Tetesi: Walimu wamegeuza Shule za Serikali kuwa Vitega Uchumi vyao

Tetesi: Walimu wamegeuza Shule za Serikali kuwa Vitega Uchumi vyao

Kuna wazazi wapo radhi kulipa 3M+ kwa ajili ya Elimu lakini wewe kuchangia pesa ndogo (kiduchu) ya masomo ya ziada na mambo mengine unafungua hadi thread.

Kama unaona Elimu ni ghali basi jaribu ujinga inawezekana usiwe ghali
mwambie ana tofauti gani na mpwayungu
 
Walimu wenyewe wanatamani watoke mapema wakafanye mambo yao, Ila wanakaa shule mpaka jioni kuwasaidia watoto wenu.

Nenda kwenye kikao cha shule mkubaliane wazazi hamtaki remedials/vipindi vya ziada uone walimu watakavyoshangilia..
Hakuna hiyo, hawafanyi bila maslahi, jaribu kawaambie wajitolee kama wasemavyo wanajitolea wakati si bila chochote, au ina maana tofauti na volunteer?
 
nashangaa mwambie wkt wa kut o m b a n a alifurahia hakukumbuka kuna malipo ya mtoto unataka aende shule bure
Ndugu acha utoto anzisha jukwaa la watoto. Kwani wewe ndiye unaye hudumia familia za Watanzania wanaotumia huduma ya shule hizo, acha kujikweza for nothing.
 
nashangaa mwambie wkt wa kut o m b a n a alifurahia hakukumbuka kuna malipo ya mtoto unataka aende shule bure
Elimu ikiwa bure hai maanishi kuwa mzazi asinunue vitabu vya kiada na ziada.
Madaftari
Chakula
Uniform etc
 
Mpeleke mwanao shule za Binafsi zipo nyingi tu, unataka waalimu wamnunulie Limu mwanao? Watoe copy Kwa hela zao? We mwenyewe unajua hali ya shule zilivyo. Unakuja kuwasimanga waalimu huku wakati wanapambania watoto wenu Kwa plan B. Wakiamua kuacha mtoto wako hatajua hata kusoma.


NB: Ningekuwa Mwalimu nisingehangaika na toto la mtu hasa hizi shule za Umma,mnawalaumu wakati anafundisha darasa halina hata miundombinu bora na Lina wanafunzi 150
Achana na watu wenye akili matope.akaulize Ada feza NI sh ngapi.afu anaesoma pale feza NI Mtoto WA anaemwambia asichangie chochote KWA mwanae anaekalia tofali KWENYE shule ya umma.baadhi ya watanzania Wana akili matope sana.
 
Ni kweli kaka, ujira ni mdogo, lakini hatuwezi kuruhusu walimu wawekeze kwenye michango,tutaumiza watu, na ajira hizi ni hiari kwa hiyo umeridhia kufanya kazi ya ualimu ridhika na mshahara wako
Wangekuwa na mbadala kuna mtu angekuwa mwalimu? Hiyo ndio hali waliyojikuta nayo, kila mtu apige kasia kwa urefu wa kamba yake asije akazama, Tanzania chini ya huyu mama ni boti iliyobotoka na inaingiza maji, wacha kila mtu ajiokoe kivyake
 
Elimu ikiwa bure hai maanishi kuwa mzazi asinunue vitabu vya kiada na ziada.
Madaftari
Chakula
Uniform etc
Ndugu hivyo hakuna mwalimu aliyewahi uliza kuhusu sare za shule,daftari au nauli za wanafunzi, wao huangalia pale palipo na maslahi hacha unafiki.
 
Wangekuwa na mbadala kuna mtu angekuwa mwalimu? Hiyo ndio hali waliyojikuta nayo, kila mtu apige kasia kwa urefu wa kamba yake asije akazama, Tanzania chini ya huyu mama ni boti iliyobotoka na inaingiza maji, wacha kila mtu ajiokoe kivyake
Naam hivyo ndivyo hali ilivyo kwa sasa.
 
Achana na watu wenye akili matope.akaulize Ada feza NI sh ngapi.afu anaesoma pale feza NI Mtoto WA anaemwambia asichangie chochote KWA mwanae anaekalia tofali KWENYE shule ya umma.baadhi ya watanzania Wana akili matope sana.
Matope tena, ndugu wewe kusomesha mtoto Feza ndio unajiona unasomesha, na wanaosomesha watoto wao Marekani huko, hujui wanakuona wewe unaesomesha Feza huna tofauti na anaye somesha Shule za secondari za Serikali.
 
Acha ujinga huyu jamaa ndo alio haribu mfumo na elimu yenyewe tutamkimbuka kwa mabaya yake
Basi kama JPM aliharibu elimu baki na huyu tuliye naye walimu waendelee kujiongeza na uzi ufungwe.
 
Si kila siku mnatukana Walimu mitandaoni badala ya kuwatia moyo kwa changamoto wanazopitia, mkishirikiana na Mpwayungu Village? Ngoja Walimu wawanyooshe.

Na bado wanasubiri NGO zinazohamasisha ushoga na usagaji ziwape hela ya kutosha ili wawafundishe watoto wenu huo ushetani. Si serikali yenu haiwajali kimaslahi?
 
Ni kweli, lakini je Serikali kuu inalijua hilo? Maana mambo hufanyika chini chini, kitu ambacho sijui kama ngazi za juu wanajua, mfano mzuri vile vitabu vilivyo katazwa kutumika na Serikali, inamaana ndio haya ya tamaa za walimu kuhamasishwa watu kutumika vitabu bila kufuata utaratibu wa Wizara husika
Ndo maana nikamuliza kama mzazi anahudhuria vikao vya shule hakuna kitu walimu wanapitisha bila ruhusa au maelezo kwa walimu hasa kinachohusu pesa shida wazazi hawahudhuri vikao vya wazazi au kama unadharura nenda shuleni kapate maelezo itaepusha hii sintofahamu
 
Sasa imekuwa kawaida watu kuanzisha nyuzi za kuwasimanga walimu...
 
Sera ya elimu bure ni ngumu sana kuitekeleza,unakuta shule yenye watoto 800 inapokea ruzuku ya sh 260,000 kwa ajili ya maswala ya steshenari kwa mwezi,pesa hiyo hiyo ununue chaki,karamu na vifaa vya kujifunzia na kufundishia mfano lesson plan na scheme of work kwa walimu,baada ya hapo njoo kwenye mitihani ya robo mhula na nusu mhula,mtihani mmoja uliochapwa kwa watoto 800,tuchukulie uwe na page 3 kwa bei ya sh 50@ page =2400 pages x 50 = 120,000 kwa somo moja tu,je kwa masomo Tisa ni sh ngapi? Ni almost 1,000,000,wakati huo ukumbuke kuwa ruzuku kwa ajili ya steshenari ni 260000 kwa mwezi.

Hivyo 260,000 Mara 6 Months ni almost 1.5M,wakati mtihani mmoja tu wa robo mhula unagharimu 1M,je chaki,karamu na vifaa vingine vinatoa wapi pesa?


Hiki kitu ni kigumu sana,naongea kwa uzoefu wangu kama nwalimu,sasa ili kukidhi mahitaji lazima mwanafunzi achangie walau ream moja kwa mwaka.

Njoo kwa walimu wa part time,lazima walipwe,Njoo kwenye uji na pesa ya kumlipa mpishi.

Kiufupi Sera ya elimu bure inachangamoto sana.

Hivyo ukiona ni gharama acha kusomesha mwanao,lakini pia gharama hizi hazizidi 50,000 kwa mwaka.
 
Umekurupuka sana kujibu

Kila mwezi shule zinapokea hela selikal kuu kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kufundishia nankujifunza (shajala)

Zile capitation ndo kazi yake kununua rim na poa wanapewa fedha za miradi kama ujenzi wa madarasa nk

Kila mwezi
Zinafanya nini?
Mkuu usemacho ni kweli kuna ruzuku, nikiwa mwalimu wa taaluma shule X mkoani Lindi wakati elimu bure inaanza,shule yangu ilikuwa inapokea sh 30000 kwa ajili ya steshenari, maana pesa hizi hutolewa kulingana na idadinya watoto,hivyo shuleni pale tulikuwa na watoto 90 tu,sasa hiyo 30000,ununue ream,chaki ,vifaa vya kufundishia na kujifunzia ,uchape mtihani ,bado nauli yakuipeleka na kuifata mitihani inawezekana kweli?

Kiufupi wazazi wanapaswa wakubali kuchangia ,hakuna kitu cha bure kwa ulimwengu wa sasa,Mimi na ualimu wangu huu watoto wangu wanasoma private,huwezi jiuliza why!?

Government schools has a za msingi na olevel ni shida tu
 
Sijawahi kuiunga mkono Sera ya elimu bure hata siku moja.
Hiyo pesa ingeelekezwa kwenye kuboresha maslahi ya wafanyakazi elimu&miundombinu.
Si,kila mtanzania anastahili kusomeshewa.
Tunazalisha kundi la wavivu na wapenda dezo wengi.
 
Back
Top Bottom