Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kinarajia kufanya uchaguzi wake mkuu hivi karibuni Jijini Dodoma kumchagua rais wa kuongoza chama hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja
Wagombea halaii waliopitishwa kupigiwa kura kwenye nafsi hiyo ni sita kati ya hao Wakili machachari Boniface Mwambukusi ni mmoja wao
Habari za uhakika zinaonyesha kuwa kuna kapeni kubwa ndani na nje ya chama hicho ili Mwambukusi ashindwe kwenye boksi la kura kwenye uchaguzi huo
Lengo ni kuhakikisha kuwa wakili huyo msomi, machachari na mwenye msimamo mkali usiyoyumba kwa Serikali hashindi kwenye uchaguzi huo na kuingoza taasisi hiyo huru ya wanasheria nchini
Ikumbukwe kuwa awali wakili Mwambukusi alienguliwa na kamati ya uchaguzi ya TLS kugombea nafasi hiyo lakini alikwenda kufungua kesi mahakama kuu kupinga kuenguliwa kwake kugombea urais wa chama hicho
Katika kesi hiyo Mwambukusi alifanikiwa kushinda na mahakama kuamuru arejeshwe kuwa mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais wa TLS
Mmoja wa mawakili ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa mawakili wengi wamejipanga kuhakikisha kuwa Mwambukusi hashindi kwenye uchaguzi huo
Inadai kwamba baada ya Mwambukusi kushinda kesi yake ya kuenguliwa kugombea uongozi TLS alikuwa akitoa maneno na kauli za kukiponda chama hicho kuwa hakijitambui na kimeshindwa kutimiza na kusimamia majukumu yake ya msingi na muhimu ambayo ni kuwatetea wananchi na kupinga uonevu na ukandamizaji nchini
Comasava
Mbona unahaha sana ndugu
Boi Manda?
Kwani cha ajabu ninini hata ikitokea ameshindwa?
Si ndiyo maana ya uchaguzi kwamba kuna options nyingi za kuchagua?
Mimi nafikiri, lililo muhimu kwa sasa ni kuhakikisha kuwa mchakato wote wa uchaguzi (kuanzia uteuzi wa wagombea, kampeni, upigaji kura, uhesabuji kura na kutangazwa kwa matokeo) lazima uwe FAIR and JUST ili kila mgombea ashinde au ashindwe kwa haki kwa maamuzi ya wapiga kura wenyewe.
Na kama transparency itatawala ktk uchaguzi huu, mimi sijaona mgombea mwingine miongoni mwa watano ambaye aggresive and vibrant kupambana na utawala huu wa kihuni chini ya CCM anayeweza kumshinda Mwabukusi.
Hawa wengine wote watano ukiwasikiliza na kuwatazama usoni wanapokuwa wanaongea unaona waziwazi kuwa wananunulika na wanaweza kuiuza TLS kirahisi tu kwa tamaa ya fedha. Lakini si Boniface Mwabukusi ambaye yeye si kwa kusema mdomoni tu bali amethibitisha hili kwa vitendo!
Na mimi nikuhakikishie jambo moja ndugu
Boi Manda figisu figisu anazopitia na kufanyiwa Wakili Boniface Mwabukusi kwa sababu ya misimamo yake mikali dhidi ya wahalifu wa sheria na katiba, ni za kitoto sana ukilinganisha na alizopitia na kufanyiwa Tundu Lissu mwaka 2017 na bado alishinda uchaguzi huo kwa kishindo..!!
Wao watumie kila aina ya silaha walizonazo kuzuia ushindi wake. Wachote na kumwaga pesa zote kwa mawakili. Jambo moja ni hili, tutachukua na kuzitumia fedha hizo lakini, yet kura zote ni kwa Boniface Mwabukusi!!
Take it or throw it , but always remember this, that, Adv. Boniface Mwabukusi iwe jua au mvua ndiye Rais wa TLS kwa miaka mitatu ijayo 2024 - 2026. Cha kumzuia Boniface Mwabukusi kushinda uchaguzi huu ni kifo pekee ambacho Mungu hajakiruhusu kwa sasa!!
TLS inahitaji kichwa ambacho ni vibrant and aggressive cha mtu kama Adv. Boniface Mwabukusi ktk kupambana na hayawani wa CCM waliozoea kuvunja sheria na katiba ya nchi bila hatua kuchukuliwa dhidi yao!