Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huwezi kumsaliti Mwamba Mbowe na Karma ikakuacha salama Babu anyongwe tu hakuna namnaMama akilisamehe lile dokta uchwara sisi tutaandamana hadi ikulu kuomba lirudishwe tena ndani.
Lile ndo limewashawishi na kuwalaghai wenzake kwamba wakifanya mapinduzi na kuwa raisi litamteuwa mwabukusi kuwa jaji mkuu wa Tanzania na mdude atapewa cheo cha kusimamia askari magereza ili alipe kisasi kwa waliompa kipondo jela enzi za Magufuli.
C muwapeleke mahakamani?Watake kumpindua Rais afu wanamuomba rais huyo huyo kuingilia kati? Wonders shall never seize. Wanajikaanga kwa mafuta yao.
C muwapeleke mahakamani?
Hajasema awape msamaha, amesema wapelekwe mahakamani.
Siamini hata wewe umekua mtu wa hovyo? Ama kweli. Utakua ndugu ktk imani si bure.Ngoja wajikaange kwa mafuta yao wenyewe hadi waive. Huu mchezo hauhitaji makasiriko.
Siamini hata wewe umekua mtu wa hovyo? Ama kweli. Utakua ndugu ktk imani si bure.
Good. Ndicho alichomaanisha wakili. Lakini wale wa akili ya kawaida hawawezi kuling'amua fumbo hili.Tafsiri rahisi hapa ni Raisi anafahamu kila kinachoendelea na yote yana baraka zake.
Itamsumbua Raisi au hao walioshitakiwa?Zigo bado linaendelea kumwangukia Rais.
Hii kesi itamsumbua sana
Tuwaachie majaji wataamua.Wewe na wenzio ndio mmechanganyikiwa hamjui hata elements za treason na coup ni zipi kisheria, kimantiki, kimtazamo na kiuhalisia.
Kwa viongozi wanaoingia madarakani kwa kupora chaguzi za nchi, hata wakipinduliwa ni sahihi.Ni heri wafe na njaa make hawana maana, rais anajitoa kuleta maendeleo wao kutwa nzima kuhamasisha mapinduzi.
Muhimili gani? Polisi si muhimili kama unavyodhani.Unataka Rais aingilie muhimili mwingine? SSH anajua mipaka yake.
Majaji wapi, hawa wanaopigiwa simu moja tu?
Nani kaomba Mwakilima au Mwabukusu
Wakili wa Wakili Boniface Mwabukusi na Mwanachama wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mpaluka Nyagali maarufu kwa jina la Mdude Nyagali wanao shikiliwa na jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa tuhuma za Uhaini, amemuomba Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuingilia kati suala la watuhumiwa hao Ili waweze kupelekwa mahakamani na haki iweze kutendeka.
Akizungumza na waandishi wa habari Wakili Philip Mwakilima amesema bado kumekua na vikwazo kwa watuhumiwa Balozi Dkt Wilbroad Slaa, Wakili Boniface Mwabukusi na Mdude Nyagali, kufikishwa mahakamani licha ya kukaa zaidi ya siku tano mahabusu tangu walipokamatwa mwishoni mwa wiki iliyopita.
Pamaoja na hayo Wakili Mwakilima amemuomba Rais Dkt Samia kuingilia kati kwa kutoa amri ya watu hao kufikishwa katika vyombo vya utoaji haki Ili waweze kutoa hakiyao ikiwemo ya matibabu kutokana na wateja wao kua na maradhi mbalimbali.
Ni kwa sababu rais Dkt Samia siyo tabia yake kubambika watu kesi, yaani hapo kuna watu anawavutia kasi ataruka nao very soon.Watake kumpindua Rais afu wanamuomba rais huyo huyo kuingilia kati? Wonders shall never seize. Wanajikaanga kwa mafuta yao.
Hilo ndio tatizo lenu kuu basi tumweke kibatala akaamue au una maoni gani?Majaji wapi, hawa wanaopigiwa simu moja tu?
Tunafahamu mfumo wetu wa haki ulivyo, na nini huwa kinaendelea nyuma ya pazia. Ukiona mtu ana imani na mfumo wetu wa kutoa haki, huyo ujue ni mfaidika wa huo mfumo, au hajui lolote. Ndio maana wawekezaji hawako tayari mashauri yao kupeleka kwenye hizi mahakama zetu.Hilo ndio tatizo lenu kuu basi tumweke kibatala akaamue au una maoni gani?
😀Wakili keshaona hii ngoma ni ngumu njia nzuri ni kuchutama tu.