Wale tuliokosea kuoa tukutane hapa

Wale tuliokosea kuoa tukutane hapa

[emoji3][emoji3] Nna mwezi mmoja toka nimefunga ndoa! Mnanitisha wakongwe! Tunavyopendana speed 120 kumbe kuna siku litashuka sitaki kuamini [emoji1787]
Enjoy tu mzee, be optimistic. Expect and do your best to make it as a beautiful experience as you can. Sio lazima kila baya lililowatokea wengine na wewe likutokee.
 
Kuna jamaa yangu yeye mpaka alijihisi ni hanithi kumbe kamchoka mwanamke wake aliyekuwa na kiburi, hila, ujeuri na dharau, of recent kila akikutana naye kitandani baada ya kuwa pamoja kwa miaka kumi ngoma haidindi kabisa ila akienda nje anapiga mashine mchepuko wake hadi unakimbia unaacha chupi kwa msela.
Unaweza kupanda kama tuu kuna maelewano na saikolojia uko fit tofauti na hata mimi nilishashindwa.
 
Hao Alpha ndio wanaojiliza kwenu au wenye pesa? Maana hata akiwa na pesa godown Zima na mwanamke akawa mwalimu tuu kama ni jeuri hapo hakuna alpha na omega ataacha kuiona 😄😄
Alpha sio hela wala sio kujiliza kwa mwanamke.

Alpha amwage chozi kwa mwanamke kisa?

Labda Alpha wa Makabe kwa kina maroon7

🙊🙊🙊🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🏃🏻‍♀️🤣🤣🤣
 
NGOMEKONGWE2021 - Tupo wengi, kiongozi. Mie pia watoto 4 kama wewe. Miaka 12 ya ndoa. Mama wa nyumbani. Tatizo hawezi kujifunza kitu.

Kila siku ni shida tupu ndani ya nyumba. Mfano, hawezi kutoa magamba ya samaki yakaisha yote kabla ya kumpika samaki. Chakula anavyonunua kwenye supermarket, ndivyo navyokipika!

Anaweza kupika nyama ya kuku na kinyeo chake ama bado kuna kiasi fulani cha vinyoya!! Hata nikimweleza vipi, akili yake haishiki!! Hataki niwafundishe watoto. Nikiwakosoa watoto kwa namna ya kuwafundisha, anakuja juu.

Watoto wananiona mimi shetani na yeye malaika. Amejenga chuki kati yangu na watoto ambao bado ni wadogo tu. Sijawahi kumpiga ama kuchepuka lakini nilikwisha mwambia kuwa tungekuwa tunaoa mara ya 2, nisingemuoa tena. Sina hamu tena hata ya kulala naye.
Dooh. Pole sana mkuu. Hayo mengine naona ni madogo madogo ila hayo ya kujenga chuki baina ya wewe na watoto ni mbaya sana, it's like the family is divided. Mungu akusaidie mkuu kutengemaza familia yako.
 
Cariha Cariha Cariha...nakuita Mara 3!Jana nililala shosti miye nimekuta mambo marefuu!
Skiliza achana na wabeing au upate mume mzungu,au alielelewa na kukuliwa Ulaya ila kwa hapa kwetu Tz utachemka,na ndo ukweli!
Wa hapa kwetu wakuhudumiwa ila sasa Muache afanye majukumu yake...
Hayo unayoyaongea never on earth hapa kwetu kibongo bongo au ukiona anakupotezea ujua ana mwenzio anampa vyote hvyo...
Nakuambia wapo ila wachache na mnooo!ukimuokota hongera
Mbona kwetu wanaume hufanya mambo mengi including cooking na hata kujifanyia mambo mengi na haijawahi kuwapunguzia uanaume wao ndani, I grow to see my aunties, ba mdogo wanafanya vitu common kabisa ambacho huku JF naona mwanaume analalamika Hadi kuvunja ndoa yake kabisa, Mimi babangu kupika sio issue hata kaka zangu na haijawahi kuwapunguzia uanaume wao so it's just a matter of perspective kwa dunia ya Sasa watu watavunja sana ndoa zao ka wanaamini kuto kumsaidia mke kazi hata akiwa kachoka kazini ndio uanauke Bora au uanaume Bora, basi before marriage tafta mwanamke anayeendana na wewe, huwezi acha kazi zako na kutimiza ndoto ukiwa wampikia mume, sijui unapinda mgongo woooi, that's why nasema watu tumetoka different backgrounds unayemuoa make sure atafanya utakavyo, na ndio naona huyu mleta mada angetakiwa aoe mke wa kijijini wa darasa la saba Ili awe mama wa nyumbani afanye hayo yote
 
Kuna wanaume wanaojielewa Hawa mind vitu vidogo sijui kubebewa maji sijui ku saviwa msosi kah in our family una jisevia, Sasa Hawa humu eti anavunja ndoa kisa mke alikuwa akitoka kazini hapiki Yani upendo unapimwa kwa kumugeuza mke house girl.
Ulitaka upendo upimwe kwa kufanyaje? Sasa mwanamke ambae hafanyi hayo unaoa Ili iwaje?
 
Shoga ukiona utumwa utasaidiwaaa
Me yoote tusaidiane lakini swala la usafi wake, kunyoa na K nitayafanya hadi kufa hata niwe nimechoka.
Mimi nisaidiwe tu tena nitafurahi sana huwa nafanya kitu nikijiskia if I don't feel doing it naacha, Yani nafanya jambo kwa kuamua na sio kuwaza Ili nisisaidiwe what I know you can't please people hata ufanyeje binadamu haturiziki, so nafanya kujifuraisha I would rather allow my partner kufanya anachojiskia kuliko Kuni force kufanya nisichotaka kabisa.
 
NGOMEKONGWE2021 - Tupo wengi, kiongozi. Mie pia watoto 4 kama wewe. Miaka 12 ya ndoa. Mama wa nyumbani. Tatizo hawezi kujifunza kitu.

Kila siku ni shida tupu ndani ya nyumba. Mfano, hawezi kutoa magamba ya samaki yakaisha yote kabla ya kumpika samaki. Chakula anavyonunua kwenye supermarket, ndivyo navyokipika!

Anaweza kupika nyama ya kuku na kinyeo chake ama bado kuna kiasi fulani cha vinyoya!! Hata nikimweleza vipi, akili yake haishiki!! Hataki niwafundishe watoto. Nikiwakosoa watoto kwa namna ya kuwafundisha, anakuja juu.

Watoto wananiona mimi shetani na yeye malaika. Amejenga chuki kati yangu na watoto ambao bado ni wadogo tu. Sijawahi kumpiga ama kuchepuka lakini nilikwisha mwambia kuwa tungekuwa tunaoa mara ya 2, nisingemuoa tena. Sina hamu tena hata ya kulala naye.
Mkuu Ili tufaidike na darasa zenu tunaomba mtuambie sku za mwanzon mlikutana vipi,ulikuwa unamchukuliaje/unamwonaje...Ili kwa sisi tunaoanza maisha tujifunze kitu.
 
Kivipi mkuu, Mimi mwanaume anayetaka eti kubebewa ndoo bafuni sijui kupika daily na nimetoka kazini kwangu naona hafai kuwa mume, zama zimechange sikuhizi wooi
Wacha wee......
 
Ulitaka upendo upimwe kwa kufanyaje? Sasa mwanamke ambae hafanyi hayo unaoa Ili iwaje?
Yani upendo unapimwa kwa kubebesha mkeo ndoo bafuni, sijui kupika, sijui nini, kwangu Mimi naona huo sio upendo ni ujinga au naishi na partner asiye elewa nini maana ya mahusiano, love ya vi condition ka hivo sio true love hiyo, maana kupika mbona na ma chef wa kiume ni wapishi wazuri ina maana nao wapewe upendo.
 
Wanakuwa brainwashed. Ni hawahawa huunga mkono ndoa za jinsia moja, n.k.

Just because kinafanywa na Wazungu haimaanishi ndiyo kipo sahihi.

Tunafeli sana.


Wale mambo yao hufanyika kisayansi baada ya tafiti, hawafanyagi mambo kienyeji kama sisi wabongo!
 
Tukumbuke chagizo za ndoa ilikuwa ni nini na inabaraka za Mungu kwa wote wawili kuwa na roho wa Mungu kwa mpango wa ndoa? Unawaza mema wakati yeye anakuwazia wewe kuwa daraja la kuvuka, kuna ndoa za Mungu na za shetani, kama hujadhamiria na kunuia ndoa kuvunjika upo mpango wa Mungu
 
Wadau,

Nimekuja kugundua nilikosea kuoa baada ya kukaa kwenye ndoa miaka 15 na kupata watoto wanne. Dah nilijichanganya nikaoa a Corporate lady ambaye alikuwa mwanasheria kule Arusha, alikuwa ana vihela flani na connections za watu wazito ndani ya bongo....duh acha kabisa!!!

Nilikuja kujuta sana manake kazi zoote na mambo yooote ya nyumbani yalikuwa yanafanywa na mabeki tatu kuanzia Kufua nguo zangu, maji ya kuoga, kupika nk alikuwa hana time kabisa na nyumba yake. Hajui chochote kinachoendelea nyumbani kwake kila kitu anabishana na kushindana.

Mtu wa vikao vya dinner karibu kila siku. Miaka ya mwanzoni nilikuwa namdunda sana sana baadaye nikapataga kesi, wakati mwingine ilibidi niingie hasara ya kumpeleka hospitali na kumhudumia manake alikuwa na watoto wadogo.

Nikaamua kuingia kwenye pombe na michepuko ili nimpuuzie. Nikawa nampuuzia kama vile hayupo na yeye akanikazia, akazidisha kiburi na jeuri nikaanza tena kumdunda nikapata tena kesi kubwa manake ilikuwa nimuulie mbali.

Sasa baadaye nikafikiria sana watoto wangu tukafikia hatua ya kuachana na kukubaliana jinsi ya kuwalea watoto. Sasa tumeweka nguvu zoote katika kuwalea watoto na hali imekuwa shwari kabisa kila mtu anaishi kivyake baada ya talaka.

Najua kuna wale watakaosema tuishi nao kwa akili. Nilijitahidi kufanya hivyo kwa miaka 15 lakini ikashindikana manake ningeishia jela baada ya kumtoa uhai na watoto wangeteseka.

Bora iwe hivi hivi wote tupo wazima wa afya.

ALAMSIKI, DUH USIOMBE KUKOSEA KUOA BORA UKOSEE KUZALIWA

KARIBU NI WADAU WENZANGU MLIOKOSEA KUOA.
Hongera kufikia hiyo hatua ya kuachana. Nina mwaka wa 17 kwenye ndoa ya mateso makubwa. Mwanamke jeuri hatari. Nimeendesha kiupole,kidini,kijeshi. Lakini wapi. Kuachana ndio hataki kabisa. Nimetumia kila mbinu,lakini anegomea ndani tu hataki kuondoka kabisa. Hongera kwako,umekiondoa kifungo cha moyo
 
Back
Top Bottom