Wakuu naomba mnieleweshe concept ya Mungu katika ukristo

Wakuu naomba mnieleweshe concept ya Mungu katika ukristo

Wakristo hapo ndipo tunapofeli tunafundisha kinyume na Biblia

Biblia inasema wazi Mungu ni mmoja tu hizi mambo za nafsi 3 tunadanganya sana

Na Yesu sio MUNGU

1 Wakorintho 11:3​

Neno: Bibilia Takatifu​

3 Lakini napenda muelewe kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, kama vile mume alivyo kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo

Kwa msingi wa andiko hilo kama Yesu ni sawa na Mungu basi tukubaliane pia mke ni sawa na mume
soma vizuri bible ni bible hiohio Ina verse zinamanisha kua Jesus yuko kitambo sana huko mbinguni na alihusika kwenye uumbaji wa hii universel. pia ni God .! alieandika ndo mzinguaji bhana mafumbo kibao kwaio kinacho tokea kila mtu anatafsiri kivyake
 
Nina shida kidogo na ongea yangu na andika yangu.. uwa ninaongea na kuandika kimamlaka zaidi ndiyo maana mtu asiyenijua anaweza hisi nafoka kumbe sio.
Nichukulie poa.

Chief,hizo verse ulizotoa hazimsemi Yesu kama ulivyoeleza hapo juu.
Yesu ni mwana wa Mungu hivyo ana uungu. kuna verse nimeisahu Mungu anamuita Yesu Mungu lakini hiyo haina maana kuwa Yesu ndiye yule Mung ambaye biblia inamsema hakuna aliyewai muona akaishi.
Maisha yake yote hapa Duniani yesu alisema Yeye ni mwana wa Mungu na ilo likafanya wayahudi wakataka kumpiga.
Katika biblia tuna Mungu Baba,mwanae Yesu Kristo na Roho wa Mungu.
Roho wa Mungu si Mungu nafsi.
Yesu Kristo si Mungu nafsi.
1Petro 3:22
"ambaye alikwenda mbinguni na sasa amekaa upande wa kulia wa Mungu, anatawala juu ya malaika, wakuu na wenye enzi".

Yesu amakee upande wa kulia wa Mungu,sasa kwanini wewe useme Yesu ni Mungu?.
Kuna kitabu nikikumbuka nitakutumia jina.
Kinasema " Jesus is God infinitely but not in personality.

Kusema Yesu ni Mungu,na roho wa Mungu ni Mungu na Baba ni Mungu automatically wanakuwa ni mungu 3 kitu ambacho kwenye biblia hakipo.
Ivi kwenye ufunuo yohana alimuona nani yule alikua uso wake unawaka kama jua na macho yatoa miale yamoto na ulimi kama panga likatalo kuwili.?
 
Habari

1. Wengine wanasema kuna Mungu Baba, mwana na roho mtakatifu

2. Wengine wanasema Mungu mmoja

3. Wengine nasikia wanasema ana nafsi tatu

Na je kama ana nafsi tatu kwa nini munamuabudu sana YESU kuliko huyu Mungu Baba

Lengo ni kuelewa kipi ni kipi maana naona kama wanatofautiana sana juu ya concept ya Mungu

Shukrani
wanamgawa Mungu kwenye utatu kama tairi za bajaji.
 
Habari

1. Wengine wanasema kuna Mungu Baba, mwana na roho mtakatifu

2. Wengine wanasema Mungu mmoja

3. Wengine nasikia wanasema ana nafsi tatu

Na je kama ana nafsi tatu kwa nini munamuabudu sana YESU kuliko huyu Mungu Baba

Lengo ni kuelewa kipi ni kipi maana naona kama wanatofautiana sana juu ya concept ya Mungu

Shukrani
ni kama ilvyo serikali, na mihimili yake mitatu
Mungu naye ni ana mihimili mitatu katika utendaji kazi wake na kila mhimili una jukumu lake-Baba ,Mwana na Roho mtakatifu
 
Habari

1. Wengine wanasema kuna Mungu Baba, mwana na roho mtakatifu

2. Wengine wanasema Mungu mmoja

3. Wengine nasikia wanasema ana nafsi tatu

Na je kama ana nafsi tatu kwa nini munamuabudu sana YESU kuliko huyu Mungu Baba

Lengo ni kuelewa kipi ni kipi maana naona kama wanatofautiana sana juu ya concept ya Mungu

Shukrani

1 Yoh 5:8​

Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.

John 10:30

I and the Father are one.”
 
Kiuhalisia hakuna Mungu ila vyoyote utakavyofikiri kuhusu hii dhana ya Mungu upo sawa kabisa, kutokana na mapokeo yako na athari za ukoloni kwenye kizazi chako .
 
Swala la kuwepo kwa mungu ni swala la lenye yakini ya kimaumbile

Mtu yoyote akipatwa na shida kubwa mfano, ugonjwa serious lazima tu akumbuke uwepo wa mungu, tena mtu anajiapia nikipona nitakesha kwenye Ibada ila akipona anaanza kuongea ufala kama wewe.


Afya njema tu inakusahaulisha.
Umeongea utumbo
 
MTU YOYOTE AKIKUAMBIA HAKUNA MUNGU AU MUNGU ANAZO NAFSI 3 AU YESU ALI SULIBIWA KWA SABABU YA DHAMBI YA ASILI... JUA TU HUYO NI MPUMBAVU TENA NI SHETANI IBILISI TENA NI MUONGO
 
Binadamu kagawanyika makundi 3 yanayounda mtu mmoja kamili! Mwili ni sehemu ya mtu inayoweza kujigawa! Roho ni sehemu ya mtu inayoweza kujigawa! Nafsi ni sehemu ya mtu inayoweza kujigawa!

Mtu anapokuwa amelala, roho hailali usingizi bali mwili! Ikitokea ukajeruhiwa na vitu kama mapenzi na dhuruma, kinachoumia ni nafsi bali mwili na roho vinashiriki kuugulia kwasababu nafsi, roho, na mwili kwa mtu aliyehai vyote viko pamoja kwa umoja!

Na Mungu ndo hivyo hivyo! Mungu Baba, Mungu mwana, Mungu Roho mtakatifu!

Kwa umoja huu ndo Mungu!

Japo wewe sio Mkristo lakini Biblia imeliweka wazi!


"NA TUMFANYE MTU KWA MFANO WETU"



Mwanzo 1:26

[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.


Kwahiyo, ndani ya Mungu kuna uwezo wa kujifanya mwili (ndivyo alivyofanya Yesu), Mungu ni Roho ndivyo alivyo (hata Yesu alivyotaka kufa yeye mwenyewe) alitoa Roho yake akafa mwili akafanya aliyoyafanya alafu akautwaa mwili uleule akafufuka na huo mwili anao mpaka leo. Ndani ya Mungu kuna huwezo wa kimamlaka (Mungu Baba) kama ilivyo ndani ya mwanadamu nguvu ya kimamlaka ni hile roho inayotawala nafsi!

Naishia hapa! Kama unataka mafunuo zaidi okoka! Mkiri Yesu Kristo kuwa ni BWANA! Na alikufia msalabani ili akurudishe kwa Mungu kwasababu hapo ulipo umepotea
Quran

5:17 - Hakika wamekufuru
walio sema: Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu.
Sema: Ni nani mwenye kumiliki chochote mbele ya Mwenyezi Mungu ikiwa Yeye angetaka kumuangamiza Masihi mwana wa Maryamu, na mama yake, na wote waliomo katika ardhi? Na mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ni vya Mwenyezi Mungu. Huumba apendavyo na Mwenyezi Mungu anao uweza juu ya kila kitu.

5:72 Hakika wamekufuru walio sema Mwenyezi Mungu ni Masihi mwana wa Maryamu, na hali Masihi mwenyewe alisema: Enyi Wana wa Israili Muabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi, kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharamishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru.

5:73 Kwa hakika wamekufuru walio sema: Mwenyezi Mungu ni wa tatu wa Utatu. Hali hakuna mungu ila Mungu Mmoja. Na ikiwa hawaachi hayo wanayo yasema, kwa yakini itawakamata adhabu chungu wale wanao kufuru.

5:74 - Je! Hawatubu kwa Mwenyezi Mungu na wakamwomba msamaha?
Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe na Mwenye kurehemu.

5:75 - Masihi mwana wa Maryam si chochote ila ni Mtume, Wamekwisha pita Mitume kabla yake. Na mama yake ni mwanamke mkweli.
Wote wawili walikuwa wakila chakula. Angalia jinsi tunavyo wabainishia alama zetu, kisha angalia vipi wanavyo zigeuza.
 
MTU YOYOTE AKIKUAMBIA HAKUNA MUNGU AU MUNGU ANAZO NAFSI 3 AU YESU ALI SULIBIWA KWA SABABU YA DHAMBI YA ASILI... JUA TU HUYO NI MPUMBAVU TENA NI SHETANI IBILISI TENA NI MUONGO
Usitukane watu kwa mtazamo wa dini yako
Hii ndio shida kubwa sana waliyonao Waislam dhidi ya imani zingine
 
Usitukane watu kwa mtazamo wa dini yako
Hii ndio shida kubwa sana waliyonao Waislam dhidi ya imani zingine
Nani muisiharamu ? Uislamu ni dini ya uongo tu
 
Back
Top Bottom