Wakili Mwambukusi huenda akashidwa kwenye kura uchaguzi wa TLS

Wakili Mwambukusi huenda akashidwa kwenye kura uchaguzi wa TLS

Ila kama hawa ni wengi si ndio Demokrasia yenyewe ? Au wameshawishiwa kwa Mlungula and if that is the case hata Taasisi yenyewe itakuwa haina legitimacy....
Walivyokata jina lake tu kwenye hukumu ya mahaka jaji kahoji hivi nyinyi TLS mnajitambua kweli?
 
Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kinarajia kufanya uchaguzi wake mkuu hivi karibuni Jijini Dodoma kumchagua rais wa kuongoza chama hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja

Wagombea halaii waliopitishwa kupigiwa kura kwenye nafsi hiyo ni sita kati ya hao Wakili machachari Boniface Mwambukusi ni mmoja wao

Habari za uhakika zinaonyesha kuwa kuna kapeni kubwa ndani na nje ya chama hicho ili Mwambukusi ashindwe kwenye boksi la kura kwenye uchaguzi huo

Lengo ni kuhakikisha kuwa wakili huyo msomi, machachari na mwenye msimamo mkali usiyoyumba kwa Serikali hashindi kwenye uchaguzi huo na kuingoza taasisi hiyo huru ya wanasheria nchini

Ikumbukwe kuwa awali wakili Mwambukusi alienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo lakini alikwenda kufungua kesi mahakama kuu kupinga kuenguliwa kwake kugombea urais wa chama hicho

Katika kesi hiyo Mwambukusi alifanikiwa kushinda na mahakama kuamuru arejeshwe kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais wa TLS

Mmoja wa mawakili ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa mawakili wengi wamejipanga kuhakikisha kuwa Mwambukusi hashindi kwenye uchaguzi huo

Inadai kwamba baada ya Mwambukusi kushinda kesi yake ya kuenguliwa kugombea uongozi TLS alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini

Comasava

Mbona unahaha sana ndugu Boi Manda?

Kwani cha ajabu ninini hata ikitokea ameshindwa?

Si ndiyo maana ya uchaguzi kwamba kuna options nyingi za kuchagua?

Mimi nafikiri, lililo muhimu kwa sasa ni kuhakikisha kuwa mchakato wote wa uchaguzi (kuanzia uteuzi wa wagombea, kampeni, upigaji kura, uhesabuji kura na kutangazwa kwa matokeo) lazima uwe FAIR and JUST ili kila mgombea ashinde au ashindwe kwa haki kwa maamuzi ya wapiga kura wenyewe.

Na kama transparency itatawala ktk uchaguzi huu, mimi sijaona mgombea mwingine miongoni mwa watano ambaye aggresive and vibrant kupambana na utawala huu wa kihuni chini ya CCM anayeweza kumshinda Mwabukusi.

Hawa wengine wote watano ukiwasikiliza na kuwatazama usoni wanapokuwa wanaongea unaona waziwazi kuwa wananunulika na wanaweza kuiuza TLS kirahisi tu kwa tamaa ya fedha. Lakini si Boniface Mwabukusi ambaye yeye si kwa kusema mdomoni tu bali amethibitisha hili kwa vitendo!

Na mimi nikuhakikishie jambo moja ndugu Boi Manda figisu figisu anazopitia na kufanyiwa Wakili Boniface Mwabukusi kwa sababu ya misimamo yake mikali dhidi ya wahalifu wa sheria na katiba, ni za kitoto sana ukilinganisha na alizopitia na kufanyiwa Tundu Lissu mwaka 2017 na bado alishinda uchaguzi huo kwa kishindo..!!

Wao watumie kila aina ya silaha walizonazo kuzuia ushindi wake. Wachote na kumwaga pesa zote kwa mawakili. Jambo moja ni hili, tutachukua na kuzitumia fedha hizo lakini, yet kura zote ni kwa Boniface Mwabukusi!!

Take it or throw it , but always remember this, that, Adv. Boniface Mwabukusi iwe jua au mvua ndiye Rais wa TLS kwa miaka mitatu ijayo 2024 - 2026. Cha kumzuia Boniface Mwabukusi kushinda uchaguzi huu ni kifo pekee ambacho Mungu hajakiruhusu kwa sasa!!

TLS inahitaji kichwa ambacho ni vibrant and aggressive cha mtu kama Adv. Boniface Mwabukusi ktk kupambana na hayawani wa CCM waliozoea kuvunja sheria na katiba ya nchi bila hatua kuchukuliwa dhidi yao!
 
Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kinarajia kufanya uchaguzi wake mkuu hivi karibuni Jijini Dodoma kumchagua rais wa kuongoza chama hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja

Wagombea halaii waliopitishwa kupigiwa kura kwenye nafsi hiyo ni sita kati ya hao Wakili machachari Boniface Mwambukusi ni mmoja wao

Habari za uhakika zinaonyesha kuwa kuna kapeni kubwa ndani na nje ya chama hicho ili Mwambukusi ashindwe kwenye boksi la kura kwenye uchaguzi huo

Lengo ni kuhakikisha kuwa wakili huyo msomi, machachari na mwenye msimamo mkali usiyoyumba kwa Serikali hashindi kwenye uchaguzi huo na kuingoza taasisi hiyo huru ya wanasheria nchini

Ikumbukwe kuwa awali wakili Mwambukusi alienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo lakini alikwenda kufungua kesi mahakama kuu kupinga kuenguliwa kwake kugombea urais wa chama hicho

Katika kesi hiyo Mwambukusi alifanikiwa kushinda na mahakama kuamuru arejeshwe kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais wa TLS

Mmoja wa mawakili ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa mawakili wengi wamejipanga kuhakikisha kuwa Mwambukusi hashindi kwenye uchaguzi huo

Inadai kwamba baada ya Mwambukusi kushinda kesi yake ya kuenguliwa kugombea uongozi TLS alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini

Comasava
Kushindwa kihalali siyo kosa wala dhambi.
 
Nimeangalia mdahalo wote leo Star TV, wagombea wote wa TLS kila mmoja ni kichwa na ana kitu kizito, wazo langu kwanza wagombea hawa waunde group la whatsapp kisha wachague m/kiti na katibu wanaobaki wawe wajumbe, uchaguzi wao ukiisha waungane upya watafute funds na kuanza kazi ya kupambana kusaka katiba Mpya na kubadili vigezo vya kuwa mbunge angalau awe graduate na waziri asiwe mbunge kuondoa mgongano wa maslahi.

Waangalie namna gani watatumia sheria tulizonazo kudai katiba mpya kwa nguvu kwa kutumia kitu inaitwa social contract theory.
Siyo tu wao kuna mawakili wengi zaidi ni vichwa ukielewa dhana ya demokrasia na uwajibikaji utaelewa kwanini watu wanataka katiba mpya na utawala bora. Huhitaji kufungua Whatsapp group kuchagua watu wakati kuna utaratibu wa kidemokrasia wa kupiga kura.
 
Back
Top Bottom