake kikawa na maswali Zaidi ya 25. Ana utaratibu wa kuhoji mpaka kufikia muda wa kuhairisha ili siku inayofuata aje na nguvu mpya na mawazo mapya. Amekuwa sana na utaratibu huo ambao kwa kweli umekuwa ukiwachanganya sana mashahidi.

Shahidi wa leo Swila ambaye leo ilikuwa siku yake ya tatu kuhojiwa tayari ameshachoka sana kwani hakumbuki tena aliyoyaongea juzi wakati akihojiwa na mawakili wengine, leo amekuja tayari kishasahau kila kitu utafikiri hakufanya rehearsal, hii ni ajabu sana.

Baada ya kuona leo anazidi kulemewa ilibidi Wakili wa Serikali anayeongoza jopo lao amsogelee na kumwelekeza amwombe Jaji kuhairisha kwa ajili ya tatizo la kiafya - Shahidi mwenyewe inaonesha alikuwa ana uwezo wa kuendela lakini wakili wake kaamua kuingilia kati ili wakampe nafasi ya kujipanga upya kutokana na namna ambavyo ameshavurunga!

Kibata Mwenyezi Mungu azidi kukubariki sana. Hukumu ya Mahakama ikitofautiana na umma tunavyoona basi Jaji huyu atakuwa na roho ngumu sana.

Anyway Acha Ibaki Hivyo!
Asingeambiwa aumwe, jana angeharibu kesi
 
Huyu bwana stahili yake ni kukuhoji kwa muda mrefu sana. Yaani kielelezo kimoja kinaweza kwake kikawa na maswali Zaidi ya 25. Ana utaratibu wa kuhoji mpaka kufikia muda wa kuhairisha ili siku inayofuata aje na nguvu mpya na mawazo mapya. Amekuwa sana na utaratibu huo ambao kwa kweli umekuwa ukiwachanganya sana mashahidi.

Shahidi wa leo Swila ambaye leo ilikuwa siku yake ya tatu kuhojiwa tayari ameshachoka sana kwani hakumbuki tena aliyoyaongea juzi wakati akihojiwa na mawakili wengine, leo amekuja tayari kishasahau kila kitu utafikiri hakufanya rehearsal, hii ni ajabu sana.

Baada ya kuona leo anazidi kulemewa ilibidi Wakili wa Serikali anayeongoza jopo lao amsogelee na kumwelekeza amwombe Jaji kuhairisha kwa ajili ya tatizo la kiafya - Shahidi mwenyewe inaonesha alikuwa ana uwezo wa kuendela lakini wakili wake kaamua kuingilia kati ili wakampe nafasi ya kujipanga upya kutokana na namna ambavyo ameshavurunga!

Kibata Mwenyezi Mungu azidi kukubariki sana. Hukumu ya Mahakama ikitofautiana na umma tunavyoona basi Jaji huyu atakuwa na roho ngumu sana.

Anyway Acha Ibaki Hivyo!
Nyi chadema acheni kujipa moyo mwenyekiti anateseka kule ndani fanyeni namna muliuaminisha umma muna wanachama milioni 8, Zitto alipomuombea kwa mama mkaja juu wakati mbowe mwenyewe alibariki Zitto kumuombea msamaha kwa mama.,

Wewe una mu-enjoy kibatala wakati siku zinakatika mwenyekiti Taifa yuko jela na kesi muiitayo ya kubambika? Mnasubiri clips za tundu lissu online akihojiana na mariam sarungi ndio muendeshe siasa, it is good for nothing
 
Kule utakonda ww mzee wao wanapelekewa msosi mzr kila siku
Mkuu umemuona Mbowe alivyo sasa hivi? Kule sio pazuri we shukuru upo uraiani unaburudishwa na Kibatala ila unadhani Mbowe anaburudika na maswali ya Kibatala kule?
 
Shemeji yako Bashite siku atakapojitokeza Mahakamani tu, suala la Lissu litaanzia hapo pia. Unadhani ni kwanini yuko MAFICHONI? Time will tell..
We endelea kushabikia umbeya wa kiasiasa maana si ndio mnaloliweza. Hilo la Lissu ni la awamu ya Magufuli na awamu hii imeanza na Mbowe na safari ndio kwanza imeanza.

Tuendelee kuburudishwa na Kibatala.
 
Back
Top Bottom