Wakristo wengi wanadanganywa kuwa kupeleka pesa na mali kanisani ndio kumtolea Mungu sadaka!

Wakristo wengi wanadanganywa kuwa kupeleka pesa na mali kanisani ndio kumtolea Mungu sadaka!

Status
Not open for further replies.
Ni uongo kwa namna gani? Ili iwe uongo tuambie kwa maandiko wakristo walitakiwa kupeleka sadaka wapi?
Nimefafanua kwenye mada yangu kwa kina.
Kwa kifupi, Sadaka ni ibada kwa 100%, na kwa uhalisia ni ile hiari ya moyo wako kutoa au kufanya jambo kwa kupenda huku ukifurahi kwa lengo la kumrudishia Mungu utukufu (Yohana 4:24).

Sasa kwa mfano, kama jirani yako hana nguo au chakula na wewe kwa hiari yako mwenyewe (sio kwa kutishwa, kuchochewa, kupangiwa au kushawishiwa) ukatoa pesa zako kwa furaha kumpa ili apate Chakula au nguo kwa lengo la kumrudishia Mungu utukufu basi hapo ndio umetoa sadaka.

Hivyo, Sadaka (lile tendo la kutoa mali/pesa zako), inaweza kutolewa mahali popote, saa yoyote, kwa mtu yoyote pale kikubwa tu Moyo wako uwe umeguswa kwa hiari, kupenda na kufurahi huku ukidhamiria kumrudishia Mungu utukufu.

Hizi blah blah zingine makanisani ni michango tu ambayo inalazishwa itolewa kwa kivuli cha kichaka cha kuitwa Sadaka lakini kwa hakika sio Sadaka 100%.
 
Sadaka zipo za aina nyingi naona umezijumla kama ni aina moja.
Rudi shule ukasome zaidi kuhusu sadaka ni nini
 
Hakuna Imani bila sadaka hata kwa shetani ili uwe viwango vya juu sadaka ni lazima tena kule wanatoa asilimia 60% ya ulichopata.
 
Kama kuna jambo ambalo wakristo wengi wanadanganywa na kuibiwa basi ni kwenye kitu kinaitwa Sadaka.
Kila ujanja ujanja wa viongozi wa kikristo kutaka kuwatapeli waumini pesa na mali zao basi sadaka ndio kichaka cha kwanza na haraka sana kinatumika. Na jambo hili lipo kwenye madhehebu yote ya kikristo na hata dini zingine.

Kupitia mada hii nitaweka sawa kwa uchache mtazamo wa sadaka kulingana na imani halisi ya kikristo kupitia Biblia.

1. Sadaka ni ibada kamili (moyo wa muumini unakwenda moja kwa moja kukutana na Mungu wake), hivyo kabla ya kuitoa jiulize haya maswali makubwa matatu:

(a)Moyo wako ni msafi kiasi gani kumkaribia Mungu kwa njia ya sadaka (yaani uhusiano wako na Mungu wako ukoje wakati ule unapotaka kutoa hiyo sadaka) (Mathayo 5:8)

(b)Mali/Pesa inayotaka kuitoa kama sadaka ni halali kiasi gani katika mtizamo wa neno la Mungu mpaka imfae Mungu. (Yohana 4:24)

(c)Hiari ya kutaka kumtolea Mungu hiyo mali/pesa itokane na kumpenda tu huyo Mungu na sio vingenevyo (2Wakorintho 9:7)

2. Sadaka halisi inatolewa moyoni mwako (yaani dhamira ya hiari kwa kupenda kutoa kitu/kufanya jambo lenye thamani nzuri, kwa kwa lengo la kumrudishia Mungu utukufu). Vitendo vya utoaji wa sadaka ndio wanadamu wanaweza kuviona, na wala hupaswi kulazimisha kutengeneza mazingira ya watu waone au wajue ulichotoa.

3. Tendo la utoaji sadaka (yaani kule kutoa pesa au mali zako) linaweza kufanyika mahali popote pale, wakati wowote ule, kwa mtu yoyote ule, kwa namna yoyote ile, kwa kiasi chochote kile, lengo kuu likiwa ni kumrudishia Mungu utukufu huku ukiufurahisha moyo wako.

4. Michango yoyote ya makanisani au taratibu zote za utoaji mali na pesa makanisani kwa jina la Sadaka, kiuhalisia SIO SADAKA. Hizo ni taratibu za makanisa tu katika kuweza kujiendesha na kufanikisha shughuli zake za kila siku ama watu fulani mahususi wazitumie. Kwanini? Mara nyingi (kama sio mara zote) hizo taratibu hazihoji anayetoa kama ni msafi kiimani, hazihoji uhalali wa kule zilipopatikana na hazipendi kumpa muumini hiari ya moyo wake kuamua kutoa au kutokutoa (muumini atawekewa kiwango, atatishwa kiimani asipotoa atapata madhara au atashawishiwa kuwa akitoa atabarikiwa). Wewe utaambiwa toa tu, tena toa nyingi uwezavyo. Ni unyonyaji kwa 100%.

5. Mwisho kabisa, kila mkristo anapaswa kujua haya:
-Hatuendi mbinguni kwa kutoa sadaka wala kwa kutokutoa sadaka hatukosi mbingu
-Hatununui baraka kwa kutoa sadaka na wala hatuvuni laana kwa kutokutoa sadaka.
-Hatulaaniwi kwa kutokutoa sadaka na wala hatuvunji laana kwa kutoa sadaka.
-Tunapaswa kutoa sadaka (popote pale, kwa namna yoyote ile, kiasi chochote kile) kwa sababu tunampenda na kumfurahia Mungu wetu, tusilazimishwe wala kushawishiwa kiujanja ujanja.
Mtoa mada tusitoe sadaka halafu tusali chini ya miti kwenye vumbi?
au tusubiri mfalme wa Morocco aje atujengee msikiti kinondoni?
 
Kama kuna jambo ambalo wakristo wengi wanadanganywa na kuibiwa basi ni kwenye kitu kinaitwa Sadaka.
Kila ujanja ujanja wa viongozi wa kikristo kutaka kuwatapeli waumini pesa na mali zao basi sadaka ndio kichaka cha kwanza na haraka sana kinatumika. Na jambo hili lipo kwenye madhehebu yote ya kikristo na hata dini zingine.

Kupitia mada hii nitaweka sawa kwa uchache mtazamo wa sadaka kulingana na imani halisi ya kikristo kupitia Biblia.

1. Sadaka ni ibada kamili (moyo wa muumini unakwenda moja kwa moja kukutana na Mungu wake), hivyo kabla ya kuitoa jiulize haya maswali makubwa matatu:

(a)Moyo wako ni msafi kiasi gani kumkaribia Mungu kwa njia ya sadaka (yaani uhusiano wako na Mungu wako ukoje wakati ule unapotaka kutoa hiyo sadaka) (Mathayo 5:8)

(b)Mali/Pesa inayotaka kuitoa kama sadaka ni halali kiasi gani katika mtizamo wa neno la Mungu mpaka imfae Mungu. (Yohana 4:24)

(c)Hiari ya kutaka kumtolea Mungu hiyo mali/pesa itokane na kumpenda tu huyo Mungu na sio vingenevyo (2Wakorintho 9:7)

2. Sadaka halisi inatolewa moyoni mwako (yaani dhamira ya hiari kwa kupenda kutoa kitu/kufanya jambo lenye thamani nzuri, kwa kwa lengo la kumrudishia Mungu utukufu). Vitendo vya utoaji wa sadaka ndio wanadamu wanaweza kuviona, na wala hupaswi kulazimisha kutengeneza mazingira ya watu waone au wajue ulichotoa.

3. Tendo la utoaji sadaka (yaani kule kutoa pesa au mali zako) linaweza kufanyika mahali popote pale, wakati wowote ule, kwa mtu yoyote ule, kwa namna yoyote ile, kwa kiasi chochote kile, lengo kuu likiwa ni kumrudishia Mungu utukufu huku ukiufurahisha moyo wako.

4. Michango yoyote ya makanisani au taratibu zote za utoaji mali na pesa makanisani kwa jina la Sadaka, kiuhalisia SIO SADAKA. Hizo ni taratibu za makanisa tu katika kuweza kujiendesha na kufanikisha shughuli zake za kila siku ama watu fulani mahususi wazitumie. Kwanini? Mara nyingi (kama sio mara zote) hizo taratibu hazihoji anayetoa kama ni msafi kiimani, hazihoji uhalali wa kule zilipopatikana na hazipendi kumpa muumini hiari ya moyo wake kuamua kutoa au kutokutoa (muumini atawekewa kiwango, atatishwa kiimani asipotoa atapata madhara au atashawishiwa kuwa akitoa atabarikiwa). Wewe utaambiwa toa tu, tena toa nyingi uwezavyo. Ni unyonyaji kwa 100%.

5. Mwisho kabisa, kila mkristo anapaswa kujua haya:
-Hatuendi mbinguni kwa kutoa sadaka wala kwa kutokutoa sadaka hatukosi mbingu
-Hatununui baraka kwa kutoa sadaka na wala hatuvuni laana kwa kutokutoa sadaka.
-Hatulaaniwi kwa kutokutoa sadaka na wala hatuvunji laana kwa kutoa sadaka.
-Tunapaswa kutoa sadaka (popote pale, kwa namna yoyote ile, kiasi chochote kile) kwa sababu tunampenda na kumfurahia Mungu wetu, tusilazimishwe wala kushawishiwa kiujanja ujanja.
Historia ya sadaka imeanzia mbali sana tangia agano la kale.
Makabila 12 ya wana Israel kati yake makabila 11 yalipewa ardhi kwenye nchi ya ahadi Canaan. Kabila moja la Lawi halikupewa ardhi wao waliachwa maalum kwa ajili ya ukuhani. hivyo hayo makabila mengine yote yalikuwa yanatoa sadaka hekaluni na makuhani kabila la Lawi waliishi kupitia sadaka za makabila mengine.
Soma agano la kale usikurupuke.
 
Isaya 1:11
Huu wingi wa sadaka zenu mnazonitolea una faida gani?

Amosi 5:22
Naam, ijapokuwa mnanitolea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za unga, sitazikubali; wala sitaziangalia sadaka zenu za amani, na za wanyama walionona.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom