Binafsi nimekuzwa na kulelewa na mzazi mmoja ambaye ni mama, sijawahi pata hata mapenzi ya baba nilipokuwa mwana.
Kulea mtoto binafsi bila msaada wowote ilikua ngumu sana kwa mzazi wangu lakini alijifunga shuka kiunoni na kutosalimu amri ya uvivu.
Kwakweli malezi ya mzazi mmoja pekee yana changamoto nyingi sana kwani kila jukumu la mtoto linasimamiwa na mzazi huyo huyo tu haswa haswa wakati ambapo mzazi huyo hana uwezo wa kumlea mwana huyo.
View attachment 1340537
Mara nyingi huenda mzazi huyo akakumbwa na huzuni ambayo inaeza mwathiri mtoto wake kisaikologia. watoto huwa na tabia ya kufanya na kutii wanachokiona. Basi tabia ya mzazi inaeza mdhuru mwanawe.
Kwa sana mzazi yule anaenda kutoa hasira zake kwa mtoto, wakati mtoto huyo hana hatia. Hii huleta huzuni nyingi kwa mwana na kumpa mafikira ya kuwa hapendwi, ama hua anahisi kama yatima.
Wewe kama mzazi unayelea mwana wako ukiwa peke yako, mbali na sababu zake huna ruhusu kumfokea mwanao bila sababu au kumchapa ovyo ovyo. Na wakati huyo mtoto amefika umri wa kubalighi basi unaweza mweleza sababu zilizofanya akuwe mtoto wa kulelewa na mzazi mmoja tu.
Zaidi ya watoto milioni 320 ni watoto wa mzazi moja, hii inaonyesha kuwa wazazi wengi wanalea watoto wao peke yao, huenda ikawa ni sababu ya talaka ama kifo cha mzazi mmoja ama ni mwanaharamu(mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa).
Wala haimaanishi kuwa mtoto aliyekuzwa na mzazi mmoja hatapata malezi bora, La hasha, mtoto anaweza kukuzwa na malishe bora pia na maadili hata kushinda mwenye wazazi wake wawili. Jambo la kusikitisha ni kwamba, watoto wengi wa mzazi mmoja wanakuwa wakubwa bila kupata mapenzi ya baba… hii huenda pia ikafanya mtoto yule, iwapo ni wa kike awe mwenye mapenzi na wanaume wenye umri kumshinda kwa sana.
Sababu zinazopelekea mtoto kulelewa bila baba
1.
Kufariki kwa baba
Hii hutokea pale ambapo mzazi wa kiume wa mtoto/watoto akafariki na mzazi aliyebaki kutofunga ndoa/ kuingia kwenye mahusiano tena au akaingia kwenye ndoa na mtu asiyekubali kubeba jukumu la kuwa baba kwa watoto hao.
2.
Kutelekezwa
Hii hutokea mzazi wa kiume wa mtoto anapotelekeza familia na kuacha jukumu lote kwa mama.
3.
Baba kukataa ujauzito
Mwanaume anaweza kukataa ujauzito kwa sababu mbalimbali kama kutokuwa tayari na malezi, kuwa na mahusiano mengine, kuhisi amesingiziwa ujauzito huo au kutotaka kuwa na mtoto na mwanamke husika.
4.
Baba kufungwa
Uamuzi wa Mahakama unaweza kusababisha mzazi wa kike kubaki na jukumu la kulea watoto au mtoto peke yake.
5.
Mama kubakwa
Vitendo vya ubakaji hususani kwa mabinti wadogo husababisha watoto kulelewa na mama pekee aidha kwa sababu ya kutomjua mhusika au kuogopa kumtaja au baada ya baba kuhukumiwa kwa kosa la ubakaji
6.
Maamuzi binafsi
Siku za karibuni kumekuwa na wimbi la wadada kutaka kulea watoto bila msaada wa wanaume kwa sababu ya nguvu ya kiuchumi hivyo kupelekea kufanya maamuzi ya kubeba ujauzito na kukataa kuendelea na mahusiano na mhusika au kumficha au kuamua kubeba ujauzito wa mume wa mtu akijua fika kuwa atakataa kuhusika na malezi.
Faida za mtoto kulelewa na baba na mama
Watoto huhitaji malezi ya pande zote mbili bila kujali wazazi wao wako pamoja au la. Wanaume wengi wamekuwa wakisahau hili na kuhisi mama ndie mwenye jukumu pekee la kulea watoto. Mara kadhaa hurudi usiku na kukuta watoto wamelala na hutoka asubuhi sana kabla hawajaamka pengine bila hata kujua wameamka vipi. Zifuatazo ni sababu kadhaa kwa nini watoto wanahitaji malezi ya baba:
Utashangaa lakini sehemu ya kwanza ya mtoto kujua mwanaume ni mtu gani, anaonekana vipi na tabia zake ni kupitia baba. Unavyoishi na familia yako ndio hivyo mtoto atajua wanaume wote wako hivyo!
Akina baba hucheza kwa namna tofauti kidogo na watu wengine
Mara kadhaa utasikia mama akigombana na baba pengine tu baba anatumia nguvu nyingi akiwa anacheza na mtoto akihisi atamuumiza! Akina baba hucheza kwa nguvu zaidi na hucheza na mtoto kwa muda mrefu zaidi hii humfanya mtoto ajihisi salama na mwenye furaha.
Utafiti unaonyesha kuwa watoto wanaolelewa na baba huwa na tabia bora zaidi kuliko watoto wanaolelewa na mama pekee
Hakuna kitu mtoto huhitaji akiwa mdogo kama rafiki wa karibu. Watoto wadogo hasa wa kike hupenda sana kuwa karibu na baba yao, kwan huhisi salama zaidi akiwa na baba nan i mtu atakayemtetea kwa mama.
Uwepo wa baba katika maisha ya mtoto humfanya ajenge hali ya kujiamini kwani huhisi siku zote kuna mtu nyuma yake kwa ajili ya kumtetea.
Kujua namna ya kuwa baba bora/namna ya kuishi na mume
Zile tabia njema anazoziona kwa baba na mama ndio hivyo hivyo atafanya kwa mpenzi wake. Wazazi husahau kuwa Watoto hujiskia vizuri sana wanapoona hali ya mawasiliano mazuri kati ya wazazi wao hata wanapokua wametengana.
Mtoto anaelelewa na mama tu huwa na njia moja tu! Nayo ni ya mama, ni vema mtoto kupata upendo wa wazazi wote wawili ili ajue ni njia ipi sahihi kwake.
Kukaa na baba nyumbani humsaidia mtoto namna ya kuheshimu mamlaka mbalimbali za mahali husika. Mfano atajifunza kuwahi kurui nyumbani, kuvaa vizuri nk.
Wanaume wana uzoefu mwingi zaidi na maisha ya kawaida hasa kuishi na watu uvumilivu nk. Ni kawaida kumkanyaga bahati mbaya mwanaume, ukamuomba msamaha na akakuelewa, lakini kwa wanawake wengi hadithi huwa tofauti. Hapa utaona ni jinsi gani busara hii anavyoihitaji mtoto kuoka kwa baba.
Kufanya kazi kwa nguvu na bidii
Wanaume pia ni watu wanaofanya kazi kwa bidii sana hii humfundisha mtoto kutokata tamaa .
Madhara ayapatayo mtoto anayelelewa na mzazi mmoja
1.
Chuki na kupunguza upendo kwa mzazi mmoja
Wazazi wanapoachana daima watoto hugawanyika, huenda wakaishi kwa baba au kwa mama, au mmoja akaishi kwa baba mwingine kwa mama, hii hupelekea chuki upande mwingine, wazazi wengi hupenda kushirikisha ugomvi wao na watoto hupenda kuzungumza kwa hasira na huenda mpaka kusema sababu ya kuachana kwao.
(mara nyingi sababu ya watu kuachana si nzuri na ni aibu kuiweka wazi hasa kwa watoto)
Baba huweza kumwambia mtoto mama yako mpuuzi sana, mama yako hana akili, mama yako malaya tabu unazopata hapa kwasababu ya umalaya wake au mama humwambia mtoto hasa anapokosea, yani unaakili kama za baba yako, usiwe chizi kama baba yako, usiwe mjinga kama baba yako.
Katika hali ya kawaida haya ni maneno machache lakini yenye ujumbe mzito na usio na busara mbele ya watoto , watoto huanza kujenga chuki kwa mzazi mmoja maana anayesema hayo ndio mzazi anayemuhudumia kwa kila kitu, mtoto lazima ataamini na kumfuata baba/mama kwa kauli zake hivi inapendeza mtoto kumuona baba/mama yake hana akili au malaya? si kauli au malezi ya kiuungwana kesho mtoto atakutusi wewe utaridhia?
2.
Mawazo / Mgogoro wa nafsi
Umri wa mtoto ni tofauti na mkubwa, hakuna mtoto anayependa kuona wazazi wake wanakosana, kupigana mpaka kufikia hatua ya kuachana, hatua ambayo humuumiza zaidi mtoto kuliko wazazi, wazazi wanaamini kwamba kwakuwa wanapesa au wanauwezo wa kumuhudumi/kuhudumia mahitaji yote kwa mtoto basi anaweza kulea, (Wazazi wengi bado hawajui maana ya malezi na haki za mtoto).
Mgogoro wa nafsi unaweza ukawa wa nje au wa ndani, yani kama mzazi unaweza kumuona mwanao hana raha na akakuleza kinachomsibu au asikueleze( unaweza kumsaidia au usiweze) lakini watoto wengi huwezi kuwakuta wanakaa chini kuwaza ila yale mawazo yanawatafuna wakiwa wamelala, wanakuwa wanafikiria sana na kuumia nafsi, mtoto anaweza kula vizuri, kulala sehemu nzuri na unahakikisha unampa kila anachohitaji lakini humuoni akiwa na afya nje au kunenepa vizuri.
Hofu, mashaka na woga ndio unakuwa sehemu ya maisha yake, anaweza kuwa mjinga na asiwe mwenye kuhoji sana, hasa utakapozidi kutaka kuilazimisha furaha yake au kila atakapomuulizia baba/mama yake nawe kumpa majibu yasio faa, Akili yake inadumaa.
3.
Mabadiliko ya kitabia
Tabia ya mtoto hujengwa na pande tatu, baba, mama na jamii inayowazunguka lakini tabia kuu ambayo mtoto ndio sura yake inatoka kwa baba na mama, wazazi wanapoachana na tabia za watoto pia hubadilika huenda zikawa nzuri au mbaya, lakini kwa asilimia kubwa tabia za watoto hao huegemea zaidi upande mmoja, upande ambao anapokea malezi, kwa mama au kwa baba.
Kama ni mtoto wakiume na anaishi na mama, kuna baadhi ya tabia za baba hasa za kiume anazikosa, kama vile ujasiri, uvumilivu njia za kutafuta pesa na hata baadhi ya mambo ya mahusiano na mabadiliko ya mwili, mama hawezi kuwa huru kumueleza mtoto wa kiume mambo ya kiume, na hata mtoto wa kiume akipatwa na ugonjwa wa siri hawezi kumueleza mama na hata kama atamueleza basi ni dhahiri amefikiria sana na amekosa msaada na ugonjwa tayari utakuwa umemtafuna
Vile vile kwa mtoto wa kike akiishi na baba ni hivyo hivyo, lakini pia huenda mtoto wa kiume akawa na tabia za kike kulingana na kuishi na mama yake muda mrefu, na mtoto wa kike akawa na tabia za kiume kulingana na kuishi na baba yake muda mrefu.
Kikubwa ni kushindwa na kudhitibi mihemko yao, kama mtoto wa kiume anaishi na mama yake, mara nyingi anajikuta huru kutoka na kufanya mambo mengine bila kujua anachokienda ni sahihi au si sahihi na kwa wakati husika au sio, na kwa mtoto wa kike ni rahisi kuwa huru maana baba ndio mtafutaji, muda mwingi anashinda kwenye mihangaiko au kazini muda wa kumchunga na kumlea mtoto anakosa.
Yote hayo ukijumuisha lazima tabia za watoto zibadilike na haziwezi kuwa sawa na walioishi na baba zao na mama zao pamoja mpaka wanakwenda kujitegema, huenda zikabadilika zikawa hasi au chanya tabia hizo inategemea na kujitambua kwa mzazi na mtoto husika.
4.
Kukosa matunzo bora iwapo mzazi aliebeba jukumu la malezi hana uchumi imara
Hayo ni baadhi ya madhara tu ambayo mtoto humkumba baada ya wazazi kutengana ila yapo mengi zaidi kuliko hayo, ewe mzazi mambo ya kuzingatia,
Michango ya wadau
Lawama isitupwe kwa wanawake pekee
--------------------
=====================
Changamoto wanazopata wanaume walio kwenye mahusiano na single mothers
---------------------------
Changamoto wanazopata single mothers walio kwenye mahusiano na wanaume wengine / ndoa na wanaume wengine
Kuolewa au kuingia kwenye mahusiano mapya hali ya kuwa ulishawahi kuzaa mtoto au watoto kuna changamoto nyingi sana mwanamke hupitia akiwa ndani ya hayo mahusiano mapya, nitaelezea baadhi ya changamoto hizo
- Mwanaume kukataa kubeba jukumu la ubaba kwa watoto wasio wa kwake, kama kuwaonesha upendo kama watoto wake au kuwapa huduma stahiki kama elimu bora na mahitaji muhimu, hali hii hujitokeza hasa kwa kuona anamsaidia mwenye jukumu ambaye ni baba wa mtoto hivyo kutokuwa tayari kufanya hivyo.
- Wanawake kuwa na hofu ya watoto wao kufanyiwa vitendo vya kikatili na baba zao wa kufikia hasa kulingana na kuongezeka kwa matukio kama hayo katika jamii
- Mama kuona kama baba wa kufikia hutoa adhabu kali kwa watoto wake hasa wanapokuwa wamekosea, na mama kutotamani mtoto kupata adhabu ya kiwango hicho na kuhisi anampa adhabu hiyo kwa kuwa si mtoto wake wa kumzaa
- Wanaume kukataa kuishi na mtoto aliomkuta naye mwanamke, hivyo kumlazimu kuwapeleka kwa ndugu zake na kusababisha mtoto kuishi bila upendo wa wazazi