Wakurya, najua mkiona hii picha hamuhitaji kutafasiriwa

Kuna mdau kasema ni mbaya hauna ladha.!
Na wewe ni kurya?
 
Reactions: 511
Kuna mdau kasema ni mbaya hauna ladha.!
Na wewe ni kurya?
Itakuwa alipewa ugali wa mtama pekee tena mgumu. Huo hapo pichani ukionja hutatamani kuacha.
Mimi sio mkurya ila nimekaa nao kama miaka 5 hivi nikiwa mwajiriwa huko.
Hasira zao zinasababishwa na kunywa damu mbichi kama maasai.
Kwetu ni lupembe
 
Itakuwa alipewa ugali wa mtama pekee tena mgumu. Huo hapo pichani ukionja hutatamani kuacha.
Mimi sio mkurya ila nimekaa nao kama miaka 5 hivi nikiwa mwajiriwa huko.
Hasira zao zinasababishwa na kunywa damu mbichi kama maasai.
Kwetu ni lupembe
Ohhh! Kumbe?
Basi sawa.!
Ila mimi rangi tu imenitisha sijui hata hiyo ladha nitaiona mdomoni.!!
 
Reactions: 511
Nilikula pale Musoma nyama choma na ugali nikaletewa na Hiko kibakuli chenye ukijani hapo, kuchovya naona sielewi nikaweka pembeni, mhudumu ananiuliza kumbe hujui Kichuli nilimwangaliaa nikamlipa nikaondoka 🤣🤣🤣🤣
 
Mimi siyo Mkurya ila kijijini kwetu hicho chakula kipo, hasa wakija wageni.
Ugali na nyama ya kuchemsha? Sehemu nyingi nyama inakaangwa na kuwekwa viungo. Kuhusu ugali, hapo naunga mkono japo sijawahi kula ugali sijui wa mtama. Ila kwa afya ni mzuri sana.
 
😂😂😂, Ndio wazo la kwanza lililonijia kichwani baada ya kuniambia sio maandazi
Mimi nilijua maandazi asee 🤣🤣
Nikawaza moja ukipiga si hoi shibe whole day unashindia Hill water 🤣🤣
 
Itakuwa alipewa ugali wa mtama pekee tena mgumu. Huo hapo pichani ukionja hutatamani kuacha.
Mimi sio mkurya ila nimekaa nao kama miaka 5 hivi nikiwa mwajiriwa huko.
Hasira zao zinasababishwa na kunywa damu mbichi kama maasai.
Kwetu ni lupembe
Lupembe hii hii 🤣
 
Reactions: 511
We jamaa ni muongo sana. Maandazi🤣
Tatizo limeletwa na mtoa mada kutudumpia home work bila maelezo kama vile mtu anavyotupia mbwa marapu rapu kimya kimya na kufurahia wanavyogombania.

Sasa kila mtu amekuja na maoni yake namna jinsi anavyotazama, hatuwez ku conclude kuwa ni uongo ama ukweli.

Rangi hiyo yaweza kuwa ni ya ugali wa ulezi ama wa mtama, lakini kwa mila na desturi ya maeneo hayo, ugali unasongwa na kupakuliwa fungu moja tu kubwa.

Hata mkiwa watu ishirini mnaweza kushea kwa kujenga duara, haugawiwi mafungu.

Hizo mboga ama kitoweo vyaweza kugawanywa namna hiyo kidogo kidogo kwenye vyombo.
 
Reactions: 511
Hiyo ilikuwa zamani.
Kwa sasa jamii nyingi zinapenda kula kila mmoja na sahani yake.
Huo ugali hapo ndivyo unavyopakuliwa kwenye migahawa yao. Tatizo hapo inaonekana kama wako home.
 
Ingekuwa wajaluo, hapo ungekuta ugali mkubwaaa kwenye sahani na mwingine mdogo kwa juu ya huo ugali mkubwa.
 
Reactions: 511
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…